Wanaochukia mapinduzi matukufu ya Zanzibar 1964 wana ajenda gani nyuma ya pazia?

Wanaochukia mapinduzi matukufu ya Zanzibar 1964 wana ajenda gani nyuma ya pazia?

Nelson...
Unanifurahisha sana.
Nyie watu hakika mahasidi sana.

Mwembechai 1984 asubuhi nakunywa chai asubuhi hotelini kwangu Madina Saudi Arabia ndipo niliposikia taarifa za Mwembechai.

Mabucha ya nguruwe 1993 kiasi cha kama wiki mbili nilikuwa Le Havre Ufaransa kisha nikaja Paris kutoka hapo nikaenda London na kutoka hapo Cardiff na kurejea Dar-es-Salaam.

Allah ndivyo alivyojaalia maisha yangu na nakueleza hapa lakini huna swali katika haya.

Moyo unakuchoma.

Unapendezwa na mabaya yanayoweza kuniangamiza mimi.

Unaumizwa na mambo ya kheri ambayo kila mzazi angependa mwanae ayapate.

Au unadhani maisha yangu ni ya kawaida mtu yeyote anaweza kuyapata?

Leo London, kesho Geneva, keshokutwa New York.

University of Johannesburg, Kenyatta University, University of Ibadan...

Unadhani mimi ni wa kukejeliwa?
Wewe huoni aibu kunivunjia adabu kwa maswali ya kipuuzi?
Kumbe ulikua Madina mzee wangu 1982 wakati wa vurugu za mwembechai basi ni vyema ukatujuza hizo taarifa zilikua zinasemaje mzee wangu.Na mabucha ya nguruwe 1993 kumbe ulikua ufaransa lakini pia unaweza kuniadithia ilikuaje mzee wangu sababu nina hakika ulipata taarifa kuhusu hilo.Ni suala la kheri kutuadithia kidogo
 
Nelson...
Nijibu nini?
Nikueleze nini?
Hapa nimeuliza kuhusu ubantu na wewe kuukimbia na kujinasibisha zaidi kinasaba kiimani na kindugu na watu wa mabara ya nje ya afrika ambao sio Wabantu.Kwanini umeukana ubantu mzee wangu na imani zake na tamaduni zake au huupendi ubantu???
 
Nelson...
Unanifurahisha sana.
Nyie watu hakika mahasidi sana.

Mwembechai 1984 asubuhi nakunywa chai asubuhi hotelini kwangu Madina Saudi Arabia ndipo niliposikia taarifa za Mwembechai.

Mabucha ya nguruwe 1993 kiasi cha kama wiki mbili nilikuwa Le Havre Ufaransa kisha nikaja Paris kutoka hapo nikaenda London na kutoka hapo Cardiff na kurejea Dar-es-Salaam.

Allah ndivyo alivyojaalia maisha yangu na nakueleza hapa lakini huna swali katika haya.

Moyo unakuchoma.

Unapendezwa na mabaya yanayoweza kuniangamiza mimi.

Unaumizwa na mambo ya kheri ambayo kila mzazi angependa mwanae ayapate.

Au unadhani maisha yangu ni ya kawaida mtu yeyote anaweza kuyapata?

Leo London, kesho Geneva, keshokutwa New York.

University of Johannesburg, Kenyatta University, University of Ibadan...

Unadhani mimi ni wa kukejeliwa?
Wewe huoni aibu kunivunjia adabu kwa maswali ya kipuuzi?
Natafuta elimu mzee wangu kutoka kwako maalim.Swali ni swali sio upuuzi
 
Nelson...
Unanifurahisha sana.
Nyie watu hakika mahasidi sana.

Mwembechai 1984 asubuhi nakunywa chai asubuhi hotelini kwangu Madina Saudi Arabia ndipo niliposikia taarifa za Mwembechai.

Mabucha ya nguruwe 1993 kiasi cha kama wiki mbili nilikuwa Le Havre Ufaransa kisha nikaja Paris kutoka hapo nikaenda London na kutoka hapo Cardiff na kurejea Dar-es-Salaam.

Allah ndivyo alivyojaalia maisha yangu na nakueleza hapa lakini huna swali katika haya.

Moyo unakuchoma.

Unapendezwa na mabaya yanayoweza kuniangamiza mimi.

Unaumizwa na mambo ya kheri ambayo kila mzazi angependa mwanae ayapate.

Au unadhani maisha yangu ni ya kawaida mtu yeyote anaweza kuyapata?

Leo London, kesho Geneva, keshokutwa New York.

University of Johannesburg, Kenyatta University, University of Ibadan...

Unadhani mimi ni wa kukejeliwa?
Wewe huoni aibu kunivunjia adabu kwa maswali ya kipuuzi?
Mzee wangu sasa mdogo wako nikiuuliza kuhusu safari zako za madina,geneva,paris,london,new york,stone town,pemba.Utasema nina maswali ya kipuuzi ndio maana sijakuuliza ila nitakuuliza wakati mwingine tukimaliza kuzungumzia mapinduzi matukufu ya zanzbar 1964
 
Mzee wangu sasa mdogo wako nikiuuliza kuhusu safari zako za madina,geneva,paris,london,new york,stone town,pemba.Utasema nina maswali ya kipuuzi ndio maana sijakuuliza ila nitakuuliza wakati mwingine tukimaliza kuzungumzia mapinduzi matukufu ya zanzbar 1964
Nelson...
Hakuweza kujizuia umetia vijembe.
Ukiniuliza New York na kwengineko ni Columbia University.

Unachokiona kwangu ni uvunjaji mabucha.

Tuendelee.
 
Natafuta elimu mzee wangu kutoka kwako maalim.Swali ni swali sio upuuzi
Nelson nyinyi hamtafuti elimu choyo kimetawala nyoyo zenu.

Ingekuwa ni suala la kusoma kutoka kwangu maswali yangekuwa kutoka ninayokuwekeeni hapa.

Wewe utaniuliza swali nikijibu utapinga nami jibu lamgu siku zote ni hakuna tatizo ikiwa huamini.

Umetaka waraka.
Nimekuwekea.

Ingekuwa mna nia njema yangekuja maswali mengine kabisa siyo kukataa.
 
Kumbe ulikua Madina mzee wangu 1982 wakati wa vurugu za mwembechai basi ni vyema ukatujuza hizo taarifa zilikua zinasemaje mzee wangu.Na mabucha ya nguruwe 1993 kumbe ulikua ufaransa lakini pia unaweza kuniadithia ilikuaje mzee wangu sababu nina hakika ulipata taarifa kuhusu hilo.Ni suala la kheri kutuadithia kidogo
Nelson...
Soma paper hii nilizungumza Kenyatta University, Nairobi 2006:

Screenshot_20230209-155849_Chrome.jpg
 
Mzee wangu sasa mdogo wako nikiuuliza kuhusu safari zako za madina,geneva,paris,london,new york,stone town,pemba.Utasema nina maswali ya kipuuzi ndio maana sijakuuliza ila nitakuuliza wakati mwingine tukimaliza kuzungumzia mapinduzi matukufu ya zanzbar 1964
Nelson...
Una sumu mbaya moyoni wa hasad.
Hakika wewe ni mtu adui.

Nililiona hili toka asubuhi.

Hukutegemea kama naweza kuchangia vizuri kwenye uzi uliofungua wa Israel.

Umeshangazwa na ninayojua kuhusu Middle East.

Umefanya kila aina ya vitimbi nisiwemo umeshindwa kunizuia.

Nimekuuliza kwa nini nialikwe mimi SUZA kuzungumza Vita Vya Hizbullah na Israel vya 2006 usialikwe wewe?

Nakuongezea kitu.

Baada ya mhadhara ule nilialikwa Centre for Foreign Relations.
 
Ukiwachunguza kwa kina utawaona ni watu ambao hawajasoma, kichwani wamekariri Qur'an tu, hawajuwi chochote kuhusu historia ya kisiwa chao. Watu dizaini hii ni wabaya kuishi nao, ni wanafiki mno.
Mbongo...
Hebu soma hayo hapo chini huenda ukapata kitu:

PITIO LA KITABU CHA KHAMIS ABDULLA AMEIR: ‘’MAISHA YANGU MIAKA MINANE NDANI YA BARAZA LA MAPINDUZI KHAINI AU MHANGA WA MAPINDUZI?’’

SEHEMU YA PILI

Huko nyuma nimeeleza kuwa nitaeleza ni waandishi gani walioandika vitabu vya kutisha. Katika makundi haya manne ni hili kundi la tatu la ‘’Waandishi Mavamizi,’’ ndiyo vitabu vyao vinatisha. Khamis Abdulla Ameir kitabu chake kinatisha lau kama haiwezekani kumjumuisha katika, ‘’Waandishi Mavamizi.’’

Khamis Abdullah Ameir kwa kuwa yeye ni mwanamapiduzi na kama mwanamapinduzi angependa mapinduzi yabaki siku zote, yawepo daima lakini mapinduzi ya neema yenye manufaa kwa Wazanzibari.

Kauli ya Khamis Abdulla Ameir iliyotawala kitabu hiki ni kuwa mapinduzi na muungano vimetokea kuwa janga kubwa kwa Wazanzibari.

Kwa ajili hii basi Khamis Abdulla Ameir amefungua mlango mpya wa kundi jipya la ‘’Waandishi Mtambuka,’’ anaeingia katika makundi yote ya waandishi.

Kinachomtofautisha yeye ni kule kusema kuwa mapinduzi ya Zanzibar ya 1964 hayajawanufaisha Wazanzibar bali yamewatwisha dhiki kubwa.

Kitabu ili kiwe kitabu ni lazima kiwe na elimu mpya ambayo haikuwapo kabla.

Vitabu vingi vilivyoandikwa kuhusu harakati za kudai uhuru wa Zanzibar vimepita kijuujuu katika kueleza mchango wa vyama vya wafanyakazi katika kupigania uhuru wa Zanzibar.

Msimamo wa Khamis Abdulla Ameir ni kuwa wakulima na wafanyakazi wawe ndiyo msingi wa mapinduzi na maendeleo ya Zanzibar.

Katika kitabu hiki Khamis Abdulla Ameir anaeleza mtanziko uliokuwapo baina ya vyama vya wafanyakazi vilivyokuwa vinaunga mkono ASP na ZNP.

Wakati ZNP ilikuwa imejikita katika kudai uhuru, ASP ilikuwa na msimamo tofauti wa kuukataa uhuru hadi pale Wazanzibar watakapokuwa wameelimika vya kutosha.

ASP ikiamini kuwa kulikuwa na Wazanzibar ambao walibaguliwa katika elimu. Wazanzibari gani walibaguliwa na Wazanzibari gani waliokuwa wakibagua?

Khamis Abdulla Ameir hakika ni mwandishi mgumu na jasiri.

Kwa ajili hii inahitaji mtu jasiri pia kufanya pitio la kitabu chake.

Katika dibaji ya kitabu hiki Ahmed Rajab anamueleza Khamis Abdulla Ameir kuwa ni mtu asiyesema, mtu mkimya.

Hili mimi nimeliandika katika mitandao ya kijamii niliposikia kuwa Khamis Abdulla Ameir ameandika kitabu.

Mimi niliyasema maneno hayo kwa kuzungumza na yeye kwa muda mfupi sana siku nilipokutana na mwandishi.

Muda wote mimi ndiye nilikuwa nazungumza yeye ananisikiliza na kutabasamu.

Hasemi ila maneno machache kitu nadra kwa wanasiasa.

Nilifurahi kuwa tathmini yangu ya Khamis Abdulla Ameir ilikuwa sawa kabisa.

Imekuwaje mtu asiyesema kasema sana katika kitabu chake?

Au ndiyo kile kisa cha bubu kusema kwa ajili ya uchungu wa mwanae?

Kitabu hiki ni kitabu cha kasi ni kitabu ambacho msomaji atajihisi yuko kwenye chombo kinachokwenda kwa mwendo mkali sana na kinaposimama kwenye kituo kimoja hakikawii haraka kinaondoka kwenda kituo kingine.

Mara yangu ya kwanza kumsikia Khamis Abdulla Ameir ilikuwa kutoka kwa Ahmed Rajab ambae aliniandikia na kunieleza historia yake akanitajia lakabu yake, ‘’Theoretician,’’ ambayo sikupata kuisikia kabla.

Ahmed Rajab alikuwa ananitahadharisha kuwa Khamis Abdulla Ameir ni mtu muhimu sana katika historia ya mapinduzi ya Zanzibar.

Wakati ule nilikuwa naandika pitio la kitabu cha Hashil Seif, ‘’Mimi Umma Party na Mapinduzi ya Zanzibar.’’

Kalamu ya Khamis Abdulla Ameir haina simile si kwa kwa kuhadithia matendo yatishayo yaliyotendeka Zanzibar wala kwa uchaguzi wa lipi aliseme na lipi aliache.

Mwandishi hakujifanyia uhariri yeye mwenyewe na inaelekea mchapaji na yeye hakuona sababu ya kuhangaika na mkasi wake wa kukata karatasi zenye yale yaogopwayo kusemwa khasa hadharani.

Nina hakika kabisa mkasi haukuwa katika zana zake za mhariri wa kitabu hiki.

Nimedokezwa kuwa wachaji wa ndani walikiogopa kitabu hiki.

Hili msomaji ataliona mapema kabisa mwanzo wa kitabu.

Mhariri alimwachia mwandishi uwanja wote atambe apendavyo.

Khamis Abdulla Ameir hakujali ikiwa anaemweleza yu hai au kafa, mtu mkubwa wa cheo au raia wa kawaida.

Mwandishi hakugeuza shingo yake kuangalia nyuma au kufikiria vipi ataonekana au kesho yake itakuwaje.

Khamis Abdulla Ameir amenyanyua shingo yake juu anatazama mbele kuangalia achangie kipi chenye manufaa kwa Wazanzibari na nchi yao kuwatahadharisha na makossa ya nyuma ili wasiyarejee tena.

Khamis Abdulla Ameir alishughulishwa na kuusema ukweli kama aujuavyo.

Hapa nitarudia kusema kuwa kitabu hiki si kitabu chepesi kukifanyia pitio hadharani.

Mwandishi hakujifanyia uhariri yeye binafsi lakini upendeleo huu unakoma kwake.

Mchambuzi w kitabu hawezi kuikanyaga ardhi aliyokanyaga Khamis Abdulla Ameir kwani yeye, mosi hana ujasiri aliokuwanao Theoretician na pili hana mbavu za kuubeba huu mzigo mzito alioubeba yeye kwani ni gunia zito lililojaa misumari yenye ncha kali.

Kitabu hiki si kitabu cha kawaida unachokikuta Masomo Bookshop.

Kitabu hiki ni kamusi la historia ya Zanzibar kuanzia pale siasa za kudai uhuru wa Zanzibar zilipoanza miaka ya 1950 hadi kufika utawala uliokuwako sasa.

Kitabu hiki, ‘’Maisha Yangu Miaka Minane Ndani ya Baraza la Mapinduzi Khaini au Mhanga wa Mapinduzi?’’ ni kitabu tofauti sana na vitabu vyote vya historia ya mapinduuzi vilivyopata kuandikwa.

Inawezekana tofauti hii imesababishwa kwanza na umri wa mwandishi na pili kuwa yeye hakuwa mchezea pembeni.

Khamis Abdulla Ameir yeye alikuwa mchezaji wa katikati.

Amenza siasa za ukombozi akiwa kijana mdogo mjini London katika miaka ya 1950.

Kaanza kushiriki harakati za kupigania uhuru wa Afrika Uingereza akisuhubiana na wazalendo wengine kama Peter Mbiu Koinange mmoja wa washirika sita wa Kenyatta maarufu kwa jina la ‘’Kapenguria Six,’’ waliofungwa Kapenguria kama wafuasi wa Mau Mau.

Kipindi hiki cha maisha ya Khamis Abdulla Ameir Uingereza ni kipindi muhimu kwa yale yatakayokuja kutokea Zanzibar hadi kufikia mapinduzi.

Ilikuwa Khamis Abdulla Ameir alipokuwa London ndipo alipofahamiana na Abdulrahman Babu na Ali Sultan.

Maisha ya vijana hawa watatu yatafungamana hadi Zanzibar itakapopata uhuru wake tarehe 10 December 1963 na kisha mapinduzi kutokea tarehe 12 Januari, 1964 mwezi mmoja baada ya uhuru huo kupatikana.

Vijana hawa watatu wote watajikuta jela wakishitakiwa kwa mauaji ya Karume mwaka wa 1972.

William Shakespeare alikuwa na ‘’Three Weird Sisters,’’ katika Macbeth.

Katika kitabu hiki tunao ukipenda, ‘’The Three Weird Brothers,’’ katika historia ya Zanzibar.

Kama Weird Sisters walivyokuwa burudani katika Macbeth, halikadhalika historia ya Khamis Abdulla Ameir, Abdulrahman Babu na Ali Sultan ni mkasa wa kutosha ndani ya kitabu hiki.

Vijana hawa wote watatu walishiriki kwanza katika kupigania uhuru wa Zanzibar kisha katika mapinduzi na mwishowe katika uendeshaji wa serikali ya Zanzibar baada ya mapinduzi.

Tofauti baina yao ni kuwa wale waliokuwa Scotland walikuwa wachawi hawa wa Zanzibar ni wanamapinduzi wa Kisoshalisti.

Hawa wote watatu wakaja kuhusishwa na mauaji ya Abeid Amani Karume.

Khamis Abdulla Ameir akiwa Memba wa Baraza la Mapinduzi kwa miaka minane.

289259033_1199733300774046_1352558069320306559_n.jpg

288791471_1199737757440267_3314978994054343513_n.jpg

Khamis Abdulla Ameir
 
Ila hili swala la wewe kukimbia ubantu na imani zake na tamaduni zake na wewe kukumbatia tamaduni na imani za wageni wa nje ya bara letu mbona hunijibu mzee wangu???
Nelson...
Swali lako ni binafsi.
Likiwa ni binafsi tunajadili kitu gani?

Kwani ni muhimu sana kwako kujua kwa nini mimi ni Muislam?
Nikikuuliza wewe kwa nini ni Mkristo utajibu nini?

Umeleta uzi wa Israel na nimejaribu kukupa historia inayoizunguka Israel lakini kuna mengi nimegundua huyajui.

Ikawa unataka kujua kama niliwahi kupata mafunzo ya silaha na hapo nikakataa kukupa jibu sasa unataka kujua kwa nini mimi Muislam.

Hapa si mahali pake.
 
Ndio tupo tunalijadili hilo hapa
Nelson,
Mnawajadili Wazanzibari.
Hawajui kitu.

Mimi nimekutana na Wazanzibari wengi sana na wengine tukawa marafiki wakubwa sana.

Inaweza kunichukua muda mrefu kama nitataka kueleza historia zao.
Wengine wa hai na wengine wameshatangulia mbele ya haki.

Soma hayo hapo chini naamini kuna utakachojifunza:

BURIANI SALIM MSOMA MSOMI MAKINI MSOMI WA SIFA NA MJUZI WA KIINGEREZA KWA KUANDIKA NA KUZUNGUMZA

Salim Msoma kwangu alikuwa kaka, rafiki na pia mwalimu wangu lau kama hili la mwisho naamini hakulijua.

Mimi na yeye tulikuwa tukiandikiana faragha na tukisomana sana katika makala zetu magazetini na kwenye mitandao.

Hapo chini ni barua niliyopokea kutoka kwa Salim Msoma miaka mitano iiyopita akitoa maoni yake kuhusu makala, ''Uchaguzi wa Zanzibar wa Mwaka wa 1961,'' ambamo niliweka nukuu ya Aman Thani akieleza uchaguzi ule jinsi ulivyokuwa.

Wasiomfahamu Salim Msoma ni kuwa Msoma ni katika wanafunzi wasomi makini wa wakati wa mapinduzi ya Afrika miaka ya 1960 kuelekea 1970.

Salim Msoma likuwa mwanachama wa University Students's African Revolutionary Front (USARF) chama ambacho kilianzishwa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam mwaka wa 1967 na wanachama wake walikuja kuacha alama katika historia za ukombozi wa nchi zao kama John Garang na Yoweri Museveni.

Siku moja tukiwa peke yetu Msoma alinidokeza kuwa yeye wakati akiwa mwanafunzi Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam alikuwa mmoja wa vijana walioingia Msumbiji kupigana bega kwa bega na FRELIMO dhidi ya Wareno.

Nilipumua kidogo.

Barua hii niliyoitaja hapo juu aliyoniandikia Salim Msoma imekaa Maktaba kama rejea yangu ya kudumu pale nilipotatazika na jambo katika siasa za Zanzibar zinazohusu uchaguzi.

Nakuwekeni hapa barua hii aliyoaniandikia miaka mitano iliyopita ila nanyi mfaidi.

‘’Sheikh Mohamed Said,

Ahsante kwa kutuletea maandishi haya ambayo yanatukumbusha historia ya karibuni ya Zanzibar.

Bila shaka waraka huu umeunakili kutoka kijitabu alokiandika mzee wetu Bw. Amani Thani Fairuz miaka kadha iliyopita na ambacho binafsi nilibahatika kukisoma.

Mimi naomba nitoe maoni ya mawili matatu kuhusu maelezo ya Mzee Amani Thani.

Kwanza nakubaliana nawe kuwa yapo ya kujifunza katika kadhia ya uchaguzi wa Januari na June 1961 Zanzibar khasa tukitilia maanani hali ya kisiasa ilivyo hii leo visiwani.

Lakini ninalotaka kuchangia mimi ni kwamba maelezo ya Mzee Fairuz kama yalivyo maandishi mengine kuhusu mada hii niliyoyasoma yanakuwa na upungufu mmoja.

Nao ni tabia ya kuelezea matukio (facts) bila ya kujadili kwa upana na kutafsiri yaliyo nyuma ya matukio hayo yaani muktadha wake (broad discussion of related issues surrounding the narrated events).

Mfano unapozungumzia suala la kuwepo VITI katika majimbo ya uchaguzi vilivyokuwa vinagombewa na kueleza matokeo ya chama kile kilipata viti kadhaa na kingine kikapata viti zaidi na kushinda bila ya pia kuonyesha TAKWIMU za kura zilizopigwa hakutowi picha sahihi kwa wasomaji kuhusu mfumo mzima wa chaguzi zile.

Hivi leo waandishi mbalimbali wanaeleza na kuonyesha jinsi ukataji wa majimbo (constituencies) ulivyokuwa wa mashaka na hila.

Imebainika majimbo yaliyokuwa na wafuasi wengi wa ASP yalitengewa viti vichache wakati majimbo yalokuwa na watu kidogo wa ZNP yalipewa viti vingi.

Ujanja huu ambao Waingereza wanauwita 'gerrymandering' ndio hatimae uliwapokonya ushindi halali ASP na kutulea mabalaa na maafa visiwani.

Wasomaji lazima waelimishwe kuwa miongoni mwa sababu za kufanyika Mapinduzi Zanzibar ni hili la kunyimwa kwa hila na ujanja haki yao ASP ya kuunda na kuongoza serikali.

Jengine ninalotaka kulieleza kwa mnasaba huu huu wa kujadili mambo badala ya kuyataja tu kijuu juu ni kitendo cha Sheikh Mohamed Shamte kujitoa ASP mwaka 1960.

Bw. Fairuz ameeleza haelewi sababu za Mzee Shamte kujitoa ASP.

Lakini kadri ya muda ulivyopita imebainika wazi kuwa ZPPP kilikuwa ni chama kilichotokana na tawi lililokuwa la Shirazi Association huko Pemba.

Mara zote imekuwa ikitolewa picha potofu kuwa Waswahili wa Zanzibar waliojitambulisha kwa jina la Shirazi Association walikuwa ni kitu kimoja (homogeneous).

Kumbe hali ni tofauti kabisa.

Washirazi wa Pemba na hata baadhi ya wale wa Unguza wamekuwa wakati wakiwemo ndani ya chama cha ASP wakipinga kile walichokihisi ujenzi wa uhusiano wa karibu kati ya ASP na TANU.

Shamte aliwakilisha hisia hizo na alikuwa hamuamini kabisa Julius Kambarage Nyerere kinyume na alivyokuwa Mzee Karume.

Na Mzee Shamte alipohisi huu usuhuba wa Nyerere na Karume unazidi kushamiri ndipo akagombana na Mzee Karume na kuamua kujitoa ASP.

Lakini kuna jambo jengine ambalo ZNP hawakupenda kuliongea.

Nalo ni kwamba huyu Mzee Shamte hapo mwanzoni alikuwa hawaamini pia Waarabu!

Inaelezwa kuwa katika mwaka ule (1959) ambao Mzee Karume kwa shinikizo la PAFMECA alianza kuhutubia mikutano kupitia jukwaa moja na Sheikh Ali Muhsin, Shamte alikuwa ni ‘’diehard,’’ mmoja wapo aliekasirishwa ndani ya ASP.

Cha kustaajabisha ni kumuona mtu yule yule alokuwa akipinga kumuona Karume akiwa pamoja na Ali Muhsin alikuja baadae kuunda Umoja na huyohuyo Ali Muhsin kuanzia uchaguzi wa 1961 na hatimae akapewa Uwaziri Mkuu ndani ya Serikali ya Uhuru 1963!

Haya ndio mambo ambayo waandishi kama Bw Fairuz wanapaswa kuyasema kwa uwazi zaidi.

Wasalam.’’

Huyu ndiye Salim Msoma msomi aliyejiamini kutokana na ukweli alioujua na wala hakuona muhali kuueleza.

Ninazo barua na makala zake nyingine nyingi ambazo kwangu ni ''Masterpiece'' na nimezihifadhi sehemu maalum.

Moja ya barua hizi ni aliyomwandikia Rais Hussein Mwinyi alipochukua uongozi wa Zanzibar kama Rais.

Hii ni barua ambayo itaishi miaka 100.

Tanzania imepoteza msomi makini ambae wengi walinufaika na fikra zake.

Buriani kaka na rafiki yangu Salim Msoma msomi makini na msomi wa sifa.
Allah amfanyie wepesi safari yake.

Amin.

245307979_1041554083258636_7753191828416171559_n.jpg

Salim Msoma​
 
Nelson...
Swali lako ni binafsi.
Likiwa ni binafsi tunajadili kitu gani?

Kwani ni muhimu sana kwako kujua kwa nini mimi ni Muislam?
Nikikuuliza wewe kwa nini ni Mkristo utajibu nini?

Umeleta uzi wa Israel na nimejaribu kukupa historia inayoizunguka Israel lakini kuna mengi nimegundua huyajui.

Ikawa unataka kujua kama niliwahi kupata mafunzo ya silaha na hapo nikakataa kukupa jibu sasa unataka kujua kwa nini mimi Muislam.

Hapa si mahali pake.
Unalikwepa hili swali mzee wangu na waafrika wengi waga wanakwepa hili swali
 
Nelson,
Mnawajadili Wazanzibari.
Hawajui kitu.

Mimi nimekutana na Wazanzibari wengi sana na wengine tukawa marafiki wakubwa sana.

Inaweza kunichukua muda mrefu kama nitataka kueleza historia zao.
Wengine wa hai na wengine wameshatangulia mbele ya haki.

Soma hayo hapo chini naamini kuna utakachojifunza:

BURIANI SALIM MSOMA MSOMI MAKINI MSOMI WA SIFA NA MJUZI WA KIINGEREZA KWA KUANDIKA NA KUZUNGUMZA

Salim Msoma kwangu alikuwa kaka, rafiki na pia mwalimu wangu lau kama hili la mwisho naamini hakulijua.

Mimi na yeye tulikuwa tukiandikiana faragha na tukisomana sana katika makala zetu magazetini na kwenye mitandao.

Hapo chini ni barua niliyopokea kutoka kwa Salim Msoma miaka mitano iiyopita akitoa maoni yake kuhusu makala, ''Uchaguzi wa Zanzibar wa Mwaka wa 1961,'' ambamo niliweka nukuu ya Aman Thani akieleza uchaguzi ule jinsi ulivyokuwa.

Wasiomfahamu Salim Msoma ni kuwa Msoma ni katika wanafunzi wasomi makini wa wakati wa mapinduzi ya Afrika miaka ya 1960 kuelekea 1970.

Salim Msoma likuwa mwanachama wa University Students's African Revolutionary Front (USARF) chama ambacho kilianzishwa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam mwaka wa 1967 na wanachama wake walikuja kuacha alama katika historia za ukombozi wa nchi zao kama John Garang na Yoweri Museveni.

Siku moja tukiwa peke yetu Msoma alinidokeza kuwa yeye wakati akiwa mwanafunzi Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam alikuwa mmoja wa vijana walioingia Msumbiji kupigana bega kwa bega na FRELIMO dhidi ya Wareno.

Nilipumua kidogo.

Barua hii niliyoitaja hapo juu aliyoniandikia Salim Msoma imekaa Maktaba kama rejea yangu ya kudumu pale nilipotatazika na jambo katika siasa za Zanzibar zinazohusu uchaguzi.

Nakuwekeni hapa barua hii aliyoaniandikia miaka mitano iliyopita ila nanyi mfaidi.

‘’Sheikh Mohamed Said,

Ahsante kwa kutuletea maandishi haya ambayo yanatukumbusha historia ya karibuni ya Zanzibar.

Bila shaka waraka huu umeunakili kutoka kijitabu alokiandika mzee wetu Bw. Amani Thani Fairuz miaka kadha iliyopita na ambacho binafsi nilibahatika kukisoma.

Mimi naomba nitoe maoni ya mawili matatu kuhusu maelezo ya Mzee Amani Thani.

Kwanza nakubaliana nawe kuwa yapo ya kujifunza katika kadhia ya uchaguzi wa Januari na June 1961 Zanzibar khasa tukitilia maanani hali ya kisiasa ilivyo hii leo visiwani.

Lakini ninalotaka kuchangia mimi ni kwamba maelezo ya Mzee Fairuz kama yalivyo maandishi mengine kuhusu mada hii niliyoyasoma yanakuwa na upungufu mmoja.

Nao ni tabia ya kuelezea matukio (facts) bila ya kujadili kwa upana na kutafsiri yaliyo nyuma ya matukio hayo yaani muktadha wake (broad discussion of related issues surrounding the narrated events).

Mfano unapozungumzia suala la kuwepo VITI katika majimbo ya uchaguzi vilivyokuwa vinagombewa na kueleza matokeo ya chama kile kilipata viti kadhaa na kingine kikapata viti zaidi na kushinda bila ya pia kuonyesha TAKWIMU za kura zilizopigwa hakutowi picha sahihi kwa wasomaji kuhusu mfumo mzima wa chaguzi zile.

Hivi leo waandishi mbalimbali wanaeleza na kuonyesha jinsi ukataji wa majimbo (constituencies) ulivyokuwa wa mashaka na hila.

Imebainika majimbo yaliyokuwa na wafuasi wengi wa ASP yalitengewa viti vichache wakati majimbo yalokuwa na watu kidogo wa ZNP yalipewa viti vingi.

Ujanja huu ambao Waingereza wanauwita 'gerrymandering' ndio hatimae uliwapokonya ushindi halali ASP na kutulea mabalaa na maafa visiwani.

Wasomaji lazima waelimishwe kuwa miongoni mwa sababu za kufanyika Mapinduzi Zanzibar ni hili la kunyimwa kwa hila na ujanja haki yao ASP ya kuunda na kuongoza serikali.

Jengine ninalotaka kulieleza kwa mnasaba huu huu wa kujadili mambo badala ya kuyataja tu kijuu juu ni kitendo cha Sheikh Mohamed Shamte kujitoa ASP mwaka 1960.

Bw. Fairuz ameeleza haelewi sababu za Mzee Shamte kujitoa ASP.

Lakini kadri ya muda ulivyopita imebainika wazi kuwa ZPPP kilikuwa ni chama kilichotokana na tawi lililokuwa la Shirazi Association huko Pemba.

Mara zote imekuwa ikitolewa picha potofu kuwa Waswahili wa Zanzibar waliojitambulisha kwa jina la Shirazi Association walikuwa ni kitu kimoja (homogeneous).

Kumbe hali ni tofauti kabisa.

Washirazi wa Pemba na hata baadhi ya wale wa Unguza wamekuwa wakati wakiwemo ndani ya chama cha ASP wakipinga kile walichokihisi ujenzi wa uhusiano wa karibu kati ya ASP na TANU.

Shamte aliwakilisha hisia hizo na alikuwa hamuamini kabisa Julius Kambarage Nyerere kinyume na alivyokuwa Mzee Karume.

Na Mzee Shamte alipohisi huu usuhuba wa Nyerere na Karume unazidi kushamiri ndipo akagombana na Mzee Karume na kuamua kujitoa ASP.

Lakini kuna jambo jengine ambalo ZNP hawakupenda kuliongea.

Nalo ni kwamba huyu Mzee Shamte hapo mwanzoni alikuwa hawaamini pia Waarabu!

Inaelezwa kuwa katika mwaka ule (1959) ambao Mzee Karume kwa shinikizo la PAFMECA alianza kuhutubia mikutano kupitia jukwaa moja na Sheikh Ali Muhsin, Shamte alikuwa ni ‘’diehard,’’ mmoja wapo aliekasirishwa ndani ya ASP.

Cha kustaajabisha ni kumuona mtu yule yule alokuwa akipinga kumuona Karume akiwa pamoja na Ali Muhsin alikuja baadae kuunda Umoja na huyohuyo Ali Muhsin kuanzia uchaguzi wa 1961 na hatimae akapewa Uwaziri Mkuu ndani ya Serikali ya Uhuru 1963!

Haya ndio mambo ambayo waandishi kama Bw Fairuz wanapaswa kuyasema kwa uwazi zaidi.

Wasalam.’’

Huyu ndiye Salim Msoma msomi aliyejiamini kutokana na ukweli alioujua na wala hakuona muhali kuueleza.

Ninazo barua na makala zake nyingine nyingi ambazo kwangu ni ''Masterpiece'' na nimezihifadhi sehemu maalum.

Moja ya barua hizi ni aliyomwandikia Rais Hussein Mwinyi alipochukua uongozi wa Zanzibar kama Rais.

Hii ni barua ambayo itaishi miaka 100.

Tanzania imepoteza msomi makini ambae wengi walinufaika na fikra zake.

Buriani kaka na rafiki yangu Salim Msoma msomi makini na msomi wa sifa.
Allah amfanyie wepesi safari yake.

Amin.

245307979_1041554083258636_7753191828416171559_n.jpg

Salim Msoma​
Tunajadili wanaopinga mapinduzi matukufu ya zanzbar ya mwaka 1964 wana ajenda gani nyuma ya pazia?????
 
Nelson nyinyi hamtafuti elimu choyo kimetawala nyoyo zenu.

Ingekuwa ni suala la kusoma kutoka kwangu maswali yangekuwa kutoka ninayokuwekeeni hapa.

Wewe utaniuliza swali nikijibu utapinga nami jibu lamgu siku zote ni hakuna tatizo ikiwa huamini.

Umetaka waraka.
Nimekuwekea.

Ingekuwa mna nia njema yangekuja maswali mengine kabisa siyo kukataa.
Mzee kutukuza mapinduzi matukufu ni choyo??
 
Unalikwepa hili swali mzee wangu na waafrika wengi waga wanakwepa hili swali
Nelson...
Kuna baadhi ya maneno inaelekea unayapenda sana.
Maneno haya ni ''mapinduzi matukufu,'' utumwa, walowezi,'' ''kukwepa,'' ''uoga''...

Mimi niogope nini na nimwogope nani?

Unaweza kupitia nyuzi na michango yangu hapa ya miaka 10 iliyopita ukitaka ushahidi.

Sikulaumu wewe ni mgeni na mimi hunijui.
Umepiga hodi mwaka wa 2022.

Mgeni sana kisha hujui mengi.

Kuhusu Zanzibar.

Nimekueleza kuwa Wazanzibari hapa walipo leo jambo muhimu kwao si mapinduzi.

Hubadiliki umeshikilia hapo hapo.
Mapinduzi matukufu, matukufu, matukufu...

Mfano wa kasuku au santuri iliyokwama.

Kama vile huamini kuwa leo Wazanzibari tatizo ni CCM Zanzibar kukubali kuwa na uchaguzi huru na wa haki kwani chaguzi zote sita zilizofanyika Wazanzibari wameuliwa kwa ajili ya uchaguzi.

Wazanzibari kwa kutafuta salama walipiga kura wawe na SUK.
Hapa ndipo walipo.

Kwa CCM Zanzibar kushindwa katika chaguzi zote sita nini tafsiri yake?
Tafsiri yake ni kuwa mapinduzi hayana maana tena vinginevyo Wazanzibari wangewachagua.

Hawako katika historia ya utumwa kamwe.

Kuna mambo huamua kuyakalia kimya kwa sababu tofauti.

Yawezekana inaweza kuwa swali ni la binafsi au nikakaa kimya kwa kuweka staha yaani kulinda heshima yangu binafsi au ya mtu mwengine.

Wewe mimi hata pale ninapoluwekea mambo muhimu katika historia yangu na historia ya Tanzania unapokuwa kimya mimi sikuchagizi kuwa lazima ujibu.

Natambua kuwa ni mambo mazito kwako sina cha kupata kwa kukuchagiza.
Naachia tuendelee na kujadili mengine.

Natambua kuwa uwezo wa kujua mambo unapishana kati ya mtu na mtu.

Kuna mtu utamwandikia mambo mazito atakejeli pengine ni kwa kushtuka na taarifa hiyo na kuna mwengine ataonyesha hisia za kuthamini ingawa atakuwa kashtuka.
 
Tunajadili wanaopinga mapinduzi matukufu ya zanzbar ya mwaka 1964 wana ajenda gani nyuma ya pazia?????
Nelson...
Lakini hilo la kupinga mapinduzi leo halipo.

Inabidi uangalie uchaguzi wa mwaka 1995 na tujiulize kwa nini CCM Zanzibar walishindwa?

Wazanzibari waliiinyima kura CCM kwa kuwa wanapinga mapinduzi?
Kama wanapinga mapinduzi sababu ni nini?

Kutokea hapo sasa unaangalia kila uchaguzi hali ndiyo hiyo hadi kufikia Wazanzibari kuamua kuwa na SUK.

Kwa nini waliamua hivyo?
Nani amefaidika na kura ya kutaka SUK?
 
Mzee kutukuza mapinduzi matukufu ni choyo??
Nelson...
Mapinduzi hayapo katika agenda ya Wazanzibari.

Kutukuza mapinduzi iweje kuwa choyo?
Sijaelewa.

Lakini ikiwa unapenda kuandika na kuyatukuza mapinduzi mitandaoni hakuna wa kukuzuia.

Ndiyo kama hivi umeleta uzi tunajadili.
Faida ya mjadala kama huu ni watu kuelimishana.

Kuna mtu hapa kasema Wazanzibar wanaijua Qur'an tu hawana lolote lingine hawajui hata historia yao.

Mimi ninaposoma vitu kama hivi najua hili ni tatizo la ujinga na dawa ya kutibu ujinga ni elimu.

Maktaba yangu ina vitabu vingi sana vilivyoandikwa na Wazanzibari wengine hujapata hata kuwasikia.

Nimeweka makala mbili nilizoandika kuwaeleza Wazanzibari wawili ambao mimi nawafahamu - Salim Msoma na Khamisi Abdulla Ameir.

Mimi nimesomeshwa Qur'an kabla hata ya kuanza darasa la kwanza na hivi ndivyo sote Waislam tunavyofanyiwa na wazee wetu akiwemo Khamisi Abdulla Ameir na Salim Msoma.

1676003271063.png
 
Nelson...
Mapinduzi hayapo katika agenda ya Wazanzibari.

Kutukuza mapinduzi iweje kuwa choyo?
Sijaelewa.

Lakini ikiwa unapenda kuandika na kuyatukuza mapinduzi mitandaoni hakuna wa kukuzuia.

Ndiyo kama hivi umeleta uzi tunajadili.
Faida ya mjadala kama huu ni watu kuelimishana.

Kuna mtu hapa kasema Wazanzibar wanaijua Qur'an tu hawana lolote lingine hawajui hata historia yao.

Mimi ninaposoma vitu kama hivi najua hili ni tatizo la ujinga na dawa ya kutibu ujinga ni elimu.

Maktaba yangu ina vitabu vingi sana vilivyoandikwa na Wazanzibari wengine hujapata hata kuwasikia.

Nimeweka makala mbili nilizoandika kuwaeleza Wazanzibari wawili ambao mimi nawafahamu - Salim Msoma na Khamisi Abdulla Ameir.

Mimi nimesomeshwa Qur'an kabla hata ya kuanza darasa la kwanza na hivi ndivyo sote Waislam tunavyofanyiwa na wazee wetu akiwemo Khamisi Abdulla Ameir na Salim Msoma.

Sasa unahama mada mzee wangu!!!Mada ni wale wanayayapinga mapinduzi matukufu ya kuwaondoa walowezi kandamizi wa kiarabu kutoka oman na vibaraka wao mwaka 1964 wana ajenda gani nyuma ya pazia?????
 
Sasa unahama mada mzee wangu!!!Mada ni wale wanayayapinga mapinduzi matukufu ya kuwaondoa walowezi kandamizi wa kiarabu kutoka oman na vibaraka wao mwaka 1964 wana ajenda gani nyuma ya pazia?????
Nelson...
Lugha hizo za "kandamizi"na mfano wa hayo yako hayapo kwa Wazanzibari.

Hutosikia lugha hiyo Zanzibar.

Yako kwako wewe Mtanganyika.
Wazanzibari wako katika kutafuta utangamano na amani ya nchi yao.

Mimealikwa Zanzibar mara nne kuzungumza hadharani na kwenye FM Stations.

NInayozungumza hapa ndiyo nizungumzayo Zanzibar.

Sijahama popote ila wewe unapenda kuiona Zanzibar ikiwa katika utengano na farka.
 
Nelson...
Lugha hizo za "kandamizi"na mfano wa hayo yako hayapo kwa Wazanzibari.

Hutosikia lugha hiyo Zanzibar.

Yako kwako wewe Mtanganyika.
Wazanzibari wako katika kutafuta utangamano na amani ya nchi yao.

Mimealikwa Zanzibar mara nne kuzungumza hadharani na kwenye FM Stations.

NInayozungumza hapa ndiyo nizungumzayo Zanzibar.

Sijahama popote ila wewe unapenda kuiona Zanzibar ikiwa katika utengano na farka.
 
Back
Top Bottom