Elections 2015 Wanaomchafua Ben Saanane huu ndio wasifu wake

Elections 2015 Wanaomchafua Ben Saanane huu ndio wasifu wake

Watu wana wivu sana .
Wakiona mtu anataka kujiendeleza na kusaidia wengine
Kwa kile alicho jaliwa, basi watafanya juu chini wajaribu kuvuruga.

Wivu kitu kibaya sana .

Na sema kila kijana mwenye uwezo anae weza kusaidia nchi
Hii kwa kile alicho jaliwa , na ajitokeze.
 
Tunaomba wasifu wake kitaaluma yaani shule. Kasoma wapi msingi,sekondari kwa ujumla. Kasomea taaluma gani chuoni na kwa ngazi gani. Tupo pamoja
 
Ben ananuka mauaji nadhani kwa aliyoyasema mchage Ben anafaa sana kubaki cdm ili mauaji yaendelee

Kumbuka hajawahi kukanatuhuma za kumuua zit to kwa kumuwekea sumu kwenya soda

Hajawahi kukana tuhuma za kuregeza bolt kwenye gari za mph zitto na mtema

Hivi mauaji unayajua wewe au kuropoka tu? Hizi propaganda za kitoto mtaacha lini nyie?

Haya mwambie ZZK au CCM awachagulie CDM mwenyekiti wa Bavicha ili roho zenu zisuuzike.....nani mnamtaka Shona, Mwampamba, Mchange au Nyakarungu? Nani wampe m-relax na roho zenu?
 
Kuwa Na Elimu Kubwa Sio Kigezo Cha Kuwa Mwenyekiti Wa BAVICHA ....ila Tunaitaji Mtu Mwenye Sifa Za Uongozi na Mwenye Uwajibikaji Mkubwa Katika Masuala Ya Vijana Kisiasa,Kijamii hata Kimaendeleo..

Atuitaji Mtu Anayesifiwa Eti Alikuwa Rais au Waziri Wa Chuo ...Izo Ni Personal Icon Katika Maisha Sio Katika Uongozi wa Siasa.

Mwenyekiti Wa BAVICHA Ni zaidi Ya Kiongozi Coz Ni Mtu Ambaye Ndiye Atafit Viati Vya John Heche Na Kuendeleza.

NAWASILISHA HOJA BINAFSI JAMA.
 
Basi agombee peke yake manake umeandika wasifu wa upande mmoja inawezekana anaoshindana nao pia wanazo sifa kali kuliko Ben, kama mna imani ni bora mwacheni apambane sio mnamtafutia mbeleko kwa kuwapaka wenye mawazo tofauti na yenu.
 
Ongeza Wasifu wake Mkuu: Ali waingia wasaliti kasha akawafyekelea mbali wote hadi basha lao Zitto ....
 
Ben anauwezo unaohitajika sana sasa hivi kutokana na changamoto zilizopo sasa lakini pia tunamhitaji sana kwa bavicha ya kesho na cdm yenye nguvu
 
-Naona dalili za hofu na kupanic tu hata kabla hajachukua fomu makumi ya watu wameingiwa na hofu, wivu, hasira na chuki huku mamilioni ya Vijana tukiwa nyuma yake.

-Tutaendelea kumpigania na kumtetea dhidi ya wale wote wanaotaka kukiharibia chama chetu taswira yake kwa siasa chafu.

-Sio utamaduni wa CHADEMA na tunaomba kamanda Ben asiwajibu chochote atuachie watu hawa wapotoshaji tuwajibu kwa hoja.

1 Ben ni afisa wa idara ya sera na utafiti ya chama. Alikuwa afisa mwanzilishi wa maswala ya kanda makao makuu.

2-Ameshiriki katika vikao vya kiutendaji ndani ya sekretarieti na hata ndani ya kamati kuu.

-Ina maana anakijua chama kwa undani tofauti na uongo wa siasa chafu.

3-Kwa wadhifa wake ndani ya chama ndiye mshauri wa kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni juu ya maswala yote ya kisera au sijui kama nimekosea.

4-Amewahi kuwa kiongozi kuanzia shele na vyuo. Alikuwa kiongozi wa Jumuiya ya watanzania katika chuo cha Allahabad-INDIA.

-Amewahi kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanafunzi wa kimataifa chuoni.

- Kipindi kilichopita nilisoma tamko lenye wasifu wake,

-Amekuwa afisa utawala na fedha katika kampuni ya Relliance, General Manager wa makampuni ya Alpha.

5-Hajawahi kutuhumiwa kutoa rushwa kwenye uchaguzi. Alienguliwa kwenye uchaguzi kwa sababu za kikanuni hasa kuunganisha nguvu na wagombea wengine.

6-Mara kadhaa amekuwa akipata misukosuko na jeshi la polisi na amekuwa na msimamo imara mara zote.

7-Kama isingekuwa anaaminika basi asingeruhusiwa kushiriki vikao vya sekretarieti na kamati kuu ya chama.

8-Anayemchafua Ben anatumiwa na baadhi ya wagombea kwa kuwa ukiwafuatilia atakuwa anamtusi Ben halafu wakati huo huo anamsifu mgombea mwingine.

9-Anayemchafua anahasira kutokana na alikuwa anawaonea huruma wasaliti waliofukuzwa na chama ambao Ben alichangia kwa kiwango kikubwa kuwafichua.l

10-Nimesikia jina "MAHAWARA" Linatajwa kuna nini?

Mwisho nawaasa tupambane kwa hoja kwa ajili yaku na BAVICHA imara kwa manufaa ya Watanzania

Mimi Alexandry NEMESI

0766468851
nyie watu wa siku hizi mnastaajabisha. nilidhani unatoa cv yake kumbe unatoa maoni tu. sasa wasifu ndio nini! hujasema ben ana elimu gani na ya wapj....huoni kama ni muhimu?
 
Ben sa8 ni kanjanja hata alichokuwa anasomea India hakieleweki alijitungia tu kama ana cheti muomben aweke kivuli cha cheti chake hapa!nawahakikishia hana vyeti vya degree wala Masters anayojitapa kaipata huko India,ameshindwa kupata kazi zaidi ya mara3 akiambiwa leta vyeti anapiga sound ila muwekeni tu huyo agombee apate kura kama alizopata Elly Mamuya ashike adabu,yeye siasa zake mwisho jf tu
 
Daima ukweli utasimama ni bahati mbya mnatumia mbinu za kizamani,

Umnafki namba moja na kundi lenu Ben aliwaacha uchi.


Kwanza naheshimu sana mchango wako na andiko lajo kuhusu Ben Saanane.

Pili binafsi nafuatilia sana maandiko na harakati za Ben saanane kwa maoni yangu huyu kijana anafaa kwenye nafasi ya utendaji zaidi mfano Katibu Mkuu wa BAVICHA ninaimani ataitendea haki nafasi hiyo.
Nafasi ya uenyekiti inahitaji mtu mwenye mvuto jukwaani anayeweza kuvutia umma ukamskiliza na kushawishi na umma ukashawishika (Hapa simaanishi Ben hawezi hapana ila ninawasiwasi na hili) pili awe ni mtu asiyeweza kuogopa vyombo vya dola,CCM na vitisho vyao (hapa simaanishi Ben hawez ila ninahofu).

Tatu na mwisho mwenyekiti anatakiwa ni kijana/mtu ambaye hajawahi kuwa na kashfa yeyote ndani ya chama ili kuwe na uamnifu kutoka kwa makundi na kuwaunganisha vijana wote ndani ya chama.

Nikiwaza haya nakuja na hitisho kuwa Ben Saanane nafasi ya katibu mkuu inamfaa sana ndani ya BAVICHA coz ni mtendani,mpanga mipango mzuri,mwanamkakati mzuri. I stand to be collected.
 
Last edited by a moderator:
Pambana lakini mwisho wa siku msije mkaitana wasaliti maana chadema sasa mbio za kugombea zipo hi hi tusubiri vita vya matusi.
 
Wanabodi heshima kwenu,

Kama mnavyojua kwa mujibu wa ratiba ya uchaguzi wa ndani wa Chama makini (CHADEMA) Unaendelea kwa kasi na kwa mafanikio makubwa katika maeneo mbali mbali ya Taifa letu,Uchaguzi huo unajumuiya pia Uchaguzi wa mabaraza ndani ya chama mojawapo likiwa ni Baraza la Vijana (BAVICHA).

Katika nafasi mbalimbali ndani ya BAVICHA kunatarajiwa kuwapo na ushindani mkali mojawapo ikiwa Mwenyekiti atakayechukua nafasi ya anayemaliza muda wake kwa mafanikio makubwa ndugu john @Heche,Katika nafasi hyo anatajwa sana Ndgu Ben saanane kama mmoja ya wagombea watarajiwa na mwenye nafasi kubwa ya kushinda nafasi hyo.

Nimekuwa mfuatiliaji mzuri wa Mwenendo wa Ben saanane nje na ndani ya Chama kimkakati hasa kiutendaji na pale ambapo maadui wanapojaribu kufanya upotoshaji au njama yoyote ovu ambyo inapangwa kwa namna moja ama nyingine kuchafua taswira njema ya Chama Kitaifa na kimataifa,Kimsingi CHADEMA inamhitaji zaidi mtu aina ya Ben saanane ndani ya BAVICHA hasa wakati huu tunapoelekea Uchaguzi wa serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom