Wanaopinga kuungama dhambi kwa Padri, ndio wapinga Kristo wanaohubiriwa na wasabato na ndio wale wanaosoma maandiko kwa kurukaruka.

Wanaopinga kuungama dhambi kwa Padri, ndio wapinga Kristo wanaohubiriwa na wasabato na ndio wale wanaosoma maandiko kwa kurukaruka.

Unasema "Leo hatuna haja ya kuungama kwa Padre kwa sababu tunaye Yesu Kristo kuhani mkuu na mwombezi"

Sasa kwanini huwa unaenda kanisani na unasikiliza maubili na mafundisho ya watumishi hata usikae mwenyewe kwako ukaomba peke yako kama unajua na kuamni Yesu Kristo yupo na huitaji kuwategemea wanadamu au watumishi???

Sent using Jamii Forums mobile app
EBR. :10:25
wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia.

Ukiwa na lingine utaniquote tena
 
Nipe kifungu cha biblia kinachosema ubatizo ni function ya quantity badala ya quality.

Sent using Jamii Forums mobile app

Hivi umelewa au umekula maharagwe ya kutoka Afghanistani? Mimi nimekuambia kwamba ubatizo ni function ya "Quality" na sio "Quantity". Na nikasema kama unadhani ubatizo ni function ya Quantity kawahini kuweka order za sabuni za kufulia na kuogea za OMO na Mshindi viwandani.Upo?
 
Mi
1. Kwa hiyo umeambiwa Binadamu hawezi kuondoa dhambi? Kajisomee
Zaidi ya Yote, Marko 2:5-10. Baadhi ya watu walipotilia shaka suala la Yesu katika ubinadamu kuwaondolea watu wengine dhambi, Yesu aliwathibitishia kuwa mwana wa mtu anao uwezo huo wa kuondoa dhambi za walimwengu:

“5Yesu alipoona imani yao, akamwambia huyo mtu aliyepooza,“Mwanangu, umesamehewa dhambi zako.” 6 Baadhi ya waalimu wa sheria waliokuwa wameketi hapo wakawaza mioyoni mwao, 7 “Anathubutuje kusema hivyo? Anamkufuru Mungu! Hakuna mtu awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake.” 8 Yesu alitambua mara mawazo yao, akawaambia, “Mbona mnawaza hivyo mioyoni mwenu? 9 Ni lipi lililo rahisi zaidi: Kumwambia mtu huyu aliyepooza, ‘Umesamehewa dhambi zako,’ au kumwambia, ‘Inuka! Chukua mkeka wako utembee?’ 10 Basi, nataka mjue kwamba Mwana wa Mtu anayo mamlaka ya kuwasamehe watu dhambi duniani.” Hapo akamwambia huyo mtu aliyepooza, 11 “Nakuambia simama; chukua mkeka wako uende nyumbani!”

2. Vile vile, kupitia Luka 5:24, tunaelezwa pia kwamba katika suala la uwezo wa Yesu kuwaondolea watu dhambi alifanya hivyo katika ubinadamu wake na sio kwa ule Umungu wake.

3. Mwinjili Matayo tena katika sura ile ya 18:15-20, anatudokeza jinsi Yesu kabla ya kuwapatia Mitume rasmi uwezo wa kuondolea watu dhambi, alipata kuwadokeza jambo hilo.Uwezo wa kufunga na kufungua ndio kule kuwaondolea watu adhabu za muda mfupi, zitokanazo na dhambi:

“15 Na ndugu yako akikukosa, enenda ukamwonye, wewe na yeye peke yenu; akikusikia, umempata nduguyo.16 La, kama hasikii, chukua pamoja nawe tena mtu mmoja au wawili, ili kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu kila neno lithibitike.17 Na asipowasikiliza wao, liambie kanisa; na asipolisikiliza kanisa pia, na awe kwako kama mtu wa mataifa na mtoza ushuru.18 Amin, nawaambieni, yoyote mtakayoyafunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni; na yo yote mtakayoyafungua duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni.19 Tena nawaambia, ya kwamba wawili wenu watakapopatana duniani katika jambo lo lote watakaloliomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni. 20 Kwa kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao.”
mifano yako yote Hanna padri naona yesu ndo anaefanya na kusamehe sasa apo sijui padre ye anaingiaje kuchukua nafasi ya yesu
 
Unataka aseme uongo wewe ulishaona kwenye biblia neno padre?

Kapingane na Waraka wa Yakobo 5:14:

“14 Je, yuko mgonjwa kati yenu? Anapaswa kuwaita wazee wa kanisa, nao watamwombea na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana.”

Neno “Wazee wa Kanisa” linamaanisha Kasisi.Biblia ya Kiswahili imejipatia neno “Wazee wa Kanisa” kutokana na neno la Kigriki (Lugha ya Agano Jipya) Presbyter lenye kumaanisha Kasisi au Baba au Padri.

Padri maana yake ni baba. Kumbe Yakobo anapowausia watu kuungama dhambi zao, anamaanisha wafanye hivyo mbele ya Mapadri ambao wao ndio wanapatiwa uwezo huo na Kristu.Kumbe, Kristu anauhisha mahusiano kati ya Mungu na mwanadamu kupitia kwa padri.

Huwezi kuwa umedandia maandiko matakatifu kwa mbele na ukafanikiwa kuyaelewa haya mambo.Basi, Imekula kwenu mazima.
 
Mambo ya kidunia yako tofauti na mambo ya kiroho. Ndio maana hata wanaokemea pepo wanakemea kwa jina la Yesu. Kama walipewa mamlaka mbona hawakemei kwa majina yao na mapepo yakatoka?

Kuna sehemu wanafunzi wa Yesu wakamjia wakamwambia hata kwa jina lako, mapepo yanatutii. Pepo hatoki kwa jina la nabii/mchungaji/kuhani/padre japo wao ndio wamefanya kazi ya kuomba. Hata kubatiza walipewa maagizo wawabatize kwa jina la baba na mwana na roho na sio wabatize kwa majina yao kwa sababu wao ndio wametenda kazi ile.



Sent using Jamii Forums mobile app

Kwani lini ulienda kuungama kwa Padri akakuondolea dhambi zako kwa jina lake badala ya lile la "Kwa Jina la Baba,Mwana na Roho Mtakatifu"? Hivi tunajadiliana na "msukule"?

Haya ndiyo madhara ya watu wanaokaa muda wote wanaang'aza macho angani kuona kama Yesu anarudi upesi.Akili zako hazipo kabisa kwenye mjadala bali ziko zinasikilizia sasa huko nje kama kuna vishindo vya Yesu kurudi.
 
Kuungama dhambi kwa Padre iko wazi sana kimaandiko. Tatizo ni walokole wengi kufikiri ukishaokoka hutendi dhambi tena. Wanajipa moyo kwa utakatifu wa kutotenda dhambi ambazo wao wanafikiri ndio dhambi ikiwemo uzinzi, kunywa pombe ( hata kama si mlevi) n.k lakini upo uovu mwingi tu wanatenda wakati mwingine kutokana na mafundisho hafifu juu ya dhambi.

Yapo mazingira unaweza kutubu mwenyewe kama upo katika sehemu ambayo hakuna padre na upo kwenye hatari.

Kingine ifahamike kitubio kinaanzia mbali kuanzia kujutia na kukusudia kuacha dhambi then unapoungama kwa Padre ni ukamilisho wa kitubio na kupokea msamaha wa Mungu na hasa inatia nguvu na faraja unaposikia Padre akitamka kwa niaba ya Kristo "umesamehewa dhambi zako usitende dhambi tena".

Sent using Jamii Forums mobile app
Naomba uthibitisho wa maaandiko palipo andikwa kuungama dhambi kwa padre.
 
Ukisoma hilo andiko lako kwa lugha ya Kingereza utaona neno forgiven ambalo limetoholewa kutoka lugha ya Kigiriki ambayo ndio iliyotumika kuandika agano jipya neno forgiven kwa Kigiriki lina maana AMPHIEN ambalo kwa Kingereza chake halisi ni have been literally

John 20:23 is not saying that Catholic priests have the authority to forgive sins. It is saying that Christian disciples have the authority to pronounce what sins "have been forgiven

Imebidi nikupe uhalisia though the choice is yours

Sent using Jamii Forums mobile app

1. Hivi Lugha ya kiingereza uliipatia wapi? Kwa Rasi Simba au kwa nani? How could the Deciples be able to pronounce the sins that are forgiven if they are in advance not aware of the particular sins?

2. Yaani umeenda kukopi ready made answers kutoka mitandao ya Ellen White bila hata kufanya editing na hivi ukashindwa kuona phrase ya kukunyongea? Angalia sasa unavyoumbuka.Unachokisema kwa majibu yako hayo ya kukariri "It is saying that Christian disciples have the authority to pronounce what sins "have been forgiven " yana tofauti gani na wanachofundisha wakatoliki?
 
imeandikwa wapi aliwapa mapadre mamlaka ya kusamehe dhambi
21 Basi Yesu akawaambia tena, Amani iwe kwenu; kama Baba alivyonituma mimi, mimi nami nawapeleka ninyi.
Yohana 20 :21

22 Naye akiisha kusema hayo, akawavuvia, akawaambia, Pokeeni Roho Mtakatifu.
Yohana 20 :22

23 Wo wote mtakaowaondolea dhambi, wameondolewa; na wo wote mtakaowafungia dhambi, wamefungiwa.
Yohana 20 :23



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ubatizo huondoa dhambi na maungamo huondoa dhambi.Kwani hujawahi kujibatiza mwenyewe kwa maana si unajua maji ndiyo yanaondoa dhambi na unafahamu fika yanapatika kwenye mito na maziwa au baharini?
Kama unaamini kwamba ubatizo unaondoa dhambi ni kwanini mnawabatiza watoto wadogo??? Huwa wana dhambi gani hasa???

NB:
UBATIZO HAUONDOI DHAMBI.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom