TAFAKURI BAADA YA HABARI.
Mkemia na Upinzanium!
Mkemia mmoja nguli, PHD (Permanent Head Damage), alijimwambafy kwa wakemia wenzie mpaka wakampa ukuu wa kitengo!
Mara baada ya kushika ofisi alifanya mambo mengi makubwa ikiwa ni pamoja na kununua vinu vingi vya kuchakata madini. ... lakini kubwa zaidi ni pale alipoutangazia umma kuwa lile tatizo la muda mrefu la madini ya 'Mwambium' kuwa na kiasi kikubwa sana cha 'Upinzanium' yeye atalimaliza na si muda mrefu atapata pure 'MWAMBIUM', yaani 99.999% pure.
Wakemia wenzie walipomuambia 'MWAMBIUM' safi kiasi hicho ni hatari na kwamba kiasi fulani cha 'Upinzanium' kinatakiwa kibakie kubalance shobo akawaambia waache kuwashwa ... huku akiwauliza wao walifanya lipi la maana kipindi chao?
Hakuishia hapo, akawatimua mateknishani wawili waliomsaidia sana wakati akiusaka ukuu na kisha kumuajiri mwanasheria, bingwa wa kumsifia, ili awanyamazishe wakemia wenzie...!
Waskia sana ... kumbe mkemia alikuwa haijui vizuri 'MWAMBIUM', kwamba ikiwa safi sana na ukaitunza sehemu moja kuzidi uzito unaokubalika huwa inajilipua yenyewe bila shinikizo la nje (SPONTANEOUS REACTION)! Sasa maabara imelipuka na CHAIN REACTION inatishia kuangamiza kiwanda chote! [emoji848][emoji848][emoji848] ... ama kweli Kemia bila Fizikia ni Maumivu! ... na nshomile waliishasemaga:" "...yakwatilwa mugogo niwe mshuma! (aliyekutwa na mkungu wa ndizi ndiye mwizi!) CASE CLOSED!
KIBURI SI MAUNGWANA!
[emoji28]
[emoji109] [emoji111][emoji111][emoji111][emoji95]