Wanaopinga mahakama Kadhi "Intellectual Arguments" only

Wanaopinga mahakama Kadhi "Intellectual Arguments" only

Status
Not open for further replies.
Duh, naona hoja ambayo ni intellectual argument ni mbili
1. inayohusiana na gharama za kuendesha kesi katika mahakama ya kadhi!
2. Waanzishe waislamu pekee

Majibu:

1. Gharama za kuendesha kesi hizo ni vema zitoke serikalini kwakuwa kadhi courts itakuwa pia imepunguza kwa kiasi kikubwa kesi za waislamu zinazofanywa na mahakama za serikali (inabidi tufanye calculation ili tupate kiasi hasa ni kesi ngapi za waislamu kwa sasa zipo mahakamani ambazo zinatakiwa kupelekwa kadhi courts na gharam yake ni shilingi ngapi each case..tukipata tuna transfer kiasi hicho kadhi courts

2. Ni muhimu kuanzishwa kisheria ili watu walioamua kufuata sheria hiyo wakubaliane na hukumu ya kadhi, kama itakuwa haitambuliki kisheria itakuwa haina maana kwasababu itakuwa hakuna tofauti ni kutokuwa na mahakama..kutambulika ni jambo la lazima ili iweze kuitwa mahakama..lakini kuhukumiwa huko ni optional siyo lazima..lakini unapokubali mahakama hiyo lazima ukubali hukumu zake..ok

tuache jazba nataka intellectual arguments ok

J

na hapo ndo kwenye tatizo. Point yako ya 2. Ikianzishwa kisheria tayari itakua imeingiliana na sheria za nchi yetu..nikimaanisha kua nchi yetu haina dini na hivyo haifungamani na umoja wowote wa kidini, ila kinchi-kimataifa inafungana na umoja wowote ule ambao hauna misingi ya kidini. Ndo maana ikasema wananchi na jumuiya zao za kidini ruksa kujiunga na jumuiya za kimataifa zenye misingi ya dini. Hope U get my point.
 
................... mleta mada amejielezea vizuri kuwa: Ndoa ya Kiislaam inatambulika kisheria, Je kwanini kataika mirathi iwe ni suala lisilo tambulika kisheria ? Ndoa na Mirathi vinaweza kutenganishwa ? (elewa Kiislaam ndoa ni Ibada na kufanya mirathi katika misingi ya kidini ni ibada pia) na linapokuja suala la uchangiaji gharama ndio inakuwa nongwa. Kwani Kodi inalipwa na jamii moja au na wengine wanalipa ? kwanini jamii moja ijifanye yenyewe ndio ina ultimantum ? Hapa ndio makubaliano ya Wakristo na Serikali (MoU) yanapoingia, kwanini kodi ya Watanzania kwa ujumla wao zilipie Taasisi za Kikistro ? Katika hili jamii zingine zilihusishwa ? consider yourself that ur an Interllectual and u a now answering the above arguments !
Sijui nieleze vipi ili nieleweke vema. Nitajaribu.
Sijakataa ndoa au mirathi kama ibada. Hoja inayotakiwa kujengwa ni kuweka taratibu za mirathi ziwiane na za ndoa ambayo tayari inakubalika kisheria. Taratibu hizo ni pamoja na kuwa na mtu au watu watakaoshughulikia. Hii ndio hoja inayotakiwa kuelezwa ili kila mmoja aelewe.

Kosa kubwa ni kuwa nguvu ya hoja inapotezwa na suala la uchangiaji. Na kwa bahati mbaya halielezwi kama uchangiaji tu bali linafungamanishwa na mambo mengine. Hapa hoja hugeuga na kuwa ' wao dhidi ya sisi'. Ni kutokana na kutoelewa ujenzi wa hoja jamii inachanganyikiwa kuwa waislam wanataka nini. Je wanataka mirathi katika mambo ya dini yao itambuliwe na ipewe nafasi au waislam wanataka kupata ruzuku kwasababu fulani anapata ruzuku. Ikifika hapo hoja inajiua yenyewe na watu wanaanza kuchangia mambo nje ya hoja.

Nitakupa mfano, lilipokuja suala la kadhi baadhi ya viongozi wa kiislam waisoelewa na wenye jazba wakaliongelea kama sharia ya dini.
Jamii nyingine ikaingiwa na hofu kuwa kwanini sharia itumike katika secular country. Zikazuka hoja za watu kukatwa mikono n.k. hali iliyopoteza kabisa hoja ya msingi.
Watu wakaelimishwa kuwa sio sharia in general bali sharia katika ndoa na mirathi na kuwa haitahusu makosa ya jinai.
Hapo wasio waislam wakaelewa na kusema hilo halina tabu kama watajitengenezea utaratibu wao. Na siku hizi hulisikii kwasababu limeelezwa kwa weledi na umma umelielewa.

Kosa lile lile linajirudia, badala ya watu kueleza umuhimu wa mirathi na ndoa kama vitu viwili katika kimoja, wamejikita katika kusema mbona ABC wanapata hiki. Sasa inaonekana suala si ibada bali kudai ruzuku. Ukiongelea mirathi na ndoa basi mweleshe asiyejua ufungamano wa vitu hivyo na sio kurukia mfumo kristo n.k. Hapa watu hawapambanishi simba na yanga.

Nasisitiza kuwa kama waislam wanaweza kufanya ibada zao bila msaada wa serikali sioni kwanini wasiombe suala la mirathi kama sehemu ya ibada likubaliwe kisheria kama sehemu ya ndoa tu na wajiwekee utaratibu wao wa kulisimamia wao wenyewe kama wanavosimamia ibada nyingine bila kuingiliwa na serikali.

Mwisho naomba unisome kama mchangiaji hilo la intellectual ni kubwa na inawezekana viatu hivyo siwezi kuvivaa, muhimu soma hoja
 
............
bado huna hoja ya ushawishi
!
Inategemea nani anataka kushawishika na utayari wa kushawishika.Ikiwa wewe tayari una opinion yako na unachotaka ni kujisikiliza kwa kupitia midomo ya watu wengine, ni dhahiri hoja yangu haitakushawishi asilani.

Hukumu za kesi wakati mwingine Majaji huzitoa kufuatia reference ya kesi nyingine
,


Kweli Stare decis na doctrines of precedent ni part of case law.Sasa wewe unataka kusema Tanzania itakurupuka tu kwenda kuchukua hukumu toka Kenya na Uganda? Na hata kama, hizo hukumu siyo binding but merely persuasive!

huongozwa na busara na mazingira ya kufanana na tukio ua kesi husika.

Still not binding.

Hili liko pia katika ushahidi, ambapo Wakili unaweza kujenga hoja (Authority) kufuatia maamuzi ya kesi fulani inayofanana na hiyo na Jaji akashawishika na kutoa hukumu (hata kama kesi ni ya 1920 !). Hivyo bado Mifano ya Kenya na Uganda matters !

Rejea my earlier argument

Mbona Wakoloni wa Kiingereza walikubali hii Mahakama ?

Ni wao, na jinsi walivyoona inawafaa.Umesahau pia kuzungumzia "native courts" chini ya mfumo wa kikoloni.


hebu onyesheni threat, yaani ambaye hahausiki atapoteza nini ?

Hakuna threat as such bali ni the way nchi ilivyo - secular state haiwezi kuburuta dini ya kila mtu ndani ya mifumo ya serikali.Mbona huzungumziii sheria za wakatoliki za ndoa chini ya sheria za kanisa?

Ndio maana mleta mada alileta angalizo la "Interllectuals" hivyo fuata ushauri wake kwenye kujenga hoja !

Hii "interllectuals" mi inaniacha hoi maana ukijaribu kuweka intellectual argument, kuna akina Anheuser wanaponda na kusema ni kimbelembele! Bora mleta mada aondoe hilo neno kwenye mada kuu!
 
Hii "interllectuals" mi inaniacha hoi maana ukijaribu kuweka intellectual argument, kuna akina Anheuse wanaponda na kusema ni kimbelembele! Bora mleta mada aondoe hilo neno kwenye mada kuu!

Wos ndio maana mchango wangu wa kwanza wenye hii mada niliadika hivi
Kama kweli unataka so called "Intellectual Arguments" basi ungeweka hii mada kwenye jukwaa la sheria ili watu wajadili kisheria sheria na kikatiba katiba. Zaidi ya hapo itakuwa n i hisia na ushasbiki wa kidini. ukichanganywa na siasa.( mleta hoja aliiweka hii mada kwenye jukwaa la siasa. na bado akawa anasema intelectual. May be inteleectual aliymmaanisha ni ya KISIASA)

Mimi comment yangu moja tu kwenye uzi niulize wachangaji wote watakapenda kuchangia na mleta mada

je wewe kama ungekuwa mwanasheria mkuu wa serikali uko tayari kurushu na kumshauri raisi akubali kuingiza rasmi mfumo wa mahakama za mila za wajaruo, wahaya, na makabila mengine kwenye mahakama ya JMT.

NB
Agalizo kuna mila zina utaratibu wao mfano wa mirathi

Sasa angalia mtu anayetaka inteectual argument alivyjibu

ni makosa kulinganisha wahaya na uislam ok..

Kwa point hiyo utaona mtu anadai kitu sababu yeye ni kundi fulani. Lakini huyo huyo hataiki kuchukua kuvua majoho ya dini na kuchukua postion ya serikali kujua kama angekwua yeye je ageruhusu mahakama kama hizo ngapi?

Anasema huwezi kulinganisha Wajaruo au na wahaya na uislam. Sababu yeye kwake uisam ni muhim zaidi. Anashindwa kutumia intellectual knowledge kuwa Tanzania kuna watu mila zao na desturi zao ni muhimu kama vile yeye kwake uislam ulivyo muhimu.

Nilitegeamea majibu ya" intellectual" anayetetea mahakama ya kadhi ni kuwa sawa ni haki hata kwa wajaruo, wahaya, na makabila mengine mahakama zao kuingizwa kwenye mfumo wa mahakam za serikali. Na iiwezekana wazee wa kijaruo mara nyingi nimesikia wanasuluisha migororo ya mirathi zao waingizwe kweye payroll ya Justice
 
Mimi napenda kujibu swali lako hivi: suala la mahakama ya kadhi ni suala linalohusu jumuiya ya waislam. hivyo si jambo la kikatiba kwa kuwa halina maslahi kwa watanzania wote. ndiyo maana Rais aliamua kulishughulikia kwani liko kwenye mamlaka yake. kitu kilichobaki ni kuangalia jinsi sheria za nchi zitakavyoweza kuhuisha suala hilo bila kuathiri uhuru wa kuabudu na kuingilia hazina ya taifa. pia sheria hizo itabidi ziache fulsa ili kama kuna dini nyingine zinataka masuala yao ambayo hayahusiani na jin
 
Kama kweli uanzishwaji wa mahakama za kadhi ni kwa ajili ya mirathi tu, basi hapo hakuna haja ya kupigishana kelele, msisitizo uelekezwe katika mafundisho ya dini juu ya namna ya kujenga familia na kugawanya mirathi.
Hapo tutakuwa tumepiga hatua katika kuzuia tatizo, badala ya kung'ang'ania mfumo wa kusubiri matatizo
 
Kama kweli uanzishwaji wa mahakama za adhi ni kwa ajili ya mirathi tu, basi hapo hakuna haja ya kupigishana kelele, msisi uelekezwe katika mafundisho ya dini juu ya namna ya kujenga familia na kugawanya mirathi.
Hapo tutakuwa tumepiga hatua katika kuzuia tatizo, badala ya kung'ang'ania mfumo wa kusubiri matatizo

Kweli kabisa.
Lakini kwani umesahau utamaduni wa kuzuia ni kama haupo?
Inabidi tujifunze utamaduni huu badala ya kusubiri tatizo litokee ndio tutafute dawa hata kama inagharimu zaidi ya uwezo wetu.
 
Nchi hii ina mambo mengi sana ya kujadili na sio haya,kuoa uoe wewe halafu uumbufu ulete kwa watu wengine si vema hata kidogo;kwanza mjadala wa mahakama za kidini MH RAIS amekataa na mjadala umefungwa.TAFADHARI Usirudie kuandika masuala haya hapa yanachochea chuki katika nchi.Tafadhari ondoa hoja hii mara moja.Pia hakuna aliye wakataza anzisheni wenyewe.
 
Kanisa Katoliki linazo mahakama zake na zinahusiana na masuala ya Ibada, ndoa na talaka vile vile. Na zinaendeshwa na Wakatoliki wenyewe na wapo watu wamesomea sheria hizo na kuna mfumo wa rufaa hadi Vaticani. Maamuzi yake yanaheshimiwa na sheria za nchi zilivyo sasa na serikali haiwezi kuingilia maamuzi ya mahakama hizo. Zina majaji na mawakili na zinafanya kazi miaka nenda rudi na hazijahitaji hata mara moja kuingizwa kwenye katiba ya nchi au kutengewa fedha za serikali. Hakuna sheria yoyote iliyotungwa yenye kuzitambua mahakama hizi kwa sababu ni sehemu ya ibada ya Wakatoliki na hatuhitaji sheria ya Bunge kutambua ni sehemu gani ya ibada yetu ni halali. Ninaamini Waislamu wakianzisha mahakama ya kadhi na kuwa ni sehemu ya ibada yao hakuna mtu atawauliza.

Mahakama za kadhi zinaweza kufanya kazi kwa mtindo huu huu. Vinginevyo, na watu wa dini nyingine nao wakitaka kuanzisha mahakama yao inayogharimiwa na Watanzania wote itakuwaje; hatuna uwezo wa kuendesha mahakama za kidini. Binafsi ninaamini (nilishalionesha hili miaka karibu mitatu nyuma) kuwa Waislamu wanaweza kabisa kuendesha mahakama zao na wanaweza kutumia serikali kufanikisha hivyo kwa mfano.

a. Taasisi za Kiislamu ziunganike na kufanya mazungumzo na serikali (kitu ambacho tayari kinafanyika) jinsi ya kuendesha mahakama hizo.

b. Waislamu wote na watu wengine (kama wapo) ambao wangependa kuona mahakama ya kadhi inakuwepo wapewe nafasi ya kuchangia kwa kukatwa mishahara yao kila mwezi ili kujenga mfumo wa kulipia hilo. Serikali inaweza kukata mishahara ya watumishi Waislamu wote (au wenye majina ya Kiislamu) unless wakatae. Kwa mfano, kama kila mfanyakazi Muislamu akikatawa shilingi 20,000 kwa mwezi na tuseme wapo wafanyakazi 200,000 tu basi kwa mwezi the Kadhi Fund itakuwa na shilingi 4,000,000,000 (shilingi bilioni 4).

c. kwa vile si Waislamu wote wako kwenye ajira rasmi basi kila msikiti wa Tanzania utatakiwa kuwa na sadaka ya Mfuko wa Kadhi ambapo Waislamu watatoa wenyewe (sijui utaratibu wa kuchangia mambo ukoje) na kwa vile tumewambiwa hiki ni kilio cha Waislamu nina uhakika fedha nyingi tu zitaweza kupatikana kila wiki au kila mwezi kuchangia ule mfuko wa kadhi.

d. Waislamu wataweza kuajiri na kulipia gharama zote za mahakama ya kadhi, serikali inaweza kusaidia kuadminister mfuko huo (kwa malipo siyo kama hisani). Kwa mfano, kwa mfano kila makato yanayosimamiwa na serikali kutakuwa na gharama ya kama shilingi 1500. Hivyo, Waislamuw wanapata fedha za kuendeshea na serikali nayo inanufaika kwa kukusanya mapato.

Mwanakijiji
a. Wakristo wenyewe watataka mahakama sasa kwa vile waislamu wameomba?? au wanataka sidhani kama itakuwa ni mahitaji yao kwakuwa kutofauta hiyo hukumu za kikristo ni dhambi kwa wakristo..kama ni dhambi then wanaogopa nini kuomba kuanzishwa siku zote?? wala hatujaona huo mfano kwa nchi nyingi za kikristo duniani mbona sijaona hiyo sheria na hukumu zikitumika? kadhi courts ambazo zipo hata kwa nchi za kikristo kwa ajili ya waislamu kwasababu ni ibada...kwa hiyo hoja yako ni uwongo au uchoyo na chuki tu kwa waislam wa Tanzania

b. Waislamu wa Tanzania wanalipa kodi kama wananchi wengine kuna kuwa na shida gani kuhudumia na pesa za serikali kwakuwa hata sasa kuna kesi za kiislamu katika mahakama za kawaida ambapo hakimu analipwa lakini anahukumu kesi ambazo hana ujuzi nayo??..kazi ya serikali ni kuhudumia wananchi wote kwahiyo hawa waislamu wanaotaka mahakama ya kadhi pesa zao zinatakuwa hizo hizo zinazoenda katika mahakama zetu ..ndio maana nikasema serikali inatakiwa kupeleka kwenye kadhi funds pesa equivalent na kesi ambazo zingeenda mahakama za sasa not otherwise..

Sijaona mantiki ya waislamu kulipia huduma ambayo serikali inatakiwa kutoa kwa wananchi wake..
 
How on hell are you going to conduct intellectual debate on non-intellectual issue? Wewe una maoni yako ambayo unataka watu waanzie hapo (kwenye calculation) wakati wengine hata concept yenyewe tu ya kuanzishwa hiyo mahakama inawatia kichefuchefu. Reading your mind, unakereka kweli kweli na ndio maana kila sentensi yako inaishia na 'OK' which means 'that is it'.

Unapowaambia wanaume unahitaji maoni halafu unachagua waseme nini ni ukosefu wa akili. Ikiwa concept yenyewe tu ni kichefu chefu, kuna haja gani ya explore second phase ambayo inainvolve calculations za hoja hewa? Wanufaikaji wa uanzishwaji wa hii mahakama ndio wanatakiwa waianzishe na kuigharamia.

Jana nilikushauri kitu, ila kwa hulka ya mtu dhaifu hukuupenda ushauri wangu na acha niurudie tena: Dini ni imani. Utekelezaji wa misingi ya imani hiyo ndio kipimo cha uhiari wa mtu kuwa wa dini hiyo au lah. Ikiwa mnachohitaji kuamuana kwa misingi ya dini yenu, basi hiyo ni sehemu ya ibada zenu na mnaweza kuyafanya hayo huko huko mnakofanyia ibada zingine. Mimi naamini Muislamu wa kweli atafanya maamuzi kwa mujibu wa sheria za kiislamu na ikiwa hataki basi huyo si muislamu, sasa kama mna mpango wa kulazimishana kuwa na imani, si mlazimishane kwa gharama zenu! Kwa mfn: Kanisa Katoliki lina mabaraza ya ndoa na ustawi wa jamii. Mambo yote yanayohusu matatizo ya ndoa na mahusiano hujadiliwa huko kwa misingi ya imani ya kikatoliki. Ikiwa mtu atapingana na maamuzi hayo ambayo yanaendana na imani ya dini, basi suala hilo litaenda mahakamani. Sasa inatuhusu nini sisi tusio waislamu kuchangia uendeshwaji wa mabaraza ya uamuzi wa ndoa za kiislamu as if ugomvi wenu unatuathiri na sisi?

Wewe umekazana kuzungumzia bajeti as if hizi hela unazozizungumzia ni za msikiti. What if Wakurya tukiamua kesi zetu wa kuwatia mkong'oto kina wife ziundiwe mahakama zake binafs kwa kuwa majaji wa mahakama za sheria hawajui mila zetu?

Intellectual gani usiyejua sheria za nchi yako? Kwanza nijuavyo mimi, Waislamu mambo yao huamuliwa mahakamani kwa mujibu wa sheria za kiislamu. Ni heri ungeniambia mnaandaa mchakato wa kuboresha uelewa wa majaji juu ya sheria za dini yenu kuliko kunilazimisha nishiriki calculation za kodi yangu kuamua matatizo yako ya wewe kuwa na wake 6 na watoto 18. Mtakuwa mna yenu, wala si dini.

Leta hoja ya msingi juu ya kwa nini wasio waislamu wawajibike kuchangia mambo yenu, sio hii.

Umekasirika na umeandika kwa hasira..sijaona unataka kusema nini?? please andika tena ukiwa umetulia ..just intellectual arguments..
 
Kama unataka kazi nenda kasome usilazimize kuanzisha NGO ili kupata ajira nenda shule.Mahakama kwa ajili ya ndoa tu tena si kwa waislamu wote ila wachache tu waliotayari,narudia tena ondoa link hii hapa maramoja.
 
Kama hukubaliani na mahakama zilizopo tafadhari sana usitende makosa,pia si lazima kuoa wanawake wengi,gawa urithi wako kabra hujafa,epuka jkulazimisha jambo alisilowezekana,pesa za kumlipa kadhi ni kodi za wananchi wote hata ambao si waislamu,kama bado hujaelewa tafadhari jiulize ni nchi ngapi zenye sheria hii?jipange upwa kwa hili mjadala umefungwa
 
Assume wewe ni muislam na una wake watatu na watoto 5:4:3 yaani 12 jumla kwa wake watatu..umefariki

Kwa sheria za ndoa ya 1971; ugawaji wa urithi huo hauwezekani japo muislam huyu aliruhusiwa kuoa kiislam

Kwanini mali yake isigawanywe kiislam?? tunataka kadhi wawasaidie hao wanawake, watoto kuhusu mgawanyiko wa mali ya muumini huyu.. siyo voluntarily iwe sheria kabisa na hukumu itolewe na mahakama..ok

Ndio maana tunataka mahakama ya Kadhi..

NB: Naomba wale wenye hasira na uislam na waislamu watuache kwanza tuseme kwanini tunataka mahakama ya kadhi ili mtuelewe

Mnataka mahakama ya qadi toka wapi? wakati imeshabainishwa kwenye ibada zenu! ushauri wa buree, Nyie wenyewe waislamu, sunni! shia! qadian!.... kaeni hata ukumbi wa diamond jubilee hall chagueni maqadi watoe hukumu za kiislamu kwa mujibu wa quran, anaewazuia kufanya ibada hiyo nani?
 
Ni kwanini waislamu hawawezi ku enforce laws zao wenyewe za kiibada kwenye mahakama zao mpaka wasaidiwe na serikali lakini madhehebu mengine ya dini yanaweza?
Madhehebu mengine yanaweza vipi, how?

Mahakama ya kanisa ikiamuru, kwa mfano, mali ya mtaliki iende kulipia ada na malezi ya mtoto, na wewe ukakaidi wanakufanya nini, wanakufukuza kwenye fellowship ya maombi ya Jumatano? Padri, Shehe, Kadhi Mkuu, hana dola, ana enforce vipi amri yake?
 
Madhehebu mengine yanaweza vipi, how?

Mahakama ya kanisa ikiamuru, kwa mfano, mali ya mtaliki iende kulipia ada na malezi ya mtoto, na wewe ukakaidi wanakufanya nini, wanakufukuza kwenye fellowship ya maombi ya Jumatano? Padri, Shehe, Kadhi Mkuu, hana dola, ana enforce vipi amri yake?
Ninachosema mimi ni kwamba mambo ya ibada inabidi yabaki kuwa ya ibada bila kuihusisha serikali. Kama mtu(muislam) kaamua kutotii sheria za kiislam(ambazo ni ibada) hauwezi kumlazimisha kutii hizo amri kwa kutumia chombo cha serikali kwa sababu katiba yetu inatupa uhuru wa kuabudu au kutoabudu kitu chochote. Kwa hiyo kama muislam yeyote kaamua kutozifuata hizo amri ni uamuzi wake na hauwezi kumlazimisha kwa sababu huko ni kuvunja katiba. Mkuu kwa tanzania yetu, amri za dini zetu siyo mikataba ambayo ni lazima kuifuata...tunao uhuru wa kuzifuata hizo sheria kama wacha Mungu wa kweli au kutumia sheria za serikali kama tumeamua kumuweka Mungu pembeni...!
 
Ninachosema mimi ni kwamba mambo ya ibada inabidi yabaki kuwa ya ibada bila kuihusisha serikali. Kama mtu(muislam) kaamua kutotii sheria za kiislam(ambazo ni ibada) hauwezi kumlazimisha kutii hizo amri kwa kutumia chombo cha serikali kwa sababu katiba yetu inatupa uhuru wa kuabudu au kutoabudu kitu chochote. Kwa hiyo kama muislam yeyote kaamua kutozifuata hizo amri ni uamuzi wake na hauwezi kumlazimisha kwa sababu huko ni kuvunja katiba. Mkuu kwa tanzania yetu, amri za dini zetu siyo mikataba ambayo ni lazima kuifuata...tunao uhuru wa kuzifuata hizo sheria kama wacha Mungu wa kweli au kutumia sheria za serikali kama tumeamua kumuweka Mungu pembeni...!

Nimependa hizo sehemu nilizo bold.

Mungu ni Imani ya mtu.Wapo wanaoamini, wapo wasioamini.Serikali ya Tanzania haina dini.Kwa msingi huo, serikali isiyo na dini, haiwezi kuwasaidia watu kufuata "amri za Mungu wao, au dini zao".

Kiserikali, kila mtu anao uhuru kuabudu atakacho na atakavyo.Ukiamua kuabudu Ng'ombe kama wanavyofanya baadhi ya watu ruksa! Ukiamua kuabudu nature, ruksa! Ukiamua kumuabudu Mungu wako unayemuamini wewe, ni wewe na Mungu wako.Haiwezi kuwa ni wewe, Mungu wako na serikali! Na hapa ndipo tunaposhindania ( bone of contention).Ni jukumu la kila mwenye dini yake kuabudu humohumo kwenye dini yake bila kuhusisha serikali isiyo na dini.

Kwa wakristo wakatoliki kwa mfano, kwenye masuala ya ndoa - wao wana sheria ya mke mmoja, na hakuna talaka hadi kifo kiwatenganishe! Hapo hapo, sheria za nchi zinaruhusu talaka.Wapo wakatoliki chungu mzima ambao wameenda mahakamani kudai talaka na hii ni kinyume kabisa na sheria za kikatoliki za ndoa. Kinachofanyika kwa mtu kama huyu, ni kwamba kanisa halitambui hiyo, na pia hawezi tena kufunga ndoa kanisani. Hatujawahi kusikia hata mara moja, wakatoliki wakiidai serikali ianzishe mahakama za kanisa ndani ya mfumo wa serikali.Wenyewe wanao utaratibu wao wa kufuata katika maswala yao, na hata kesi kama hizi, wanafuata hizo taratibu kivyao bila kuingiza dini nyingine maana kwa kufanya hivyo itakuwa kuingilia uhuru wa imani za wengine na hii ni kinyume na uhuru wa mtu binafsi chini ya katiba.Mara ngapi tunasikia pingamizi kanisani kwa mtu anayetaka kufunga ndoa na huku pale ambapo ametenda kinyume na matakwa ya sheria za kikristo katoliki? Ndio utaratibu, na wasioridhika wamepeleka rufaa hadi Vatican - MAKAO MAKUU YA KANISA KATOLIKI..Hii yote ni nje ya mfumo wa utoaji haki wa Serikali. mfumo unaotegemezwa na walipa kodi wote - wakristo, waislam na hata wasio na dini..Pale mhusika anapokaidi/kukiuka, basi hutengwa na kanisa.
 
Mwanakijiji
a. Wakristo wenyewe watataka mahakama sasa kwa vile waislamu wameomba?? au wanataka sidhani kama itakuwa ni mahitaji yao kwakuwa kutofauta hiyo hukumu za kikristo ni dhambi kwa wakristo..kama ni dhambi then wanaogopa nini kuomba kuanzishwa siku zote?? wala hatujaona huo mfano kwa nchi nyingi za kikristo duniani mbona sijaona hiyo sheria na hukumu zikitumika? kadhi courts ambazo zipo hata kwa nchi za kikristo kwa ajili ya waislamu kwasababu ni ibada...kwa hiyo hoja yako ni uwongo au uchoyo na chuki tu kwa waislam wa Tanzania

b. Waislamu wa Tanzania wanalipa kodi kama wananchi wengine kuna kuwa na shida gani kuhudumia na pesa za serikali kwakuwa hata sasa kuna kesi za kiislamu katika mahakama za kawaida ambapo hakimu analipwa lakini anahukumu kesi ambazo hana ujuzi nayo??..kazi ya serikali ni kuhudumia wananchi wote kwahiyo hawa waislamu wanaotaka mahakama ya kadhi pesa zao zinatakuwa hizo hizo zinazoenda katika mahakama zetu ..ndio maana nikasema serikali inatakiwa kupeleka kwenye kadhi funds pesa equivalent na kesi ambazo zingeenda mahakama za sasa not otherwise..

Sijaona mantiki ya waislamu kulipia huduma ambayo serikali inatakiwa kutoa kwa wananchi wake..

hivi kazi ya serkali ni kuchonga Misalaba na kugaramia watu kwenda hija maka! Mbona unalazimisha mbuzi kula nyama?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom