Pre GE2025 Wananchi wa Kilimanjaro wachangishana kurekebisha barabara mbovu yenye urefu wa kilomita 72

Pre GE2025 Wananchi wa Kilimanjaro wachangishana kurekebisha barabara mbovu yenye urefu wa kilomita 72

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
..mnaojidanganya ni nyinyi mnaoamini kwamba miundombinu yote ya Kilimanjaro imejengwa na serikali baada ya uhuru.

..wilaya ya Same walikuwa na utaratibu wa wananchi kujitolea kufanya kazi za maendeleo unaitwa " msaragambo. "

..Uchimbaji wa barabara ya Same-Vudee kwa nguvu za wananchi ulimshangaza Mwalimu Nyerere mpaka akawapa jina wana Same kuwa ni " wachina wa Tanzania. "
Aaah umesahau, siyo kabla ya uhuru, ni kabla ya ujio wa Mjerumani.
 
..mnaojidanganya ni nyinyi mnaoamini kwamba miundombinu yote ya Kilimanjaro imejengwa na serikali baada ya uhuru.

..wilaya ya Same walikuwa na utaratibu wa wananchi kujitolea kufanya kazi za maendeleo unaitwa " msaragambo. "

..Uchimbaji wa barabara ya Same-Vudee kwa nguvu za wananchi ulimshangaza Mwalimu Nyerere mpaka akawapa jina wana Same kuwa ni " wachina wa Tanzania. "
Mkuu watu wanaaminishwa tu chuki dhidi ya mkoa wa K'njaro , hawafanyi hata ka utafiti kadogo

Mtu aliyetengeneza ramani ya barabara ya Mwanga kwenda Milimani Ugweno na Usangi anajulikana.
Mtu huyo hakuwa na certificate lakini alifanya kazi katika serikali upande wa barabara zama hizo wakiitwa ''Com works' yaani common works au CW. Aliombwa na Machifu wa Ugweno na Usangi na akajulikana kama ''Soveya'
Watu hawakujua Soveya ni '' Surveyor'. Ukoo wake upo

Picha za Nyerere akiwa juu ya Land Rover za kueneza TANU Milimani Ugweno na Usangi Zipo na ni kabla ya Uhuru. Mwafrika wa kwanza kupeleka gari anajulikana '' Kajiru'' kama sitakosea kutoka kitabu cha Profesa na ilikuwa miaka ya 1950+

Wataalam wa Baruti na kuvunja miamba koo zao zipo na zinajulikana.

Ukienda Same kule Mbaga kule milimani utashangaa sana jinsi miamba ilivyovunjwa na nguvu ya umma ilivyojenga barabara na miundo mbinu nyingine.

Nimeona dispensary na ipo hadi leo ilijengwa 1905 kwa nguvu za Wananchi.

Zipo shule za Misheni na za Umma zikijulikana kama NA au native authority zipo zimejengwa kabla ya Uhuru

Nimetembea na kuishi sana kuanzi Nanjoka Tunduru hadi Nyakatende Musoma.
Naliendele Mtwara hadi Katoma Kagera.
Pangani Tanga hadi Ujiji Kigoma . Matema Mbeya Beach hadi Ikwiriri Pwani n.k.
Kidogobasi Ifakara hadi Bahi Dodoma. Matombo Morogoro hadi Isevya Tabora.
Ngaranairobi Arusha hadi Mpanda

Nimeona mazuri lakini mabaya pia! Wananchi hawawezi kufyeka barabara wanasubiri serikali

Jamani tuwape MAUA yao wananchi wa K'njaro, tuache wivu, Wazee wao waliwekeza katika Msaragambo

Kinachofanyika Kiruweni katika mada hii ni ''encore'' wao walianza kujiletea maendeleo siku nyingi
 
Waige ufala? huu ni ufala mkubwa mno, pesa za kodi wanaagiza V8 Japani then za kukarabati Barabara hakuna, za kuwalipa Bongo Movie waende Korea zipo ila za Barabara hakuna. Za kugharamaikia kuendesha Ikulu mbili za Dar na Dodoma zipo ila za Barabara hakuna.

Za safari za nje zipo ila za Barabara hakuna.

Huu ni uzuzu yale yale ya kuchangishana kukimbiza ile kibatari.
Kaa apo usubiri kila kitu ufanyiwe na Serikali...Nyie ndio mnaoishi kwa shemeji zenu hadi utu uzima
 
..sidhani kama ni kipindi cha Wajerumani, au kabla ya hapo.
Unafikiri ng'ombe na mbuzi wa;llipita wapi kama hakuna vijia vya kwendea milimani huko.

Mchaga akikwambia barabara miaka 60 nyuma elewa kuwa hicho ni kijia, siyo barabara.
 
Tozo yako na kodi yako, inafanya mambo mengi ambayo kwa namna moja au nyingine wanainchi wanaila kwenye maeneo kama vile
1. Ujenzi wa barabara kiwango cha rami
2. Kupeleka fedha shuleni kulipia elimu kuanzia primary hadi advance
3. Kujenga vituo vya afya , zahanati, na hospitali na kununua vifaaa tiba na kutoa mishahara na motisha mbalimbali kwa watumishi wa kada ya afya, elimu, ulinzi na usalama n.k
4. Kununua zana za ulinzi na kulipa mishahara na motisha kwa watumishi wa eneo hilo.
5. Kutoa ajira na kupandisha madaraja kwa watumishi wapya na walioko kazini.

Hivyo jamaa yanguuu kodi na tozo tunazotozwa ni raia wenyewe ndio wanufaika kwa sehemu ya matumizi kama nilivyoorodhesha apo juuu.
Hivyo kwa mkutadha huo ni vyema wananchi kama hao walioamua kujenga barabara kwa nguvu zao, hiii ndio ujamaa na kujitegemea.
Mkuu, kabla hujanijibu kwa kirefu namna hii, unapaswa uelewe tofauti kati ya tozo na kodi. Mimi nimeongelea tozo, wewe unaongelea mambo yanayofanywa na kodi.

Sasa kwa kiingereeza, tozo ni levy, wakati kodi ni tax. Hivi ni vitu viwili tofauti, na sheria za nchi yeyote zinasema hupaswi kutoza kodi ya kitu kile kile mara mbili. Kwa taarifa yako, ili kutovunja sheria, serikali ya CCM huwa inatoza watu kodi na tozo, na kusema hawavunji sheria! Kwa mfano ukinunua umeme Luku au airtime, unalipa kodi (VAT) na tozo (levy), halafu serikali inasema hatukutozi kodi mara mbili, na kodi yetu sio kubwa, huku wakijua wamei break mara mbili ili isionekane kubwa. Ni uongozi wa nchi wanaojua wananchi wake ni mbumbumbu ndio wanafanya vitu kama hivi na wananchi hawaji juu dhidi ya serikali kama wanavyofanya Kenya!

Tozo huwa zina makusudi na matumizi maalum, na zinafanyiwa kitu kinaitwa "ring-fencing". Kwa mfano, tozo kwenye LUKU (REA levy) inatakiwa ikaeneze umeme vijijini lakini serikali haipeleki hizo fedha huko. Tozo kwenye bei ya mafuta (road maintanance levy) inatakiwa itumike kurekebisha barabara na kuhakikisha hakuna mashimo barabarani lakini serikali haipeleki hizo fedha huko wanampa Mwigulu anunue ma-VX ya wake wa maraisi wastaafu kila baada ya miaka mitano sijui, au kupeana posho zisizo na mshiko.

Sasa tozo za miamala ya fedha na simu ni kitu ambacho Samia kwa maneno yake mwenyewe alisema kitatumika kwa ajili ya zahanati na barabara vijijini. Na walipokuja kugundua tozo ziliingiza serikalini fedha nyingi sana kuliko walivyotarajia, wakaamua basi fedha za tozo ziingie kwenye matumizi ambayo yanapaswa kubebwa na kodi, na mengine ambayo sidhani hata kama yanapitishwa na Bunge. Na pia nina wasiwasi kama tozo zinahesabika kama sehemu ya makusanyo ya serikali ambayo yanapangiwa bajeti na Bunge. Tozo mara nyingi ndio fedha zinaliwa sana na viongozi mafisadi.

Ndio maana nikasema, kama tuliambiwa tukubali tozo ili zijenge barabara vijijini na zahanati, na ikaonekana fedha za tozo ni nyingi sana zaidi ya ilivyotarajiwa, kwa nini tuendelee kujitolea fedha kwa ajili ya vitu hivi? Hizo fedha za tozo siku hizi zinapelekwa wapi?
 
Mkuu, kabla hujanijibu kwa kirefu namna hii, unapaswa uelewe tofauti kati ya tozo na kodi. Mimi nimeongelea tozo, wewe unaongelea mamno yanayofanywa na kodi.

Sasa kwa kiingereeza, tozo ni levy, wakati kodi ni tax. Hivi ni vitu viwili tofauti, na sheria za nchi yeyote zinasema hupaswi kutoza kodi ya kitu kile kile mara mbili. Kwa taarifa yako, ili kutovunja sheria, serikali ya CCM huwa inatoza watu kodi na tozo, na kusema hawavunji sheria! Kwa mfano ukinunua umeme Luku au airtime, unalipa kodi (VAT) na tozo (levy), halafu serikali inasema hatukutozi kodi mara mbili, na kodi yetu sio kubwa, huku wakijua wamei break mara mbili ili isionekane kubwa. Ni uongozi wa nchi wanaojua wananchi wake ni mbumbumbu ndio wanafanya vitu kama hivi na wananchi hawaji juu dhidi ya serikali kama wanavyofanya Kenya!

Sasa tozo za miamala ya fedha na simu ni kitu ambacho Samia kwa maneno yake mwenyewe alisema kitatumika kwa ajili ya zahanati na barabara vijijini. Na walipokuja kugundua tozo ziliingiza serikalini fedha nyingi sana kuliko walivyotarajia, wakaamua basi fedha za tozo ziingie kwenye matumizi ambayo yanapaswa kubebwa na kodi, na mengine ambayo sidhani hata kama yanapitishwa na Bunge. Na pia nina wasiwasi kama tozo zinahesabika kama sehemu ya makusanyo ya serikali ambayo yanapangiwa bajeti na Bunge. Tozo mara nyingi ndio fedha zinaliwa sana na viongozi mafisadi.

Ndio maana nikasema, kama tuliambiwa tukubali tozo ili zijenge barabara vijijini na zahanati, na ikaonekana fedha za tozo ni nyingi sana zaidi ya ilivyotarajiwa, kwa nini tuendelee kujitolea fedha kwa ajili ya vitu hivi? Hizo fedha za tozo siku hizi zinapelekwa wapi?
Nimekudadafulia namna tozo zinavyotumikaaaa. Bado kitu gani hujaelewaaa
 
Nimekudadafulia namna tozo zinavyotumikaaaa. Bado kitu gani hujaelewaaa
Bado huelewi tofauti ya kodi na tozo. Rudia kusoma nime edit

Haya hapa chini si matumizi ya tozo, ni matumizi ya kodi. Hapo ndipo unapokosea

1. Ujenzi wa barabara kiwango cha rami - inatumika kodi sio tozo
2. Kupeleka fedha shuleni kulipia elimu kuanzia primary hadi advance - inatumika kodi sio tozo
3. Kujenga hospitali na kununua vifaaa tiba na kutoa mishahara na motisha mbalimbali kwa watumishi wa kada ya afya, elimu, ulinzi na usalama n.k inatumika kodi sio tozo
4. Kununua zana za ulinzi na kulipa mishahara na motisha kwa watumishi wa eneo hilo - inatumika kodi sio tozo
5. Kutoa ajira na kupandisha madaraja kwa watumishi wapya na walioko kazi - inatumika kodi sio tozo
 

Changamoto ya ubovu wa miundombinu ya barabara katika eneo la Kiruweni, Kata ya Mwika Kusini, Wilaya ya Moshi, imewalazimu wananchi wa eneo hilo waishio maeneo mbalimbali nchini kuchangishana fedha na kuanza ujenzi wa barabara zenye urefu wa kilomita 72 kwa kiwango cha changarawe.

Eneo hilo ambalo wananchi wake wanajishughulisha na uzalishaji wa ndizi na kilimo cha mazao mbalimbali, limekuwa na changamoto kubwa ya miundombinu ya barabara.

Hali hii imewalazimisha kusafirisha mizigo kwa kichwa hadi sokoni, hivyo kushindwa kufikia ndoto zao za kujikwamua kiuchumi.

Chimbuko la wazo la ujenzi wa barabara lilianzia katika Usharika wa Kiruweni wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), baada ya mvua kubwa zilizonyesha mwishoni mwa Machi na Aprili, 2024.

Mvua hizo zimesababisha barabara hizo zishindwe kupitika kwa vyombo vya usafiri, zikiwamo pikipiki.

Akizungumza kuhusu ujenzi huo, Mchungaji Kiongozi wa Usharika wa Kiruweni, Joram Mamuya amesema barabara hizo zimefikia hatua mbaya na kufanya wananchi kushindwa kutumia vyombo vya usafiri na hivyo kulazimika kubeba mazao yao kichwani kuyapeleka sokoni, huku wakitembea umbali mrefu.

INASIKITISHA WALLAH.
 
Back
Top Bottom