Wanaochukia mapinduzi matukufu ya Zanzibar 1964 wana ajenda gani nyuma ya pazia?

Wanaochukia mapinduzi matukufu ya Zanzibar 1964 wana ajenda gani nyuma ya pazia?

Nelson...
Sikulazimishi kuamini kitu chochote.

Huna elimu ya kusoma vitabu.

Umeandika sana hapa lakini unaandika mtindo unaitwa "barua" huna rejea yoyote.

Huenda hujui kama hapa uko katika ukumbi wa elimu na elimu yote duniani iko katika vitabu.

Na ni nani wanaandika vitabu?

Vitabu vinaandikwa na watu wenye maarifa.

Na maarifa yanapatikana vipi?

Maarifa yanapatikana kwa kusoma vitabu.

Hujamsoma, Hashil Seif wala Khamis Abdulla Ameir lakini uko hapa unajadili historia ya Zanzibar na Mohamed Said aliyetafiti historia ya Zanzibar na kuzungumza historia hiyo hadharani Zanzibar kwa kualikwa na wenyewe wasomi wa Kizanzibari.

PS: Acha !!! na ??? ukifanya hivyo katika unachoandika hii inakuonyesha wewe kuwa hujui sheria za uandishi.

Chuo chochote duniani mwaka wa kwanza wanasomesha namna ya kuandika.

Nadhani umenielewa.
Unataka nitoe rejea kwa waandishi wa mrengo wako haiwezekani!!Mfano hata wewe umeandika vitabu ila maarifa yako yana walakini kuhusu mambo mengi kiimani,kisiasa na kiuchumi!!!Vitabu ni mawazo ya muhusika na mapendeko yake bali mimi nazungumzia ukweli!!!Kuhusu uhandishi ndio maana kuna wahariri!!Usitoke nje ya mada
 
Sasa mzee wangu wewe ni mfuasi wa hizbu na chochote utakachoandika kuhusu Hanga ni kwa nia ya kuipaka matope ASP na SMZ!!!!Watu kusoma sio shida!!!Bali shida ni mrengo wa mwandishi na nia yake!!
Nilikuuliza hivi Hizbu iliundwa na Nani ? ASP lilikuwa Chama cha waafrika tu ,bila makabila mengine , unakimbia
 
Nelson,
Tufahamishe mitazamo ya Hanga tungependa kuelimika.

NB: Nimeandika makala ya Hanga na ilisomwa na watu 10,000 katika blog yangu: mohamedsaidsalum.blogspot.com


Ingia hapo fanya search.
Wewe ni mwanachama wa hizbu hakuna haja
 
Mkali...
Wazanzibari wanajulikana kwa mila, lafidh na utamaduni wao halikadhalika Watanganyika.

Isipokuwa wachache kutoka Pwani.
Upo sahihi, lkn sababu ya muungano hauoni ni nzito....ni kama ndoa Maana Tanganyika na Zanzibar ni kama mume na mke, je mume hapaswi kumfaham zaidi mke wake?

Tafadhali sheikh Said, heb tuelezee kwanini wazanzibari hawakudai uhuru kutoka utawala wa Sultan
 
Nelson...
Chuo Kikuu Cha Dar-es-Salaam sikuwa nafanya ubishi kwani si tabia yangu.

Chuo Kikuu nilikuwa nawashangaza walimu wangu kwa yale niliyokuwa nayajua katika historia ya Tanganyika.

Nakumbuka siku nilipomwambia mwalimu wangu kuwa Julius Nyerere hakuasisi TANU kama inavyoelzwa.

Kishindo chake kilikuwa kizito.
"Una hakika na unalosema?"

Nikamjibu mwalimu kuwa chama cha TANU kimetoka mbali sana toka 1929 babu zangu walipounda African Association.

Nikamweleza mwalimu hadi kufika kwa Nyerere Dar-es-Salaam na kukutana na Abdul Sykes.

Siku nyingine nikamshangaza mwalimu mwingine akisomesha historia ya vyama vya wafanyakazi.

Nikamwambia kuwa hicho kitabu anachotumia kina makosa.

Nikasema hakijamtaja babu yangu ambae maisha yake ni katika sehemu ya historia ya vyama vya wafanyakazi Tanganyika.

Darasa zima likaangua kicheko.
Walidhani nafanya maskhara.

Nikaeleza historia ya babu yangu Salum Abdallah akiwa muasisi wa TANU Tabora na muasisi wa Tanganyika Railways African Union (TRAU) na Kassanga Tumbo 1955.

Nikaeleza mgomo wa 1960 uliodumu siku 82.

Darasa zima lilikuwa kimya kama limemwagiwa maji baridi.

Siwezi kubishana kuhusu historia hizi kwani mimi ni sehemu ya historia hii.

Anaeleta ubishi ni yule ambae unaumia roho hataki kukubali kuwa historia yote hii ni ya wazalendo hao niliowataja na wao hawamo.


Kulia ni Kassanga Tumbo na Pembeni yake ni Salum Abdallah
Unakataa mzee wangu bali ulikua mwanafunzi usiyekua na nidhamu UDSM
 
Nelson...
Ukweli haukataliki muhimu ni kuwa uwe kweli ni ukweli.

Lakini ni muhimu ujue kuwa kuna propaganda nyingi katika historia ya utumwa.

Unazungumza utumwa Zanzibar lakini umekuwa kimya kuhusu Transatlantic Slave Trade.

Yawezekana huna ujuzi wala maarifa ya historia hii.

Ninapokusoma jinsi unavyoandika na hata pale ninapokuongoza katika kanuni za uandishi unakuwa mkaidi na kurejea katika makosa yale yale basi najua kuwa hapa hakuna kitu.

Sultan kaondoka Zanzibar hana damu katika vidole vyake.
Jela za mateso na mauaji ziliingia Zanzibar baada ya mapinduzi.

Historia ya jela hizi Wazanzibari wote wangependa kusahau.

Wazanzibari wameukataa utawala ulioko madarakani toka 1964 kwenye sanduku la kura mara sita kuanzia 1995.

Nakupa yote haya kwa ushahidi na jambo la kusikitisha maraisi wote hao wameshindwa na mgombea yule yule mmoja.

Kilele cha fedheha hii ni pale baada ya kushindwa wa 2015.
Uchaguzi ule ukafutwa.

Kila uchaguzi damu ya Wazanzibari inamwagika.
Wewe unakuja na lugha "Wabantu hatusahau."

Wajue kwanza Wazanzibari ni nani.
Ndipo nikakuuliza nini tafsiri ya CCM kushindwa kila uchaguzi?

Wazanzibari wanayakataa mapinduzi?

Huenda hadi hapa tulipo hujanijua labda ungenijua ungechukua tahadhari lau kidogo.

Nimeshiriki katika uandishi wa historia ya mapinduzi nikiwa Mtafiti Msaidizi wa Dr. Harith Ghassany.

Mradi huu ulichukua miaka saba kukamilika.

Kitabu kutokana na utafiti huu kipo mtandaoni bure, "Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru."

Dr. Ghassany haitaji kuelezwa.

Nimealikwa Zanzibar mara nne kufanya mihadhara ya wazi kuhusu historia ya Zanzibar:

Zanzibar State University, Mwinyi Baraka Foundation, na mara mbili na Zanzibar Institute of Research and Public Policy (ZIRPP) kufanya pitio kwa vitabu viwili kuhusu historia ya mapinduzi.

Nimezungumza kuhusu kitabu cha Hashir Seif Hashir: "Mimi Umma Party na Mapinduzi ya Zanzibar," na kitabu cha Khamis Abdulla Ameir, "Maisha Yangu."

137500652_876727469741299_9203091834821513436_n.jpg

136946625_876725959741450_7412006285885219892_n.jpg
Hiyo picha inanipa jibu kwanini unapinga mapinduzi matukufu
 
Upo sahihi, lkn sababu ya muungano hauoni ni nzito....ni kama ndoa Maana Tanganyika na Zanzibar ni kama mume na mke, je mume hapaswi kumfaham zaidi mke wake?

Tafadhali sheikh Said, heb tuelezee kwanini wazanzibari hawakudai uhuru kutoka utawala wa Sultan
Mzee wangu Said Mohammed hawezi kujibu hili swali!!!Hizbu walikua vibaraka wa masultani since chama hicho kimeanzishwa!!
 
Nitakufunza mzee wangu ila sasa uwe tayari kufundishika
Nelson...

Utanifariji sana kuwa leo na mimi nakaa kusomeshwa kwani nimezoea kusomesha wengine.

Nasubiri darasa lako kwa hamu.

Naamini kipo nitakachojifunza kutoka kwako:

PUBLICATIONS/RESEARCH PAPERS/ARTICLES
  1. The Life and Times of Abdulwahid Sykes 1924 –1968 The Untold Story of the Muslim Struggle against British Colonialism in Tanganyika, Minerva Press London, 1998 translated into Kiswahili as Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes 1924-1968 Historia Iliyofichwa Kuhusu Harakati za Waislam Dhidi ya Ukoloni wa Waingereza, Phoenix Publishers, Nairobi, 2002.
  2. The Torch on Kilimanjaro, Oxford University Press, Nairobi, 2006.
  3. Contributing author for an African anthology: The Mermaid of Msambweni and Other Stories, Oxford University Press 2007, Nairobi.
  4. Contributing author Dictionary of African Biography (DAB), Oxford University Press 2011, New York.
  5. Uamuzi wa Busara, Abantu Publications 2008, Dar es Salaam.
  6. Watu Mashuhuri Katika Uhuru wa Tanganyika No. 1, Ibn Hazm Media Centre, 2018, Dar es Salaam.
  7. Watu Mashuhuri Katika Uhuru wa Tanganyika No.2, Ibn Hazm Media Centre 2018, Dar es Salaam.
  8. Dar es Salaam na Wazalendo Wake Mashujaa Katika Kupigani Uhuru wa Tanganyika Ibn Hazm Media Centre 2018, Dar es Salaam.
  9. Watu Mashuhuri Katika Kuulingania Uislam Tanzania, Sheikh Ilunga, Ibn Hazm Media Centre 2018, Dar es Salaam.
  10. Dola, Kanisa na Tatizo la Udini Tanzania, Ibn Hazm Media Centre, 2018, Dar es Salaam.
  11. The School Trip to Zanzibar, Africa Proper Education Network 2020, Dar es Salaam.
  12. Rajabu Ibrahim Kirama, Jemadari wa Vita Kuwa Jemadari wa Uislam, Readit, 2020, Dar es Salaam.
  13. In Praise of Ancestors (1987) Africa Events (London).
  14. Abdulwahid Sykes: Founder of Political Movement (1988) Africa Events (London).
  15. Islam and Politics in Tanzania (1989) Al Haq International (Karachi).
  16. The Plight of Tanzanian Muslim (1993) Change (Dar es Salaam).
  17. Tanzania - The "Secular" Unsecular State (1995) Change (Dar es Salaam).
  18. The Question of Muslim Stagnation in Education in Tanzania - A Muslim Riddle (Paper presented at the Conference of the Global World of the Swahili. Intercultural Dialogue on the Indian Ocean Zanzibar, February 20 - 23, 2003).
  19. Islamic Education and Intellectualism in Eastern Africa ‘Themes from the Pulpit in Tanganyika (Tanzania Mainland) 1800 – 2000’ (Paper presented at International Symposium on Islamic Civilisation in Eastern Africa Kampala, Uganda organised by the Islamic Conference Research Centre for Islamic History, Art and Culture (IRCICA), Istanbul and the Islamic University in Uganda, Mbale December 15th – 17th 2003).
  20. Sheikh Hassan bin Ameir - The Moving Spirit of Muslim Emancipation in Tanganyika (1950 – 1968) (Paper presented at Youth Camp Organised by Zanzibar University, World Assembly of Muslim Youth (WAMY) and Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) 27th February – 4th March 2004).
  21. Islamic Movement and the Christian Lobby in Tanzania - the Experience of the late Prof. Kighoma Ali Malima (1938 – 1995) (Paper Presented to Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) Sokoine University of Agriculture (SUA) Morogoro 11th April 2004).
  22. Terrorism in East Africa the Tanzanian Experience (Paper Presented at the Conference on Islam, Terrorism and African Development University of Ibadan, Nigeria 8th - 10th February 2006).
  23. Al Marhum Sheikh Kassim bin Juma bin Khamis (1940 – 1994) and the Pork Riots of 1993. (Paper Presented at the Regional Conference on Islam in Eastern Africa: Islam Encounter with the Challenges of the 21st Century 1st - 3rd August 2006, Kenyatta University, Nairobi.
  24. Muslim Bible Scholars of Tanzania – The Legacy of Sheikh Ahmed Deedat (1918 – 2005) Paper Presented at the International Symposium on Islamic Civilisation in Southern Africa Organised by The Organisation of Islamic Conference Research Centre for Islamic History, Art and Culture (IRCICA) The National AWQAF Foundation of South Africa (AWQAF SA 1 – 3 September 2006 University of Johannesburg.
  25. Tanzania: A Nation Without Heroes Seminar Organised by IFRA French Institute for Research in Africa and BIEA British Institute in East Africa 23rd and 24th September 2013 at IFRA Nairobi.
  26. Awards: Several Awards
  27. Visiting Scholar: (2011).
  28. University of Iowa, Iowa City, USA.
  29. Northwestern University, Chicago, Illinois, USA.
  30. Zentrum Moderner Orient (ZMO), Berlin.
  31. OTHER COUNTRIES VISITED
  32. Zambia, Ethiopia, Great Britain, Swaziland, Msumbiji, Zimbabwe, Zambia, Sudan, Egypt, Saudi Arabia, United Arab Emirates, Oman, Yemen, Uganda, Switzerland, Iran, France, Netherlands, Turkey and Abu Dhabi.
 
Unataka nitoe rejea kwa waandishi wa mrengo wako haiwezekani!!Mfano hata wewe umeandika vitabu ila maarifa yako yana walakini kuhusu mambo mengi kiimani,kisiasa na kiuchumi!!!Vitabu ni mawazo ya muhusika na mapendeko yake bali mimi nazungumzia ukweli!!!Kuhusu uhandishi ndio maana kuna wahariri!!Usitoke nje ya mada
Nelson...
''uhandishi''
 
Mnachonga ngenga tu mmewahi kuona Video za vita vya mapinduzi hayo ya ZANZIBAR miaka ile nyie?!... wana sababu zao ndo mana hawataki, usilolijua ni sawa na usiku wa giza. Tuweke udini na urangi pembeni...,haki na maslahi kwanza!
 
Back
Top Bottom