#COVID19 Wanaoipinga chanjo ya Covid-19 ipo siku watapanga foleni kuchanjwa

#COVID19 Wanaoipinga chanjo ya Covid-19 ipo siku watapanga foleni kuchanjwa

Kuna tofauti kati ya kuamini sayansi na kuamini wanasayansi,tafiti za kisayansi zinafadhiliwa na wasio wanasayansi na hawafanyi hivyo kwa sababu ya kuamini sayansi.
 
Corona ni ugonjwa wa wazee kwahiyo inabidi tuwaweke lockdown wazee na sie vijana tuendelee na maisha kama kawaida,kwa kufanya hivyo tutaondoa hivi vifo vya wazee na kupunguza wingi wa wagonjwa huko hospitali.

Nasema uongo ndugu zangu?
 
Kuna watu wanaishi kwa kuamini kila taarifa.Kwa ujumla ulimwengu wa leo unaendeshwa na habari za uzushi na uongo.Unaposikia au kuambiwa jambo lolote lazima ulichekeche. Ndio maana tukaambiwa akili za kuambiwa changanya na za kwako.

Kuhusu chanjo ya Covid-19, kuna watu tena viongozi wakubwa wa nchi wanasema eti wazungu wanataka kutuangamiza sisi ngozi nyeusi hasa Wafrika eti kupitia hii chanjo.Hiki ni kichekesho kabisa.

Wazungu waliotengeneza chanjo ya Covid-19 ndio waliotengeneza chanjo ya Polio,Kansa ya shingo ya kizazi, hadi chanjo za magonjwa ya mifugo.
Ni hawa hawa ndio wanaotutengenezea vifaa tiba na madawa ya magonjwa mengine km Malaria,Kifua kikuu,STDs,UTI, n.k. Km kweli wangekuwa na ajenda ya kutuua na kutuangamiza si wangeshafanya hivyo "a long ago" kabla ya uwepo wa kizazi chetu cha kuhoji hoji na kudadisi mambo??? Sisi tumeshindwa kutengeneza hata "tooth pick" sembuse chanjo ya Covid-19? Jamani!! Tuache mzaha beee!

Ajenda pekee ya mzungu na mataifa yaliyoendelea ni kuona Wafrika tukiendelea kuwategemea wao kwa kila kitu ili tuendelee kuwa soko kwa bidhaa zao na hatimaye waendelee kututawala. Kama kweli hatutaki kutawaliwa kibiashara na kiuchumi basi tuanze kuchukua hatua za kimkakati na sio hizi za kukurupuka.

Afrika ndio bara lenye idadi kubwa ya vijana,na idadi hii itaendelea kuongezeka muongo kwa muongo. Idadi hii ya vijana inatengeneza soko kubwa kwa bidhaa za kisasa km smartphone,Tvs,nguo, nk. Hivyo wazo la kuangamiza Waafrika ni wazo la mtu asiyejua mifumo ya kibiashara ya dunia ya leo. Kumuangamiza Mwafrika ni kuangamiza biashara ya dunia nzima.

Dunia ya leo ni vigumu kuishi ukitegemea kile unachokiamini peke ako.Tuko katika zama za kuingiliana sana. Kukataa kabisa chanjo ya Covid-19 ni kukataa biashara na wenzako na mwishowe utajikuta umetengwa "and you will suffer the consequences".

Leo hii kitu pekee wanachojivunia Korea Kaskazini ni kumiliki mabomu ya Nyuklia basi. Lakini wananchi wake wanaendelea kuishi katika umasikini wa kutupwa kwa sababu ya kuchukua misimamo mikali isiyo na tija.

Ni kweli hatutakiwi kupokea kila kitu kama jalala lakini si vema kujifanya kichwa ngumu wakati hao tunaowaletea ukaidi ndio wanaotufanya tuwe hivi tulivyo.

Tupokee chanjo ya Covid-19 kiroho safi tu, huku tukiendelea kumuomba Mungu atuepushe na hili janga. Hamna namna wajameni.!
Swali ni kwamba chanjo ya COVID 19 ni ipi? Kila nchi ina chanjo yake nyingine hadi 2 ambazo wanasema "zinaonyesha matokeo mazuri" chanjo zilizopo bado hazijajaribiwa Afrika kujua km hayo matokeo mazuri yatapatikana kwa hiyo viongozi wetu wapo makini hawataki tuwe sehemu ya majaribio. Mara WHO itakapokuwa na chanjo halisi kwa virusi hivyo hakuna nchi itaacha kuchanja wananchi wake, tuwe na subra.
 
Elon Musk huyu ni tajiri yeye kashasema hawezi kupata chanjo hayupo kwenye hatari ya kupata Corona

Ndugu wewe kwenye ukoo na Family yenu mmezika wangapi waliopata Corona.
Kwa nini tukilimbie chanjo wakati hatupo kwenye hatari ya kupata Corona
 
Wewe tafuta chanjo, chanjwa endelea na maisha, wasiotaka waache, HUJAKATAZWA MKUU, NENDA KACHANJWE..
 
Elon Musk huyu ni tajiri yeye kashasema hawezi kupata chanjo hayupo kwenye hatari ya kupata Corona

Ndugu wewe kwenye ukoo na Family yenu mmezika wangapi waliopata Corona.
Kwa nini tukilimbie chanjo wakati hatupo kwenye hatari ya kupata Corona
Ndugu zetu wengi wanakufa. Taaarifa ya daki inaonyesha chanzo cha kifo ni pneumonia.
 
Wewe tafuta chanjo, chanjwa endelea na maisha, wasiotaka waache, HUJAKATAZWA MKUU, NENDA KACHANJWE..
Niende nikachanjwe wapi wakati mzee meko kakataa kuipokea? Hata nikienda Kenya bado mm simo katika bajeti
 
Hajakataa Ila alisema tujipe muda

Maneno matupu hayavunji mfupa. Kweli hajakataa?

IMG_20210214_214251_251.jpg


Hivi anajua kuwa tuna janga? Janga hili linamhusu? Katamka hataki kusikia hadithi za Corona. Yeye anataka kazi tu.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Corona ni ugonjwa wa wazee kwahiyo inabidi tuwaweke lockdown wazee na sie vijana tuendelee na maisha kama kawaida,kwa kufanya hivyo tutaondoa hivi vifo vya wazee na kupunguza wingi wa wagonjwa huko hospitali.

Nasema uongo ndugu zangu?
 
Wenzako walienda nje kuchanjwa na badala yake wakatuletea korona ya ajabu ajabu, hizo zinazoitwa chanjo hazina life-long immunity, itabidi uchanje kila baada ya miezi 6. Yaani makampuni ya kutengeza hiyo dawa inayoitwa chanjo yatapiga hela balaa, na watu wataendesha maisha kwa ncha ya sindano.....maisha ya kitumwa yaani.
 
Hivi kuna mtu anapinga chanjo?, Au anashauri ipatikane iliyothibitishwa ni bora zaidi, kuliko sasa ni nyingi hata nyungu zetu tunaweza sema ni kundi la chanjo
 
Back
Top Bottom