Wanaosema bandari imeuzwa wanavikosea heshima vyombo vyetu vya Ulinzi na Usalama

Point, tatizo ni intellectual resources na kuendeleza culture of status quo. Tafiti zinaonesha kua kwenye
utoaji huduma usiposhirikisha sector binafsi mambo yanalala na ufanisi unakuwa mdogo sababu panakuwa hakuna ushindani. Hata ukiwa na trained members na high tech bila kushirikisha sector binafsi mambo ya ujanjaujanja na mazoea hayakosi si tunajuana pwana.
 

Kanyaga twende, hakuna kurudi nyuma. Walioaminiwa kulinda rasilimali za nchi wamenyamaziswa. sasa ni wakati wa kila mtu kupiga kelele za kusema hapanaaaaaa.
 
Ni siasa za hovyo tu. Na wote wanaowaamini hawana akili.

Inafikia mwezi sasa. Nimeuliza swali kwa kila mtu, ni kifungu kipi cha mkataba kinasema Bandari imeuzwa hadi leo sijajibiwa!
Bila ukomo maana yake nini?
Kwa hiyo na wewe unajiita msomi?

Waoneshe kwenye mkataba muda gani na faida gani tutapata sisi kama taifa ili tuwaelewe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sekta binafsi bila usimamizi pia ni Holela. Pia haziwezi toa public goods kwani hazina faida. Kuna sekta huwa sio lazima kupata faida ila athari zake kwenye sekta nyingine ndio huzingatiwa.
 
Tatizo huna uelewa mpana. Wewe fikra zako zinaishia katika uelewa finya wa maana ya neno 'kuuzwa'. Wewe kuuzwa linaishia kama vile mtu anavyouza nyanya au magimbi. Au unavyoweza kuuza nyumba.

Hujyi maana ya:

1) kuuza nchi
2) kuuza uhuru
3) kuuza utu

Mathalani ukaambiwa kuwa utasaidiwa pesa ya kugharamia kampeni za ubunge, lakini wewe uhakikishe huyo atakayegharamia kampeni zako anapewa eneo la karibu na bandari. Na wewe ukakubali kuwa utahakikisha watu waliokuwa karibu na bandari wanaondolewa ili huyo atakayegharamia kampeni zako anapewa ardhi anaypitaka. Hapo umeuza sehemu ya nchi, japo hakuna mahali inapoonekana uliuza kipande hicho cha nchi kwa kiasi gani. Lakini pia umeuza uhuru wako kwa sababu unatenda bila ya utashi wako.

Kwa ujumla mkataba wa bandari, unauza uhuru wa Taifa katika kufanya maamuzi yake bila ya kuingiliwa na mtu yeyote. Mkataba wa bandari, unauza bandari na ardhi yetu kwa DP kwa sababu kunamfanya DP amiliki shughuli za bandari milele, labda aamue yeye kuacha.
 
Ni siasa za hovyo tu. Na wote wanaowaamini hawana akili.

Inafikia mwezi sasa. Nimeuliza swali kwa kila mtu, ni kifungu kipi cha mkataba kinasema Bandari imeuzwa hadi leo sijajibiwa!
Narrow mind.
 
Hivyo vyombo havijali kuhusu umeme, maji, tozo, bei za chakula, ujenzi
Kanyaga twende, hakuna kurudi nyuma. Walioaminiwa kulinda rasilimali za nchi wamenyamaziswa. sasa ni wakati wa kila mtu kupiga kelele za kusema hapanaaaaaa.
Hivi vyombo vipo kulinda genge la watu wachache ndani ya CCM sio maslahi na ustawi wa Tanganyika.
 
Sekta binafsi bila usimamizi pia ni Holela. Pia haziwezi toa public goods kwani hazina faida. Kuna sekta huwa sio lazima kupata faida ila athari zake kwenye sekta nyingine ndio huzingatiwa.
Kuhusu bandari wewe una maoni gani? binafsi naona sector binafsi ihusishwe pakubwa ila kuwe na check and balance kwenye terms za uendeshaji na mafunzo kwa watu wetu.
Sekta binafsi bila usimamizi pia ni Holela. Pia haziwezi toa public goods kwani hazina faida. Kuna sekta huwa sio lazima kupata faida ila athari zake kwenye sekta nyingine ndio huzingatiwa.
 
Akili bumunda nafikir zitakua zimekuelewa maana umejitolea kufafanua kwa kina.
 
Kinacholalamikiwa kwenye huo mkataba wa Dpworld ni vile vipengere vilivyomo kwenye ule mkataba.
Ukivisoma vile vipengere vya ule mkataba ni kama kuiuza au kuziuza zile bandali zote za Tanzania bara kwa Dpworld.
 
Wanaotetea wanasema hao ajira zitamwagika sana, dakika 4 baadaye anasahau alichokuwa anazungumza anasema hao dp zinafanya kazi mashine tu.
Acha tu aisee..Yan vyombo na idara za serikali zote zimejaa wapumbavu waliotukuka..Sijui wanawapataje hawa watenda kazi wa serikal??
Ni wajinga wajingaaaaa!!! Halaf sasa ukiwaona hata hawaendani na walivyo
 
Acha tu aisee..Yan vyombo na idara za serikali zote zimejaa wapumbavu waliotukuka..Sijui wanawapataje hawa watenda kazi wa serikal??
Ni wajinga wajingaaaaa!!! Halaf sasa ukiwaona hata hawaendani na walivyo
Acha hasira utapoteza rationality, kesho unaweza kuwa wewe na ukaitwa mjinga vilevile.
 
Acha hasira utapoteza rationality, kesho unaweza kuwa wewe na ukaitwa mjinga vilevile.
Sasa nikiitwa mjinga na kwel nima ujinga tatizo liko wapi?
Let's call a spade , spade.. black and white.
Hiz hekima za kijinga jinga ndio zimetufikisha hapa tulipo
 
Naona kama wewe ndiye unawakumbusha watu, waiporomoshe hiyo heshima kwavyo.
 
Imeuzwa ndio, ndio maana tunahoji...

Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
 
Mara imeuzwa, mara imetolewa bure, ehee tuchukue lipi!
 
Watu wana mahaba na Waarabu waliomuuza babu yake Mike Tyson Marekani.. wanajua ni faida eti.. so wanataka na wao wauzwe
 
Tulipo tapeliwa GESI kupitia mikataba mibovu kati serikali yetu na mabepari, hivyo vyombo vya usalama havikuwepo?!!!
👇👇
 
Ha haaaa vyombo hivi hivi au vingine si vilikuwepo toka enzi za Loliondo inauzwa kwa mwarabu. Hebu tuache kidogo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…