Wanasiasa na tabia za kizandiki ni Kama chapati na supu

Wanasiasa na tabia za kizandiki ni Kama chapati na supu

John Kwambaza

Member
Joined
Jul 15, 2021
Posts
6
Reaction score
4
Nadhani kama ningepewa task ngumu zaidi ni kutafuta mwanasiasa mmoja asiye mzandiki. Nalazimika kuhukumu kwamba pengine siasa ni uzandiki na uzandiki ndio siasa yenyewe.

Mjadala wenye afya kwa taifa unakuwa mzuri, Hadi pale wanasiasa wanapouteka nyara. Hoja ya katiba mpya na bandari ni mifano hai. Muda mwingine wanajisahau na kutamka maneno yenye maslahi kwa upande wao tu.

Huko kwenye majukwaa ndio taifa limegawanywa kimkakati katika makundi mawili, yaani CCM na non CCM. Kiufupi Kama wewe sio CCM manake ni kinyume chake, nadhani huu ni uzandiki wa hatari Sana kwa afya ya taifa.

Ikitokea mtu anatoa maoni yake kuhusu katiba mpya au Bandari, inatokea tu kwamba msimamo wake huchukuliwa katika misimamo ya kisiasa, hakuna maoni nje ya siasa.

Je, haiwezekani mtu akakosa mrengo wa kisiasa na bado akatoa maoni kama Mtanzania?
 
Kabla sijatoa komenti tafadhali mtoa post usitaje au kuorodhesha vyakula penda hapo juu.,
 
And then every Tanzanian has rights to speak out,opinion etc kwahy katiba imetoa dhamana hvyo si vibaya kwa mtu yeyote anavyofikiri na kama zikiwa pumba atawappa kuku hata ikiwa mchele atakula na wanawe,
 
Dunia hii imejaa uzandiki na hadaa nyingi sana. Wale wenye kuonekana wema na watakatifu machoni mwa watu wengi, nyuma yao kumejaa uharibifu mwingi sana. Ni mfano wa kaburi ambalo limepambwa kwa vitu vya kifahari, lakini ndani yake kuna mzoga uliokwisha oza na kutoa harufu mbaya sana. Pengine ni vyema tukatafari kipande kifuatacho kutoka katika maneno ya Injili.
Kabla sijatoa komenti tafadhali mtoa post usitaje au kuorodhesha vyakula penda hapo juu.,
Mathayo 7

13. “Ingieni kwa kupitia mlango mwembamba. Kwa maana njia inayoongoza kwenda kwenye maangamizi ni pana, na mlango wa kuingilia humo ni mpana; na waendao njia hiyo ni wengi.

14. Lakini njia inayoongoza kwenda kwenye uzima wa milele ni nyembamba, na mlango wa kuingilia humo ni mwembamba; ni watu wachache tu wanaoweza kuingia katika njia hiyo.

15. “Jihadharini na manabii wa uongo. Wao huja kwenu wakionekana kama kondoo kwa nje, lakini kwa ndani ni mbwamwitu wakali.

16. Mtawatambua kwa matendo yao. Je, watu huchuma zabibu katika miti ya miiba, au tini katika mbigili? La!

17. Basi, mti mzuri huzaa matunda mazuri, na mti mbaya huzaa matunda mabaya.

18. Mti mzuri hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mbaya hauwezi kuzaa matunda mazuri.

19. Kila mti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa motoni.

20. Kwa hiyo, mtawatambua kwa matendo yao.

21. “Si kila aniambiaye, ‘Bwana, Bwana’, ataingia katika ufalme wa mbinguni; ila ni yule tu anayetimiza matakwa ya Baba yangu aliye mbinguni.

22. Wengi wataniambia siku ile ya hukumu: ‘Bwana, Bwana! Kwa jina lako tulitangaza ujumbe wako, na kwa jina lako tuliwatoa pepo na kufanya miujiza mingi’.

23. Hapo nitawaambia: ‘Sikuwajua nyinyi kamwe; ondokeni mbele yangu, enyi watenda maovu.’
 
Dunia hii imejaa uzandiki na hadaa nyingi sana. Wale wenye kuonekana wema na watakatifu machoni mwa watu wengi, nyuma yao kumejaa uharibifu mwingi sana. Ni mfano wa kaburi ambalo limepambwa kwa vitu vya kifahari, lakini ndani yake kuna mzoga uliokwisha oza na kutoa harufu mbaya sana. Pengine ni vyema tukatafari kipande kifuatacho kutoka katika maneno ya Injili.Mathayo 7

13. “Ingieni kwa kupitia mlango mwembamba. Kwa maana njia inayoongoza kwenda kwenye maangamizi ni pana, na mlango wa kuingilia humo ni mpana; na waendao njia hiyo ni wengi.

14. Lakini njia inayoongoza kwenda kwenye uzima wa milele ni nyembamba, na mlango wa kuingilia humo ni mwembamba; ni watu wachache tu wanaoweza kuingia katika njia hiyo.

15. “Jihadharini na manabii wa uongo. Wao huja kwenu wakionekana kama kondoo kwa nje, lakini kwa ndani ni mbwamwitu wakali.

16. Mtawatambua kwa matendo yao. Je, watu huchuma zabibu katika miti ya miiba, au tini katika mbigili? La!

17. Basi, mti mzuri huzaa matunda mazuri, na mti mbaya huzaa matunda mabaya.

18. Mti mzuri hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mbaya hauwezi kuzaa matunda mazuri.

19. Kila mti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa motoni.

20. Kwa hiyo, mtawatambua kwa matendo yao.

21. “Si kila aniambiaye, ‘Bwana, Bwana’, ataingia katika ufalme wa mbinguni; ila ni yule tu anayetimiza matakwa ya Baba yangu aliye mbinguni.

22. Wengi wataniambia siku ile ya hukumu: ‘Bwana, Bwana! Kwa jina lako tulitangaza ujumbe wako, na kwa jina lako tuliwatoa pepo na kufanya miujiza mingi’.

23. Hapo nitawaambia: ‘Sikuwajua nyinyi kamwe; ondokeni mbele yangu, enyi watenda maovu.’
umenukuu vema
 
Back
Top Bottom