Wananchi wa tabaka la chini wazidi kuonewa na umasikini uliokithiri, huku Viongozi wakiendelea kuishi kihafahari kupitia kodi za walala hoi

Wananchi wa tabaka la chini wazidi kuonewa na umasikini uliokithiri, huku Viongozi wakiendelea kuishi kihafahari kupitia kodi za walala hoi

Bila kichapo kutembea V8 zikawa hazipandiki hatuwezi heshimiana.


[emoji23][emoji23][emoji23] yani kinatakiwa kinuke mwanzo mwisho barabara ziwe hazipitiki ni kipigo tu. Uone kama hawajakaa kamati ya maridhiano
Na hapo ndio litakua suluhisho la kudumu
Hawatakuja kujisahau tena
 
Hakika mkuu, mimi nakula nashiba lakini naumia napoona wenzangu wana njaa najikuta machozi yanatoka lakini nashangaa aina ya viongozi wetu mbona hawana huruma, wanaendesha maV8 ikiwa watu hawana maji, chakula, vitu havishikiki wapo tu kama mazuzu.
Na wala hawajali kuhusu hilo ni ufala mno
 
Issue sio elimu yangu ata kama ni duni Lakini naona.

Mimi ningekuwa kiongozi nisingeweza kulala kwa amani kwenye geti la askari wakati mitaa michache na nyumba yangu:

Kuna mama anatandikwa na mumewe

Nipite ferry nione mtoto mdogo sijui analala wapi alawatiwe

Nimuone mtu anaangaika kuuza bidhaa nisitafute mbinu za kuakikisha anapata kula ya uhakika

Nione bidhaa zinapanda niache wakati najua wananchi maskini wanaumia.

Na mambo mengine nisikuongopee mimi kama Kilatha nchi kama hiyo ntapigana mpaka naingia kaburini.

Yaani sitoweza kulala kwa amani kama nipo poa. Na nikisema poa yangu ni hela ya kubadili mboga tu.

Especially kwa watoto wadogo yaani nione mtoto wa mchanga mpaka umri wa miaka 16 analala mtaani mjomba huo ugomvi wake auwezi kuwa mdogo kama nina nafasi; yaani mwili unanisisimuka serious nikifikiria how stupid and vulnerable people are at that age.

Labda mi mwenyewe ningekuwa muokota makopo inawezekana ningekuwa na changamoto zingine; lakini kiongozi siwezi vumilia miaka 800.
Mkuu hata wewe ukiwa kiongozi huwezi kuyatimiza hayo.
Mifumo ya duniani imewekwa na watu na imewapangia watu madaraja.
Kila mtu yupo kwenye daraja lake, kulihama unatakiwa ujitume.
Mifumo tumeirithi na wala hatuielewi inavyofanta kazi.
Viongozi wengi na watu wengi wa Africa hawana uwezo wa kuyatimiza hayo unayoyalalamikia hivyo jali bisiness zako.
Kumbuka kuna watu hizo hali wanaona ni halali kwao hata ukimpa milion 10 leo kesho unamkuta vile vile.
Maana ya maisha ni tofauti kwa kila mtu, kwa hio usijitie huzuni kwa jambo ambalo huwezi kamwe kulitatua, kama unataka kutatua anza kuwasaidia hao wanaokuzungika uone impact yake.
 
Mazingira ya tulipotokea yanachangia tunapoishia lakini kuna watu wana roho mbaya. Uwezi zuia tamaa za watu wote kwenye nchi ya watu takribani million 50-60 mtu anaekupa hiyo kazi anakuonea.

Lakini wewe kiongozi kwenye nchi ya watu maskini kwa mshahara wako na posho ni zaidi ya millioni kumi kwa mwezi lazima uwe na wasi na watu wako maskini.

Nyumba ghorofa bule

Watoto wako wanasoma private kwa gharama za walipa kodi

Na mambo mengine ya ovyo unayofaidi kwa kodi zao.

Sasa chukulia wewe umetoka familia maskini unaweza vipi kulala kwa amani; wakati umefika hapo kwa madai ya kusaidia watu maskini unasahau vipi ulipotoka.

Unajua uongozi ni dhamana hizi nchi za wenzetu awawezi kukuacha kama ugusi jamii.

Yaani mimi sio kiongozi lakini napata shida nikiona umaskini wa watu wengine mpaka mwili unanisisimuka na siishi kwa kodi zao.

Unakuwaje comfortable na watu maskini bei za bidhaa zikipanda, hao watu wakiwa hawana access na medical care, mazingira ya elimu ovyo.

Seriously mimi naishi kijijini ila siku niliyokuja mjini niliogopa na kuishi kwa kuumia sana mpaka kuna anasa kufanya naona aibu kwa hela niliyoitafuta mwenyewe kutoka kijijini.

Wewe Kiongozi una raha gani unaeishi kwa kodi za hawa watu bila ya mbinu za kuwatoa hao watu walipo.

Aiwezekani sio sawa hawa watu mnaowalelea kuwa viongozi. Aiwezekani mtu raia kama mimi unamuona unajisikia vibaya halafu kiongozi wake aone poa.

The woman has to go; kumvumilia huyu mama ni kiwango chetu cha upuuzi.
mkuu toka tupate uharo 1961 hakuna unafuu we umeona leo
 
Brother uongozi ni kitu kigumu sana na pia ni kitu kirahisi sana inategemea na vitu vingi ili kuwa rahisi au kuwa vigumu..

Africa na Tanzania, tunajikita sana kuwalaumu viongozi wetu lakini pia tunasahau maendeleo sio jambo la mchezo mchezo na linahitaji nguvu na akili za watu wooote. JE WATU WOTE WAKO TAYARI KUWEKEZA NGUVU NA AKILI ZAO KWA MUDA MREFU ILI MAENDELEO YAJE KWA MANUFAA YA VIZAZI VIJAVYO?..

Ulaya na America hasa USA hazikuendelea kwa sababu ya akili na nguvu ya mtu mmoja na bado ziaendelea pia sio kwa sababu na akili ya mtu mmoja bali ni KUJITOA (sucrifice ) ya watu wengi wenye lengo moja...

Historia ya Ulaya na USA kufikia maendeleo inapaswa kutupa somo kubwa sana WaAfrica kabla ya kuanza kulaumia wakati hata sisi tunaolaumu hatutimiza wajibu wetu..

JPM akiwa Rais alijaribu kuleta utawala wa kinyapara aka man to man (japo alikuwa na mapungufu yake) ili kila mtu sasa ashiliki kufanya kazi na kuwa na lengo moja kama Taifa, maendeleo maendeleo, kwa wakati huu WaAfrica wanahitaji ukatili ili wajenge nchi zao na then huko mbele woote watajifunza na kukaa kwenye mstari lakini ZILISIKIKA KELELE KILA KONA ZA NCHI NA DUNIA..

Samahani kama niko nje ya maada.
Well said bro [emoji122][emoji122][emoji122]
 
Brother uongozi ni kitu kigumu sana na pia ni kitu kirahisi sana inategemea na vitu vingi ili kuwa rahisi au kuwa vigumu..

Africa na Tanzania, tunajikita sana kuwalaumu viongozi wetu lakini pia tunasahau maendeleo sio jambo la mchezo mchezo na linahitaji nguvu na akili za watu wooote. JE WATU WOTE WAKO TAYARI KUWEKEZA NGUVU NA AKILI ZAO KWA MUDA MREFU ILI MAENDELEO YAJE KWA MANUFAA YA VIZAZI VIJAVYO?..

Ulaya na America hasa USA hazikuendelea kwa sababu ya akili na nguvu ya mtu mmoja na bado ziaendelea pia sio kwa sababu na akili ya mtu mmoja bali ni KUJITOA (sucrifice ) ya watu wengi wenye lengo moja...

Historia ya Ulaya na USA kufikia maendeleo inapaswa kutupa somo kubwa sana WaAfrica kabla ya kuanza kulaumia wakati hata sisi tunaolaumu hatutimiza wajibu wetu..

JPM akiwa Rais alijaribu kuleta utawala wa kinyapara aka man to man (japo alikuwa na mapungufu yake) ili kila mtu sasa ashiliki kufanya kazi na kuwa na lengo moja kama Taifa, maendeleo maendeleo, kwa wakati huu WaAfrica wanahitaji ukatili ili wajenge nchi zao na then huko mbele woote watajifunza na kukaa kwenye mstari lakini ZILISIKIKA KELELE KILA KONA ZA NCHI NA DUNIA..

Samahani kama niko nje ya maada.
Usifananishe ulaya, marekani na Tanzania. Wenzetu rule of law inafanya kazi kwelikweli haichagui huyu ni waziri au mbunge
Na wana taasisi imara ambazo zipo fair kwa kila mtu na sio km Tanzania raisi ndie anaeamua keki ya taifa apewe nani. na wote ni mashuhuda jinsi teuzi zinavyofanyika tanzania ni full kupeana vyeo

Leo hii unaweza kuwa na nia ya kuanzisha biashara fulani hpa Tanzania na ukashindwa kufanikisha kwa sababu tu huna connection na watu wazito wa nchi

Kaka yangu alishangahangaikia kibali cha kufungua bureau de change bot kwa miaka mitatu na hakufanikiwa .hii scenerio ingekuwa tofauti km angekuwa mtoto wa kigogo.
 
Hao wanaitwa elite class ni watu wasiozidi elfu hamsini na ndio wafaidika wakuu wa keki ya taifa

Wameshika nyanja zote za uchumi na kitovu chake kikuu ni kamati kuu ya chama cha mapinduzi.

Wote hawa hawana njaa na hakuna mtoto anaetoka kwenye hii class akasoma kayumba school au akakosa ajira akimaliza chuo na huwezi kukuta wanakaa sehemu ambazo umeme na maji ni changamoto

Na wameweka vikwazo kibao kwa watu wasiotoka kwenye class yao kujikwamua kiuchumi, ndio maana ukianzisha kabiashara kadogo unakutana na lundo la tozo za vibali.

Ndio maana wengine wameamua kuwa chawa tu ilimradi waingie kwenye hiyo class, mfano halisi ni bashite amejipenyeza penyeza mpaka kaingia ndani ya system na leo inamfaidisha kwa kumlinda kwa madudu aliyofanya
 
Issue sio elimu yangu ata kama ni duni Lakini naona.

Mimi ningekuwa kiongozi nisingeweza kulala kwa amani kwenye geti la askari wakati mitaa michache na nyumba yangu:

Kuna mama anatandikwa na mumewe

Nipite ferry nione mtoto mdogo sijui analala wapi alawatiwe

Nimuone mtu anaangaika kuuza bidhaa nisitafute mbinu za kuakikisha anapata kula ya uhakika

Nione bidhaa zinapanda niache wakati najua wananchi maskini wanaumia.

Na mambo mengine nisikuongopee mimi kama Kilatha nchi kama hiyo ntapigana mpaka naingia kaburini.

Yaani sitoweza kulala kwa amani kama nipo poa. Na nikisema poa yangu ni hela ya kubadili mboga tu.

Especially kwa watoto wadogo yaani nione mtoto wa mchanga mpaka umri wa miaka 16 analala mtaani mjomba huo ugomvi wake auwezi kuwa mdogo kama nina nafasi; yaani mwili unanisisimuka serious nikifikiria how stupid and vulnerable people are at that age.

Labda mi mwenyewe ningekuwa muokota makopo inawezekana ningekuwa na changamoto zingine; lakini kiongozi siwezi vumilia miaka 800.
Ukitaka kujua tabia ya mtu mpe vitu vitatu;
1.Mpe pesa
2.Mpe madaraka
3..Mpe uhuru
#Gombea uraisi kama sifa ,zina kuruhusu
 
Usifananishe ulaya, marekani na Tanzania. Wenzetu rule of law inafanya kazi kwelikweli haichagui huyu ni waziri au mbunge
Na wana taasisi imara ambazo zipo fair kwa kila mtu na sio km Tanzania raisi ndie anaeamua keki ya taifa apewe nani. na wote ni mashuhuda jinsi teuzi zinavyofanyika tanzania ni full kupeana vyeo

Leo hii unaweza kuwa na nia ya kuanzisha biashara fulani hpa Tanzania na ukashindwa kufanikisha kwa sababu tu huna connection na watu wazito wa nchi

Kaka yangu alishangahangaikia kibali cha kufungua bureau de change bot kwa miaka mitatu na hakufanikiwa .hii scenerio ingekuwa tofauti km angekuwa mtoto wa kigogo.

Brother, hiyo Ulaya na America zilikuwa shit kama unavyoona au zaidi ya ilivyo Tanzania...hayo unayoyasema ni kwa sasa wamestaarabika baada ya big struggle na watu wengi kuumia na kufa...

Primitive stage wameziishi sana huko nyuma... Tanzania kwa sasa ndio iko kwenye hizo stage za uprimitive, kifupi woote tu bado ni primitive na tunaishi kigangaganga tu...

Kutoka hapa lazima upitie stages kadhaa za mateso na maumivu makali..
 
Viongozi tunaowasema humu ni ndugu zetu, wajomba zetu, shangazi zetu nk, wakija kwenye vikao vyetu vya harusi na misiba wakitoa vitita vya hela tunashangilia na kupiga vigelegele huku tukijua hizo hela ni mali za watanzania masikini....tuanze kuwakataa huku kwenye ngazi ya familia tuje kwenye ngazi ya vitongoji, wilaya na mikoa..

Unakuta kiongozi anayesifika kwa uchafu na ujinga woote huko kwao ndio anapewa uchifu na kutukuzwa na jamii yake nakuitwa mtemi...halafu leo hii tunawalaumu hao hao viongozi...

kila mtu atimize majukumu yake, popote alipo apinge ujinga, kwa kukemea, hata kuuondoa na mikono yake....tusitoe rushwa, tuwapige mawe wakija vijijini na mijini kwetu, tuwapuuze, tusiwakaribishe kwenye nyumba zetu za ibada na jamii zetu...huko makanisani na misikitini watu hawa hawa tunaowaita wezi ndio tunapokea michango yao na kuwa wafadhili wetu...na wengine tunawapokea kwenye vyama vyetu na kuwaita makamanda.....
 
Viongozi wetu naona wanazidi kungaa tu na kuongezeka mashavu

Huku sisi tukizidi kupauka.
 
Hao wanaitwa elite class ni watu wasiozidi elfu hamsini na ndio wafaidika wakuu wa keki ya taifa

Wameshika nyanja zote za uchumi na kitovu chake kikuu ni kamati kuu ya chama cha mapinduzi.

Wote hawa hawana njaa na hakuna mtoto anaetoka kwenye hii class akasoma kayumba school au akakosa ajira akimaliza chuo na huwezi kukuta wanakaa sehemu ambazo umeme na maji ni changamoto

Na wameweka vikwazo kibao kwa watu wasiotoka kwenye class yao kujikwamua kiuchumi, ndio maana ukianzisha kabiashara kadogo unakutana na lundo la tozo za vibali.

Ndio maana wengine wameamua kuwa chawa tu ilimradi waingie kwenye hiyo class, mfano halisi ni bashite amejipenyeza penyeza mpaka kaingia ndani ya system na leo inamfaidisha kwa kumlinda kwa madudu aliyofanya
System haina mwenyewe. Hata hao wakubwa walikuwa chawa tu kabla ya wao pia kushikwa mkono.
 
Back
Top Bottom