Wanasheria Njaa: Mnaaibisha Fani nzima ya Sheria

Wanasheria Njaa: Mnaaibisha Fani nzima ya Sheria

Hahaha kama learned nameless girl anaweza kututengenezea ka "contract" kwa maana ya tafsiri ya wasomi wa sheria.... Why not?

Usisahau ualimu sio proffesion, usije ukataka nikufundishe kufunga socket ya three switches lol

Hivi ni kweli wanasheria watu wanatengeneza Contracts ? ama wana google templates na ku-edit kukidhi haja ya mteja ? Serious wanasheria wetu ni wazuri sana kwa Ku-kudesa toka Google results
 
Here comes another learned brother. Nashauri utumie kiswahili ili sisi ambao si wasomi tukuelewe. Mathalani hapo ulipoandika "he don't know".... kwa umburula wangu ulonifanya nikaishia VETA na kumzidi kielimu comrade Nyani Ngabu, nlishakariri eti ulipaswa uandike "he doesn't know"

Wasomi mtuhurumie ambao hatujaenda shule. Tumieni lugha ya taifa tuwaelewe.

Ngoja nikazimue zangu mi fundi mchundo.

umeona eeeh wanakimbilia kwenye kingereza kwa madai layman hatuwezi kuelewa
 
Last edited by a moderator:
Wakuu Mgunduziforeva na nameless girl,

Kama kweli nyie ni wanasheria ambao napaswa kuwahitaji kunitetea, inakuwaje form four mbeba maboksi Nyani Ngabu anawashinda kwa hoja ndogo namna hii? Nitawaaminije kwenye cases zinazohitaji hoja kubwa kama hii ndogo mnashindwa kujibu na mapovu yanawatoka.

Wakati nawaacheni mmalizane na Ngabu mi nina kaswali ka kizushi.... Kwanini nyie lawyers mnapenda kujiita "wasomi"??? Taaluma yenu pekee ndo ina watu walioqualify kuitwa wasomi?

Tahadhari, tofauti na Ngabu aliyeishia kidato cha nne, mi baada ya kidato cha nne nlifanikiwa kusomea ufundi umeme, namiliki cheti cha VETA.

Acha kushadidia mambo usiyoyafahamu,hiyo hoja ya Nyani Ngabu aliyotushinda iko wapi? Siwezi kuendelea kubishana na Nyani kwa sababu nimeshamfahamu ni mtu wa aina gani.
Lawyer's stock in trade is TIME and ADVICE. So I can't waste my precious time arguing with an imbecile like him. He is not only an ignorant but also a fool.
 
Last edited by a moderator:
umeona eeeh wanakimbilia kwenye kingereza kwa madai layman hatuwezi kuelewa

Hili ni jukwaa la sheria ,hivyo sioni umuhimu wa wewe ambaye sio mwanasheria kuja kushadidia mada ambazo hauzifahamu. Makosa madogo madogo ya lugha ni kawaida sana. Hata hao wenye lugha zao wanafanya hayo makosa. Kwa mfano mimi sio Muingereza na kiingereza ni lugha yangu ya pili,tena nimeanza kujifunza nikiwa darasa la tatu,hivyo sijisikii vibaya katu mtu akikosoa matumizi yangu ya lugha hiyo. Kwa muungwana kukosolewa kunajenga na wala hakubomoi.
 
Hivi ni kweli wanasheria watu wanatengeneza Contracts ? ama wana google templates na ku-edit kukidhi haja ya mteja ? Serious wanasheria wetu ni wazuri sana kwa Ku-kudesa toka Google results

Mkuu unawachokoza wasomi wetu ujue.
 
Acha kushadidia mambo usiyoyafahamu,hiyo hoja ya Nyani Ngabu aliyotushinda iko wapi? Siwezi kuendelea kubishana na Nyani kwa sababu nimeshamfahamu ni mtu wa aina gani.
Lawyer's stock in trade is TIME and ADVICE. So I can't waste my precious time arguing with an imbecile like him. He is not only an ignorant but also a fool.

Kaka msomi punguza jazba. Kama screen unaitolea povu namna hii, ukikutana naye si utamjambia kabisa?
 
Hivi ni kweli wanasheria watu wanatengeneza Contracts ? ama wana google templates na ku-edit kukidhi haja ya mteja ? Serious wanasheria wetu ni wazuri sana kwa Ku-kudesa toka Google results

kweli eh,basi nakushauri usimlipe ada yake ya uwakili kama anadesa kila kitu kutoka google. Ila kama anasoma vitu kutoka google,then anavitranslate katika local setting to suit your particular case,he is damn good and you should pay him his legal fees.
 
Hili ni jukwaa la sheria ,hivyo sioni umuhimu wa wewe ambaye sio mwanasheria kuja kushadidia mada ambazo hauzifahamu. Makosa madogo madogo ya lugha ni kawaida sana. Hata hao wenye lugha zao wanafanya hayo makosa. Kwa mfano mimi sio Muingereza na kiingereza ni lugha yangu ya pili,tena nimeanza kujifunza nikiwa darasa la tatu,hivyo sijisikii vibaya katu mtu akikosoa matumizi yangu ya lugha hiyo. Kwa muungwana kukosolewa kunajenga na wala hakubomoi.

Kwahiyo kama si mwanasheria sipaswi kuja jukwaa la sheria. Kwahiyo we mwanasheria pia hupaswi kuingia jukwaa la madaktari, right?
 
Kwahiyo kama si mwanasheria sipaswi kuja jukwaa la sheria. Kwahiyo we mwanasheria pia hupaswi kuingia jukwaa la madaktari, right?

sijasema haupaswi kuja ila haupaswi kushadidia mada ambazo you are less informed.Mimi siwezi kwenda kwenye jukwaa la madaktari na kuanza kushadidia mada ambazo sizifahamu.Huo ni ujuha
 
Kaka msomi punguza jazba. Kama screen unaitolea povu namna hii, ukikutana naye si utamjambia kabisa?

siwezi ila tu namuona kama mtu mwenye matatizo mengi ikiwa ni pamoja na ya akili.
 
Mimi nafikiri labda malalamiko yako yangekuwa kwa nini wanasheria hukubali kutetea watu hata kama wana makosa. Kwa uelewa wangu mdogo, mimi naona kama ndio kazi yao kutumia loopholes zozote zilizopo ili 'kuokoa' wateja wao. Kwa sababu hata wale ambao tumewaona walikuwa na makosa, kwa kutumia vipengele na 'kazi' makini za wanasheria, wameweza kukwepa mkono wa sheria.....Na mara nyingine wale wasio na hatia wakakosa wanasheria wanaojua kutumia vizuri jukwaa la sheria, huishia kutiwa hatiani...

Wanasheria msitutoe macho, ila huu ni mtazamo wetu nanyi mnaweza kutuelimisha zaidi kama tunavyofikiri sivyo uhalisia ulivyo...
 
Hili ni jukwaa la sheria ,hivyo sioni umuhimu wa wewe ambaye sio mwanasheria kuja kushadidia mada ambazo hauzifahamu. Makosa madogo madogo ya lugha ni kawaida sana. Hata hao wenye lugha zao wanafanya hayo makosa. Kwa mfano mimi sio Muingereza na kiingereza ni lugha yangu ya pili,tena nimeanza kujifunza nikiwa darasa la tatu,hivyo sijisikii vibaya katu mtu akikosoa matumizi yangu ya lugha hiyo. Kwa muungwana kukosolewa kunajenga na wala hakubomoi.

kwa hiyo kwenye jukwaa la sheria haruhusiwi mtu wa kawaida kusema chochote?kama wewe ni mwanasheria basi unatakiwa utusaidie sie ambao hatujui hiyo sheria kuielewa na si kusema tusishadadie mambo ambayo siyaelewi na nijuavyo mimi hakuna aliezaliwa anajua
 
kwa hiyo kwenye jukwaa la sheria haruhusiwi mtu wa kawaida kusema chochote?kama wewe ni mwanasheria basi unatakiwa utusaidie sie ambao hatujui hiyo sheria kuielewa na si kusema tusishadadie mambo ambayo siyaelewi na nijuavyo mimi hakuna aliezaliwa anajua

We ni msomi? Wanasheria wote ni wasomi.
 
Back
Top Bottom