Wananchi Katavi watakiwa kutokwepa kulipa kodi ya ardhi

Wananchi Katavi watakiwa kutokwepa kulipa kodi ya ardhi

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Baadhi ya wakazi wa mkoa wa Katavi wameiomba serikali kuona namna bora ya kuwapunguzia wananchi Kodi ya ardhi na kodi ya jengo ambapi imekua mzigo kwa wananchi hao kulipa kodi mbili kutokana na serikali kukata fedha kupitia mfumo wa LUKU huku kodi ya ardhi ikitakiwa kulipiwa katika ofisi za ardhi.

Ismail Mwakiagi, Shaban Ngomoli na Johari Tito wamesema kodi ya ardhi na kodi ya jengo zimekua zikiwachangana ambapo wameiomba serikali kufuta kodi mojawapo ili kupunguza mzigo mkubwa kwa wananchi.

Kamishina msaidizi wa ardhi mkoa wa Katavi Chidiel Mrutu amesema kodi ya ardhi inapaswa ilipwe kila mwaka ambapo ifikapo juni 30 kuhakikisha kila mdaiwa analipa kodi hiyo huku akidai kupelekwa katika vyombo vya sheria kwa yeyote atakaye kaidi.

Mrutu amesisitiza kila mdaiwa kuhakikisha analipa kodi hiyo katika ofisi za ardhi ili kuongeza pato la serikali kwa maslahi ya Taifa.
 
Back
Top Bottom