Wananchi wa Niger waunga mkono mapinduzi ya kijeshi. Wanasisa wa Kiafrika wanakuwa vibaraka wa mabeberu na kuwasahau wananchi

Wananchi wa Niger waunga mkono mapinduzi ya kijeshi. Wanasisa wa Kiafrika wanakuwa vibaraka wa mabeberu na kuwasahau wananchi

Kuchukua nchi kijeshi sio suluhu maana mwisho wa siku hata jeshi lenyewe linaongozwa na wachumia tumbo, fuatilia kwa makini viongozi waandamizi jeshini, wakiingizwa mfukoni kwa tamaa zao yanakua yake yale na tatizo hauwezi ukawakosoa.

Kimsingi ni kusisitiza utawala wa sheria na uwajibishanaji, hakuna beberu huja na kupora kwa nguvu, mnawapa nyie wenyewe kwa tamaa za wachache. Haitokuja niwalaumu hao mabeberu maana hawaibi au kuchukua kwa kutumia mabavu, kuanzia wazungu, Wachina na hata Waarabu hawa hawa mnaosema wanajichukulia bandari zenu, hakuna anayetumia mtutu.

Waafrika tujilaumu wenyewe, hebu angalia hii picha Lagos ilivyokua wakati wa utawala wa mzungu miaka ya 60


main-qimg-e3b041e2e8af618221131f998a12ea2d
Usipokunywa chang'aa una point nzuri,Leo nimekuelewa[emoji13]
 
Nina umri wa kutosha kuelewa kuwa 90% ya mapinduzi ya kijeshi huwa hayaleti maendeleo yoyote. Mengi huwa yana nguvu ya soda tu na baadaye huharibu nchi zao kwa kuondoa misingi ya utawala bora.

(1) Amin alipopindua Uganda, wanafunzi wa Makerere na umma mkubwa wa Kampala walifurahi na kuandamana kwa furaha kwa vile walimchukia Obote. Baada ya mwaka mmoja wakaanza kulia.

(2) Baada ya kuuwawa kwa Rais Shermake wa Somalia kwa sababu za kikabila kulitokea vurugu na hadi Siad Bare akaingilia kati kijeshi kuchukua madaraka. Matokeo yake Somalia imekuwa ni lawless state kwa zaidi ya miaka 50 sasa. Ni nchi ambayo watu wake ndio wakimbizi wengi duniani.

(3)Baada ya njaa ya Ethiopia ya mwaka 1974 ambapo mfalme Haile Selassie alikuwa akiishi maisha ya kifahari, jeshi lilimpindua na watu wengi walifurahi. Hata hivyo utawala wa kijeshi wa ethiopia uliirudisha nyuma sana ethipoia kiasi kuwa mpaka leo unajua jinsi waethiopia huwa wanashikwa wakikimbilia nchi nyinghine. Ni miaka ya hivi karibuni tu baada ya utawala wa kiraia kurudi ndipo Ethiopia imeanza kuimarika.

(4) Nigeria walilimpindua na kumwua aliyekuwa Waziri Mkuu Tafawa Balewa pamoja na wasaidizi wake Ahmadu Belo, Samuel Ankintola, Festos Okotie-Oboh. Kuna raia walifurahia mapinduzi hayo na kuna walioyapinga. Matokeo yake Nigeria ilivurumisha na vita ya wenyewe kwa wenyewe huko Biafra na kugeuka nchi yenye rushwa kwa muda mrefu sana hadi miaka ya hivi karibuni tu ndipo wameanza kustabilize na kurudia utawala wa kiraia.

(5) Chad

(6) Sudan
(7) Central African Republic
(7) Equatorial Guinea

Mifano ya kupinga mapinduzi ya kijeshi ipo mingi sana; labda uondoe yale ya Nasser, ingawa alifariki baada ya muda mfupi na hatujui nchi ingeendeleaje iwapo angekaa madarakani muda mrefu. Mtu mwingine labda ni Ghadaffi ingawa alikuwa anawapa raia wake vitu vya bure, hakujenga taifa imara kwa maana ya kuwa na one man rule. Baada ya kupinduliwa na yeye tunaijua Libya ikoje kwa vile watu wake wengi walikuwa hawakuandaliwa mabadiliko ya uongozi. Thomas Sankara alikuwa ameleta matumaini lakini naye alipinduliwa na kuuwawa baada bya muda mfupi na mwanajeshi mwenzie; matokeo yake tunaijua Burkina Faso ikoje hadi leo.
Ahsante Mkuu....
Tujiulize who engineered all those coups?
Vipi kwa Nchi ambazo hazijaexperience mapinduzi, zina utofauti wowote na hizi zilizopitia tawala za Kijeshi?
Ukikaa vizuri utaona Kuwa nchi haziendelei sio kwa sababu ya Mapinduzi, ila kuna factor zingine pia.
 
Ahsante Mkuu....
Tujiulize who engineered all those coups?
Vipi kwa Nchi ambazo hazijaexperience mapinduzi, zina utofauti wowote na hizi zilizopitia tawala za Kijeshi?
Ukikaa vizuri utaona Kuwa nchi haziendelei sio kwa sababu ya Mapinduzi, ila kuna factor zingine pia.
NAKAZIA
 
Katika hali ya kawaida, ungetegemea wananchi kutokuunga mkono mapinduzi dhidi ya viongozi wao waliowachagua wenyewe.

Tatizo ni kwamba baada ya kuchaguliwa viongozi huamua kuwa vibaraka wa mabeberu wa nchi za magharibi na kuwasahau wananchi waliowaweka madarakani.

Sasa Rais aliyepinduliwa badala ya kutetewa na wananchi wake, anatetewa na mabeberu wa magharibi.

Ni aibu!!
Kawaida fisadi hutetewa na fisadi mwenzie😂
 
Watawala wa kiafrika bila kuwa na mfumo au kitu Cha kuwalazimisha wawatumikie wananchi wanajisahau sana, uchaguzi umeshindwa kwa sababu ni kitu Cha miaka mingi hivyo wakishaingia madarakani hawana hofu na uchaguzi Wanajua wataiba tu kura.
 
Niger kuunga au kutokuunga mkono inategemea ni kabila gani linaloshika madaraka.

Hakuna utaifa kuna ukabila.
 
Jeshi ni mali ya wananchi na always lipo sahihi.
Jeshi umtii raisi aliyepo madarakani lakin rais aliyepo madarakani asipowatii wananchi ni haki yake kupinduliwa
 
Nina umri wa kutosha kuelewa kuwa 90% ya mapinduzi ya kijeshi huwa hayaleti maendeleo yoyote. Mengi huwa yana nguvu ya soda tu na baadaye huharibu nchi zao kwa kuondoa misingi ya utawala bora.

(1) Amin alipopindua Uganda, wanafunzi wa Makerere na umma mkubwa wa Kampala walifurahi na kuandamana kwa furaha kwa vile walimchukia Obote. Baada ya mwaka mmoja wakaanza kulia.

(2) Baada ya kuuwawa kwa Rais Shermake wa Somalia kwa sababu za kikabila kulitokea vurugu na hadi Siad Bare akaingilia kati kijeshi kuchukua madaraka. Matokeo yake Somalia imekuwa ni lawless state kwa zaidi ya miaka 50 sasa. Ni nchi ambayo watu wake ndio wakimbizi wengi duniani.

(3)Baada ya njaa ya Ethiopia ya mwaka 1974 ambapo mfalme Haile Selassie alikuwa akiishi maisha ya kifahari, jeshi lilimpindua na watu wengi walifurahi. Hata hivyo utawala wa kijeshi wa ethiopia uliirudisha nyuma sana ethipoia kiasi kuwa mpaka leo unajua jinsi waethiopia huwa wanashikwa wakikimbilia nchi nyinghine. Ni miaka ya hivi karibuni tu baada ya utawala wa kiraia kurudi ndipo Ethiopia imeanza kuimarika.

(4) Nigeria walilimpindua na kumwua aliyekuwa Waziri Mkuu Tafawa Balewa pamoja na wasaidizi wake Ahmadu Belo, Samuel Ankintola, Festos Okotie-Oboh. Kuna raia walifurahia mapinduzi hayo na kuna walioyapinga. Matokeo yake Nigeria ilivurumisha na vita ya wenyewe kwa wenyewe huko Biafra na kugeuka nchi yenye rushwa kwa muda mrefu sana hadi miaka ya hivi karibuni tu ndipo wameanza kustabilize na kurudia utawala wa kiraia.

(5) Chad

(6) Sudan
(7) Central African Republic
(7) Equatorial Guinea

Mifano ya kupinga mapinduzi ya kijeshi ipo mingi sana; labda uondoe yale ya Nasser, ingawa alifariki baada ya muda mfupi na hatujui nchi ingeendeleaje iwapo angekaa madarakani muda mrefu. Mtu mwingine labda ni Ghadaffi ingawa alikuwa anawapa raia wake vitu vya bure, hakujenga taifa imara kwa maana ya kuwa na one man rule. Baada ya kupinduliwa na yeye tunaijua Libya ikoje kwa vile watu wake wengi walikuwa hawakuandaliwa mabadiliko ya uongozi. Thomas Sankara alikuwa ameleta matumaini lakini naye alipinduliwa na kuuwawa baada bya muda mfupi na mwanajeshi mwenzie; matokeo yake tunaijua Burkina Faso ikoje hadi leo.
Mtaandika mpaka herufi zote ziishe.... Mtaandika magazeti na mavitabu msipoangalia na kujitafuta ndio kitawakuta hichi .... Endeleeni tu kujipakulia minyama ...si mnakula asali...wenzenu huko wanakula mnafu na mchunga .....
 
Kiongozi yeyeto asiyejali maslai ya wananchi, mapinduzi ndio jibu sahihi kwake
 
Kwa nini wananchi washangilie kipinduliwa kwake badala ya kuwa naye bega Kwa bega... !!? Waliyemchagua DOMOcratically??!
Vi vil rais anakuwa madarakani halafu anafanya vibaya kama alivyokuwa jiwe lakini utaratibu wa kumuondoa kwa kura unakuwa pale pale sio kupinduliwa
 
Katika hali ya kawaida, ungetegemea wananchi kutokuunga mkono mapinduzi dhidi ya viongozi wao waliowachagua wenyewe.

Tatizo ni kwamba baada ya kuchaguliwa viongozi huamua kuwa vibaraka wa mabeberu wa nchi za magharibi na kuwasahau wananchi waliowaweka madarakani.

Sasa Rais aliyepinduliwa badala ya kutetewa na wananchi wake, anatetewa na mabeberu wa magharibi.

Ni aibu!!
Huyo Rais kama wanamuona mzuri Macron amkabidhi kiti chake awaongoze pale paris
 
Nina umri wa kutosha kuelewa kuwa 90% ya mapinduzi ya kijeshi huwa hayaleti maendeleo yoyote. Mengi huwa yana nguvu ya soda tu na baadaye huharibu nchi zao kwa kuondoa misingi ya utawala bora.

(1) Amin alipopindua Uganda, wanafunzi wa Makerere na umma mkubwa wa Kampala walifurahi na kuandamana kwa furaha kwa vile walimchukia Obote. Baada ya mwaka mmoja wakaanza kulia.

(2) Baada ya kuuwawa kwa Rais Shermake wa Somalia kwa sababu za kikabila kulitokea vurugu na hadi Siad Bare akaingilia kati kijeshi kuchukua madaraka. Matokeo yake Somalia imekuwa ni lawless state kwa zaidi ya miaka 50 sasa. Ni nchi ambayo watu wake ndio wakimbizi wengi duniani.

(3)Baada ya njaa ya Ethiopia ya mwaka 1974 ambapo mfalme Haile Selassie alikuwa akiishi maisha ya kifahari, jeshi lilimpindua na watu wengi walifurahi. Hata hivyo utawala wa kijeshi wa ethiopia uliirudisha nyuma sana ethipoia kiasi kuwa mpaka leo unajua jinsi waethiopia huwa wanashikwa wakikimbilia nchi nyinghine. Ni miaka ya hivi karibuni tu baada ya utawala wa kiraia kurudi ndipo Ethiopia imeanza kuimarika.

(4) Nigeria walilimpindua na kumwua aliyekuwa Waziri Mkuu Tafawa Balewa pamoja na wasaidizi wake Ahmadu Belo, Samuel Ankintola, Festos Okotie-Oboh. Kuna raia walifurahia mapinduzi hayo na kuna walioyapinga. Matokeo yake Nigeria ilivurumisha na vita ya wenyewe kwa wenyewe huko Biafra na kugeuka nchi yenye rushwa kwa muda mrefu sana hadi miaka ya hivi karibuni tu ndipo wameanza kustabilize na kurudia utawala wa kiraia.

(5) Chad

(6) Sudan
(7) Central African Republic
(7) Equatorial Guinea

Mifano ya kupinga mapinduzi ya kijeshi ipo mingi sana; labda uondoe yale ya Nasser, ingawa alifariki baada ya muda mfupi na hatujui nchi ingeendeleaje iwapo angekaa madarakani muda mrefu. Mtu mwingine labda ni Ghadaffi ingawa alikuwa anawapa raia wake vitu vya bure, hakujenga taifa imara kwa maana ya kuwa na one man rule. Baada ya kupinduliwa na yeye tunaijua Libya ikoje kwa vile watu wake wengi walikuwa hawakuandaliwa mabadiliko ya uongozi. Thomas Sankara alikuwa ameleta matumaini lakini naye alipinduliwa na kuuwawa baada bya muda mfupi na mwanajeshi mwenzie; matokeo yake tunaijua Burkina Faso ikoje hadi leo.
Mbona haujataji misri
Siku zote mifano mibaya ndo mnaitoa kuwatisha watu
 
Majirani msijisahau sana. Msijiamini sana .Maana mambo hubadilika muda wowote.
 
Kumbuka rais aliyepinduliwa aliekwa madarakani na demokrasia, sio kidikteta
Lakini baada ya kuwekwa madarakani akawageuka wananchi na kuamua kuwafurahisha mabeberu!!! Hao hao wananchi waliomchagua ndio wanafurahia yeye kupinduliwa!!! Demokrasia ni kukubaliana na matakwa ya wengi!!
 
Vi vil rais anakuwa madarakani halafu anafanya vibaya kama alivyokuwa jiwe lakini utaratibu wa kumuondoa kwa kura unakuwa pale pale sio kupinduliwa

Wewe unaamini matokeo ya uchaguzi wa kupiga kura barani Africa??

Ingekua kuna chaguzi huru na za haki basi wanajeshi wasingekua na haja za kupindua nchi.


Afrika hakuna uchaguzi huru.
 
Back
Top Bottom