Pre GE2025 Wananchi wa Kilimanjaro wachangishana kurekebisha barabara mbovu yenye urefu wa kilomita 72

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Ndugu yangu nimepita Kijijini kwetu hivi karibuni, hali ya barabara ni mbaya mno

Utasema hatukusanyi Kodi, ili hali Wilaya yetu ni Moja ya Wilaya 20 Bora zinazokusanya Kodi kubwa.

Tunasubiri mwakani 2025 tuwaondoe kupitia Boksi la Kura, maana utasema hatuna Mbunge wala wa kututetea 🙌
 
Unaweza kupumzika sasa mkuu.
Unaongea mambo ya kufikirika sana...
Kwamba at the moment mwenye shida ya barabara ni serikali au Wananchi?
Kwanini usiwasifie hao wananchi na kuilaum serikal ya eneo husika kutokutelekeza majukum yake.

Muathirika wa moja kwa moja wa miundombinu mibovu ni nani?
Wacha hizi siasa za kwenye egg shell...

Mimi nawapongeza hao wanachi kwa kazi nzuri na kujitambua...

Kutoka utumwani ni pamoja na kuweza kujitegemea kifikra...
Hapo hakuna siasa za uchawa ni kaz tu.
 
Ni ya kufikirika kwa Taifa lenye wajinga kama wewe, unazania ni kweli pesa hazipo? Narudia tena tuendelee na uzezeta make ni mtaji
 
Wachaga ndio walivo hawaingoji serikali
 
So swala ka kujitegemea liko kwa wananchi tu? Serikalini mbona wao wanaishi ki anasa? hizo pesa zinatoka wapi?
Na hao hao Raia wataimbiwa nyimbo walipe kodi zaidi na zaidi ili waletewe maendeleo, endeleeni na ujinga make ni mtaji
 
Hongera sana!
 
SEREKALI IONE AIBU, WANANCHI HAO NI WALIPA KODI KAMA WENGINE, WAMEANZA HATUA MOJA, SEREKALI IMALIZIE HATUA YA PILI, IWAPE LAMI (BITUMEN)
Iwe ni aina fulani ya ppp,
WATANZANIA WATAKAOONYESHA JUHUDI FULANI ZA KIMAENDELEO SEREKALI YETU IWE NA UTARATIBU WA KUWASHIKA MKONO WANANCHI HAO, ITAONGEZA BIDII NA KUHARAKISHA MAENDELEO YA TANZANIA YETU.
 
people must stop to pay taxes and use all that money to buils their own roads.
I agree that the government isn't doing much, if anything, to help our communities/towns

But consider this. The people in Kiruweni want the road fixed now because they know the government won't do it anytime soon.

Even though they are spending their own money instead of waiting for the government, it may seem like a loss because they're still paying taxes without getting the road fixed. However, in the long run it's a win for them.

The less we rely on the government, the more power we have.
 
Ujinga ni nini?
Kwamba serikal kuacha kujenga reli kunakuzuia kusafirisha mazao yako...? Au ujinga ni kutafuta njia mbadala?

You are so irrelevant
Nimekuuliza Kodi zinaenda wapi? Mbona Serijali isiyo kuwa na pesa tunaona kwa macho ni inavyo ishi kwa anasa?

Kuna siku kwenye hio Barabara utaenda msafara wa V8 kama 30 kwenda kuitazama na kuwapongeza wilio jitolea.
 
Wachaga hatujalala.

Kuchangishana kujenga barabara za vijiji hatujaanza leo.

Lyamungo - Kibosho road, sehemu kubwa ya hii barabara imejengwa kwa michango ya wananchi. Pia kuna sehemu nyingine nyingi wanafanya hivi.

Pia si kweli eti mkuu wa mkoa amewaamsha. Kwa hakika mkuu wa mkoa yeye ndiye anaamshwa.

Hapo hakuna cha mkono wa kinachoitwa serikali. Nguvu za wanakijiji hizo na ndugu wanaoishi mikoa mwingine lakini wanatoa hapo kijijini.

Kama hufahamu sasa fahamu.

 
Nimekuuliza Kodi zinaenda wapi? Mbona Serijali isiyo kuwa na pesa tunaona kwa macho ni inavyo ishi kwa anasa?

Kuna siku kwenye hio Barabara utaenda msafara wa V8 kama 30 kwenda kuitazama na kuwapongeza wilio jitolea.
Your point of Kodi and all those are valid,

Issue hapa ni kwamba wanachi wanataka barabara now, just that...

Hilo la kusubiri serikal wananchi wa Moshi wamewaachia wengine mkuu... hilo sio jambo la kupongezwa? wakae walie hamna barabara?
 
Mama yeye anakopa Kwa ajili ya matumbo ya Wahuni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…