Wanaopewa ajira kwenye vyombo vyetu vya ulinzi wawe wanaoipenda kazi hiyo kwa moyo na kujivunia kuifanya

Kiranja wa jamii

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2023
Posts
441
Reaction score
1,065
Yanayoendelea sasa kwa baadhi ya askari wa jeshi la polisi ni matokeo ya watu kufanya kazi wasiyoipenda. Hawawezi kuifanya kwa ufanisi.

Hapo zamani za kale kimbilio la waliokosa ajira ilikuwa fani ya ualimu. Kilichotokea ni kushuka kwa kiwango cha elimu nchini kwasababu ya kukosa morali ya kufanya kazi kwa walimu.

Siku za hivi karibuni kwenye elimu hakuna ajira mpeto mpeto tena na wanaotakiwa kusoma fani hiyo wanatakiwa wawe na ufaulu mzuri tofauti na ilivyokuwa awali.

Pia soma: Simiyu: Mkuu wa Mkoa athibitisha kifo cha Mtu mmoja katika Maandamano ya Busega

Toka zamani za kale kwenye majeshi yetu wamekuwa wakipokea vijana wenye ufaulu tofauti tofauti kuanzia wenye ufaulu wa juu, wa kati, wa chini na hata waliofeli.

Hata hivyo, tofauti na zamani za kale ambapo walioomba kujiunga na majeshi yetu walikuwa wale "wanaopenda" /wenye hobby ya kazi hiyo awe amefaulu au amefeli, siku hizi huko kwenye majeshi imekuwa kimbilio la waliokosa ajira.

Ukiangalia vijana wanaojiunga na majeshi yetu hata wale ambao ni wahitimu wa chuo kikuu, kwa asilimia kubwa halikuwa chaguo lao la kwanza. Wengi wanaenda ilimradi ni ajira itakayompa kipato na mbaya zaidi hata wanaoingia huko baadhi yao wanavutwa na "wajomba".

Matokeo yake ndio hiki kinachoendelea kwasasa kwenye baadhi ya maeneo hasa upande wa jeshi la polisi.

Weledi umeporomoka kwa kiasi kikubwa kwasababu walioko huko hawana furaha na kazi yao kwasababu halikuwa chaguo lao.

Sehemu ya kutumia maneno, wanatumia risasi za moto. Kwasababu wanajua kukoki silaha tu na kurusha risasi, hawana muda wa kutumia akili zao kwasababu hata mafunzo hawakuyazingatia kwani haikuwa hobby yao.

Tabia ya wazazi kuwalazimisha vijana kwenda kufanya kazi sehemu ambayo sio chaguo lao kwasababu za kujipatia kipato ni kudidimiza maendeleo ya nchi na ustawi wa jamii.

Daktari anayefanya kazi hiyo bila kuipenda hatawaheshimu wagonjwa kwasababu hakujiandaa kuwa daktari. Matokeo yake wagonjwa wengi watakufa mikononi mwake, wengine wataongeza usugu wa magonjwa kwa kupewa dozi isiyo sahihi. Hali kadhalika kwa askari anayefanya kazi hiyo ambayo haikuwa chaguo lake.

Ili ufanikiwe na ufanye kazi kwa weledi lazima ufanye kile unachokipenda na unakiweza na unajivunia kukifanya. Kazi yako ukiipenda utaifanya kwa weledi na hautopenda ichafuke.
 
Mimi nashauri waache pia kuajiri watu wenye D mbili pekeee kwenye vyeti vyao vya form four.
 
Asilimia 90 plus ya Askari Police ni watu ambao wali fail mitihani kidato cha 4 au 6. Wengi sana ni kidato cha nne. Ambao walipata Zero au Division 4 iliyo dhohofu sana.

Mimi nimesoma O Level na jamaa zangu wawili ambao walikuwa watukutu sana. Hawa walikuwa ni ndugu. Wavuta bhangi na mmoja alikuwa pia mwizi mzuri sana. It was a boarding school. Alikuwa akiiba hadi nyama na wali kwa siku za nyama na wali.

Huyu mmoja yeye alikuwa angalau si mwizi wa kutambulika. Ila alikuwa anavuta sana bhangi na kutukana. Kifupi jamaa walikuwa watu wa hovyo. Matokeo ya mwisho waliambulia zero.

Kwa sasa ni Askari polisi wapo Mkoa flani pembezoni mwa nchi.

The same A Level namfahamu ndugu yangu ambaye alikuwa mbabe sana. Alikuwa anapenda yale maisha ya black americans kule America. Wanawake, pombe, bhangi, ugomvi. Na alikuwa na tattoo ya Nanga. Alikuwa akikamatwa kila wakati akihusishwa na matukio mabaya. Analala ndani siku mbili tatu anatoka.

Nikaja kutana naye miaka ya 2000 akiwa ni Askari. Na ile tatto alijiunguza na pasi ili itoke. Pamebaki kovu tu. Bado jamaa hajaacha uharamia. ila kwa sasa ana kitambulisho na uniform ambazo zinampa uhalali wa kufanya uharifu.

Asilimia kubwa sana ya Askari police na wanajeshi kiasi ipo hivyo. Angalau kwa wanajeshi huwa nidhamu inasisitizwa sana na hatukutani nao sana kwenye maisha ya kila siku. Ila ikitokea nao utaona ni wale wale tu.

Kwa kiasi kikubwa askari polisi wetu uelewa wao mdogo, hawajiamini, hawajui kujenga hoja, wanapenda kuonekana wababe, hawafikirii, wana upeo mdogo, hawana Elimu.

Wachache sana utawakuta na sifa hizo na hawa huwa hawapewi vyeo vikubwa sana. Sababu huwa wanaonekana hawajaiva au kukomaa kuwa polisi.

Serikali duniani zinapenda kuwa na police kama mbwa ambao hawana akili. Ili akimwambia shika huyo anaenda shika. Haulizi kwa sababu gani. Akiambiwa muume huyo anauma bila kuuliza why.

Sasa mbwa hao pia huwa wanakuwepo vichaa na hawa sababu hawapati matibabu kwa wakati au hawapati kabisa basi huanza hata kuuma uma hovyo. Kuna ambao hupenda harufu ya damu. Nao wanapitia humo humo.

Mi Namshukuru Mungu katika familia yetu hakuna ambaye alilaaniwa kuwa police. Yule wa upande wa Mama ambaye ni police pamoja na kuwa ana cheo watu wanamdharau sana katika ndugu. Hana heshima na hatembelewi kabisa. Analalamika sana kuwa ni kama ametengwa. Watu wanasema tu kwa pembeni kuwa anafanya kazi ya laana toka miaka ya nyuma.
 
Asilimia 90 plus ya Askari Police ni watu ambao wali fail mitihani kidato cha 4 au 6. Wengi sana ni kidato cha nne. Ambao walipata Zero au Division 4 iliyo dhohofu sana.

Mimi nimesoma O Level na jamaa zangu wawili ambao walikuwa watukutu sana. Hawa walikuwa ni ndugu. Wavuta bhangi na mmoja alikuwa pia mwizi mzuri sana. It was a boarding school. Alikuwa akiiba hadi nyama na wali kwa siku za nyama na wali.

Huyu mmoja yeye alikuwa angalau si mwizi wa kutambulika. Ila alikuwa anavuta sana bhangi na kutukana. Kifupi jamaa walikuwa watu wa hovyo. Matokeo ya mwisho waliambulia zero.

Kwa sasa ni Askari polisi wapo Mkoa flani pembezoni mwa nchi.

The same A Level namfahamu ndugu yangu ambaye alikuwa mbabe sana. Alikuwa anapenda yale maisha ya black americans kule America. Wanawake, pombe, bhangi, ugomvi. Na alikuwa na tattoo ya Nanga. Alikuwa akikamatwa kila wakati akihusishwa na matukio mabaya. Analala ndani siku mbili tatu anatoka.

Nikaja kutana naye miaka ya 2000 akiwa ni Askari. Na ile tatto alijiunguza na pasi ili itoke. Pamebaki kovu tu. Bado jamaa hajaacha uharamia. ila kwa sasa ana kitambulisho na uniform ambazo zinampa uhalali wa kufanya uharifu.

Asilimia kubwa sana ya Askari police na wanajeshi kiasi ipo hivyo. Angalau kwa wanajeshi huwa nidhamu inasisitizwa sana na hatukutani nao sana kwenye maisha ya kila siku. Ila ikitokea nao utaona ni wale wale tu.

Kwa kiasi kikubwa askari polisi wetu uelewa wao mdogo, hawajiamini, hawajui kujenga hoja, wanapenda kuonekana wababe, hawafikirii, wana upeo mdogo, hawana Elimu.

Wachache sana utawakuta na sifa hizo na hawa huwa hawapewi vyeo vikubwa sana. Sababu huwa wanaonekana hawajaiva au kukomaa kuwa polisi.

Serikali duniani zinapenda kuwa na police kama mbwa ambao hawana akili. Ili akimwambia shika huyo anaenda shika. Haulizi kwa sababu gani. Akiambiwa muume huyo anauma bila kuuliza why.

Sasa mbwa hao pia huwa wanakuwepo vichaa na hawa sababu hawapati matibabu kwa wakati au hawapati kabisa basi huanza hata kuuma uma hovyo. Kuna ambao hupenda harufu ya damu. Nao wanapitia humo humo.

Mi Namshukuru Mungu katika familia yetu hakuna ambaye alilaaniwa kuwa police. Yule wa upande wa Mama ambaye ni police pamoja na kuwa ana cheo watu wanamdharau sana katika ndugu. Hana heshima na hatembelewi kabisa. Analalamika sana kuwa ni kama ametengwa. Watu wanasema tu kwa pembeni kuwa anafanya kazi ya laana toka miaka ya nyuma.
 
Kuna askari mmoja wa kike nilienda kituo kimoja aisee yule dada Mungu ambariki sana yule ni zaidi ya askari alitoa ushirikiano mzuri sana.
Kwanza kauli zake tu unajua kweli huyu yuko kusaidia jamii mpaka namaliza kumtoa ndugu yangu mwenyewe bila hata kuniomba nilimpa asante ya wekundu wawili.
Askari wastaarabu na wanao ipenda kazi yao wapo ila wengi wao dah?!!Sijui akili zao wameziachaga wapi.Mtu umeenda kituoni kumtoa ndugu yako unaanza kufokewa km mtoto. Sometime ni kuheshim serikali tu ila mtu unaweza kumtoa kolomeo mtu maana anae kufokea ukimwangalia ni fala mmoja kavaa sare....harafu hata sababu ya kukukoromea hana ni ubabe wa kijinga tu.
 
Sio lazima upate PT 32.
Ukiwa tu huna akili, huwezi kujiongeza, uko tayari kupokea amri au kutumwa wewe Ni police material.
 
Back
Top Bottom