Aaah umesahau, siyo kabla ya uhuru, ni kabla ya ujio wa Mjerumani...mnaojidanganya ni nyinyi mnaoamini kwamba miundombinu yote ya Kilimanjaro imejengwa na serikali baada ya uhuru.
..wilaya ya Same walikuwa na utaratibu wa wananchi kujitolea kufanya kazi za maendeleo unaitwa " msaragambo. "
..Uchimbaji wa barabara ya Same-Vudee kwa nguvu za wananchi ulimshangaza Mwalimu Nyerere mpaka akawapa jina wana Same kuwa ni " wachina wa Tanzania. "
Ndio maana nimekwambia huo ni uongo, kama ni kweli tuambie ni kijiji gani huko Mwanza wananchi waliojichanga kutengeneza barabara za mawe kijiji kizima?
Wewe unajua barabara za urefu wa km 72? Wape maua yao tu hao wachaga na wakristo wa huko Kilimanjaro.
Mkuu watu wanaaminishwa tu chuki dhidi ya mkoa wa K'njaro , hawafanyi hata ka utafiti kadogo..mnaojidanganya ni nyinyi mnaoamini kwamba miundombinu yote ya Kilimanjaro imejengwa na serikali baada ya uhuru.
..wilaya ya Same walikuwa na utaratibu wa wananchi kujitolea kufanya kazi za maendeleo unaitwa " msaragambo. "
..Uchimbaji wa barabara ya Same-Vudee kwa nguvu za wananchi ulimshangaza Mwalimu Nyerere mpaka akawapa jina wana Same kuwa ni " wachina wa Tanzania. "
Kaa apo usubiri kila kitu ufanyiwe na Serikali...Nyie ndio mnaoishi kwa shemeji zenu hadi utu uzimaWaige ufala? huu ni ufala mkubwa mno, pesa za kodi wanaagiza V8 Japani then za kukarabati Barabara hakuna, za kuwalipa Bongo Movie waende Korea zipo ila za Barabara hakuna. Za kugharamaikia kuendesha Ikulu mbili za Dar na Dodoma zipo ila za Barabara hakuna.
Za safari za nje zipo ila za Barabara hakuna.
Huu ni uzuzu yale yale ya kuchangishana kukimbiza ile kibatari.
Aaah umesahau, siyo kabla ya uhuru, ni kabla ya ujio wa Mjerumani.
Unafikiri ng'ombe na mbuzi wa;llipita wapi kama hakuna vijia vya kwendea milimani huko...sidhani kama ni kipindi cha Wajerumani, au kabla ya hapo.
Mkuu, kabla hujanijibu kwa kirefu namna hii, unapaswa uelewe tofauti kati ya tozo na kodi. Mimi nimeongelea tozo, wewe unaongelea mambo yanayofanywa na kodi.Tozo yako na kodi yako, inafanya mambo mengi ambayo kwa namna moja au nyingine wanainchi wanaila kwenye maeneo kama vile
1. Ujenzi wa barabara kiwango cha rami
2. Kupeleka fedha shuleni kulipia elimu kuanzia primary hadi advance
3. Kujenga vituo vya afya , zahanati, na hospitali na kununua vifaaa tiba na kutoa mishahara na motisha mbalimbali kwa watumishi wa kada ya afya, elimu, ulinzi na usalama n.k
4. Kununua zana za ulinzi na kulipa mishahara na motisha kwa watumishi wa eneo hilo.
5. Kutoa ajira na kupandisha madaraja kwa watumishi wapya na walioko kazini.
Hivyo jamaa yanguuu kodi na tozo tunazotozwa ni raia wenyewe ndio wanufaika kwa sehemu ya matumizi kama nilivyoorodhesha apo juuu.
Hivyo kwa mkutadha huo ni vyema wananchi kama hao walioamua kujenga barabara kwa nguvu zao, hiii ndio ujamaa na kujitegemea.
Nimekudadafulia namna tozo zinavyotumikaaaa. Bado kitu gani hujaelewaaaMkuu, kabla hujanijibu kwa kirefu namna hii, unapaswa uelewe tofauti kati ya tozo na kodi. Mimi nimeongelea tozo, wewe unaongelea mamno yanayofanywa na kodi.
Sasa kwa kiingereeza, tozo ni levy, wakati kodi ni tax. Hivi ni vitu viwili tofauti, na sheria za nchi yeyote zinasema hupaswi kutoza kodi ya kitu kile kile mara mbili. Kwa taarifa yako, ili kutovunja sheria, serikali ya CCM huwa inatoza watu kodi na tozo, na kusema hawavunji sheria! Kwa mfano ukinunua umeme Luku au airtime, unalipa kodi (VAT) na tozo (levy), halafu serikali inasema hatukutozi kodi mara mbili, na kodi yetu sio kubwa, huku wakijua wamei break mara mbili ili isionekane kubwa. Ni uongozi wa nchi wanaojua wananchi wake ni mbumbumbu ndio wanafanya vitu kama hivi na wananchi hawaji juu dhidi ya serikali kama wanavyofanya Kenya!
Sasa tozo za miamala ya fedha na simu ni kitu ambacho Samia kwa maneno yake mwenyewe alisema kitatumika kwa ajili ya zahanati na barabara vijijini. Na walipokuja kugundua tozo ziliingiza serikalini fedha nyingi sana kuliko walivyotarajia, wakaamua basi fedha za tozo ziingie kwenye matumizi ambayo yanapaswa kubebwa na kodi, na mengine ambayo sidhani hata kama yanapitishwa na Bunge. Na pia nina wasiwasi kama tozo zinahesabika kama sehemu ya makusanyo ya serikali ambayo yanapangiwa bajeti na Bunge. Tozo mara nyingi ndio fedha zinaliwa sana na viongozi mafisadi.
Ndio maana nikasema, kama tuliambiwa tukubali tozo ili zijenge barabara vijijini na zahanati, na ikaonekana fedha za tozo ni nyingi sana zaidi ya ilivyotarajiwa, kwa nini tuendelee kujitolea fedha kwa ajili ya vitu hivi? Hizo fedha za tozo siku hizi zinapelekwa wapi?
Bado huelewi tofauti ya kodi na tozo. Rudia kusoma nime editNimekudadafulia namna tozo zinavyotumikaaaa. Bado kitu gani hujaelewaaa
Changamoto ya ubovu wa miundombinu ya barabara katika eneo la Kiruweni, Kata ya Mwika Kusini, Wilaya ya Moshi, imewalazimu wananchi wa eneo hilo waishio maeneo mbalimbali nchini kuchangishana fedha na kuanza ujenzi wa barabara zenye urefu wa kilomita 72 kwa kiwango cha changarawe.
Eneo hilo ambalo wananchi wake wanajishughulisha na uzalishaji wa ndizi na kilimo cha mazao mbalimbali, limekuwa na changamoto kubwa ya miundombinu ya barabara.
Hali hii imewalazimisha kusafirisha mizigo kwa kichwa hadi sokoni, hivyo kushindwa kufikia ndoto zao za kujikwamua kiuchumi.
Chimbuko la wazo la ujenzi wa barabara lilianzia katika Usharika wa Kiruweni wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), baada ya mvua kubwa zilizonyesha mwishoni mwa Machi na Aprili, 2024.
Mvua hizo zimesababisha barabara hizo zishindwe kupitika kwa vyombo vya usafiri, zikiwamo pikipiki.
Akizungumza kuhusu ujenzi huo, Mchungaji Kiongozi wa Usharika wa Kiruweni, Joram Mamuya amesema barabara hizo zimefikia hatua mbaya na kufanya wananchi kushindwa kutumia vyombo vya usafiri na hivyo kulazimika kubeba mazao yao kichwani kuyapeleka sokoni, huku wakitembea umbali mrefu.