Wanapotupita wazungu hata kwa wenye Elimu ya Chini kuliko sisi

Wanapotupita wazungu hata kwa wenye Elimu ya Chini kuliko sisi

Mparee2

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2012
Posts
3,092
Reaction score
5,386
Baada ya kuwachunguza sana hawa watu, niligundua yafuatayo;
  • Huthamini sana kazi (Kazi kwanza)
  • Wana amini kwenye matokeo (result oriented)
  • Hutimiza malengo ya kila siku/wiki/mwezi na yasipofikiwa hutathimini kujua walipo kwama
  • Hufanya kazi kwa weledi na kujituma sana (huingia kazini mapema na kutoka kazini pale tu anapokamilisha malengo ya siku husika)
  • Hupatikana kwenye simu muda wote wakihitajika hata iwe jumapili/Siku kuu na asipo pokea hupiga ndani ya muda mfupi kufuatilia
  • Hawana visingizio vya kumfanya achelewe au asiingie kazini (Sio waongo)
  • Hutoa taarifa rasmi in advance kama hatakuwepo/atachelewa kazini na muda wa uhakika atakao kuwepo ofisini
  • Mteja/mgeni wa kikazi akifika ofisini kwake ni mfalme wakati wote; Wapo tayari kuahirisha chochote wamsikilize au kuelekeza mtu wa kumhudumia
  • Ni waaminifu sana ( sio wezi). Hata kama ni mlevi akiachiwa Godown la pombe anajiandikia mwenyewe alichokunywa ili akatwe kwenye mshahara
Sisi tunashindwa wapi? Tubadilikeni; tuaminike! Ili tusiishie vyeo vya kawaida kwenye mataasisi makubwa ya ndani naya kimataifa
 
Back
Top Bottom