Wananchi wa Niger waunga mkono mapinduzi ya kijeshi. Wanasisa wa Kiafrika wanakuwa vibaraka wa mabeberu na kuwasahau wananchi

Wananchi wa Niger waunga mkono mapinduzi ya kijeshi. Wanasisa wa Kiafrika wanakuwa vibaraka wa mabeberu na kuwasahau wananchi

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2015
Posts
13,897
Reaction score
18,477
Katika hali ya kawaida, ungetegemea wananchi kutokuunga mkono mapinduzi dhidi ya viongozi wao waliowachagua wenyewe.

Tatizo ni kwamba baada ya kuchaguliwa viongozi huamua kuwa vibaraka wa mabeberu wa nchi za magharibi na kuwasahau wananchi waliowaweka madarakani.

Sasa Rais aliyepinduliwa badala ya kutetewa na wananchi wake, anatetewa na mabeberu wa magharibi.

Ni aibu!!
 
Katika hali ya kawaida, ungetegemea wananchi kutokuunga mkono mapinduzi dhidi ya viongozi wao waliowachagua wenyewe!! Tatizo ni kwamba baada ya kuchaguliwa viongozi huamua kuwa vibaraka wa mabeberu wa nchi za magharibi na kuwasahau wananchi waliowaweka madarakani! Sasa Rais aliyepinduliwa badala ya kutetewa na wananchi wake, anatetewa na mabeberu wa magharibi!! Ni aibu!!

Hii inatakiwa kuwa wake-up call kwa viongozi wote wa Africa walioamua kuweka vichwa vyao kwenye Vyungu wakaacha wananchi wao kwenye lindi la Umasikini

Urithi wa Taifa unagawanywa Bure kwa Mzungu halafu mzawa na makodi kibao kwenye kila kitu anachofanya
Hata biashara, Unatozwa kodi kwa wazo tuu kabla hujalijaribu kama litakutoa

Tujifunze kwa Niger
Wazungu wanatutisha kuwa sisi sio kitu bila wao kumbe wao ndio sio lolote bila sisi Angalia France alivyofukuzwa Niger na west Africa in general anavyolia
Viongozi wetu waanze kuandaa Mikataba ambayo itadai 50/50 ya kile ambacho mzungu ana kihitaji zaidi toka kwetu

Sio anakuja anachukua makaa ya mawe

Gas , Madini Aina zote mpaka wanyama anatajirisha kwao halafu anakukopesha pesa Ile Ile ambayo alitakiwa kukupa kama share
Ukiwa Kwao watoto wao wanakuambia"rudini kwenu Africa dark continent" kumbe wao ndio walitakiwa kuondoka kwetu

Wanasahau kuwa Wakati wao wakila nyama mbichi na kuishi mapangoni, Africa tulisha Gundua moto na kuanza kula vya kupikwa Na Mataifa Tajiri kama Mali Etc au turudie kusoma Habari za Timbuktu, Mansa Musa Kan Kan, Biashara za Sofala nk

West Africa ndio Eneo pekee limekuwa la moto miaka yote naona Ile Arab springs ikija ukanda huu
Kitu ambacho Mkoloni wa Leo alijisahau ni kuwa waasisi wa mapinduzi haya wamepita kwenye vikosi vyao high level training
Hata Idd Amin

Kiongozi yeyote asie Jali masilahi ya Raia wake Hana haja ya kusalia madarakani anatakiwa kuondoka kwa njia yeyote Ile.

Mapinduzi ndio uelekeo wa sasa
Rais Utimize ahadi, Boresha maisha ya watu wako au Uondolewe.
 
Ni kosa kuunga mikono uongozi wa kijeshi, na watajilaumu sana baadaye, uongozi wa kijeshi huwa haukosolewi, sio kama hapo Bongo leo mnamsema mama Samia kwa issue ya bandari, mna uhuru wa kumkatalia, ingekua jeshi hamngesema chochote, jeshi lingewapa Waarabu bandari zote kibabe tu bila kukosolewa.

Na wala haitachukua muda kabla huyo kiongozi wa kijeshi hajaingizwa mkenge na wanaoiba raslimali za nchi, na siku akianza kuwaskliza, hakuna mwananchi atamkosoa.
 
Watawala wa nchi za ECOWAS wameingiwa na wasiwasi mkubwa kwa sababu yaliyotokea Niger, Burkina Faso, Guinea na kwengineko yanaweza yakawafikia wao. Ndio maana sasa wanawakimbilia mabwana zao wa Marekani na Ufaransa wawalinde wasipinduliwe nao. Ubeberu umekataliwa na wananchi wa Afrika magharibi
 
Mapinduzi sahihi na bora Afrika ni yale mapinduzi matukufu ya ZANZIBAR....

Baada ya mapinduzi hayo tukaasisi chama kiitwacho "MAPINDUZI"....

Hiki ndicho chama bora ambacho hakitoi upenyo wa MAPINDUZI YA KIJESHI.....

LIDUMU TAIFA LA JMT ,amen[emoji120]
 
Mapinduzi sahihi na bora Afrika ni yale mapinduzi matukufu ya ZANZIBAR....

Baada ya mapinduzi hayo tukaasisi chama kiitwacho "MAPINDUZI"....

Hiki ndicho chama bora ambacho hakitoi upenyo wa MAPINDUZI YA KIJESHI.....

LIDUMU TAIFA LA JMT ,amen[emoji120]
Endeleeni kuwaabudu mabeberu wa Kiarabu
 
Nina umri wa kutosha kuelewa kuwa 90% ya mapinduzi ya kijeshi huwa hayaleti maendeleo yoyote. Mengi huwa yana nguvu ya soda tu na baadaye huharibu nchi zao kwa kuondoa misingi ya utawala bora.

(1) Amin alipopindua Uganda, wanafunzi wa Makerere na umma mkubwa wa Kampala walifurahi na kuandamana kwa furaha kwa vile walimchukia Obote. Baada ya mwaka mmoja wakaanza kulia.

(2) Baada ya kuuwawa kwa Rais Shermake wa Somalia kwa sababu za kikabila kulitokea vurugu na hadi Siad Bare akaingilia kati kijeshi kuchukua madaraka. Matokeo yake Somalia imekuwa ni lawless state kwa zaidi ya miaka 50 sasa. Ni nchi ambayo watu wake ndio wakimbizi wengi duniani.

(3)Baada ya njaa ya Ethiopia ya mwaka 1974 ambapo mfalme Haile Selassie alikuwa akiishi maisha ya kifahari, jeshi lilimpindua na watu wengi walifurahi. Hata hivyo utawala wa kijeshi wa ethiopia uliirudisha nyuma sana ethipoia kiasi kuwa mpaka leo unajua jinsi waethiopia huwa wanashikwa wakikimbilia nchi nyinghine. Ni miaka ya hivi karibuni tu baada ya utawala wa kiraia kurudi ndipo Ethiopia imeanza kuimarika.

(4) Nigeria walilimpindua na kumwua aliyekuwa Waziri Mkuu Tafawa Balewa pamoja na wasaidizi wake Ahmadu Belo, Samuel Ankintola, Festos Okotie-Oboh. Kuna raia walifurahia mapinduzi hayo na kuna walioyapinga. Matokeo yake Nigeria ilivurumisha na vita ya wenyewe kwa wenyewe huko Biafra na kugeuka nchi yenye rushwa kwa muda mrefu sana hadi miaka ya hivi karibuni tu ndipo wameanza kustabilize na kurudia utawala wa kiraia.

(5) Chad

(6) Sudan
(7) Central African Republic
(7) Equatorial Guinea

Mifano ya kupinga mapinduzi ya kijeshi ipo mingi sana; labda uondoe yale ya Nasser, ingawa alifariki baada ya muda mfupi na hatujui nchi ingeendeleaje iwapo angekaa madarakani muda mrefu. Mtu mwingine labda ni Ghadaffi ingawa alikuwa anawapa raia wake vitu vya bure, hakujenga taifa imara kwa maana ya kuwa na one man rule. Baada ya kupinduliwa na yeye tunaijua Libya ikoje kwa vile watu wake wengi walikuwa hawakuandaliwa mabadiliko ya uongozi. Thomas Sankara alikuwa ameleta matumaini lakini naye alipinduliwa na kuuwawa baada bya muda mfupi na mwanajeshi mwenzie; matokeo yake tunaijua Burkina Faso ikoje hadi leo.
 
Nina umri wa kutosha kuelewa kuwa 90% ya mapinduzi ya kijeshi huwa hayaleti maendeleo yoyote. Mengi huwa yana nguvu ya soda tu na baadaye huharibu nchi zao kwa kuondoa misingi ya utawala bora.

(1) Amin alipopindua Uganda, wanafunzi wa Makerere na umma mkubwa wa Kampala walifurahi na kuandamana kwa furaha kwa vile walimchukia Obote. Baada ya mwaka mmoja wakaanza kulia.

(2) Baada ya kuuwawa kwa Rais Shermake wa Somalia kwa sababu za kikabila kulitokea vurugu na hadi Siad Bare akaingilia kati kijeshi kuchukua madaraka. Matokeo yake Somalia imekuwa ni lawless state kwa zaidi ya miaka 50 sasa. Ni nchi ambayo watu wake ndio wakimbizi wengi duniani.

(3)Baada ya njaa ya Ethiopia ya mwaka 1974 ambapo mfalme Haile Selassie alikuwa akiishi maisha ya kifahari, jeshi lilimpindua na watu wengi walifurahi. Hata hivyo utawala wa kijeshi wa ethiopia uliirudisha nyuma sana ethipoia kiasi kuwa mpaka leo unajua jinsi waethiopia huwa wanashikwa wakikimbilia nchi nyinghine. Ni miaka ya hivi karibuni tu baada ya utawala wa kiraia kurudi ndipo Ethiopia imeanza kuimarika.

(4) Nigeria walilimpindua na kumwua aliyekuwa Waziri Mkuu Tafawa Balewa pamoja na wasaidizi wake Ahmadu Belo, Samuel Ankintola, Festos Okotie-Oboh. Kuna raia walifurahia mapinduzi hayo na kuna walioyapinga. Matokeo yake Nigeria ilivurumisha na vita ya wenyewe kwa wenyewe huko Biafra na kugeuka nchi yenye rushwa kwa muda mrefu sana hadi miaka ya hivi karibuni tu ndipo wameanza kustabilize na kurudia utawala wa kiraia.

(5) Chad

(6) Sudan
(7) Central African Republic
(7) Equatorial Guinea

Mifano ya kupinga mapinduzi ya kijeshi ipo mingi sana; labda uondoe yale ya Nasser, ingawa alifariki baada ya muda mfupi na hatujui nchi ingeendeleaje iwapo angekaa madarakani muda mrefu. Mtu mwingine labda ni Ghadaffi ingawa alikuwa anawapa raia wake vitu vya bure, hakujenga taifa imara kwa maana ya kuwa na one man rule. Baada ya kupinduliwa na yeye tunaijua Libya ikoje kwa vile watu wake wengi walikuwa hawakuandaliwa mabadiliko ya uongozi. Thomas Sankara alikuwa ameleta matumaini lakini naye alipinduliwa na kuuwawa baada bya muda mfupi na mwanajeshi mwenzie; matokeo yake tunaijua Burkina Faso ikoje hadi leo.
Umri wako hauja kusaidia kitu maana sujaona gadafi gapo pia unafananisha mapinduzi yaliofanywa na uneducated na haya ya Sasa yanayofanywa na educated person? Unafananisha enzi Dunia IPO gizani na Sasa ambapo baada ya mapinduzi unaweza Kodi mpaka consultant wa kiulinzi achilia mbali wa kiuchumi loh
 
Katika hali ya kawaida, ungetegemea wananchi kutokuunga mkono mapinduzi dhidi ya viongozi wao waliowachagua wenyewe.

Tatizo ni kwamba baada ya kuchaguliwa viongozi huamua kuwa vibaraka wa mabeberu wa nchi za magharibi na kuwasahau wananchi waliowaweka madarakani.

Sasa Rais aliyepinduliwa badala ya kutetewa na wananchi wake, anatetewa na mabeberu wa magharibi.

Ni aibu!!
Laana tupu kwa viongozi.

Mtu anawaza kuiba mali za umma kwa ulafi kisha anataka aungwe mkono na wale wenzangu wa pangu pakavu tia mchuzi.


Kuna mataifa ya kiafrika mengine serikali na viongozi wao wamegeuka mbwa mwitu, yaani wao ni kutapanya mali, kodi za kikoloni, kuuza raslimali za umma kwa bei ya chenji, kutetea wezi wenzao, kutekeleza mipango miovu ya usitawi wa jamii ikiwemo utoaji wa elimu duni kwa wananchi wa kawaida.



Viongozi wanawabebesha wananchi mzigo mzito usiobebeka wa kulipia madeni ya vitu ambavyo havikufanyika au vimefanyika chini ya kiwango, mikataba ya hovyo et al.
 
Umri wako hauja kusaidia kitu maana sujaona gadafi gapo pia unafananisha mapinduzi yaliofanywa na uneducated na haya ya Sasa yanayofanywa na educated person? Unafananisha enzi Dunia IPO gizani na Sasa ambapo baada ya mapinduzi unaweza Kodi mpaka consultant wa kiulinzi achilia mbali wa kiuchumi loh
Kwa vile unasoma na mindest fulani huwezi kuelewa mambo kwani kama hata kuweza kusoma Ghadafi kweny post hiyo ni dhahiri hujui unachosma au unachofikiria. Kuhusu kuelimika, elewa kuwa hilo ni jamo relative sana na linategemea jamii husika. Tulipoata uhuru watu wenye digrii walikuwa hawachache sana, na baraza la mawaziri la nyerere halikuwa na graduate yeyote ispokuwa yeye mwenyewe; wengine wote walikuwa ni darasa la 12. 14 na diploma lakini waliongoza vizuri.

Kuongoza nchi hakuhitaji elimu kubwa sana ya darasni bali kunahitaji busara, ambayo mtu anaposhindwa kua mapinduzi yoyte hutenganisha watu basi busara yake inakuwa ni questionable sana. Mapinduzi ya kijehsi husababisha ukabila sana hasa katika nchi za kiafrika zenye makabila kibao..

Hata hivyo tambua pia kuwa hata kama hujali elimu zao za kijeshi walikuwa na elimu za kutosha za kiraia kuweza kururhusiwa kwenye vyuo vikubwa vya kijeshi kama Sandhurst. Hissene Hebre wa Chad alikuwa na degree ya political Science, Colonel Ojukwu alikuwa na Masters ya History, Mobutu alikuwa na diploma ya Accounting ila kwa vile hakupata kazi ya accounting wakati wa mkoloni akaamua kusomea journalism pia ambayo ndiyo aliyotumia kujipatia madaraka ya kisiasa.

Hata kama umri wangu haujanisaidia kitu, ni afadhali mimi ninajua mambo kuliko wewe mwenye akili ya kuku wa kienyeji unayekurupika hata kinyesi na kukila bila kutafuna.
 
Ni kosa kuunga mikono uongozi wa kijeshi, na watajilaumu sana baadaye, uongozi wa kijeshi huwa haukosolewi, sio kama hapo Bongo leo mnamsema mama Samia kwa issue ya bandari, mna uhuru wa kumkatalia, ingekua jeshi hamngesema chochote, jeshi lingewapa Waarabu bandari zote kibabe tu bila kukosolewa.

Na wala haitachukua muda kabla huyo kiongozi wa kijeshi hajaingizwa mkenge na wanaoiba raslimali za nchi, na siku akianza kuwaskliza, hakuna mwananchi atamkosoa.
Ukiona wananchi wanaunga mkono mapinduzi ya kijeshi ujue serikali ilishawatelekeza siku nyingi!! Watawala walishakuwa vibaraka wa mabeberu wa nchi za magharibi!! Watawala wanapokea rushwa halafu wanauza raslimali kwa bei ya kutupa!! Mabeberu hawana aibu, wako tayari kumpigania kibaraka wao kinyume na matakwa ya raia walio wengi, kwao hiyo ndiyo demokrasia wanayodai!! Najua MK254 wewe ni mshabiki wa mabeberu na hufumbia macho maovu yao yote!!
 
Laana tupu kwa viongozi.

Mtu anawaza kuiba mali za umma kwa ulafi kisha anataka aungwe mkono na wale wenzangu wa pangu pakavu tia mchuzi.


Kuna mataifa ya kiafrika mengine serikali na viongozi wao wamegeuka mbwa mwitu, yaani wao ni kutapanya mali, kodi za kikoloni, kuuza raslimali za umma kwa bei ya chenji, kutetea wezi wenzao, kutekeleza mipango miovu ya usitawi wa jamii ikiwemo utoaji wa elimu duni kwa wananchi wa kawaida.



Viongozi wanawabebesha wananchi mzigo mzito usiobebeka wa kulipia madeni ya vitu ambavyo havikufanyika au vimefanyika chini ya kiwango, mikataba ya hovyo et al.
Halafu nchi za magharibi ni wanafiki sana!! Hudai kutetea demokrasia sasa wanaona kabisa matakwa ya wananchi walio wengi lakini bado wanaamua kumpambania kibaraka wao. Demokrasia ni kufuata matakwa ya walio wengi, lakini hapo hilo watalifumbia macho!!
 
Nina umri wa kutosha kuelewa kuwa 90% ya mapinduzi ya kijeshi huwa hayaleti maendeleo yoyote. Mengi huwa yana nguvu ya soda tu na baadaye huharibu nchi zao kwa kuondoa misingi ya utawala bora.

(1) Amin alipopindua Uganda, wanafunzi wa Makerere na umma mkubwa wa Kampala walifurahi na kuandamana kwa furaha kwa vile walimchukia Obote. Baada ya mwaka mmoja wakaanza kulia.

(2) Baada ya kuuwawa kwa Rais Shermake wa Somalia kwa sababu za kikabila kulitokea vurugu na hadi Siad Bare akaingilia kati kijeshi kuchukua madaraka. Matokeo yake Somalia imekuwa ni lawless state kwa zaidi ya miaka 50 sasa. Ni nchi ambayo watu wake ndio wakimbizi wengi duniani.

(3)Baada ya njaa ya Ethiopia ya mwaka 1974 ambapo mfalme Haile Selassie alikuwa akiishi maisha ya kifahari, jeshi lilimpindua na watu wengi walifurahi. Hata hivyo utawala wa kijeshi wa ethiopia uliirudisha nyuma sana ethipoia kiasi kuwa mpaka leo unajua jinsi waethiopia huwa wanashikwa wakikimbilia nchi nyinghine. Ni miaka ya hivi karibuni tu baada ya utawala wa kiraia kurudi ndipo Ethiopia imeanza kuimarika.

(4) Nigeria walilimpindua na kumwua aliyekuwa Waziri Mkuu Tafawa Balewa pamoja na wasaidizi wake Ahmadu Belo, Samuel Ankintola, Festos Okotie-Oboh. Kuna raia walifurahia mapinduzi hayo na kuna walioyapinga. Matokeo yake Nigeria ilivurumisha na vita ya wenyewe kwa wenyewe huko Biafra na kugeuka nchi yenye rushwa kwa muda mrefu sana hadi miaka ya hivi karibuni tu ndipo wameanza kustabilize na kurudia utawala wa kiraia.

(5) Chad

(6) Sudan
(7) Central African Republic
(7) Equatorial Guinea

Mifano ya kupinga mapinduzi ya kijeshi ipo mingi sana; labda uondoe yale ya Nasser, ingawa alifariki baada ya muda mfupi na hatujui nchi ingeendeleaje iwapo angekaa madarakani muda mrefu. Mtu mwingine labda ni Ghadaffi ingawa alikuwa anawapa raia wake vitu vya bure, hakujenga taifa imara kwa maana ya kuwa na one man rule. Baada ya kupinduliwa na yeye tunaijua Libya ikoje kwa vile watu wake wengi walikuwa hawakuandaliwa mabadiliko ya uongozi. Thomas Sankara alikuwa ameleta matumaini lakini naye alipinduliwa na kuuwawa baada bya muda mfupi na mwanajeshi mwenzie; matokeo yake tunaijua Burkina Faso ikoje hadi leo.
Vp hapa jirani Rwanda kwa kagame?
 
Ukiona wananchi wanaunga mkono mapinduzi ya kijeshi ujue serikali ilishawatelekeza siku nyingi!! Watawala walishakuwa vibaraka wa mabeberu wa nchi za magharibi!! Watawala wanapokea rushwa halafu wanauza raslimali kwa bei ya kutupa!! Mabeberu hawana aibu, wako tayari kumpigania kibaraka wao kinyume na matakwa ya raia walio wengi, kwao hiyo ndiyo demokrasia wanayodai!! Najua MK254 wewe ni mshabiki wa mabeberu na hufumbia macho maovu yao yote!!

Kuchukua nchi kijeshi sio suluhu maana mwisho wa siku hata jeshi lenyewe linaongozwa na wachumia tumbo, fuatilia kwa makini viongozi waandamizi jeshini, wakiingizwa mfukoni kwa tamaa zao yanakua yake yale na tatizo hauwezi ukawakosoa.

Kimsingi ni kusisitiza utawala wa sheria na uwajibishanaji, hakuna beberu huja na kupora kwa nguvu, mnawapa nyie wenyewe kwa tamaa za wachache. Haitokuja niwalaumu hao mabeberu maana hawaibi au kuchukua kwa kutumia mabavu, kuanzia wazungu, Wachina na hata Waarabu hawa hawa mnaosema wanajichukulia bandari zenu, hakuna anayetumia mtutu.

Waafrika tujilaumu wenyewe, hebu angalia hii picha Lagos ilivyokua wakati wa utawala wa mzungu miaka ya 60


main-qimg-e3b041e2e8af618221131f998a12ea2d
 
Nina umri wa kutosha kuelewa kuwa 90% ya mapinduzi ya kijeshi huwa hayaleti maendeleo yoyote. Mengi huwa yana nguvu ya soda tu na baadaye huharibu nchi zao kwa kuondoa misingi ya utawala bora.

(1) Amin alipopindua Uganda, wanafunzi wa Makerere na umma mkubwa wa Kampala walifurahi na kuandamana kwa furaha kwa vile walimchukia Obote. Baada ya mwaka mmoja wakaanza kulia.

(2) Baada ya kuuwawa kwa Rais Shermake wa Somalia kwa sababu za kikabila kulitokea vurugu na hadi Siad Bare akaingilia kati kijeshi kuchukua madaraka. Matokeo yake Somalia imekuwa ni lawless state kwa zaidi ya miaka 50 sasa. Ni nchi ambayo watu wake ndio wakimbizi wengi duniani.

(3)Baada ya njaa ya Ethiopia ya mwaka 1974 ambapo mfalme Haile Selassie alikuwa akiishi maisha ya kifahari, jeshi lilimpindua na watu wengi walifurahi. Hata hivyo utawala wa kijeshi wa ethiopia uliirudisha nyuma sana ethipoia kiasi kuwa mpaka leo unajua jinsi waethiopia huwa wanashikwa wakikimbilia nchi nyinghine. Ni miaka ya hivi karibuni tu baada ya utawala wa kiraia kurudi ndipo Ethiopia imeanza kuimarika.

(4) Nigeria walilimpindua na kumwua aliyekuwa Waziri Mkuu Tafawa Balewa pamoja na wasaidizi wake Ahmadu Belo, Samuel Ankintola, Festos Okotie-Oboh. Kuna raia walifurahia mapinduzi hayo na kuna walioyapinga. Matokeo yake Nigeria ilivurumisha na vita ya wenyewe kwa wenyewe huko Biafra na kugeuka nchi yenye rushwa kwa muda mrefu sana hadi miaka ya hivi karibuni tu ndipo wameanza kustabilize na kurudia utawala wa kiraia.

(5) Chad

(6) Sudan
(7) Central African Republic
(7) Equatorial Guinea

Mifano ya kupinga mapinduzi ya kijeshi ipo mingi sana; labda uondoe yale ya Nasser, ingawa alifariki baada ya muda mfupi na hatujui nchi ingeendeleaje iwapo angekaa madarakani muda mrefu. Mtu mwingine labda ni Ghadaffi ingawa alikuwa anawapa raia wake vitu vya bure, hakujenga taifa imara kwa maana ya kuwa na one man rule. Baada ya kupinduliwa na yeye tunaijua Libya ikoje kwa vile watu wake wengi walikuwa hawakuandaliwa mabadiliko ya uongozi. Thomas Sankara alikuwa ameleta matumaini lakini naye alipinduliwa na kuuwawa baada bya muda mfupi na mwanajeshi mwenzie; matokeo yake tunaijua Burkina Faso ikoje hadi leo.
Mi nadhani ni kwasababu jumuia za kimataifa huzitenga nchi zilizopinduliwa kijeshi.
 
Katika hali ya kawaida, ungetegemea wananchi kutokuunga mkono mapinduzi dhidi ya viongozi wao waliowachagua wenyewe.

Tatizo ni kwamba baada ya kuchaguliwa viongozi huamua kuwa vibaraka wa mabeberu wa nchi za magharibi na kuwasahau wananchi waliowaweka madarakani.

Sasa Rais aliyepinduliwa badala ya kutetewa na wananchi wake, anatetewa na mabeberu wa magharibi.

Ni aibu!!
Kumbuka rais aliyepinduliwa aliekwa madarakani na demokrasia, sio kidikteta
 
Back
Top Bottom