Wananchi wawashambulia wabunge kufuatia adhabu kwa Askofu Gwajima na Silaa

Wananchi wawashambulia wabunge kufuatia adhabu kwa Askofu Gwajima na Silaa

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Joined
Jul 5, 2012
Posts
13,171
Reaction score
23,996
Ukichunguza kwa makini utagundua kuwa wananchi wengi hawakubaliani na serikali kwenye suala la chanjo za korona.

Huhitaji kufanya utafiti wa kina kujua ukweli wake kwa sababu utapata maoni ya wananchi kwenye video za YouTube katika channel kama Millard Ayo ambazo hazifungamani kisiasa katika kutoa habari.

Kama ukitaka kujua mawazo ya wananchi wengi angalia sehemu ya maoni hasa kama wachangiaji wamekuwa zaidi ya 800.

Wabunge waliochangia maazimio ya Kamati ya bunge ambao waliwashambulia Askofu Gwajima na Jerry Silaa wameshambulia sana na wananchi kwenye sehemu ya maoni.

Kwa taasisi yenye watu mwenye akili timamu na ambao wanatumia fikra timamu katika kuchambua maswala mbali mbali watayachukua maoni ya wananchi kama picha na kiakisi kwa yale wanayofanya kama bunge na serikali.

Mfano ni hii video ya YouTube ambayo baadhi ya wabunge walikuwa wanawashambulia kina Askofu Gwajima na Jerry Silaa ambayo imepata wachangiaji zaidi ya 1000. Soma maoni ya wachangiaji utagundua kinachoendelea katika fikra za watanzania wengi.

VIDEO:


Kwa maoni haya ya wananchi ni lazima Bunge na Serikali wajitathimini kwa yale wanayoyafanya kwa sababu inaonekana hayana maslahi kwa wananchi wengi!

Bunge na serikali wanatakiwa wajue Askofu Gwajima na Jerry Silaa ni sauti ya watanzania wengi walioko “nyikani”.

Serikali na bunge waache “kushupaza shingo” kama hawataki kuvunjika kwa sababu kwenye siasa hakuna watu wajinga na wasio wajinga bali kuna watu wanakubaliana na serikali au hawakubaliani na serikali.

Mmarekani aitwaye George Carlin aliwahi kusema, “Never underestimate the power of stupid people in large groups.”

Muda ni mwalimu wa kweli!
 
Kwahyo gwajua kutoa shtuma ambazo ameshindwa kuzithibitisha bado wananchi wengi wawashambulia wabunge? Ndio maana hata chini anaweza kuongoza hii nchi kwa aina hiyo ya wananchi

Wewe kuandika tu kiswahili ni majanga, unadhani unaweza kujua na kuchambua vizuri hoja za Askofu Gwajima kama “sauti ya nyikani” na kinachoendelea nchini!
 
Swala la chanjo Gwajima kapata uungaji mkono kwa wananchi wengi kwasababu kuu moja ni Legacy ya upumbavu wa Mwendazake kuwaongopea wananchi na kuwashawishi wananchi kuwa chanjo ni feki na kutumia kivuli Cha dini

Yaani legacy ya upumbavu halafu inaungwa mkono na wananchi wengi!

Una maana taifa lina wapumbavu wengi!

Kuita watu wengi ni wapumbavu ndio upumbavu wenyewe!

Hoja yako haina mantiki yoyote!
 
Kupata takwimu ya WANANCHI WENGI HUMU MITANDAONI kuko "biased" sana......

Juzi baada ya mh.Spika kuteleza ulimi na kutamka "jina la bwana Yesu badala ya bwana Yusufu" hukohuko ulipotuchukulia TAKWIMU zako ,HAO WANANCHI USEMAO NAO WALILIPUKA kuanza kumshambulia kwa KUKOSEA KULE ijapokuwa ULIMI HAUNA MFUPA NA YEYOTE ALIYEKUWA ANAFUATILIA VYEMA MTIRIRIKO WA MAELEZO YAKE alimuelewa vyema tu......

Hizo takwimu zako unazichukua kutokana na makundi yafuatayo:

1)Wasio na uelewa mpana juu ya nchi na taasisi ya bunge la JMT

2)Vijana wa upinzani wenye kupinga kila jambo linalofanywa na utawala ulio chini ya CCM

3)Vijana walio "desperate" kimalezi ,kifikra na kimtazamo wasiojishughulisha TAFAKURI zaidi ya "KULIPUKA" katika kila jambo kuntu"substantial"....


Binafsi ninaiunga mkono KAMATI YA BUNGE YA MAADILI ,HAKI NA KINGA kwa kuwahoji akina Askofu Gwajima na kutoa MAAZIMIO YALE....

#NchiHaiendeshwiKwaMihemkoKoko
#NchiKwanza
#SiempreJMT
 
Kumuamini Gwajima kwenye issue ya kisayansi wakati yeye ni mfufua misukule ni ujinga mtupu, hayo maoni ya kundi la wajinga mliowaathiri mind zao kwa ule upuuzi wenu sio sababu ya kujivunia kazi mliyofanya.
Ujinga uliopitiliza....
 
Kumuamini Gwajima kwenye issue ya kisayansi wakati yeye ni mfufua misukule ni ujinga mtupu, hayo maoni ya kundi la wajinga mliowaathiri mind zao kwa ule upuuzi wenu sio sababu ya kujivunia kazi mliyofanya.

Kwa hiyo unataka wakuamini wewe kwenye issue ya kisayansi wakati hujulikani!

Hakuna aliyelazimishwa kumuamini Askofu Gwajima bali nguvu ya hoja zake kama sehemu ya “sauti iliyoko nyikani”.
 
Swala la chanjo Gwajima kapata uungaji mkono kwa wananchi wengi kwasababu kuu moja ni Legacy ya upumbavu wa Mwendazake kuwaongopea wananchi na kuwashawishi wananchi kuwa chanjo ni feki na kutumia kivuli Cha dini
Ww mwenye akili hebu tuambie ukichanjwa huumwi corona ama huwezi ambukizwa korona ukijibu hilo basi nitaenda kuchanjwa
 
Mtamtea Gwajima kwa hoja zipi?

Alisema yafuatayo:-

1) Nitamfufua yule Mbunge mwanamke.....mpaka Leo holaaa.

2) Mimi ni mtu wa mbinguni na UVIKO hautaingia Tanzania.....holaaaaa

Sasa tunasubiri kuwaona MADAKTARI WETU WANAOTUHIMIZA CHANJO "wakianguka" mmoja baada ya mwingine kwa kuwa "mtu wa mbinguni" amewaombea LAANA YA KIFO kutoka kwa "Mungu anayemuabudu"

#NchiKwanza
#SiempreJMT
#VivaBungeLaJMT
#ChanjoNiBoraKulikoTiba
 
Kwahyo gwajua kutoa shtuma ambazo ameshindwa kuzithibitisha bado wananchi wengi wawashambulia wabunge? Ndio maana hata chini anaweza kuongoza hii nchi kwa aina hiyo ya wananchi
walioharibu ni hao akina Gwajima na Mollel walianza kwa kuisema vibaya chanjo lakini ndiyo hao hao leo wanasema ni nzuri, wananchi washike lipi?
 
Yaani legacy ya upumbavu halafu inaungwa mkono na wananchi wengi!

Una maana taifa lina wapumbavu wengi!

Kuita watu wengi ni wapumbavu ndio upumbavu wenyewe!

Hoja yako haina mantiki yoyote!
Muulize hiyo chanjo ukichanjwa huwezi ugua corona au ndo bado lazima uvae mibarakoa km kawa na kuugua corona kuko palepale .Mtu yeyote anae kimbilia kutukana huwa hana hoja.
 
Kumuamini Gwajima kwenye issue ya kisayansi wakati yeye ni mfufua misukule ni ujinga mtupu, hayo maoni ya kundi la wajinga mliowaathiri mind zao kwa ule upuuzi wenu sio sababu ya kujivunia kazi mliyofanya.
Kwahiyo watz watakuwa wengi sana ni wapumbavu?

Yani katika watu milion 60 hakuna werevu walau milion 1 wa kwenda kushambulia zile chanjo chap?

Yani hata wasomi wetu wa vyuo vikuu, madaktari, manesi, na watumishi wengine wa umma?

Chadema ina wafuasi manasema zaidi ya milion 7, nao siyo werevu kiasi cha kwenda kushambulia zile chanjo milion 1 chap ziishe?
 
Back
Top Bottom