Wananchi wa kata ya Bwawani Arusha waandamana kulazimisha TAKUKURU wamwachie Mtendaji Kata aliyewekwa Ndani na Makonda; wadai RC hasikilizi wananchi

Wananchi wa kata ya Bwawani Arusha waandamana kulazimisha TAKUKURU wamwachie Mtendaji Kata aliyewekwa Ndani na Makonda; wadai RC hasikilizi wananchi

Resilience

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2023
Posts
1,096
Reaction score
4,948
Siku chache baada ya RC Makonda kuelekeza TAKUKURU wamweke ndani Mtendaji Kata ya Bwawani na asipewe dhamana kwa tuhuma za kuchukua rushwa milioni moja; wananchi wa kati hiyo zaidi ya mia mbili wamekodi magari na kwenda ofisi za TAKUKURU kushinikiza mtendaji huyo aachiwe huru kwani mafisadi wakiongozwa na madiwani na viongozi wa CCM waliofisadi kata hiyo wameanza kutumia ulaghai kuwakandamiza wananchi.

Wananchi wamesema mtendaji huyo alipangiwa kufanya kazi kata hiyo mwaka 2019. Alipoanza kazi mashamba ya kijiji yalikuwa yanatumika na viongozi kulima na kujimilikisha kama ya kwao. Mtendaji aliwanyang'anya mashamba hayo viongozi akiwemo diwani na kuwapa wananchi jambo ambalo viongozi hao wa CCM walichukizwa nalo.

Wakati anapangwa kufanya kazi katika kata hiyo hakuna fedha iliyokuwa inakusanywa kama ushuru kutoka kwenye mali za kata; kwa sasa mashamba yanachangia zaidi ya milioni 30.

Amefanikisha kujenga kituo cha afya na shughuli za maendeleo zinaendelea. Aidha, wakati anaingia wanafunzi walikuwa wanapeleka mahindi na maharage kwa ajili ya chakula ila sasa hivi mtendaji huyo ametenga ekari 20 kwa ajili ya shule na kwa mwaka huu shule imevuna zaidi ya gunia 80 zinazotumika kulisha wanafunzi.

Kuhusu rushwa ya milioni moja inayodaiwa na Mkuu wa Mkoa, wananchi wamesema fedha hizo zilitolewa adharani na hazikuwahi kukabidhiwa kwa mtendaji badala yake zilielekezwa kununua vifaa vya ujenzi na kwamba Makonda alipaswa kuwahoji wananchi kuliko kutoka na taarifa ofisini kwake na kwenda kuwakamata watu wasio na hatia kwa maelekezo ya mafisadi wanaotumia mali za umma kuwaumiza viongozi wenye maono kama mtendaji.

Wananchi hao wameitaka TAKUKURU kufanya kazi kwa utaalamu badala ya kufanya kazi kisiasa. Wamehoji kama kweli kulikuwepo rushwa kwanini TAKUKURU haikuwahi kuchunguza badala yake inapokea maelekezo? Wamehoji kwanini TAKUKURU wameshindwa kufika kijijini kufanya mahojiano na wananchi badala yake wamejazana kumweka mahabusu mtendaji ambaye dhamana ni haki yake?

Mwisho, wananchi wanadai mambo aliyoyafanya mtendaji wa Bwawani yanastahili pongezi na siyo kuadhibiwa kama mkuu wa Mkoa anavyofanya. Kama mkuu wa mkoa ana vyombo alipaswa kubaini mapema kwamba viongozi wa CCM wa kata wanatumia ofisi yake kupambana na watendaji wa serikali wanaowatumikia wananchi kwa haki.
 
Kama hilo jambo Lina ukweli kabisa najua RC Makonda Yumo humu ndani na antenda kuliadress vyema na haki itapatikana....Wahuni nao wanakuja Kasi ...yahani ni wazee wa Copy tu.
 
Hao wananchi wana haraka ya nini?Anahojiwa hajahukumiwa.Ikiwa hana hatiia kwenye tuhuma hizo za kushiriki kuuza eneo la kijiji na sio rushwa ya milioni 1 ataachiwa.Ikiwa ameshiriki hatua za kisheria zitachukuliwa.
Wananchi hao walikuwepo kwenye mkutano na hakuna aliyepinga tuhuma hizo.
Mtendaji aliulizwa kwanini hakutangazia wananchi mkutano huo na hakuwa na majibu ya kuridhisha.
Kupelekwa Takukuru sio kuhukumiwa.
 
Hao wananchi wana haraka ya nini?Anahojiwa hajahukumiwa.Ikiwa hana hatiia kwenye tuhuma hizo za kushiriki kuuza eneo la kijiji na sio rushwa ya milioni 1 ataachiwa.Ikiwa ameshiriki hatua za kisheria zitachukuliwa.
Wananchi hao walikuwepo kwenye mkutano na hakuna aliyepinga tuhuma hizo.
Mtendaji aliulizwa kwanini hakutangazia wananchi mkutano huo na hakuwa na majibu ya kuridhisha.
Kupelekwa Takukuru sio kuhukumiwa.
Kwani ninyi mlikuwa na haraka gani ya kumweka ndani tena bila dhamana jambo lililo kinyume na Sheria za nchi, kwa nini msingejipa muda wa kuchunguza? Je hivi ndivyo haki inavyotendwa?

Yeye athulumiwe haki yake kwa uonevu baadae mumwachie kirahisi halafu useme eti ni haki.

Acheni dhuluma, timizeni wajibu kwa kufuata taratibu na Sheria, hizi sifa za kijinga zinaumiza wengine wasio na hatia.
 
Kinachosumbuwa Arusha ni siasa na chuki na sio kingine.
Siasa siyo jambo baya. Watanzania kwa ulaghai wa CCM tumefanywa kudhani kuwa uroho na ulafi wa madaraka, kuwindana ili kuangamizana kwa sababu za madaraka ni siasa. La hasha. Na mbaya zaidi tumeanishwa kuwa kupigania haki tunazostahili na kutaka tuongozwe na viongozi compitent ni siasa, na siasa ni jambo baya kama wewe siyo mwanasiasa.
 
Inaonekana aliewasikiliza wananchi na kusema haya ni miongoni mwa watu wema na wapenda haki
Ni jukumu la Makonda kufuatilia kwa undani badala ya kutoa maelekezo na majibu haraka hadharani

Kesi nyingi huwa ni za chuki na husda kwa hiyo viongozi wawe makini kutokuangukia kwenye mtego
Natumaini atapata haki yake na hata amuweke kuwa msaidizi wa msaidizi wake tena
Naona ajira nje nje sasa
 
Hao wananchi wana haraka ya nini?Anahojiwa hajahukumiwa.Ikiwa hana hatiia kwenye tuhuma hizo za kushiriki kuuza eneo la kijiji na sio rushwa ya milioni 1 ataachiwa.Ikiwa ameshiriki hatua za kisheria zitachukuliwa.
Wananchi hao walikuwepo kwenye mkutano na hakuna aliyepinga tuhuma hizo.
Mtendaji aliulizwa kwanini hakutangazia wananchi mkutano huo na hakuwa na majibu ya kuridhisha.
Kupelekwa Takukuru sio kuhukumiwa.
Kumuhoji mtu lazima umkamate na kumuweka jela??
 
Kinachosumbuwa Arusha ni siasa na chuki na sio kingine.
Siasa sio jambo baya, ni haki ya raia kushiriki katika harakati za kisiasa kadri inavyowapendeza bila kuvunja sheria yoyote.
 
Back
Top Bottom