Wananchi kukosa imani na Polisi: CCM yaagiza Jeshi la Polisi lichunguzwe

Wananchi kukosa imani na Polisi: CCM yaagiza Jeshi la Polisi lichunguzwe

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM iliyokutana jana Dodoma, chini ya Mwenyekiti wake Samia Suluhu, imeiagiza Serikali kuchunguza mwenendo wa Jeshi la Polisi baada ya wananchi kupoteza imani na Jeshi hilo.

Inadaiwa Maofisa wa Polisi hawaaminiki na wanaonekana kutenda majukumu yao bila kufuata Mwongozo wao wa kisheria (PGO).

Shaka Hamdu Shaka amezungumza hayo alipokuwa anaongea na Waandishi wa Habari kuhusu kikao hicho cha CCM kilichofanyika jana.

Akiongea na waandishi leo Machi 12, 2022, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Shaka Hamdu Shaka amesema ‘’Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa imeielekeza Serikali kuangalia upya mwenendo wa Jeshi la Polisi nchini ambao umekuwa hauridhishi na kulalamikiwa na wananchi kutokana na matendo yanayofanywa na baadhi ya maofisa na askari wa Jeshi hilo kinyume na muongozo wa kazi za Jeshi la Polisi"
 
Kwa katiba yetu, ni mtu mmoja tu, hubadili mfumo mzima. Mkiwa na Rais katili, kila chombo cha serikali huwa katili. Mkiwa na Rais muungwana, kila chombo kinabadilika.

Rais Samia, tunakuomba ulibadilishe jeshi la polisi kutoka kwenye ukatili kwenda kqenye ustaaabu na utu. Ustaarabu ni kufuata taratibu na sheria.
 
Hiyo Kamati Kuu ya wanafiki hilo jeshi la polisi likifanya kazi kwa manufaa ya CCM kwa kuwaumiza wapinzani mbona huwa hawaagizi lichunguzwe?

Waambie ukweli, ushirikiano haramu uliopo kati ya jeshi la polisi na CCM ndio chanzo cha wananchi kutoliamini hilo jeshi, imani ya wananchi itaanza kurudi kwa jeshi endapo polisi wataanza kufanya kazi kwa weledi na kuacha ushabiki wa kisiasa.
 
Nani atawachunguza hawa? Ni bora zaidi watoke nje ya jeshi hilo.
 
Hiyo kamati kuu inamjumbe alishasema "tutapigwa tu".

Mfumo wetu wa vyombo vya usalama unaendekeza matumizi ya nguvu zaidi ya akili. Hao kina Kingai wanadhani watajifunza namna mpya ya kufanya kazi sasa hivi.
 
Hiyo Kamati Kuu ya wanafiki hilo jeshi la polisi likifanya kazi kwa manufaa ya CCM kwa kuwaumiza wapinzani mbona huwa hawaagizi lichunguzwe?

Waambie ukweli, ushirikiano haramu uliopo kati ya jeshi la polisi na CCM ndio chanzo cha wananchi kutoliamini hilo jeshi, imani ya wananchi itaanza kurudi kwa jeshi endapo polisi wataanza kufanya kazi kwa weledi na kuacha ushabiki wa kisiasa.
Jeshi la polisi linaendeshwa na CCM. Hakuna kitu linachokifanya ambacho CCM hawakitaki. Hakuna uchunguzi wowote hapo. Na zaidi: Unawatumia polisi kuiba kura halafu unategemea polisi hao hao wakuheshimu wakati wanajua kama siyo wao wewe usingengepata ule wadhifa?
 
16451705215243.jpg
 
Ikiwa hujawahi wewe mwenyewe ,ndugu ama jamaa yako wakaribu kukutana na kadhia ya hawa jamaa hutowezakuona madhaifa ya jeshi la polisi. Kiufupi waha jamaa wananongwa hasa upande wa kubambikia kesi wako vizuri sana
 
Kesi ya ubambikaji ya Mbowe na ugaidi imeaacha Polisi uchi wa mnyama.

Imagine, Polisi aliyefuzu CCP-Moshi hajui PGO ni nini!!!

Kina Kingai wako wengi kama sio wote ndani ya Jeshi la Polisi.

IGP Sirro mwenyewe aiulizwa Intellijesia maana yake nini, alishindwa vibaya kujibu akidai hizo ni siri za Jesho-upuuzi mtupu!

Wenzetu nchi zilizostaarabika wanakuwa proffessional katika suala la Rapid Response, uchunguzi hasa ule wa Forensic, na hata masuala la kuzingatia sheria za utendaji kazi.

Kama maafisa kama Kingai na IGP wake wanapwaya, hili si jeshi la kutegemewa kitaalam.
 
Back
Top Bottom