KERO Wanaofanya uvuvi Mto Ngerengere eneo la Tungi na Kihonda wawe makini, kuna mashimo yaliyochimbwa wakati wa ujenzi wa SGR yana kina kirefu

KERO Wanaofanya uvuvi Mto Ngerengere eneo la Tungi na Kihonda wawe makini, kuna mashimo yaliyochimbwa wakati wa ujenzi wa SGR yana kina kirefu

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Bado Hujasema

Member
Joined
Dec 1, 2024
Posts
12
Reaction score
14
Mimi ni mkazi wa Mfaranyaki, Kata ya Tungi, Manispaa ya Morogoro, mtaani kwetu tumechoshwa na matukio ya watu kupata majanga ikiwemo kupoteza Maisha katika eneo hilo la Mto Ngerengere uliokatisha Kata ya Tungi na Kihonda.

Mto huo umekuwa ni kero na tishio kutokana na watu kupoteza maisha wanapofanya shughuli za uvuvi na vifo eneo hilo, hiyo inatokana na kina kilichoongezeka katika mashimo yaliyochimbwa katika ndani ya mto wakati wa ujenzi wa Reli ya Kisasa ya SGR.

Nakumbuka Disemba 16, 2024, Mwanaume anayekadiriwa kuwa na Umri wa Miaka 27, ambaye jina lake halijafahamika mkazi wa mtaa huo alipoteza maisha baada ya kutumbukia ndani ya Mto huo wakati akifanya shughuli ya uvuvi.

Kipindi cha Mwaka 2024 tayari inadaiwa jumla ya watu wanne wamepoteza maisha wakati wakiendelea na shughuli za uvuvi katika mto hali ambayo inatishia usalama wa watu wa eneo hilo hasa wanaofanya shughuli za uvuvi na kujipatia kipato.

Hali hii inatufanya kuwa na hofu katika eneo hili, hao ni watu wazima tunakuwa na hofu, watoto pia wanaweza kupoteza maisha maana kuna wengine wanakuja kucheza kando ya mto huo.

Nashauri Serikali kupitia watu wa Bonde Wami/Ruvu kwa kushirikiana na Manispaa ya Morogoro kuweka tahadhari juu ya uwepo wa kina kirefu maeneo hayo au kutafuta njia mbadala kutokana na watu kuendelea kutochukua tahadhari wakati wa shughuli za uvuvi jambo linalohatarisha usalama wa watu hao.

Wakati huohuo, umakini unatakiwa kuongezeka kwa wote wanaofanya shughuli zao maeneo hayo watambue kuwa kina ni kirefu tofauti na hali inavyoonekana kwa juu.
IMG-20250107-WA0025.jpg
IMG-20250107-WA0023.jpg
IMG-20250107-WA0031.jpg


IMG-20250107-WA0017.jpg
IMG-20250107-WA0019.jpg
 

Attachments

  • IMG-20250107-WA0021.jpg
    IMG-20250107-WA0021.jpg
    844.1 KB · Views: 2
  • IMG-20250107-WA0029.jpg
    IMG-20250107-WA0029.jpg
    754.4 KB · Views: 2
  • IMG-20250107-WA0035.jpg
    IMG-20250107-WA0035.jpg
    1 MB · Views: 2
  • IMG-20250107-WA0034.jpg
    IMG-20250107-WA0034.jpg
    1 MB · Views: 3
Mbaya zaidi ni kwamba
  1. Hayo maji yenyewe yana sumu/kemikali zinazomwagwa na viwanda
  2. Hayo maji pamoja na sumu/kemikali yanatumiwa na watu majumbani
  3. Hayo maji yanatumiwa kumwagilia mbogamboga na mazao mengine mashambani
  4. Hao samaki wenyewe huenda wanasumu pia kwakuwa wanaishi kwenye maji yenye kemikali za viwandani
  5. Hao wahanga wanaopoteza maisha wameanza baada ya reli kujengwa, siku za nyuma hapakuwepo vifo
  6. Kikosi cha uokoaji huwa ni kama hakipo inapotokea majanga wanakuja na pump ya kufyonza maji ya mto
  7. Serikali haikupiga uzio wa kuzuia watu kuyafikia hayo mashimo maana hayaonekani yamefunikwa na maji
 
Mimi ni mkazi wa Mfaranyaki, Kata ya Tungi, Manispaa ya Morogoro, mtaani kwetu tumechoshwa na matukio ya watu kupata majanga ikiwemo kupoteza Maisha katika eneo hilo katika Mto Ngerengere uliokatisha Kata ya Tungi na Kihonda.

Mto huu umekuwa ni kero na tishio kutokana na watu kupoteza maisha wanapofanya shughuli za uvuvi na vifo eneo hilo, hiyo inatokana na kina kilichoongezeka katika mashimo yaliyochimbwa katika ndani ya mto wakati wa ujenzi wa Reli ya Kisasa ya SGR.

Nakumbuka Disemba 16, 2024, Mwanaume anayekadiriwa kuwa na Umri wa Miaka 27, ambaye jina lake halijafahamika mkazi wa mtaa huo alipoteza maisha baada ya kutumbukia ndani ya Mto huo wakati akifanya shughuli ya uvuvi.

Kipindi cha Mwaka 2024 tayari jumla ya watu 4 wamepoteza maisha wakati wakiendelea na shughuli za uvuvi katika mto hali ambayo inatishia usalama wa watu wa eneo hilo hasa wanaofanya shughuli za uvuvi na kujipatia kipato.

Hali hii inatufanya kuwa na hofu katika eneo hili, hao ni watu wazima tunakuwa na hofu, watoto pia wanaweza kupoteza maisha maana kuna wengine wanakuja kucheza kando ya mto huo.

Nashauri Serikali kupitia watu wa Bonde Wami/Ruvu kwa kushirikiana na Manispaa ya Morogoro kufukia mashimo yaliyochimbwa katika mto huo wakati wa ujenzi wa Reli ya Kisasa ya SGR, kutokana na watu kuendelea kuyatumia katika shughuli za uvuvi jambo linalohatarisha usalama wa watu hao.

Wakati huohuo umakini unatakiwa kuongezeka kwa wote wanaofanya shughuli zao maeneo hayo watambue kuwa kina ni kirefu tofauti na hali inavyoonekana kwa juu.View attachment 3194864View attachment 3194865View attachment 3194868

Sentensi hii 👉 "Mto huu umekuwa ni kero na tishio" sio sahihi hata kidogo. Kwani mto ndo umewafuata watu? Huo mto ni Fursa kubwa kwenu. Wale wasiosikia "maonyo" au wasiotaka kujifunza kwenye matukio hayo mabaya basi hakuna namna ya kuwasaidia. Kuna Serikali ya kijiji, Baraza la Kata n.k. Wekeni sheria na atakayeikiuka awajibike kuongeza kwenye mapato ya Kijiji.
 
Sentensi hii 👉 "Mto huu umekuwa ni kero na tishio" sio sahihi hata kidogo. Kwani mto ndo umewafuata watu? Huo mto ni Fursa kubwa kwenu. Wale wasiosikia "maonyo" au wasiotaka kujifunza kwenye matukio hayo mabaya basi hakuna namna ya kuwasaidia. Kuna Serikali ya kijiji, Baraza la Kata n.k. Wekeni sheria na atakayeikiuka awajibike kuongeza kwenye mapato ya Kijiji.
Nilibahatika kuwasikia wakazi wa huko wakielezea kilichopo kwamba, huo mto haukuwa na historia ya kuua watu, hizo shughuli walikuwa wanafanya enzi na enzi, wajenzi wa reli walikuja wakachimba mashimo marefu approx 10 metres deep, hayo mashimo ndiyo yameharibu sura na tabia ya mto, hivi sasa unaua watu wengi
 
Mimi ni mkazi wa Mfaranyaki, Kata ya Tungi, Manispaa ya Morogoro, mtaani kwetu tumechoshwa na matukio ya watu kupata majanga ikiwemo kupoteza Maisha katika eneo hilo katika Mto Ngerengere uliokatisha Kata ya Tungi na Kihonda.

Mto huu umekuwa ni kero na tishio kutokana na watu kupoteza maisha wanapofanya shughuli za uvuvi na vifo eneo hilo, hiyo inatokana na kina kilichoongezeka katika mashimo yaliyochimbwa katika ndani ya mto wakati wa ujenzi wa Reli ya Kisasa ya SGR.

Nakumbuka Disemba 16, 2024, Mwanaume anayekadiriwa kuwa na Umri wa Miaka 27, ambaye jina lake halijafahamika mkazi wa mtaa huo alipoteza maisha baada ya kutumbukia ndani ya Mto huo wakati akifanya shughuli ya uvuvi.

Kipindi cha Mwaka 2024 tayari jumla ya watu 4 wamepoteza maisha wakati wakiendelea na shughuli za uvuvi katika mto hali ambayo inatishia usalama wa watu wa eneo hilo hasa wanaofanya shughuli za uvuvi na kujipatia kipato.

Hali hii inatufanya kuwa na hofu katika eneo hili, hao ni watu wazima tunakuwa na hofu, watoto pia wanaweza kupoteza maisha maana kuna wengine wanakuja kucheza kando ya mto huo.

Nashauri Serikali kupitia watu wa Bonde Wami/Ruvu kwa kushirikiana na Manispaa ya Morogoro kufukia mashimo yaliyochimbwa katika mto huo wakati wa ujenzi wa Reli ya Kisasa ya SGR, kutokana na watu kuendelea kuyatumia katika shughuli za uvuvi jambo linalohatarisha usalama wa watu hao.

Wakati huohuo umakini unatakiwa kuongezeka kwa wote wanaofanya shughuli zao maeneo hayo watambue kuwa kina ni kirefu tofauti na hali inavyoonekana kwa juu.View attachment 3194864View attachment 3194865View attachment 3194868

Kwanini unawashitua, Watanzania wana asili ya ubishi wa kijinga, ungewaacha tu wazame.
 
Nilibahatika kuwasikia wakazi wa huko wakielezea kilichopo kwamba, huo mto haukuwa na historia ya kuua watu, hizo shughuli walikuwa wanafanya enzi na enzi, wajenzi wa reli walikuja wakachimba mashimo marefu approx 10 metres deep, hayo mashimo ndiyo yameharibu sura na tabia ya mto, hivi sasa unaua watu wengi
Watu wasiende kufanya shughuli mtoni kizembe. Wachukue Tahadhari.
Eti "Walikuwa wanafanya enzi na enzi........" Hawakubaliani na mabadiliko? Ukisikia Kuti la mazoea ndo hivo.
 
Mimi ni mkazi wa Mfaranyaki, Kata ya Tungi, Manispaa ya Morogoro, mtaani kwetu tumechoshwa na matukio ya watu kupata majanga ikiwemo kupoteza Maisha katika eneo hilo katika Mto Ngerengere uliokatisha Kata ya Tungi na Kihonda.

Mto huu umekuwa ni kero na tishio kutokana na watu kupoteza maisha wanapofanya shughuli za uvuvi na vifo eneo hilo, hiyo inatokana na kina kilichoongezeka katika mashimo yaliyochimbwa katika ndani ya mto wakati wa ujenzi wa Reli ya Kisasa ya SGR.

Nakumbuka Disemba 16, 2024, Mwanaume anayekadiriwa kuwa na Umri wa Miaka 27, ambaye jina lake halijafahamika mkazi wa mtaa huo alipoteza maisha baada ya kutumbukia ndani ya Mto huo wakati akifanya shughuli ya uvuvi.

Kipindi cha Mwaka 2024 tayari jumla ya watu 4 wamepoteza maisha wakati wakiendelea na shughuli za uvuvi katika mto hali ambayo inatishia usalama wa watu wa eneo hilo hasa wanaofanya shughuli za uvuvi na kujipatia kipato.

Hali hii inatufanya kuwa na hofu katika eneo hili, hao ni watu wazima tunakuwa na hofu, watoto pia wanaweza kupoteza maisha maana kuna wengine wanakuja kucheza kando ya mto huo.

Nashauri Serikali kupitia watu wa Bonde Wami/Ruvu kwa kushirikiana na Manispaa ya Morogoro kufukia mashimo yaliyochimbwa katika mto huo wakati wa ujenzi wa Reli ya Kisasa ya SGR, kutokana na watu kuendelea kuyatumia katika shughuli za uvuvi jambo linalohatarisha usalama wa watu hao.

Wakati huohuo umakini unatakiwa kuongezeka kwa wote wanaofanya shughuli zao maeneo hayo watambue kuwa kina ni kirefu tofauti na hali inavyoonekana kwa juu.View attachment 3194864View attachment 3194865View attachment 3194868

Hao wavuvi hawajui kusoma kwenye hayo maeneo wameweka kabisa bango la Tahadhari
 
Mbaya zaidi ni kwamba
  1. Hayo maji yenyewe yana sumu/kemikali zinazomwagwa na viwanda
Ni shughuli zinazofanywa na binadamu mwenye akili na utashi. Wanaomwaga sumu; wakiamua wanaweza kuacha au kutafuta mahali mbadala pa kumwaga sumu hiyo.
2. Hayo maji pamoja na sumu/kemikali yanatumiwa na watu majumbani
Binadamuu (Watu) wenye akili na Utashi wanafahamu fika kwamba maji hayo ni Hatari kwa Afya zao lakini bado kwa makusudi wanayatumia majumbani. Kwa nini wasiyaepuke?
3. Hayo maji yanatumiwa kumwagilia mbogamboga na mazao mengine mashambani
Wanaomwagilia mbogamboga na mazao mwengine mashambani ni Binadamu mwenye akili na Utashi. Watu hao wakiamua kwa kuzingatia matokeo mabaya ya matumizi ya maji hayo wataacha. (Hata hivyo kiwango cha athari kwa Ulaji wa mazao sio changamoto sana).
4. Hao samaki wenyewe huenda wanasumu pia kwakuwa wanaishi kwenye maji yenye kemikali za viwandani
Hiyo 👆 ni kweli.
5. Hao wahanga wanaopoteza maisha wameanza baada ya reli kujengwa, siku za nyuma hapakuwepo vifo
Hii imekaa kiimani zaidi. Ni sawa na kusema Wanaoteka watu siku za nyuma Utekaji watu haukuwepo.
6. Kikosi cha uokoaji huwa ni kama hakipo inapotokea majanga wanakuja na pump ya kufyonza maji ya mto
Wewe Ungeshauri wafanyeje mkuu?
7. Serikali haikupiga uzio wa kuzuia watu kuyafikia hayo mashimo maana hayaonekani yamefunikwa na maji
Watu( Binadamu mwenye akili na Utashi) amini asiamini, hata ungetumia bunkers au electrified fence; binadamu akiamua kupita atapita tu. Ila ng'ombe unapiga sanzu tu inatosha- hawapiti.
Nimebold neno Binadamu mwenye akili na Utashi kuonesha ni kwa kiwango gani hayo uliyoyaita ni kero; Mhusika mkuu ni Waathirika wenyewe. Wakiamua wanaweza kupata ufumbuzi au suluhisho.
 
Duh aiseee hatari
Sio kidogo. Ni hatari kubwa zaidi pale inapokuwa ni watu wenye Akili na Utashi wanaamua kwa makusudi mazima kwenda huko kwenye Hatari mtoni ilhali wanajijua kwa uhakika kwamba endapo likitokea la kutokea hawana maarifa ya kujiokoa.
 
Kumbe ukiacha mafuriko yanayosababishwa na mitaro ya reli kuelekezwa kwenye makazi ya watu, bado kuna ya mto!!!
 
Kumbe ukiacha mafuriko yanayosababishwa na mitaro ya reli kuelekezwa kwenye makazi ya watu, bado kuna ya mto!!!
Dah! Jamaa wanapata mafuriko mawili. 1. Kutoka mitaro ya reli, 2. Kutoka kwenye mto. Pole zao sana.
 
Ni shughuli zinazofanywa na binadamu mwenye akili na utashi. Wanaomwaga sumu; wakiamua wanaweza kuacha au kutafuta mahali mbadala pa kumwaga sumu hiyo.

Binadamuu (Watu) wenye akili na Utashi wanafahamu fika kwamba maji hayo ni Hatari kwa Afya zao lakini bado kwa makusudi wanayatumia majumbani. Kwa nini wasiyaepuke?

Wanaomwagilia mbogamboga na mazao mwengine mashambani ni Binadamu mwenye akili na Utashi. Watu hao wakiamua kwa kuzingatia matokeo mabaya ya matumizi ya maji hayo wataacha. (Hata hivyo kiwango cha athari kwa Ulaji wa mazao sio changamoto sana).

Hiyo 👆 ni kweli.

Hii imekaa kiimani zaidi. Ni sawa na kusema Wanaoteka watu siku za nyuma Utekaji watu haukuwepo.

Wewe Ungeshauri wafanyeje mkuu?

Watu( Binadamu mwenye akili na Utashi) amini asiamini, hata ungetumia bunkers au electrified fence; binadamu akiamua kupita atapita tu. Ila ng'ombe unapiga sanzu tu inatosha- hawapiti.
Nimebold neno Binadamu mwenye akili na Utashi kuonesha ni kwa kiwango gani hayo uliyoyaita ni kero; Mhusika mkuu ni Waathirika wenyewe. Wakiamua wanaweza kupata ufumbuzi au suluhisho.
Naona wafanyakazi wa kiwanda cha MO umekuja ,
Unajua kiwanda cha MO kinavyo mwaga maji machafu kwenye kiwanda chake cha textile.

Mo alitakiwa Aya treat maji humo humo kiwandani kwake , yatoke yakiwa meupe, Kuna kipindi cha jk Kuna waziri alifika kiwandani hapo na akakiri uharifu wa mazingira unao fanywa na kiwanda cha MO na kuamriasha kiwanda hicho kufuata Sheria .lakini jamaa ni MTU anayependa kitonga, ku treat maji anaona ni gharama zinaongezeka ,kwake ni bora TU ayatiririshe mtoni ,(rangirangi na harafu Kali za kemikali)
 
Mto sio kero ulitaka wachimbe hayo maeneo? wangekunyang'anya shamba lako ndio ungesema kero labda
 
Back
Top Bottom