Lol...
Qurani inaeleza behaviour zenu toka mwanzo zinatokana na wivu na husda kwani sisi tuko kwenye haki na tunaenda paradise na nyie mnajua mnatumikia shetani..hamtupati..
Sasa niambie katika biblia "mgawanyo wa mali ukoje kwa wakristo wote duniani" usiniambie hukumu ya state courts??? NIL
Ililazimu ieleze na ndio maana nikakwambia, mwandishi wa Quran (sijui ni nani) alichelea kuwa asipowaambia hivi hamtajiandaa kupinga kila mtakaloambiwa. Kwa kuambiwa kwenu hivyo, mnajiwekea ukuta wa kukataa kuelewa lolote lisemwalo na hilo ndio lengo la mwandishi, asiwapoteze kwa gharama yeyote. Na ukitaka kujua ukweli wa hili, tazama unavyokuwa mkali kuhusu internet, hupendi watu wafahamu jambo na kuhoji, nafuu yako ni wengine wasijue ili waendelee kuamini wanachoamini bila kupima.
Turudi kwenye hili
swali kichekesho la mgawanyo wa mali kwenye Biblia. (Ni kichekesho kwa kuwa Wakristo hawaishi kwa sheria, bali imani). Nirejee kauli yako kuhusu kwa nini mnadai mahakama ya Kadhi, ulisema ni IBADA. Sasa tofauti na ibada zenu, ibada zetu zipo mioyoni mwetu kwa imani na tumaini la kuyapata yale tuliohidiwa na Bwana wa Ulimwengu huu, pasina shuruti wala malazimishano.
Haya mambo unayoyaongea na kuyaita sheria, ni agano la Mungu na Waisraeli akiwatoa utumwani Masri. Rejea
Yohana 1:16-17 "Kwa kuwa katika utimilifu wake sisi sote tulipokea neema juu ya neema. Kwa kuwa torati ilitolewa kwa mkono wa Musa; neema na kwelizilikuja kwa mkono wa Yesu Kristo" Kama ibada yenu Waislamu ilikuja kwa Torati, basi tambua ya kuwa Neema yetu na Kweli tunaipata kwa Yesu.
Hizo sheria zenu ni zao la Agano la Kale la Mungu na Wayahudi ambalo hata hivyo walilivunja. Hata Mungu kwa kuona ugumu wa sheria, alituletea imani mioyoni mwetu na ikatuletea amani na uchaji.
Tazama
Yeremia 31:31-34 "Angalia, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapofanya Agano Jipya na nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda. Si kwa mfano wa agano lile nililofanya na baba zao, katika siku zile nilipowashika mkono, ili kuwatoa katika nchi ya Misri; ambalo agano langu hilo walilivunja, ingawa nalikuwa Mume kwao, asema Bwana. Bali Agano hili nitakalolifanya na nyumba ya Isaraeli, baada ya siku zile asema Bwana, NITATIA SHERIA YANGU NDANI YAO, NA KATIKA MIOYO YAO NITAIANDIKA; NAMI NITAKUWA MUNGU WAO, nao watakuwa WATU WANGU. Wala hawatamfundisha kila mtu jirani yake, na kila mtu ndugu yake wakisema, mjue Bwana; kwa maana watanijua wote, tangu mtu aliye mdogo miongoni mwao, hata aliye mkubwa miongoni mwao, asema Bwana; maana nitausamehe uovu wao wala dhambi yao sitaikumbuka tena".
Nachotaka uone hapa ni kuwa, sheria inayotuongoza imeandikwa ndani yetu tofauti ya ile ya Musa iliyokuwa kwenye mawe hata iliwashinda wakaivunja. Bwana aliliona hili hata akaweka agano jipya ndani yetu. (kwa hiyo elewa ni kwa
imani na sio
mahakama)
Amri kumi za Musa bado hazijawapa nafasi ya kuishi kwa amani kiasi mnataka na mahakama na nguvu ya kisheria ya kutekeleza hukumu za mahakama hiyo, lkn Yesu alitupa amri moja kwa kila anayeamini:
Yohana 13:34 "amri mpya nawapeni, Mpendane. Kama mimi nilivyowapenda ninyi, mpendane hivyo hivyo"
Bwana Topical, ukimpenda mke wako hutamdhulumu mali yake na kumpa kaka yako. Ukimpenda mke wako, hutamfanya sex toy yako wala hutambadilishana kama bidhaa au kumtoa kwa wanaume wengine kama mnavyofanya.
Kuomba mahakama ni dalili ya kushindikana kwa imani. Shuruti haiji ilipotawala hiyari. Nikiwa muislamu nitayafuata ya Allah kwa imani na wala sitasubiri kadhi atume polisi kuja kunidhalimisha nitimize vifungu vya ibada. Kinachowafanya mlidai la enforcement ya hukumu ni upungufu wa imani.
Yesu ndio baba wa logic, na haya unayajua pia. Maswali yote ya sheria aliyajibu kwa hekima hata sheria ikakosa maana kwa waiaminio. Kama unabisha hili niulize nikufafanulie kwa nini naamini Yesu ni wa imani na sio sheria.
Hatuitumainii sheria kwa namna ile unavyoihitaji wewe. Shida yenu ni kwamba, muumini aliyeacha wosia kuwa sehemu ya mali yake ipelekwe msikitini waliobaki huwa hawafanyi hivyo. Kwa kuwa hawafanyi hivyo basi ndio mnataka namna ya kumaliza tatizo kwa sheria na hukumu, lkn mmeshajiuliza kwa nini hawatekelezi?
TIA SHERIA KTK MIOYO YA WAISLAMU HALAFU UTAONA KAMA ITAHITAJI MAHAKAMA KUWAFANYISHA WATU IBADA. FUNDISHENI MISIKITINI JUU YA UMUHIMU WA KUMTIII ALLAH NA SIO KUWALAZIMISHA WATU KWA NGUVU KANA KWAMBA ALLAH HAKUSEMA KUWA ATAWAHUKUMU YEYE MWENYEWE WASIOMTII.
Mazinge uliyemzungumzia jana ni yupi Topical?