Wanaochukia mapinduzi matukufu ya Zanzibar 1964 wana ajenda gani nyuma ya pazia?

Tatizo huyo mzee Okello ametengwa sana, hatajwi kwenye maskani yoyote hata ile maskani maarufu ya CUF pale stone town hawezi tajwa na ukimtaja unaeza fukuzwa kama mhaini wewe!
Today,
Kassim Hanga hatajwi katika mapinduzi ya Zanzibar.
 
Hawezi kukubali mzee wangu sababu tayari ana chuki na watu wa imani nyingine na wale waliowaondoa walowezi wa kiarabu zanzbar
Nelson,
Wewe ndiyo una chuki.
Angalia maneno unayotumia.

Ningekuwa nina chuki na Wakristo nisingeweza kuandika vitabu na vikasomwa na watu wengi.

Wala hapa JF nisingesomwa na watu wengi kama hivi.
Ningekuwa naeneza chuki katika jamii nisingepewa tuzo ya JF katika uandishi.


Tuzo kutoka Maxence Melo wa JF​
 
Zanzibar kulikuwa na mapinduzi au mauaji ya kimbari acheni uhuni Zanzibar kuna historia ya kipuuzi
Ya kumuondoa mlowezi wa kiarabu kama alivyofanya kwa babu zetu japo ukweli unafichwa!!!!Wangapi wanakumbuka mji wa zanzbar ulipowaka moto miaka ya 1800,s?????Waarabu walifanya nini wabantu weusi??????Au historia inafichwa makusudi kuwatetea walowezi wa kiarabu
 
Walowezi wa kiarabu ndiwo wanaokutawala hivi sasa 😝😝
 
Umekimbia hili Swali la Sheikh Mohammed Said

Nelson,
Huwa sikwepi swali.

Ubaguzi siku zote tunao katika jamii ila unapishana kwa viwango.
Mimi naweza nikakuuliza Tanzania Bara kuna ubaguzi?

Nini jibu lako?
 
Umekimbia hili Swali la Sheikh Mohammed Said

Nelson,
Huwa sikwepi swali.

Ubaguzi siku zote tunao katika jamii ila unapishana kwa viwango.
Mimi naweza nikakuuliza Tanzania Bara kuna ubaguzi?

Nini jibu lako?
Gavana,
Hili ni swali gumu sana kwao.
Kinachowashangaza ni hii subra yetu.
 
Hiyo picha haifanyi wewe kuondoa mtazamo wako dhidi ya watu wengine!!!Hasa wale waliopambania uhuru wa tanganyika na mapinduzi matukufu ya zanzbar 1964!!!Na pia haifichi hulka yako kwa watu wenye imani nyingine tofauti na yako!!!!Pia haiondoi huba yako kwa walowezi wa kiarabu na hizbu zanzbar!!!!
 
Nelson,
Huwa sikwepi swali.

Ubaguzi siku zote tunao katika jamii ila unapishana kwa viwango.
Mimi naweza nikakuuliza Tanzania Bara kuna ubaguzi?

Nini jibu lako?
Mzee wangu Kwahiyo walowezi wa kiarabu hawakua wabaguzi kabisa kwa wabantu!!!Huwezi amini wala kukubali hilo litakuumiza sababu una nasaba nao za kindugu na kiimani?????
 
Kwenu ni mapinduzi....
Kwao ni uvamizi na mauaji ya kimbari....

Duniani kote hakuna tabaka tawala ambalo linafurahia mapinduzi baada ya kuondolewa kinguvu kwenye nafasi yao ya kimamlaka. Mapinduzi ni sera yenye kuacha maumivu makali kwa jamii nzima.
Upo sahii Mkuu ndio maana waarabu,machotara na vibaraka wao wanapinga mapinduzi matukufu ua zanzbar wakitumia kisingizio cha unasaba wa kindugu na dini!!!
 
Tatizo huyo mzee Okello ametengwa sana, hatajwi kwenye maskani yoyote hata ile maskani maarufu ya CUF pale stone town hawezi tajwa na ukimtaja unaeza fukuzwa kama mhaini wewe!
Sass unategemea CUF(HIZBU) wamtaje mzee okelo???
 
Baharia...
Mdomo haumkatai bwana wake.

Wapemba na Waunguja wamekuwapo toka dunia ilipoumbwa na hayo anayosema Nyerere hayakutokea.
Hapa sasa mzee wangu unanidanganya!!!Wewe unajua dunia imeumbwa mwaka gani na visiwa hivyo vimeanza kukaliwa na watu mwaka gani???
 
Baharia...
Mdomo haumkatai bwana wake.

Wapemba na Waunguja wamekuwapo toka dunia ilipoumbwa na hayo anayosema Nyerere hayakutokea.
Hapa mzee saidi inaonyesha huijui historia ya dunia!!!!Wewe unajua historia ya visiwa hivyo wakazi wake wa kwanza ni watu wa nasaba gani?????Au unadhani historia imeanzia walipokuja waarabu pwani ya afrika mashariki???????Usiniangushe mzee saidi
 
Hii mind set ya Oman oriented anayo mzee wangu said mohamed kwa kisingizio cja unasaba wa kindugu na kidini
 
Ukweli lazima usemwe mzee na mabaya ya wadhalimu lazima yasemwe hata vipite vizazi 100!!!!!!Wabantu hatusahau
Nelson...
Ukweli haukataliki muhimu ni kuwa uwe kweli ni ukweli.

Lakini ni muhimu ujue kuwa kuna propaganda nyingi katika historia ya utumwa.

Unazungumza utumwa Zanzibar lakini umekuwa kimya kuhusu Transatlantic Slave Trade.

Yawezekana huna ujuzi wala maarifa ya historia hii.

Ninapokusoma jinsi unavyoandika na hata pale ninapokuongoza katika kanuni za uandishi unakuwa mkaidi na kurejea katika makosa yale yale basi najua kuwa hapa hakuna kitu.

Sultan kaondoka Zanzibar hana damu katika vidole vyake.
Jela za mateso na mauaji ziliingia Zanzibar baada ya mapinduzi.

Historia ya jela hizi Wazanzibari wote wangependa kusahau.

Wazanzibari wameukataa utawala ulioko madarakani toka 1964 kwenye sanduku la kura mara sita kuanzia 1995.

Nakupa yote haya kwa ushahidi na jambo la kusikitisha maraisi wote hao wameshindwa na mgombea yule yule mmoja.

Kilele cha fedheha hii ni pale baada ya kushindwa wa 2015.
Uchaguzi ule ukafutwa.

Kila uchaguzi damu ya Wazanzibari inamwagika.
Wewe unakuja na lugha "Wabantu hatusahau."

Wajue kwanza Wazanzibari ni nani.
Ndipo nikakuuliza nini tafsiri ya CCM kushindwa kila uchaguzi?

Wazanzibari wanayakataa mapinduzi?

Huenda hadi hapa tulipo hujanijua labda ungenijua ungechukua tahadhari lau kidogo.

Nimeshiriki katika uandishi wa historia ya mapinduzi nikiwa Mtafiti Msaidizi wa Dr. Harith Ghassany.

Mradi huu ulichukua miaka saba kukamilika.

Kitabu kutokana na utafiti huu kipo mtandaoni bure, "Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru."

Dr. Ghassany haitaji kuelezwa.

Nimealikwa Zanzibar mara nne kufanya mihadhara ya wazi kuhusu historia ya Zanzibar:

Zanzibar State University, Mwinyi Baraka Foundation, na mara mbili na Zanzibar Institute of Research and Public Policy (ZIRPP) kufanya pitio kwa vitabu viwili kuhusu historia ya mapinduzi.

Nimezungumza kuhusu kitabu cha Hashir Seif Hashir: "Mimi Umma Party na Mapinduzi ya Zanzibar," na kitabu cha Khamis Abdulla Ameir, "Maisha Yangu."


 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…