jingalao
JF-Expert Member
- Oct 12, 2011
- 36,197
- 29,717
Wasalamu!
Tumeingia kwenye awamu nyingine ya kusaka viongozi wetu wa awamu ya tano/sita katika ngazi ya Urais,Ubunge na Udiwani.
Naipongeza Serikali chini ya Rais Shupavu John Pombe Magufuli kwa kitufikisha hatua hii kwa amani,usalama na Siha njema.Hili halikuwezekana hivi hivi bali kwa ujasiri,akili ,maarifa na kujifunza kwake kusikokoma.
Nchi ilipitia changamoto mbalimbali nzito na za aina ya kipekee.Nchi ilipitia matishio ya kugawanywa,kuhujumiwa kiuchumi,chembechembe za usaliti wa wazi,ugaidi,majanga ya hali ya hewa,njaa na hatimaye COVID 19 Pandemic.
Tukitafakari wagombea wa mwaka 2015 hasa yule aliyetaka tuamini kuwa ndiye angefaa utaona ni namna gani tulimuhitaji Rais tuliyenaye.
Tukiwatazama wabunge na madiwani wanaomaliza muda wao tunaweza kujua nani walikuwa real kwa maslahi ya wananchi wanyonge na nani waliingia kwa upepo tu na hivyo baada ya kuingia hawakufanya lolote.
Tumeshuhudia kuibuka kwa wanaharakati vibaraka na wadhalilishaji wanaodakia matukio mbalimbali na kuyatolea maoni yasiyo na utatuzi endekevu...yaani ni basket mouths na makasuku wa mambo yasiyo na tija kwa wavuja jasho na hufanya hivi kwa manufaa ya matumbo yao tu.
Niingie kwenye kuminanane kwa kuishawishi jamii hasa hii ya tunaojiita Great thinkers kwa kuwaeleza kuwa tutumie uwezo wetu kuwafikiria wasio na uwezo au wenye uhitaji wa yale ambayo baadhi yetu tumeyapata.
Yaani tufikiri kwenye ngazi ya familia hasa za pembezoni zinavyoishi na hatimae tuwatengenezee fursa na juhudi zao zilipe kwa manufaa yao na vizazi vijavyo.mfikirie mjamzito anayeishi kilometa 200 mwituni kutoka makao makuu ya wilaya kuifuata hospitali ama mahitaji muhimu.
Tukiwaza kwa muktadha huu hatutababaishwa na wanahabari failures au wanaharakati wachumia tumbo au vibaraka wa makampuni makubwa kuzisemea shida halisi za mtanzania.
Aidha tuondokane na hulka za kuiga iga upuuzi wa walami ndio tukafanya kuwa muelekeo endelevu wa Taifa.
Kwa kifupi tuweke agenda nyeti ya maendeleo ya vitu,miundombinu na watu kama dira ya aina ya viongozi tunaotakiwa kuwa nao.
Nitamdharau sana mwanasiasa au msomi au mtu maarufu atakayetaka kutulazimisha tuimbe nyimbo za miaka ya vita kuu ya dunia au harakati za ukombozi.
Nitamdharau mwanasiasa atakayetaka tuige nchi zinazopigania haki ya ndoa za jinsia moja n.k wakati umeme haupo kwenye baadhi ya maeneo.
Nitamdharau kiongozi wa dini kujidharaulisha kwa kudakia mada za kisanii na kutaka kuwaaminisha waaumini wake juu ya usanii huo.
Uzoefu katika miaka mitano unadhihirisha kuwa Tanzania ina resources zote yaani watu,watu wenye weledi,miongozo mizuri,maji,umeme tuli,mafuta tuli,ardhi kubwa,mawe na madini muhimu n.k vyote hivi havijawa explored ili kuleta tija ...
Awamu ya Rais Magufuli imetufunza jambo kuu yaani UWAJIBIKAJI na Uchapaji kazi unalipa.Pia USIMAMIZI (UONGOZI) sahihi unalipa.hivyo sio muda wa kukosea.
Kupitia waraka huu niwaase wahusika wote kwenye kilinge cha siasa kujikita kwenye hoja nzito ya kuwasaidia wananchi na tuwapime wagombea kwa muktadha huo.
Tusiwasemee wananchi tuwaache wayaseme ya kwao ambayo ni muhimu.
KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA!!
Tumeingia kwenye awamu nyingine ya kusaka viongozi wetu wa awamu ya tano/sita katika ngazi ya Urais,Ubunge na Udiwani.
Naipongeza Serikali chini ya Rais Shupavu John Pombe Magufuli kwa kitufikisha hatua hii kwa amani,usalama na Siha njema.Hili halikuwezekana hivi hivi bali kwa ujasiri,akili ,maarifa na kujifunza kwake kusikokoma.
Nchi ilipitia changamoto mbalimbali nzito na za aina ya kipekee.Nchi ilipitia matishio ya kugawanywa,kuhujumiwa kiuchumi,chembechembe za usaliti wa wazi,ugaidi,majanga ya hali ya hewa,njaa na hatimaye COVID 19 Pandemic.
Tukitafakari wagombea wa mwaka 2015 hasa yule aliyetaka tuamini kuwa ndiye angefaa utaona ni namna gani tulimuhitaji Rais tuliyenaye.
Tukiwatazama wabunge na madiwani wanaomaliza muda wao tunaweza kujua nani walikuwa real kwa maslahi ya wananchi wanyonge na nani waliingia kwa upepo tu na hivyo baada ya kuingia hawakufanya lolote.
Tumeshuhudia kuibuka kwa wanaharakati vibaraka na wadhalilishaji wanaodakia matukio mbalimbali na kuyatolea maoni yasiyo na utatuzi endekevu...yaani ni basket mouths na makasuku wa mambo yasiyo na tija kwa wavuja jasho na hufanya hivi kwa manufaa ya matumbo yao tu.
Niingie kwenye kuminanane kwa kuishawishi jamii hasa hii ya tunaojiita Great thinkers kwa kuwaeleza kuwa tutumie uwezo wetu kuwafikiria wasio na uwezo au wenye uhitaji wa yale ambayo baadhi yetu tumeyapata.
Yaani tufikiri kwenye ngazi ya familia hasa za pembezoni zinavyoishi na hatimae tuwatengenezee fursa na juhudi zao zilipe kwa manufaa yao na vizazi vijavyo.mfikirie mjamzito anayeishi kilometa 200 mwituni kutoka makao makuu ya wilaya kuifuata hospitali ama mahitaji muhimu.
Tukiwaza kwa muktadha huu hatutababaishwa na wanahabari failures au wanaharakati wachumia tumbo au vibaraka wa makampuni makubwa kuzisemea shida halisi za mtanzania.
Aidha tuondokane na hulka za kuiga iga upuuzi wa walami ndio tukafanya kuwa muelekeo endelevu wa Taifa.
Kwa kifupi tuweke agenda nyeti ya maendeleo ya vitu,miundombinu na watu kama dira ya aina ya viongozi tunaotakiwa kuwa nao.
Nitamdharau sana mwanasiasa au msomi au mtu maarufu atakayetaka kutulazimisha tuimbe nyimbo za miaka ya vita kuu ya dunia au harakati za ukombozi.
Nitamdharau mwanasiasa atakayetaka tuige nchi zinazopigania haki ya ndoa za jinsia moja n.k wakati umeme haupo kwenye baadhi ya maeneo.
Nitamdharau kiongozi wa dini kujidharaulisha kwa kudakia mada za kisanii na kutaka kuwaaminisha waaumini wake juu ya usanii huo.
Uzoefu katika miaka mitano unadhihirisha kuwa Tanzania ina resources zote yaani watu,watu wenye weledi,miongozo mizuri,maji,umeme tuli,mafuta tuli,ardhi kubwa,mawe na madini muhimu n.k vyote hivi havijawa explored ili kuleta tija ...
Awamu ya Rais Magufuli imetufunza jambo kuu yaani UWAJIBIKAJI na Uchapaji kazi unalipa.Pia USIMAMIZI (UONGOZI) sahihi unalipa.hivyo sio muda wa kukosea.
Kupitia waraka huu niwaase wahusika wote kwenye kilinge cha siasa kujikita kwenye hoja nzito ya kuwasaidia wananchi na tuwapime wagombea kwa muktadha huo.
Tusiwasemee wananchi tuwaache wayaseme ya kwao ambayo ni muhimu.
KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA!!