Kungwi Mtoto
JF-Expert Member
- Jun 27, 2018
- 796
- 776
hilo tu waliona je la mashekhe wanaizibua watoto mitaroo.. yule ustadhi wa mwanza aliyeshikwa ugoni kwa kuharibu vitoto alivyokuwa anavifundisha chuo..vepee!!! Msipende kuhukumu watu angalia matendo yako kwanza ..... kila mtu asimamie imani yake kikamilifu...Mapadri hawahawa waosifika kwa kuwazibua watoto mitaro afu ndo haohao wanaondoa dhambi?
Kweli imani zá watu!
Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa mbona unawasambulia wasabato tu? Kwani hamna walutheran, walokole, waanglicana, wamoravian, nakadhalika? Cha muhimu muombe Roho Mtakatifu akupe mwongozo wa kusoma biblia vizuri na akupe ufahamu wa kuelewa. Mungu akubariki sana
Sent using Jamii Forums mobile app
Kanisa la roma halijawahi kuwa la kweli hata siku moja, lenyewe ndilo lililo waua wakina petro.
Hahaah sasa mkuu tupo kwenye uhalali wa mapadri kusamehe watu dhambi! Wewe unakimbilia kwa wasabato! Hii maada inawahusu hao wasabato?Kanisa la sabato lililoanzishwa kwa misingi ya "kisangoma" (na hadi leo linaendelea na muelekeo huo huo),ndio la kweli?
Ombeni labda nisiwe hai na JF ifungwe. Nina orodha mambo ya mama yenu, Ellen White na wapiga ramli wenzie kama 1000 hivi, tena ya hovyo sana. Nitayachambua moja baada ya jingine tena kwa uweledi unaostahili. Ni lazima mfike mahali muelewe kwamba kupiga kwenu kelele haimaanishi kwamba watu hawakuwa na majibu ya ujinga na upotoshaji wenu.
Unajua kama padri nae huwa anaungama dhambi?Kwa jina la baba na mwana na roho mtakatifu.
Namwungamia Mungu Mwenyezi nawe padre wangu.Sikuungama tangu..........Niliondolewa dhambi, nikatimiza malipizi. Dhambi zangu ni hizi......
Najuta dhambi zangu zote.
Ee Yesu unihurumie.
Huo hapo juu ndio utaratibu wa kuungama wakatoliki. Je kuna mahali panaonyesha kwamba wakatoliki huungama moja kwa moja kwa padre? Padre huwa ni msimamizi tu wakati muumini anamwungamia Mungu wake, na tena mwishoni ni yeye yule Yesu anayeombwa huruma yake.
Hebu tuache kushuhudia uwongo jamani, tutahukumiwa kwao.
Wakatoliki wenzangu naomba tufuatilie na kutetea imani yetu kwa nguvu zote na ushahidi usio na shaka.
Sent using Jamii Forums mobile app
Yesu wangu...unamaanisha walionje ya ukatoriki au wasioungama kwa padri wote ni motoni kwakuwa hawajasamehewa?Kama umesoma uzi vizuri utabaini kwamba uwezekano huo ungalikuwapo basi Yesu Kristu asingaliweka miundo mbinu hiyo ya Upatanisho.Kwa kuwa Yesu ni Mungu alijua watu kwa kujiungamia wenyewe wangaliishia kufanya sarakasi tu.Kuungama dhambi kunahusisha kufanya malipizi,waaidha kurudisha ulivyochukua kama alivyofanya Zakayo.
Ni kwamba tunalazimika kuungama dhambi ili mahusiano yetu na Mungu yawe mazuri.Dhambi ina madhara yafuatayo:mosi,inaleta mahusiano mabaya kati ya mwanadamu na Mungu.Pili,kati ya mtu mmoja na mwingine na tatu, kwa mtu mwenyewe.
Kumbe tofauti na Wakristu wengine wanavyoelewa, dhambi haiharibu tu mahusiano kati ya mwanadamu na Mungu, bali pia kati ya wanadamu na wanadamu.Mt.Paulo anatueleza mara nyingi sana katika barua zake kuwa sisi ni viungo katika mwili wa Kristu na kwamba yeye (nafsi ya Pili) na Mungu baba ni wamoja Rejea Warumi 12:5):
“Hali kadhalika ingawa sisi ni wengi, tu mwili mmoja kwa kuungana na Kristo, na kila mmoja ni kiungo cha mwenzake.”
Kwa hiyo, ni mantiki hiyo kwamba kwa sababu sisi kila mmoja ni kiungo cha mwenzake,basi dhambi ya mtu mmoja haiishii katika kumuumiza mhusika pekee, bali madhara yake lazima yamguse na mwingine katika mnyororo ule ule unaotuunga kwa Kristu.(Rejea 1 Kor 12:26):
“26 Kama kiungo kimoja kinaumia viungo vyote huumia pamoja nacho. Kiungo kimoja kikisifiwa viungo vingine vyote hufurahi pamoja nacho.”
UNACHOONGELEA WEWE UNAMAANISHA KUTUBU
Injili ya Marko 1:1-5, nayo inatueleza kuwa watu walikuwa wanamwendea Yohana Mbatizaji wakishakutubu na wakishaungama dhambi zao, walibatizwa ili kupokea ondoleo la dhambi zao:
“4 Yohane Mbatizaji alitokea jangwani, akahubiri kwamba watu watubu na kubatizwa ili Mungu awasamehe dhambi zao. 5 Watu kutoka sehemu zote za Yudea na wenyeji wote wa Yerusalemu walimwendea, wakaziungama dhambi zao, naye akawabatiza katika mto Yordani”.
Katika ya aya 4 na 5 ya Injili hiyo ya Marko, tunapata maneno mawili “Kutubu” na “kuungama” ambayo yana maana tofauti.
Na mwinjili Marko, anapotuandikia hivyo anamaanisha kwamba kulikuwa na mambo mawili yanafanyika kwa mtaka ubatizo kabla hajabatizwa.Mosi, kutubu dhambi na pili,kuungama dhambi.
KUTUBU, kunatofuatiana na KUUNGAMA kwa sababu, kutubu ni hali ya kuugua moyoni.KUTUBU ni kitendo cha kujutia tendo fulani.Kutubu hufanyika moyoni, wakati kuungama kunafanyika nje ya nafsi ya mtu.
Kuungama ni kusema nje ya moyoni na mbele ya mtu mwingine kuwa umekosa.Kumbe, Marko anapotumia maneno hayo mawili sio kama anataka kutueleza maana ile ile moja ya kujutia dhambi moyoni bali kuweka wazi hizo dhambi zenyewe.
Yakobo naye katika 5:14-15, anatupatia picha halisi ya maana ya neno kuungama anapotumia neno “ungamianeni” dhambi zenu.Ikiwa Yakobo alitaka kumaanisha mtu kusema dhambi zake kimoyokimoyo, basi angalitumia neno jingine na wala sio ungamieneni:
“14 Je, yuko mgonjwa kati yenu? Anapaswa kuwaita wazee wa kanisa, nao watamwombea na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana.15 Wakiomba kwa imani mgonjwa ataponyeshwa; Bwana atampatia nafuu, na dhambi alizotenda zitaondolewa.16 Basi, ungamanieni dhambi zenu, na ombeaneni, ili mpate kuponywa. Sala ya mtu mwema ina nguvu ya kutenda mengi.”
Nafikri tutumie kiyunani ndicho ambacho kwa asilimia nyingi biblia imetoka ktk maneno ya kiyunaniAliyekufundisha hivyo, alisoma Biblia kwa kurukaruka. Maneno "Kristo" na "Kristu" ni maneno yenye maana sawa tu.La kwanza limetoholewa kutoka Kigriki na la pili limetoholewa kutoka Kilatini.
Kuhusu makasisi ni kweli wanashida na hata yule aliyepita ni matatizo yalisababisha ajiuzuru si kama alipenda. Hata huyu wakimkomalia ataenda na maji. Na akijiuzuru huyu waafrika weusi mtapata papa wa kwanza.Mbona bado uko hapa tu? Nilifikiria umeshafika Vatikani kwenda kumshinikiza ili ajiuzulu upesi kama anavyotakiwa.
Ok ni sawa. Ndiyo maana wengi tumezoea Kristo kwasababu biblia iliandikwa ktk kigiriki na kiyunani ktk lugha ya mwanzo.Hii nchi tunasafari ndefu..
Na tatizo lingine ni lugha yetu kiswahili imekiwa ni lugha masikini..inakopa maneno huku na huko .
Ni hivi mpendwa(Uende ukawaelimishe na wengine)
Hakuna tofauti ya maneno Kristo na Kristu...maneno yote hayo mawili yametoholewa kwenye lugha mbili za Biblia...yaani Kilatini na Kigiriki..
Kristu.....ni kilatini..."Kristus"...sisi kwa kiswahili tukatohoa Kristu..
Kristo...ni Kigiriki..."Kristos".....sisi tukatohoa kwa kiswahili Kristo .
Ukifuatilia kwa makini maneno mengi ya Kilatini yanaishia ni ....us-
Mfano...Augustus, Cornelius, Titus, Anacketus, Thaddeus...
Vivyo hivyo kwa Kigiriki
Ahsante
Kanisa lina maana nyingiRoman Catholic ndiyo kanisa aliliacha Yesu na akirudi atakuta kanisa moja aliloliacha
Sijawai kwenda kwa padri kufanya hivyo. Je mimi ni mkosefu ?Ni kuhani...ndiye aliyepewa mamlaka ya kufundisha neno la Mungu ili watu waupate uzima wa milele...
Pia ndiye aliyepewa mamlaka ya Kusamehe dhambi kupitia kwa Yesu Kristo
Suala hapa sio kutubu dhambi kwa Padri au hadharani ..Walokole wanawazungumzia wanaoenda mbele ya padri (mmoja). Sasa je huko kwa Waprotestanti unapotaja dhambi zako hadharani huku TV ikirusha matangazo? Huwa nawashangaa Waprotestant, wanakuwa wakipinga jambo fulani la RC, lakini kwa mlango wa pili wanalitekeleza. Mtu unashika microphone unaongea katika LIVE TV broadcasting mbele ya ulimwengu jinsi ulivyokuwa malaya, ulikuwa jambazi, ulikuwa mchawi ukasababisha ajali ishirini za magari, ulikuwa mlevi wa kupindukia, ulikuwa unakashifu Roho wa Bwana, je, vyote hivyo kuviongea mbele ya madhabahu huku TV ikikurusha LIVE duniani kote, halafu unakuja kumshangaa Mkatoliki anavyoungama dhambi zake mbele ya padri! Maajabu hayatawaisha Waprotestanti!
nilikuuliza hukujibu hata wwBado hujajibu swali nililokuuliza...
Ukipata jibu nitaku-quote post yako...
Hakuna swali ambalo mnauliza halijajibiwa na post ya kwanza(uzi)...nilikuuliza hukujibu hata ww
Kwani wewe unatumia nini...??Mtoa mada najua umetumia muda mwingi kukaririshwa vitu vingi ili uwe kibaraka wao. Ila kwa kipindi hiki mnaelekea kukwama kabisa! Hakuna tena wa kudanganyika na vitabu vyenu vyenye tafsiri isiyo rasmi.