Wanasheria wa lady JD wamtaka Gardner kuomba msamaha kwa maneno yake ya kidhalilishaji

Wanasheria wa lady JD wamtaka Gardner kuomba msamaha kwa maneno yake ya kidhalilishaji

Ukimjibu mtu aliyekutana utamthibishia kuwa lengo lake limetimia la kukuumiza,kukufedhehesha etc....but when u choose to keep quite atajidharau mwenyewe,au atazidi kutukana at the end atajiona kichaa,binafsi nashukuru dharau zimenisaidia saaaaana
 
Jide angetulia tuu ila naona amesukumwa na mashabiki. .
 
Hahahaaa....hiyo barua imeandaliwa na wanasheria?

Kabla hata sijaenda mbali katika kuikatakata mapanga.....hebu oneni hicho kipengele namba moja.

Hata wao wameshindwa kutamka moja kwa moja kuwa mteja wao katukanwa. Sasa wanamtaka Gadna aombe msamaha kwa msingi upi ilhali yeye hakutaja mtu?

Kama Gadna anahitaji kuomba msamaha basi huyo mwanamke naye anahitaji kumwomba msamaha Gadna kwa kumuimba kwenye huu wimbo wake mpya.

The theatre of the absurd!
 
Yaani hapo hamna kesi kabisa. Hakuna sehemu yoyote kwenye ile kauli Gadna alitaja jina la mtu. Alitumia neno " yule mtoto wa kike". Sasa Jay dee ni mtoto jamani? Gadna komaa kakangu usiombe msamaha wala nini. Tena kama vipi wafungulie kesi kwa kosa la kukuandikia barua kwenye karatasi isiyo na mistari.
Kifungu cha sheria gani kinasema karatasi lazma iwe na mistari?
 
Huyu dada anawaimba wenzie akisifiwa anaona raha, wakimjibu anaanzisha nongwa... hatari sana.

Ila kama nakumbuka vizuri kwenye ile clip jamaa alikuwa anajibu swali ambalo jide alitajwa, labda cyber law ya sikuizi itasaidia. Plus kwenye barua haionekani huo msamaha unatakiwa uombwe ndani ya muda gani.
Labda hujaisoma yote mkuu, ni ndani ya siku7 baada ya kupokea taarifa hiyo.
 
Labda hujaisoma yote mkuu, ni ndani ya siku7 baada ya kupokea taarifa hiyo.

Sikukiona hicho kipengele mkuu, mimi kwangu naona mwisho hiyo demand namba 3. Ila pamoja na kwamba kesi hii ni ya kishambenga, sio ya kudharau, kunakuwaga na suprise nyingi sana ndani ya kesi
 
Mambo mengine michosho na vichekesho tupu
Mkuu kudhalilishwa mbele ya hadhira kubwa sio jambo la kushabikia au kulipuuzia.Mwache dada jay dee aombwe msamaha tena hadharani kama alivyomdhalilisha hadharani.Tukipuuzia kila jambo mwishowe watu watawindana na kusababisha maafa.Kheri jay dee amekuwa muungwana sana.
 
She tried to,ila fans wake ndo wamezidi kuchochea...G aombe tu msamaha yaishe maisha yaendelee [emoji124] [emoji124] [emoji124] [emoji124] [emoji124]
Hilo ni tego la kisheria..hapo kwamba Gadna asipoomba msamaha basi ajiandae kupandishwa mahakamani, na fine atayopigwa hatoweza ilipa.
 
Gadner kama unatusoma au kuna watu watasoma humu mna mawasiliano wakuambie uachana kabisa na huu upuuzi wa jidy, she wont stop until you are finished. Kama angekuwa mungu its obvious angekunyima breath! anachotaka hapo mshindane kutoa pesa kwa mawakili bila shaka akutoe kabisa kwenye reli yako! believe or not its a game with a full budget. inavyoonyesha alikuacha kwa media huko rohoni ana hali mbaya bado anakutaka, anajidai ana furaha ambayo hana. wanaojiita mashabiki wake wako very narrow minded, wanataka wewe tu uwe gunia la mchanga la mazoezi ya ngumi.
siku zote anaamini pesa ina value kuliko utu wa mtu, kwani kuzaliwa mwanaume ni dhambi kutokuwa na hela kama mwanamke! kwani kuna wanawake wangapi wanafadhili game na waume zao lakini utadhani mfadhili ni mwanaume anavyoheshimiwa! man will always be a man. kama kuna wa kumuomba msamaha gadner ni muumba wako sio hiki kibibi kinachotaka ukipigie magoti after everything ili kikutungie nyimbo tena ukiwa umepiga magoti, hahaha. akuache ufanye yako bana, kina roho mbaya kama sura yake, alaaa. kama vipi toa namba au account tupitishe donei uweke mawakili wakukutetea huko mahakamani. mbele kwa mbele
Nimependa hii
 
Sheria bwana unaweza kushangaa Gadna akashinda kesi.
 
Mambo mengine michosho na vichekesho tupu
Ze ndii ndii ndii [emoji1] [emoji1] akiomba radhi ita undo kitendo cha kukojozwa kwa 15yrs!! Mambo mengine bana [emoji16] [emoji16] [emoji16]
 
Mtoto wa kike anaweza kuwa yoyote, na aliyefanya hayo kwa miaka 15 unaweza kupata jawabu alikuwa anamsema nani.
Una uhakika gani kwamba kwa miaka hyo yoote 15 alikua na jide tu, pia neno kumkojoza unalielewaje kwa mfano unavyompeleka mtoto chooni akakojoe unaenda kumfanya nini? Hii kesi naona wanataka kumpa ti ulaji gadna
 
Una uhakika gani kwamba kwa miaka hyo yoote 15 alikua na jide tu, pia neno kumkojoza unalielewaje kwa mfano unavyompeleka mtoto chooni akakojoe unaenda kumfanya nini? Hii kesi naona wanataka kumpa ti ulaji gadna
Kesi zingine zinasikitisha sana. Je wakati Gadna anatamka kumkojoza jina la Jide lilitamkwa? Au bado wanaoneana wivu?
 
Hawa wote bado wanapendana na ndio maana wanafatiliana kama hivi kuimbana na kusemana ila ukiangalia kwa undani bado kuna love kati yao sema wanachofanya sasa ni kuoneshana Nani zaidi
 
Back
Top Bottom