Wanapotukosoa tunawatukana na kuwaita mabeberu, jina linabadilika na kuwaita wafadhili wetu wa maendeleo mara tu wanapoanza kutugawia pesa!

Wanapotukosoa tunawatukana na kuwaita mabeberu, jina linabadilika na kuwaita wafadhili wetu wa maendeleo mara tu wanapoanza kutugawia pesa!

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Ni tabia iliyozoeleka kwa watawala wetu wa serikali ya awamu ya tano kujihami na kuwaita wazungu wa nchi za nje, kuwa ni mabeberu, wanapokuwa wametukosoa katika uimarishaji wa demokrasia, uhuru wa wananchi kujieleza na tunashauriwa tuzingatie haki za binadamu.

Lakini kitu cha ajabu ni pale wazungu hao hao, "wanapomwaga" pesa zao katika kutusaidia kwenye miradi mbalimbali, tunapiga "U turn" na tunawasifia na kuwaita kuwa hao ni wahisani wetu na wafadhili wa maendeleo!

Tukizingatia kuwa nchi yetu katika utawala huu wa awamu ya tano kumekuwa na ukiukwaji wa hali ya juu sana wa haki za binadamu, kwa wananchi wengi kubambikiwa kesi za utakatishaji pesa na Jeshi letu la Polisi nchini!

Pale ambapo mwananchi ataamua kutumia haki yake ya kikatiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ibara ya 18(1), kwa kutuhubutu kukemea ukiukwaji huo mkubwa wa binadamu, wananchi hao nao watajumuishwa kuwa ni wasaliti wa nchi yetu na ni watu wanaotumiwa na mabeberu wa nje, kwa vile hawafurahii maendeleo yetu!

Watanzania wenzangu hivi mnaona limekaa sawa kweli hili jambo?
 
Mabeberu yamepandikiza vibaraka wao kwenye mitandao ya kijamii masaa yoote kuanzisha nyuzi za kuikashifu serikali na kuwatetea mabeberu eti wanaisaidia nchi kimaendeleo? Tangu lini misaada ya mabeberu iliishawahi kutukomboa na umasikini zaidi ya kutudidimiza kwa masharti kandamizi. Mfano: mabeberu yalijenga (tena chini ya kiwango) barabara ya Uhuru kuanzia mnara wa saa hadi Boma (Zilipo ofisi za mkuu wa mkoa wa DSM) kwa mkopo wenye riba kubwa tena kandamizi tangu Baba wa taifa Nyerere na mkopo umemalizika kulipwa katika awamu ya JPM (zaidi ya miaka 50 ). Na kipindi choote hicho kila mwaka barabara inaharibika na kutengenezwa upya jinsi ilivyokuwa imejengwa kimagumashi na hao mabeberu. Kuweni wazalendo na acha kushobokea viposho mnavyolipwa kila mkiposti Uzi wa kuikashifu serikali
 
Watu hawatambui kuwa palipo na "beberu' pia yupo "mbuzi jike" haijalishi kwa wanyama ama nchi. Hivyo basi ni kama tunajitukana sisi wenyewe, wakitukosoa tunawaona ni wabaya, lkn tunaanza kuwasifu na kuwaita kuwa ni wafadhili ama wahisani wa maendeleo yetu tunapoona utamu wa fedha zao.

Ni sawa kabisa ya tabia za mademu wasiojielewa wanapowaita wanaume kwa majina mabaya pale fedha ya matumizi ikitoweka, lkn mwanaume anapambwa kwa majina mazuri ya kimahaba pale anapomuwezesha kifedha na kumpeleka ktk uchumi mtamu wa kati.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mabeberu yamepandikiza vibaraka wao kwenye mitandao ya kijamii masaa yoote kuanzisha nyuzi za kuikashifu serikali na kuwatetea mabeberu eti wanaisaidia nchi kimaendeleo? Tangu lini misaada ya mabeberu iliishawahi kutukomboa na umasikini zaidi ya kutudidimiza kwa masharti kandamizi. Mfano: mabeberu yalijenga (tena chini ya kiwango) barabara ya Uhuru kuanzia mnara wa saa hadi Boma (Zilipo ofisi za mkuu wa mkoa wa DSM) kwa mkopo wenye riba kubwa tena kandamizi tangu Baba wa taifa Nyerere na mkopo umemalizika kulipwa katika awamu ya JPM (zaidi ya miaka 50 ). Na kipindi choote hicho kila mwaka barabara inaharibika na kutengenezwa upya jinsi ilivyokuwa imejengwa kimagumashi na hao mabeberu. Kuweni wazalendo na acha kushobokea viposho mnavyolipwa kila mkiposti Uzi wa kuikashifu serikali
Nijibu swali langu Mkuu No retreat no surrender ni kwanini tunawatukana na kuwaita mabeberu, pale wanapokosoa Sera zetu na jina linabadilika ghafla na kuwaita wafadhili wetu wa maendeleo pale tu wanapoanza kutumwagia pesa?
 
Mabeberu yamepandikiza vibaraka wao kwenye mitandao ya kijamii masaa yoote kuanzisha nyuzi za kuikashifu serikali na kuwatetea mabeberu eti wanaisaidia nchi kimaendeleo? Tangu lini misaada ya mabeberu iliishawahi kutukomboa na umasikini zaidi ya kutudidimiza kwa masharti kandamizi. Mfano: mabeberu yalijenga (tena chini ya kiwango) barabara ya Uhuru kuanzia mnara wa saa hadi Boma (Zilipo ofisi za mkuu wa mkoa wa DSM) kwa mkopo wenye riba kubwa tena kandamizi tangu Baba wa taifa Nyerere na mkopo umemalizika kulipwa katika awamu ya JPM (zaidi ya miaka 50 ). Na kipindi choote hicho kila mwaka barabara inaharibika na kutengenezwa upya jinsi ilivyokuwa imejengwa kimagumashi na hao mabeberu. Kuweni wazalendo na acha kushobokea viposho mnavyolipwa kila mkiposti Uzi wa kuikashifu serikali
Kuna mimtu humu ina amini bila wazungu hapa duniani ni pazito sana
 
Nijibu swali langu Mkuu No retreat no surrender ni kwanini tunawatukana na kuwaita mabeberu, pale wanapokosoa Sera zetu na jina linabadilika ghafla na kuwaita wafadhili wetu wa maendeleo pale tu wanapoanza kutumwagia pesa?
Beberu au Mabeberu ni jina linalotokana na mfumo wa juu wa unyonyaji (ubepari uliokomaa na kuvuka mipaka na kuingia nchi nyingine). Mnyonyaji hutumia mbinu ya chambo (misaada) ili kutengeneza mazingira ya kukunyonya. Hiyo unayosema misaada au fedha ni kama chambo (cha kumvutia samaki ili umnase) na hazina tija yoyote. Wanatake advantage ya uelewa mdogo na umasikini wa waafrica au nchi masikini na kuzinyonya. Kwaufupi "it is unfair trade/relationship".
Kwa mfano: kama wewe ni mwanaume unatembea unakutana na binti ana njaa! Unachukulia njaa yake kumrubuni ili kumuingilia kimwili alafu baadaye useme nilimsaidia kumpa chakula? Ndivyo mabeberu walivyo. Mabeberu sio watu! Ni wakandamizaji! Marekani na nchi nyingi za magharibi zimejengwa kwa damu za mamillioni ya roho za wafrica (waliokufa) watumwa waliotekwa na kudhalilishwa utu wa mwanadamu kuliko wakati wote wa historia ya binadamu. Alafuu wanaanza kuzitungia sera nchi za kiafrica zinazojikongoja ziinuke kiuchumi. Sera hizo ni: Uhuru wa habari, Uhuru wa kujieleza, mapenzi kwa watoto wa shule na akibeba mimba umuache aendelee na shule, ushoga na usagaji, n.k., n.k, mambo mengi mabaya ambayo wakati wanajaenga jamii na miji yao yalikandamizwa sana. Sasa wanapandikiza mapandikizi ya mabeberu kwenye mitandao ili kushawishi utekelezaji wa sera potovu na kiongozi (kama JPM) ambaye amesimama kuliletea taifa maendeleo wanamuanzishia thread za kumkashifu! Hatutakubali!
 
Beberu au Mabeberu ni jina linalotokana na mfumo wa juu wa unyonyaji (ubepari uliokomaa na kuvuka mipaka na kuingia nchi nyingine). Mnyonyaji hutumia mbinu ya chambo (misaada) ili kutengeneza mazingira ya kukunyonya. Hiyo unayosema misaada au fedha ni kama chambo (cha kumvutia samaki ili umnase) na hazina tija yoyote. Wanatake advantage ya uelewa mdogo na umasikini wa waafrica au nchi masikini na kuzinyonya. Kwaufupi "it is unfair trade/relationship".
Kwa mfano: kama wewe ni mwanaume unatembea unakutana na binti ana njaa! Unachukulia njaa yake kumrubuni ili kumuingilia kimwili alafu baadaye useme nilimsaidia kumpa chakula? Ndivyo mabeberu walivyo. Mabeberu sio watu! Ni wakandamizaji! Marekani na nchi nyingi za magharibi zimejengwa kwa damu za mamillioni ya roho za wafrica (waliokufa) watumwa waliotekwa na kudhalilishwa utu wa mwanadamu kuliko wakati wote wa historia ya binadamu. Alafuu wanaanza kuzitungia sera nchi za kiafrica zinazojikongoja ziinuke kiuchumi. Sera hizo ni: Uhuru wa habari, Uhuru wa kujieleza, mapenzi kwa watoto wa shule na akibeba mimba umuache aendelee na shule, ushoga na usagaji, n.k., n.k, mambo mengi mabaya ambayo wakati wanajaenga jamii na miji yao yalikandamizwa sana. Sasa wanapandikiza mapandikizi ya mabeberu kwenye mitandao ili kushawishi utekelezaji wa sera potovu na kiongozi (kama JPM) ambaye amesimama kuliletea taifa maendeleo wanamuanzishia thread za kumkashifu! Hatutakubali!
Tunacho-differ na wewe ni iweje hao unaowaita mabeberu, usheherekee kupokea misaada yao wakati nyuma ya pazia unawaita mabeberu/wanyonyaji?

Kama kweli unachukia vitendo vyao, basi ungekata mawasiliano nao na hata hiyo misaada ungewagomea kuipokea

Kinyume cha hapo ni unafiki wa hali ya juu
 
Back
Top Bottom