Wanaolilia legacy ya Hayati Magufuli someni alichoandika Bollen Ngetti

Kuacha legacy ni jambo moja, na watu waliaochiwa legacy kufanikiwa kuiendeleza legacy hiyo ni jambo jingine.

Ni kweli kabisa Mwalimu Nyerere ameacha legacy lakini je, tunafanikiwa kuifuata na kuendelea kuifuata kwa kiwango gani? Na kama hatufanikiwi, ni kwa nini, wakati legacy aliyoaicha tunaipenda?

Kwa Tanzania ya wakati huu, bora kiongozi akaacha kumbukumbu kama vile ya kujenga angalau darasa la moja tu shule ya msingi kuliko kuacha legacy

Legacy za viongozi wetu hatuwezi kwenda nazo na kuziendeleza kama tunavyopenda kutookana na ukweli kuwa kwa wakati huu tunao maadui wengi mno walitapakaa ndani na nje ya nchi, na wana nguvu kuliko sisi

Hata hivyo, maadui hawa wanaotuletea shida kufuata legacy za viongozi wengi hawawezi hata siku moja kuja na kubomoa Tanzanie Bridge iliyojengwa na Rais SSH

Kwa hali hiyo ni bora viongozi wetu wakaendeea na Magufulification style na si kujikita kwenye kuacha legacy ambazo waTanzania hawawezi tena kwenda nazo kama inavyotakiwa kwa sababu hawana uwezo wa kufanya hivyo.
Kama hoja yako nimeielewa lakini
 
Hivi kuanzisha mfumo wa vyama vingi mwaka 1992 haitoshi kusema mwinyi aliacha legacy
Hapana; legacy ni kama model ya kitu au jambo ambayo kiongozi huwa anaacha halafu watu wake wanakuwa wanaitumia kila mara kama chombo cha kuwasaiidia kuendelea kutatua matatizo yao mbali mbali ya sasa na ya wakati ujao pia,

Legacy kwa maana nyingine, ni Falsafa sahihi na haifanyi kazi kwenye tukio la wakati mmoja tu kama vile lile la vyama vingi vya siasa
Legacy inafanya kazi kuanzia pale ilipoaznia na kuendelea hata milele
 
Hivi mtu mwenyewe alishakufa mbona bado watu wanaumia
Kulingana na mleta mada; huyu mtu Hayati JPM hajaacha legacy yoyote ila amefanikiwa kuacha matendo makuu ya ajabu ambayo hadi muda huu bado yapo kwenye Kumbukumbu za waTanaznia

Kulinagana na mwandishi ni kwamba Mwalimu Nyerere yeye alifanikiwa pia kuacha vyote, legacy na kumbukumbu za matendo makuu, kitu ambacho ni sahihi kabisa

hata hivyo, tahadhari pekee ninayopenda kutoa mimi hapa ni kwamba, legacy isipoambatana na matendo makuu inakuwa si lolote si chochote kwa sababu legacy ni FALSAFA tu, ambayo watu wakifanikiwa kuielewa vizuri na kutumia, wanaweza kufanikiwa. Hata hivyo ikitokea kwa bahati mbaya wakashindwa kuielewa au kuikubali, haiwezi kuwasaidia chochote na itakuwa haina faida yoyote kwao; kiasi kwamba wanaweza kumuona kiongozi bora kuwa ni yule aliyewahi kuwajjengea darasa moja tu la shule ya msingi, kuliko yule aliyewahi kuacha legacy ambayo haikuwahi kuambatana na matendo makuu au ambayo hawakuweza kuikubali

Mwalimu alifanikiwa kujenga viwanda nchi nzima na hicho ndicho wanachokikumbuka kwa akili zao zote hadi sasa kuzidi hata wanavyoweza kuwa wanaikumbuka FALSAFA yake ya Siasa ya Ujama na Kujitegema

Kwa hali waliyonayo kwa wakati huu, Watanzania wanahitaji kutendewa matendo makuu ya kuwapeleka kwenye maendelea na si kuaminishwa kwenye FALSAFA peke yake

Mungu aendelee na Mama SSH kwa kishindo kikuu
 
Ujamaa wa nyerere uko wapi? Hata iwe kawacha legacy hiyo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…