Wanasiasa ambao Mama hawezi kuwafukuza, wanafunguka, anaoweza kuwafukuza wako kimya, na hata hawamtetei wala kummunga mkono?Unagundua nini?

Hata yeye wakati Hayati JPM anachoma vifalanga vya kuku alikaa kimya mpaka JPM alivyofariki ndiyo akalaumu. Hivyo wana CCM wenzake wamekaa kimya mpaka akiacha uraisi kwa namna yoyote ndiyo watasema.
 
Sukuma Gang wanatapatapa tu
 
Haya tumepata AGENDA mpya ya kufungia MWAKA.
 
Bora Magufuli alikopa ila hakukuwekea tozo na vitu havikupanda sababu ya makodi kama sasa hivi

Huenda hukuwa hapa nchini wakati bidhaa zikipanda. Mafuta ya kula yalipanda wakati wake, sukari ilipanda pia wakati wake, mpaka akina Makonda wakawa wanazunguka kwenye maghala ya wafanyabiashara. Waulize wenzio waliokuwa hapa nchini.
 
Huenda hukuwa hapa nchini wakati bidhaa zikipanda. Mafuta ya kula yalipanda wakati wake, sukari ilipanda pia wakati wake, mpaka akina Makonda wakawa wanazunguka kwenye maghala ya wafanyabiashara. Waulize wenzio waliokuwa hapa nchini.
Ukiacha mafuta na sukari kipi kilipanda tena?

Nondo ilikuwa inauzwa elfu 30 kama ilivyo sasa?
Mafuta yalikuwa yanauzwa 2600 kama ilivyo sasa?
Ukikuwa unalipia maelfu kadhaa ukifanya miamala kama ilivyo sasa? Hivi utalinganisha upandaji wa sukari na huu uliopo sasa hivi?
 
Bwana Job anasema ipo siku Bongo itapigwa mnada, Mama anasema lazima akope.

Magufuli alitubana tulipe kodi akaonekana mbaya, Mama hataki tulipe lodi twende tukakope anaonekana mbaya.
Bri kila kitu kinatakiwa kuwa na kiasi.
1. Kodi za kiasi
2. Mikopo ya kiasi pia
Kila kitu kikizidi ni hatari kwa uchumi
 
Ndugai ametoa opinion yake bila woga kama wengi mnavyotaka. Huenda hata “hapambani” na Mama Samia as such

Tena kamalizia na kibwagizo kwamba “2025 mtaamua… kuwatoa waliopo sawa…”. Nadhani kinachowatesa baadhi ya watetezi wa Mama kipo kwenye kibwagizo hicho.
 
Bro uza ubongo huo maana unakaa nao kwa hasara, Magufuli alitubana tulipe kodi akaonekana mbaya, kisha deni la taifa likapaa kwa 20t within 5yrs! Sasa tunalipa kodi, lakini anakopa offcamera!
Fafanua kwenye hiyo tirioni 20 riba ya mikopo ya nyuma tirioni ngapi?
 
Kiuhalisia makamu wa Raisi na waziri mkuu ilitakiwa wajiuzuru kwa sababu hawaendani kabisa na utawala wa mama. Lakini ajabu wote wametulia kama mabubu mama akiachia ngazi ndiyo wanaanza kuyasema mabaya yake.

Nonsense
Mbona hata yeye alikaa kimya enzi za jpm

Malipo ni hapa hapa duniani
 
Mama hawezi kumfukuza spika,hiyo mandate hana labda ccm wamuondoe uspika

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
 
Mama endelea kupiga kazi wanakupinga utawanyamazisha kwa maendeleo yanayotokana na jitihada zako.
 
Mama kwa miezi 8 amekopa trilioni ngapi, ngapi zimeenda kisiwani na ngapi zimebaki Tanganyika? Zilizobaki Tanganyika zinafanya nini? Ukijumlisha na TOZO zilizotangazwa mara moja tu, mpaka sasa zimekusanywa ngapi na zinaenda wapi?

1.3t ya IMF pekee yake ingeingia mtaani, kila mtu angejua kuna pesa inazunguka ku-stimulate uchumi, ila tunachokiona ni kinyume, genge la wanyanganyi ndo linaibuka kwa kasi!
 
Bro uza ubongo huo maana unakaa nao kwa hasara, Magufuli alitubana tulipe kodi akaonekana mbaya, kisha deni la taifa likapaa kwa 20t within 5yrs! Sasa tunalipa kodi, lakini anakopa offcamera!
Lilipaa kwa kiasi gani!!??
sio unaongea bla bla za vijiweni weka data
 
Ni staili yake tu yakutongoza, hapendi makelele wala sifa, na hafagilii wanao jipendekeza na viongozi wanatambua Hilo.... Angekua magu wangetoka wengi Sana si kwamba Kwakua walikuwa wanamuunga mkono kutoka moyoni Bali Kwakua walitambua anafagilia wanaoweza kujipendekeza
 
Huenda hukuwa hapa nchini wakati bidhaa zikipanda. Mafuta ya kula yalipanda wakati wake, sukari ilipanda pia wakati wake, mpaka akina Makonda wakawa wanazunguka kwenye maghala ya wafanyabiashara. Waulize wenzio waliokuwa hapa nchini.
Walifanikiwa kushusha bei
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…