Wananchi Mwanza wadaiwa kuzuia watu waliovalia kiraia kuondoka na watuhumiwa, waita Mkuu wa Kituo Pamba kuja kuwatambua

Wananchi Mwanza wadaiwa kuzuia watu waliovalia kiraia kuondoka na watuhumiwa, waita Mkuu wa Kituo Pamba kuja kuwatambua

Wakuu, tukio hili inasemekana limetokea Mwanza ambapo watu waliojitambulisha kama polisi waenda kukamata watu eneo hilo, raia wakazuia gari hilo mpaka mkuu wa kituo pamba aende kuwatambua kuwa kweli ni polisi.

Mwenye taarifa juu ya kilichojiri atujuze.

Kidogo kidogo safari inaanza.

Ni lazima ipo siku tutafika tu huko wanakotaka tufike, safari ndio imeshaanza hivi.
 
Hatimaye elimu inayotolewa na Chadema imesambaa Nchi nzima.
Litakuwa jambo jema sana kama taarifa hii ni ya kweli.Kwani haya ndiyo tuliyo himiza CHADEMA wayape kipaumbele.

Sasa tusubiri wezi wa kura na wao wakomeshwe hivi hivi kwenye kila kituo cha kupigia kura.
Ikitokea ikawa hivyo, hakuna sababu tena ya kuwa na hofu katika chaguzi zinazo fuata.
 
Hao kiujumla ni watekaji na wananchi wamefanya makosa kumwita ocd Kuja kuwatambua.kitendo Cha kumwita ocd tayari hao waharifu wamekuwa salama maana wanatoka humohumo kwenye vyombo vya ulinzi.kama wao wanavyokuja pasipo kufuata utaratibu wa kumkamata na wananchi wanahaki kuwashughulikia Kwa kipigo bila kumjulisha mkuu wa kituo.Ilitakiwa waumalize mchezo palepale ili kumaliza huu uhuni wa kuteka lakini Kwa Sasa wasitarajie kupewa mrejesho wowote.
 
Wapo sahihi kabisa. Askari anayepaswa kufanya arresting anatakiwa awe amevaa uniform.
Inapendeza kuona watu wameanza kuamka na wanajitolea kusimamia utekelezwaji wa sheria na taratibu.
Wananchi waichukue hii PGO wakaisoma na kuielewa na kuisambaza kwa wananchi wengine ili waweze kuwasimamia vizuri Polisi katika utendaji wao.
Hii kitubtaahira Kingai hana hamu nayo hasa akimkumbuka peter Kibatala
 
Wakuu, tukio hili inasemekana limetokea Mwanza ambapo watu waliojitambulisha kama polisi waenda kukamata watu eneo hilo, raia wakazuia gari hilo mpaka mkuu wa kituo pamba aende kuwatambua kuwa kweli ni polisi.

Mwenye taarifa juu ya kilichojiri atujuze.

Hongera sana kwa wananchi wa Mwanza. Serikali itunge sheria ya mtu kukamatwa. Hatukubali tena kukamatwa kizembe.
 
Uko sahihi mkuu 'Paki'; lakini kweli serikali inahitaji kukumbushwa maswala kama haya?
Huko serikalini kweli hakuna wanao liona tatizo hili hadi wananchi waingilie kati? Serikali ipo kufanya nini?

Kwa nini serikali ndio wawe wafanya uhalifu; ambao wananchi sasa inalazimika kuingilia kuuzuia! Hii si aibu kwa viongozi wakuu wa serikali?
Kuna mambo yanasikitisha sana. Hii siyo ishara njema kwa serikali sababu huko serikslini asilimia zaidi ya 90 hawajui wafanyacho wala wanachopaswa kufanya. Inapotokea wananchi wanaanza kuamka na kuchukua hatua ya kuisimamia serikali kama hivi, huo ndiyo huwa ni mwanzo wa kuanguka kwa seriksli,
Hili tukio la Mwanza inapaswa liongelewe sana, lisambazwe nchi nzima wananchi wazidi kuamka, hasa kipindi hiki ambacho nchi inaelekea kwenye uchaguzi, mtaona jinsi CCM inavyoenda kushindwa kwa kishindo
 
Back
Top Bottom