KERO Wananchi wa Unyianga Singida na shida ya maji

KERO Wananchi wa Unyianga Singida na shida ya maji

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Mliogwa

Member
Joined
Jun 6, 2024
Posts
37
Reaction score
37
Sisi Wananchi wa Kijiji cha Unyianga kilichopo Kata ya Mtamaa, Manispaa ya Singida tunalia kukosa huduma ya maji safi, ni miaka kadhaa sasa tangu ‘Danganya Toto’ ya kujengewa Tenki la Maji na kuwekwa mabomba ifanyike lakini hadi leo hatujawahi ona maji yakitoka.

Tulijengewa tenki la maji na sehemu za mabomba ambayo maji ya kutoka kwenye tenki hilo yatakuwa yanatoka. Tenki hilo lililopo kwenye jiwe kubwa lilitupa matumaini makubwa ya kupata maji ya bomba ambayo tuliambiwa yangevutwa kutoka Mwankoko.

Hadi leo hii Desemba 2024, hatujaona maji tunaishia kunywa maji ya Kisima tu, mbaya zaidi mabomba hayo mengi yameibwa kwasababu yalionekana hayana kazi.

Mh. Mussa Sima, Mbunge wetu tunaomba uone aibu kidogo katika hili, unatusahau sana sisi huku Vijijini ambao ndio tunaoteseka zaidi na hii adha ya maji.

IMG-20241214-WA0023.jpg

IMG-20241214-WA0025.jpg

IMG-20241214-WA0020.jpg

IMG-20241210-WA0001.jpg

IMG-20241214-WA0013.jpg

IMG-20241214-WA0012.jpg

IMG-20241214-WA0010.jpg

IMG-20241214-WA0007.jpg

Majibu ya Mamlaka ~ SUWASA yafafanua hoja ya Mdau kuhusu uhaba wa maji Kata za Unyianga na Mtamaa Mkoani Singida
 
Back
Top Bottom