Wananchi Wanaozunguka Uwanja wa Ndege wa KIA Watakiwa kuwa na Subira ya Malipo ya Maeneo yao

Wananchi Wanaozunguka Uwanja wa Ndege wa KIA Watakiwa kuwa na Subira ya Malipo ya Maeneo yao

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

WANANCHI WANAOZUNGUKA UWANJA WA NDEGE WA KIA WATAKIWA KUWA NA SUBIRA YA MALIPO YAO

Serikali imewataka wananchi wanaozunguka uwanja wa ndege wa KIA kuwa na subra wakati wanasubiri malipo ya fidia ya maeneo yao kwani tayari imeshafanya tathmini na uthamini kwasasa wapo katika hatua za mwisho za utekelezaji wa adhima hiyo.

Wito huo umetolewa na Naibu Waziri Ujenzi na Uchukuzi Mhe. Atupele Mwakibete kufuatia swali la Kimkakati la Mbunge wa Jimbo la Hai Mhe. Saashisha Elinikyo Mafuwe June 20, 2023 bungeni jijini Dodoma la kutaka kujua lini zoezi la kulipa fidia kwa wananchi wanaozunguka uwanja huo litaanza ambapo ameuliza kuwa

“Wananchi wanaozunguka uwanja wa Ndege wa KIA wamekwisha kufanyiwa tathmini baadhi ya maeneo ambayo yanapaswa kupisha uwanja huo Je? ni lini Serikali itaanza kulipa wananchi hawa fidia?” Mhe. Mafuwe

“Serikali imeshafanya tathmini na uthamini, kinachoendelea sasa tumeshapeleka daftari kwa mthamini Mkuu wa serikali tayari kwaajili ya malipo na kwenda kulipeleka hazina hivyo niwaombe wananchi wawe watulivu wakati wanasubiri malipo yao” Mhe. Mwakibete
 

Attachments

  • vlcsnap-2023-06-20-03h04m53s207.png
    vlcsnap-2023-06-20-03h04m53s207.png
    155.2 KB · Views: 11
  • vlcsnap-2023-06-20-03h05m11s252.png
    vlcsnap-2023-06-20-03h05m11s252.png
    160.4 KB · Views: 14
Kijiografia uwanja wa KIA Umekaa eneo zuri sana kufanyiwa uboreshaji na pia kuongezwa runways. Pia eneo Hilo limekaa poa Sana kujengwa hoteli za kimataifa
 
Back
Top Bottom