Wananchi tuamke...viongozi kutokuheshimu Katiba wala viapo vyao, Idara ya Mahakama imetuangusha!

Wananchi tuamke...viongozi kutokuheshimu Katiba wala viapo vyao, Idara ya Mahakama imetuangusha!

Mag3

Platinum Member
Joined
May 31, 2008
Posts
13,413
Reaction score
23,592
Watanzania wenzangu, kuna mengi ya kusikitisha yanayoendelea ndani ya nchi yetu na kubwa kuliko yote ni ukiukwaji mkubwa wa haki za msingi za raia wa taifa hili. Haki hizi ni zile zilizoorodheshwa ndani ya maazimio ya msingi tuliyokubaliana wananchi kama dira yetu na taratibu za maisha kijamii.

Tofauti na wanyama wa porini, binadamu huandaa namna ya kuendesha maisha yao kama mtu moja, familia na jamii katika taifa. Kufanikiwa katika hili kuna misingi tuliyoafiki kuijenga kama taifa na hivyo tumejiwekea sheria, kanuni na taratibu ambazo lazima zihifadhiwe, zilindwe na kutetewa na wote.

Ndio maana tunapomchagua kiongozi, tunahakikisha tunahodhi madaraka kama wanachi ya kumwajibisha kiutekelezaji kama ataenda kinyume na makubaliano yetu. Hivyo kitu cha kwanza kabisa anachotakiwa kufanya ni kuapa kwamba hatavuka mipaka ya uongozi kama iliyooainishwa ndani ya Katiba

Naomba nianze sasa kwa kunukuu Sehemu ya Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inavyosema kuhusu idara ya Mahakama...


107A.-(1) Mamlaka ya utoaji haki katika Jamhuri ya Muungano itakuwa mikononi mwa Idara ya Mahakama na Idara ya Mahakama ya Zanzibar, na kwa hiyo hakuna chombo cha Seriikali wala cha Bunge au Baraza la Wawakilishi la Zanzibar kitakachokuwa na kauli ya mwisho katika utoaji haki.


(2) Katika kutoa uamuzi wa mashauri ya madai na jinai kwa kuzingatia sheria, Mahakama zitafuata kanuni zifuatazo, yaani:


(a) kutenda haki kwa wote bila ya kujali hali ya mtu kijamii Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (b) kutochelewesha haki bila sababu ya kimsingi;


(c) kutoa fidia ipasayo kwa watu wanaoathirika kutokana na makosa ya watu wengine, na kwa mujibu wa sheria mahususi iliyotungwa na Bunge;


(d) kukuza na kuendeleza usuluhishi baina ya wanaohusika katika migogoro; Uhuru wa Mahakama Sheria ya 2000 Na.3 ib.17

107B. Katika kutekeleza mamlaka ya utoaji haki, mahakama zote zitakuwa huru na zitalazimika kuzingatia tu masharti ya Katiba na yale ya sheria za nchi.

Tukiendelea hebu tujikumbushe alichoapa Rais John Pombe Magufuli baada ya kutangazwa na Tume ya Uchaguzi kuwa mshindi wa Urais November mwaka 2015...


2%2B%25282%2529.jpg

"Mimi John Pombe Joseph Magufuli naapa kwamba nitakuwa mwaminifu kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na nitalinda na kuitetea Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilivyowekwa kisheria.

Ewe Mwenyezi Mungu nisaidie.

Mimi John Pombe Joseph Magufuli naapa nitatenda kazi zangu za Urais wa Jamhuri ya Tanzania kwa uaminifu kwa kutimiza wajibu wa kazi hizo kwa bidii na moyo mkunjufu na kwamba nitawatendea haki watu wote kwa mujibu wa sheria, mila na desturi za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila woga, bila upendeleo, huba wala chuki.

Ewe Mwenyezi Mungu nisaidie."


5.jpg

Kaimu Jaji Mkuu Prof Ibrahim Hamis Juma akiapa atakavyokuwa mwaminifu kwa Jamhuri ya Muungano kwa kulinda uhuru wa Mahakama na kusimamia kikamilifu Mamlaka ya utoaji haki.

Jaji Mkuu ndiye Kiongozi wa Mahakama ya Rufani na pia Mkuu wa Idara ya Mahakama kama ilivyofafanuliwa katika ibara ya 116 ya Katiba.

Je ukimya wa Jaji Mkuu Katiba inaposiginwa, hati za mahakama kudharauliwa na haki za raia kuminywa kunatupa picha gani wananchi?


PIX1.jpg

Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Ferdinand Wambali ambaye ndiye msaidizi maalum wa Jaji Mkuu katika utendaji wa kazi katika Mahakama Kuu na Mahakama nyinginezo zote za ngazi ya chini yake, na katika madaraka hayo Jaji Kiongozi atatekeleza kazi na shughuli atakazoagizwa au kuelekezwa mara kwa mara na Jaji Mkuu, na kwa madhumuni ya ibara hii, Jaji Kiongozi atajulikana pia kama Mkuu wa Mahakama Kuu.

Je ukimya wa Idara ya Mahakama, mawakili wanaponyanyaswa na vyombo vya dola na ofisi zao kushambuliwa tuutafsirije sisi raia?
 
Hahahaaaa, kodi za Wananchi ni tamu sana, hata wewe ukipewa hicho cheo, kesho tu utasahau yote Uliyotuapia, Mwl Nyerere peke yake ndiye aliweza. Labda tusubiri karne ya 22
 
Wananchi wapi hao waamke? Unajichosha tu na bandiko lako
Tukinyamaza si ndio watalala moja kwa moja...ndugu yangu kuna watu sasa hivi hawalali kwa kelele zetu, wanapata ukichaa kwa kelele zetu. Tuzidi tu kupiga kele na muda si mrefu utawasikia wenyewe nao wakianza kupiga mayowe kwa hofu!
 
Tukinyamaza si ndio watalala moja kwa moja...ndugu yangu kuna watu sasa hivi hawalali kwa kelele zetu, wanapata ukichaa kwa kelele zetu. Tuzidi tu kupiga kele na muda si mrefu utawasikia wenyewe nao wakianza kupiga mayowe kwa hofu!
Mkuu mimi nimenawa mikono nimeamua tu kuwa kimya.. Litakalo kuja lije tu hakuna jipya dunia hii yote ni marudio tu, kama ni kuchinja wananchi wake wacha achinje, kama ni kutawala miaka 100 sawa.. Vunja katiba anavyotaka sawa tu maana nchi ya baba yake hii nk
 
Kw
Tukinyamaza si ndio watalala moja kwa moja...ndugu yangu kuna watu sasa hivi hawalali kwa kelele zetu, wanapata ukichaa kwa kelele zetu. Tuzidi tu kupiga kele na muda si mrefu utawasikia wenyewe nao wakianza kupiga mayowe kwa hofu!
Kwa hiyo unawachochea? Angalia usije kujikojolea nguoni ili kukwepa mkojo wa kupima usipatikane.
 
Tatizo Tanzania wanaharakati wamelala sana hawana faida sasa nani atawapigania Watanzania?
 
Inasikitisha na kutia huzuni ukiona nyumba zinabomolewa na serikali wakati mahakama imetoa zuio LA kutobomolewa nyumba hizo.
Haki yetu tutapata wapi serikali hii inapotutendea isivyo haki na kupuuza amri za mahakama zetu?
Watanzania tujitafakari tumekosea wapi vinginevyo tutaangamia mmoja baada ya mwingine maana hakuna aliyesaalama kwa mwendo huu.
 
Inadaiwa "Stop Order" ya mahakama haikupelekwa TANROADS na badala yake karani wa mahakama akaenda kuibandika kwenye kila nyumba ambayo inajiandaa kubomolewa....

Sina hakika na si mtaalamu wa sheria miye, kiasi ambacho ninajiuliza tu kwamba, iwapo huo utaratibu unakubalika kisheria (kubandika stop order ama wito (samansi) ya mahakama) mlangoni ama Vinginevyo......
 
Inasikitisha na kutia huzuni ukiona nyumba zinabomolewa na serikali wakati mahakama imetoa zuio LA kutobomolewa nyumba hizo.
Haki yetu tutapata wapi serikali hii inapotutendea isivyo haki na kupuuza amri za mahakama zetu?
Watanzania tujitafakari tumekosea wapi vinginevyo tutaangamia mmoja baada ya mwingine maana hakuna aliyesaalama kwa mwendo huu.
Kibisa
 
Inasikitisha na kutia huzuni ukiona nyumba zinabomolewa na serikali wakati mahakama imetoa zuio LA kutobomolewa nyumba hizo.
Haki yetu tutapata wapi serikali hii inapotutendea isivyo haki na kupuuza amri za mahakama zetu?
Watanzania tujitafakari tumekosea wapi vinginevyo tutaangamia mmoja baada ya mwingine maana hakuna aliyesaalama kwa mwendo huu.
.
Umeliona wapi hilo zuio la kubomoa?
Nani au taasisi gani imepuuza amri ya mahakama?
Fanya uchunguzi yakinifu kabla hujatoa hitimisho na kuanza kutoa lawama zisizo na msingi.
 
.
Umeliona wapi hilo zuio la kubomoa?
Nani au taasisi gani imepuuza amri ya mahakama?
Fanya uchunguzi yakinifu kabla hujatoa hitimisho na kuanza kutoa lawama zisizo na msingi.
Wewe mwenye ufahamu nzuri na uliyefanya uchunguzi na usiye na lawama tuambie usahihi wa nini kinaendelea kwenye bomoabomoa za huko Dar. Au we ndo unabomoa nyumba za watu yawezekana hata kibanda hujawahi kujenga.
 
Wewe mwenye ufahamu nzuri na uliyefanya uchunguzi na usiye na lawama tuambie usahihi wa nini kinaendelea kwenye bomoabomoa za huko Dar. Au we ndo unabomoa nyumba za watu yawezekana hata kibanda hujawahi kujenga.
kwa taarifa yako ubomoaji unafanyika kwa mujibu wa sheria. Ni kweli kuna baadhi (sio wote) ya waliobomolewa majengo yao walifungua kesi mahakamani. Cha kushangaza wanadai mahakama imetoa zuio wakati kiukweli mahakama haijatoa zuio lolote dhidi ya serikali au Tanroads. Kuna baadhi walionesha makaratasi (nami mimeyaona) wakidai ndio zuio jenyewe, ukweli ni kwamba lile si zuio la mahakama. Mengi yameandikwa stop order. Stop order sio amri ya zuio inayotakiwa kuombwa na kutolewa na mahakama dhidi ya serikali. Kwanza nina mashaka na hao waliosambaza hizo stop order. Mahakama haiwezi kutoa kitu kama stop order dhidi ya serikali.

kwa kifupi hizo mnazoziita stop oder si zuio la kuzuia serikali au chombo au taasisi ya serikali isifanye utekelezaji wa mipango yake.
 
kwa taarifa yako ubomoaji unafanyika kwa mujibu wa sheria. Ni kweli kuna baadhi (sio wote) ya waliobomolewa majengo yao walifungua kesi mahakamani. Cha kushangaza wanadai mahakama imetoa zuio wakati kiukweli mahakama haijatoa zuio lolote dhidi ya serikali au Tanroads. Kuna baadhi walionesha makaratasi (nami mimeyaona) wakidai ndio zuio jenyewe, ukweli ni kwamba lile si zuio la mahakama. Mengi yameandikwa stop order. Stop order sio amri ya zuio inayotakiwa kuombwa na kutolewa na mahakama dhidi ya serikali. Kwanza nina mashaka na hao waliosambaza hizo stop order. Mahakama haiwezi kutoa kitu kama stop order dhidi ya serikali.

kwa kifupi hizo mnazoziita stop oder si zuio la kuzuia serikali au chombo au taasisi ya serikali isifanye utekelezaji wa mipango yake.
So, Stop Order kitu gani kutoka mahakama ni kisichoheshimika na serikali yetu?
 
So, Stop Order kitu gani kutoka mahakama ni kisichoheshimika na serikali yetu?
.
Stop order ni uhuni tu unaofanywa na makarani kuhadaa wasiojua sheria. Kuna mawakili pia wanafanya michezo kama hii. Serikali haifanyi kazi kwa vistop order, wala haizuiwi kufanya chochote kisa kuna kitu kinaitwa stop order. stop order ni uhuni wa kutishia wasiojua sheria tu.

Katika sheria kuna zuio ambalo huombwa kwa mujibu wa vifungu vya sheria na husikilizwa kwa utaratibu maalum (kati ya muomba zuio na muombewa zuio), baada ya hapo mahakama hufanya upembuzi na ikijiridhisha kuwa kuna haja ya kutoa zuio hutoa zuio. Kuna namna pia ya kufikisha zuio kwa mtu au taasisi iliyolengwa na hilo zuio, sio kwenda kubandika sijiu mlangoni sijui chooni au barabarani kama vile ni wito wa kawaida tu wa mahakama.

Zuio la mahakama ni amri ya kipekee, haiendeshwi ua kuchukuliwa kama amri zingine za kawaida au wito wa kawaida, hii ni kutokama na mazingira inayotolewa na jinsi nature yake ilivyo. Amri ya zuio inao utaratibu wa kipekee kabisa kuanzia mtu binafsi, taasisi binafsi, mashirika ya umma, makampuni, taasisi za serikali, serikali za mitaa na hata serikali kuu. hii inamaana kuwa kuomba, kusikilizwa na kutolewa kwa Amri ya Zuio inatofautiana sana kutokana na wahusika wa kesi yenyewe, mfano kumzuia mtu binafsi au kampuni binafsi ni totauti kabisa na kuizuia serikali.

Stop order haiwezi kulinganishwa na Amri ya Zuio kwa namna yoyote ile. Stop order ni zao tofauti kabisa na amri ya zuio katika sheria.
 
We hujui sheria,nyamaza.Unatangaza ujinga wako kwenye hilo eneo.Eti makarani ndio huandaa stop order.
 
.
Stop order ni uhuni tu unaofanywa na makarani kuhadaa wasiojua sheria. Kuna mawakili pia wanafanya michezo kama hii. Serikali haifanyi kazi kwa vistop order, wala haizuiwi kufanya chochote kisa kuna kitu kinaitwa stop order. stop order ni uhuni wa kutishia wasiojua sheria tu.

Katika sheria kuna zuio ambalo huombwa kwa mujibu wa vifungu vya sheria na husikilizwa kwa utaratibu maalum (kati ya muomba zuio na muombewa zuio), baada ya hapo mahakama hufanya upembuzi na ikijiridhisha kuwa kuna haja ya kutoa zuio hutoa zuio. Kuna namna pia ya kufikisha zuio kwa mtu au taasisi iliyolengwa na hilo zuio, sio kwenda kubandika sijiu mlangoni sijui chooni au barabarani kama vile ni wito wa kawaida tu wa mahakama.

Zuio la mahakama ni amri ya kipekee, haiendeshwi ua kuchukuliwa kama amri zingine za kawaida au wito wa kawaida, hii ni kutokama na mazingira inayotolewa na jinsi nature yake ilivyo. Amri ya zuio inao utaratibu wa kipekee kabisa kuanzia mtu binafsi, taasisi binafsi, mashirika ya umma, makampuni, taasisi za serikali, serikali za mitaa na hata serikali kuu. hii inamaana kuwa kuomba, kusikilizwa na kutolewa kwa Amri ya Zuio inatofautiana sana kutokana na wahusika wa kesi yenyewe, mfano kumzuia mtu binafsi au kampuni binafsi ni totauti kabisa na kuizuia serikali.

Stop order haiwezi kulinganishwa na Amri ya Zuio kwa namna yoyote ile. Stop order ni zao tofauti kabisa na amri ya zuio katika sheria.

Mkuu hivi unatuona mabwege, stop order na amri ya zuio tofauti yake ni nini? Au yofauti yake moja ni kwa kiingereza na nyingine ni kwa kiswahili? Acha uhuni wa kitoto bana.
 
Back
Top Bottom