Wananchi Mwanza wadaiwa kuzuia watu waliovalia kiraia kuondoka na watuhumiwa, waita Mkuu wa Kituo Pamba kuja kuwatambua

Kidogo kidogo safari inaanza.

Ni lazima ipo siku tutafika tu huko wanakotaka tufike, safari ndio imeshaanza hivi.
 
Hatimaye elimu inayotolewa na Chadema imesambaa Nchi nzima.
Litakuwa jambo jema sana kama taarifa hii ni ya kweli.Kwani haya ndiyo tuliyo himiza CHADEMA wayape kipaumbele.

Sasa tusubiri wezi wa kura na wao wakomeshwe hivi hivi kwenye kila kituo cha kupigia kura.
Ikitokea ikawa hivyo, hakuna sababu tena ya kuwa na hofu katika chaguzi zinazo fuata.
 
Hao kiujumla ni watekaji na wananchi wamefanya makosa kumwita ocd Kuja kuwatambua.kitendo Cha kumwita ocd tayari hao waharifu wamekuwa salama maana wanatoka humohumo kwenye vyombo vya ulinzi.kama wao wanavyokuja pasipo kufuata utaratibu wa kumkamata na wananchi wanahaki kuwashughulikia Kwa kipigo bila kumjulisha mkuu wa kituo.Ilitakiwa waumalize mchezo palepale ili kumaliza huu uhuni wa kuteka lakini Kwa Sasa wasitarajie kupewa mrejesho wowote.
 
Hii kitubtaahira Kingai hana hamu nayo hasa akimkumbuka peter Kibatala
 
Hongera sana kwa wananchi wa Mwanza. Serikali itunge sheria ya mtu kukamatwa. Hatukubali tena kukamatwa kizembe.
 
Kuna mambo yanasikitisha sana. Hii siyo ishara njema kwa serikali sababu huko serikslini asilimia zaidi ya 90 hawajui wafanyacho wala wanachopaswa kufanya. Inapotokea wananchi wanaanza kuamka na kuchukua hatua ya kuisimamia serikali kama hivi, huo ndiyo huwa ni mwanzo wa kuanguka kwa seriksli,
Hili tukio la Mwanza inapaswa liongelewe sana, lisambazwe nchi nzima wananchi wazidi kuamka, hasa kipindi hiki ambacho nchi inaelekea kwenye uchaguzi, mtaona jinsi CCM inavyoenda kushindwa kwa kishindo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…