Wananchi wa kata ya Bwawani Arusha waandamana kulazimisha TAKUKURU wamwachie Mtendaji Kata aliyewekwa Ndani na Makonda; wadai RC hasikilizi wananchi

Wananchi wa kata ya Bwawani Arusha waandamana kulazimisha TAKUKURU wamwachie Mtendaji Kata aliyewekwa Ndani na Makonda; wadai RC hasikilizi wananchi

Hao wananchi wana haraka ya nini?Anahojiwa hajahukumiwa.Ikiwa hana hatiia kwenye tuhuma hizo za kushiriki kuuza eneo la kijiji na sio rushwa ya milioni 1 ataachiwa.Ikiwa ameshiriki hatua za kisheria zitachukuliwa.
Wananchi hao walikuwepo kwenye mkutano na hakuna aliyepinga tuhuma hizo.
Mtendaji aliulizwa kwanini hakutangazia wananchi mkutano huo na hakuwa na majibu ya kuridhisha.
Kupelekwa Takukuru sio kuhukumiwa.
 
Inaonekana aliewasikiliza wananchi na kusema haya ni miongoni mwa watu wema na wapenda haki
Ni jukumu la Makonda kufuatilia kwa undani badala ya kutoa maelekezo na majibu haraka hadharani

Kesi nyingi huwa ni za chuki na husda kwa hiyo viongozi wawe makini kutokuangukia kwenye mtego
Natumaini atapata haki yake na hata amuweke kuwa msaidizi wa msaidizi wake tena
Naona ajira nje nje sasa
Haki gani hasa huyo Afisa Mtendaji Kata ataipata wakati amewekwa ndani mahabusu?? Kitendo tu Cha kumuweka ndani mahabusu tayari umeingilia haki zake na pia kuvunja haki yake ya kuwa huru uraiani. Je, atalipwa Fidia kwa huwa muda ambao atakuwa yupo kizuizini huko mahabusu???
 
Tuhuma za mtendaji zilitakiwa zianzie kwa wananchi na si ofisini kwa Makonda.
 
Siku chache baada ya RC Makonda kuelekeza TAKUKURU wamweke ndani Mtendaji Kata ya Bwawani na asipewe dhamana kwa tuhuma za kuchukua rushwa milioni moja; wananchi wa kati hiyo zaidi ya mia mbili wamekodi magari na kwenda ofisi za TAKUKURU kushinikiza mtendaji huyo aachiwe huru kwani mafisadi wakiongozwa na madiwani na viongozi wa CCM waliofisadi kata hiyo wameanza kutumia ulaghai kuwakandamiza wananchi.

Wananchi wamesema mtendaji huyo alipangiwa kufanya kazi kata hiyo mwaka 2019. Alipoanza kazi mashamba ya kijiji yalikuwa yanatumika na viongozi kulima na kujimilikisha kama ya kwao. Mtendaji aliwanyang'anya mashamba hayo viongozi akiwemo diwani na kuwapa wananchi jambo ambalo viongozi hao wa CCM walichukizwa nalo.

Wakati anapangwa kufanya kazi katika kata hiyo hakuna fedha iliyokuwa inakusanywa kama ushuru kutoka kwenye mali za kata; kwa sasa mashamba yanachangia zaidi ya milioni 30.

Amefanikisha kujenga kituo cha afya na shughuli za maendeleo zinaendelea. Aidha, wakati anaingia wanafunzi walikuwa wanapeleka mahindi na maharage kwa ajili ya chakula ila sasa hivi mtendaji huyo ametenga ekari 20 kwa ajili ya shule na kwa mwaka huu shule imevuna zaidi ya gunia 80 zinazotumika kulisha wanafunzi.

Kuhusu rushwa ya milioni moja inayodaiwa na Mkuu wa Mkoa, wananchi wamesema fedha hizo zilitolewa adharani na hazikuwahi kukabidhiwa kwa mtendaji badala yake zilielekezwa kununua vifaa vya ujenzi na kwamba Makonda alipaswa kuwahoji wananchi kuliko kutoka na taarifa ofisini kwake na kwenda kuwakamata watu wasio na hatia kwa maelekezo ya mafisadi wanaotumia mali za umma kuwaumiza viongozi wenye maono kama mtendaji.

Wananchi hao wameitaka TAKUKURU kufanya kazi kwa utaalamu badala ya kufanya kazi kisiasa. Wamehoji kama kweli kulikuwepo rushwa kwanini TAKUKURU haikuwahi kuchunguza badala yake inapokea maelekezo? Wamehoji kwanini TAKUKURU wameshindwa kufika kijijini kufanya mahojiano na wananchi badala yake wamejazana kumweka mahabusu mtendaji ambaye dhamana ni haki yake?

Mwisho, wananchi wanadai mambo aliyoyafanya mtendaji wa Bwawani yanastahili pongezi na siyo kuadhibiwa kama mkuu wa Mkoa anavyofanya. Kama mkuu wa mkoa ana vyombo alipaswa kubaini mapema kwamba viongozi wa CCM wa kata wanatumia ofisi yake kupambana na watendaji wa serikali wanaowatumikia wananchi kwa haki.
Wananchi au wewe ndio unataka
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Kumuhoji mtu lazima umkamate na kumuweka jela??
Unapotuhumiwa unawekwa mahabusu ili kuzuia usiingilie na kujaribu kuharibu ushahidi lakini inategemea na tuhuma zinazokukabili.Pia usisahau kuna haki ya dhamana kwa tuhuma ambazo unaweza kuwekewa dhamana.
 
Tuhuma za mtendaji zilitakiwa zianzie kwa wananchi na si ofisini kwa Makonda.
Zilianzia kwa wananchi kwenye mkutano wa kutatua kero na sio ofisini kwa Makonda. Get your facts right.Wacha kukurupuka
 
Unapotuhumiwa unawekwa mahabusu ili kuzuia usiingilie na kujaribu kuharibu ushahidi lakini inategemea na tuhuma zinazokukabili.Pia usisahau kuna haki ya dhamana kwa tuhuma ambazo unaweza kuwekewa dhamana.
Sheria za Tanzania zinataka mtu akikamatwa na polisi afikishwe mahakamani ndani ya masaa 48 na mahakama ndio inatakiwa itoe maamuzi kama aendelee kushikiliwa rumande au aachiwe kwa dhamana au bila dhamana, sio mkuu wa mkoa au wilaya na polisi wake wajiamulie tu kumuweka mtu ndani jela kadri wanavyoona wao inafaa.
 
Haki gani hasa huyo Afisa Mtendaji Kata ataipata wakati amewekwa ndani mahabusu?? Kitendo tu Cha kumuweka ndani mahabusu tayari umeingilia haki zake na pia kuvunja haki yake ya kuwa huru uraiani. Je, atalipwa Fidia kwa huwa muda ambao atakuwa yupo kizuizini huko mahabusu???
Ndio maana nikasema haya maamuzi ya kuyatoa mbele ya watu tena haraka ni ujinga na sio haki kabisa
Makonda kamuonea bila kuchunguza
Chawa hawa wabaya mno
 
Haki gani hasa huyo Afisa Mtendaji Kata ataipata wakati amewekwa ndani mahabusu?? Kitendo tu Cha kumuweka ndani mahabusu tayari umeingilia haki zake na pia kuvunja haki yake ya kuwa huru uraiani. Je, atalipwa Fidia kwa huwa muda ambao atakuwa yupo kizuizini huko mahabusu???
Hiyo assumption yako ni kwamba hana hatia.Well and good.Je kama tuhuma hizo ni za kweli kipi kifanyike?A coin has always two sides.
 
How do you make press conference and you don't know how to express. Haya mambo ya kutoa maamuzi yanahitaji uelewa wa hali ya juu sana na sio kukurupuka
 
Hiyo assumption yako ni kwamba hana hatia.Well and good.Je kama tuhuma hizo ni za kweli kipi kifanyike?The coin has always two sides.
Tumia kichwa chako kufikiria badala ya kubebea meno tu, anayeweza kuthibitisha hizo tuhuma kama ni kweli ni mahakama pekee, kuendelea kumuweka jela kabla mahakama haijazithibitisha ni ukiukwaji mkubwa wa haki yake ya kuwa raia huru uraiani.
 
Zilianzia kwa wananchi kwenye mkutano wa kutatua kero na sio ofisini kwa Makonda. Get your facts right.Wacha kukurupuka
Kama ni hivyo hawa wananchi waliokwenda Takukuru ni wa wapi! Inawezekana wale waliokwenda kwa Makonda walitengenezwa ili wamtie matatani.
 
Hiyo assumption yako ni kwamba hana hatia.Well and good.Je kama tuhuma hizo ni za kweli kipi kifanyike?A coin has always two sides.
Kwani Mahakama zipo ili kufanya kazi gani?
Je, Paul Makonda kama Mkuu wa Mkoa kazi yake ni kuthibitisha tuhuma kwa watu wanaotuhumiwa kwa makosa mbalimbali????

Inavyoonekana wewe ni 'mbumbumbu' kama alivyo huyo Makonda wako.
 
Siku chache baada ya RC Makonda kuelekeza TAKUKURU wamweke ndani Mtendaji Kata ya Bwawani na asipewe dhamana kwa tuhuma za kuchukua rushwa milioni moja; wananchi wa kati hiyo zaidi ya mia mbili wamekodi magari na kwenda ofisi za TAKUKURU kushinikiza mtendaji huyo aachiwe huru kwani mafisadi wakiongozwa na madiwani na viongozi wa CCM waliofisadi kata hiyo wameanza kutumia ulaghai kuwakandamiza wananchi.

Wananchi wamesema mtendaji huyo alipangiwa kufanya kazi kata hiyo mwaka 2019. Alipoanza kazi mashamba ya kijiji yalikuwa yanatumika na viongozi kulima na kujimilikisha kama ya kwao. Mtendaji aliwanyang'anya mashamba hayo viongozi akiwemo diwani na kuwapa wananchi jambo ambalo viongozi hao wa CCM walichukizwa nalo.

Wakati anapangwa kufanya kazi katika kata hiyo hakuna fedha iliyokuwa inakusanywa kama ushuru kutoka kwenye mali za kata; kwa sasa mashamba yanachangia zaidi ya milioni 30.

Amefanikisha kujenga kituo cha afya na shughuli za maendeleo zinaendelea. Aidha, wakati anaingia wanafunzi walikuwa wanapeleka mahindi na maharage kwa ajili ya chakula ila sasa hivi mtendaji huyo ametenga ekari 20 kwa ajili ya shule na kwa mwaka huu shule imevuna zaidi ya gunia 80 zinazotumika kulisha wanafunzi.

Kuhusu rushwa ya milioni moja inayodaiwa na Mkuu wa Mkoa, wananchi wamesema fedha hizo zilitolewa adharani na hazikuwahi kukabidhiwa kwa mtendaji badala yake zilielekezwa kununua vifaa vya ujenzi na kwamba Makonda alipaswa kuwahoji wananchi kuliko kutoka na taarifa ofisini kwake na kwenda kuwakamata watu wasio na hatia kwa maelekezo ya mafisadi wanaotumia mali za umma kuwaumiza viongozi wenye maono kama mtendaji.

Wananchi hao wameitaka TAKUKURU kufanya kazi kwa utaalamu badala ya kufanya kazi kisiasa. Wamehoji kama kweli kulikuwepo rushwa kwanini TAKUKURU haikuwahi kuchunguza badala yake inapokea maelekezo? Wamehoji kwanini TAKUKURU wameshindwa kufika kijijini kufanya mahojiano na wananchi badala yake wamejazana kumweka mahabusu mtendaji ambaye dhamana ni haki yake?

Mwisho, wananchi wanadai mambo aliyoyafanya mtendaji wa Bwawani yanastahili pongezi na siyo kuadhibiwa kama mkuu wa Mkoa anavyofanya. Kama mkuu wa mkoa ana vyombo alipaswa kubaini mapema kwamba viongozi wa CCM wa kata wanatumia ofisi yake kupambana na watendaji wa serikali wanaowatumikia wananchi kwa haki.
Hawa wananchi wapewe maua yao
 
Nchi inashangaza kiongozi atoke huko apelekwe Arusha , bora kuacha wan-Arush watafute kiongozi miongoni mwa jamii zao ndio tatizo mpaka mkurugenzi wa jiji ni mwizi.
 
Fi
Haki gani hasa huyo Afisa Mtendaji Kata ataipata wakati amewekwa ndani mahabusu?? Kitendo tu Cha kumuweka ndani mahabusu tayari umeingilia haki zake na pia kuvunja haki yake ya kuwa huru uraiani. Je, atalipwa Fidia kwa huwa muda ambao atakuwa yupo kizuizini huko mahabusu???
Fidia muhimu
 
Tumia kichwa chako kufikiria badala ya kubebea meno tu, anayeweza kuthibitisha hizo tuhuma kama ni kweli ni mahakama pekee, kuendelea kumuweka jela kabla mahakama haijazithibitisha ni ukiukwaji mkubwa wa haki yake ya kuwa raia huru uraiani.
Wewe ndio unatumia akili?Kabla ya Mahakama kuthibitisha kwamba mtu ana hatia au la si lazima kuwe na due process.
Polisi ndio wana kazi ya kuhifadhi watuhumiwa,wakili wa Serikali anapeleka kesi Mahakamani na Mahakama inaamua kama yuko guilty au la.
Unapotuhumiwa kijinai haki yako ya kuwa uraiani inakuwa sio haki tena mpaka upewe dhamana Polisi au Mahakamani baada ya kufikishwa huko
Wisdom is chasing you but you are always faster.
 
Wewe ndio unatumia akili?Kabla ya Mahakama kuthibitisha kwamba mtu ana hatia au la si lazima kuwe na due process.
Polisi ndio wana kazi ya kuhifadhi watuhumiwa,wakili wa Serikali anapeleka kesi Mahakamani na Mahakama inaamua kama yuko guilty au la.
Unapotuhumiwa kijinai haki yako ya kuwa uraiani inakuwa sio haki tena mpaka upewe dhamana Polisi au Mahakamani baada ya kufikishwa huko
Wisdom is chasing you but you are always faster.
Siyo kila tuhuma ya jinai basi mtuhumiwa ni lazima awekwe ndani mahabusu. It depends.

Isitoshe, dhamana ni haki yake ya msingi kupewa huyo Afisa aliyetuhumiwa. Hata aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Bw. Ditopile Mzuzuli alipewa dhamana na kuachiwa huru licha ya kwamba aliua mtu makusudi (dereva wa daladala) tena mchana kweupe huku abiria wake waliokuwepo kwenye hiyo daladala wakishuhudia alivyokuwa akiuawa huyo dereva.
 
Back
Top Bottom