Wanasiasa na viongozi wa dini ni tishio kubwa la ustawi wa jamii ya watanzania na Afrika

Wanasiasa na viongozi wa dini ni tishio kubwa la ustawi wa jamii ya watanzania na Afrika

Escrowseal1

JF-Expert Member
Joined
Dec 17, 2014
Posts
4,618
Reaction score
4,605
Viongozi wa dini. Hili eneo wengi wanaliogopa ila ni eneo hatari sana linaloathiri ustawi wa watu wetu. Lina uhusiano mkubwa sana na politicians. Eneo la dini limekuwa hatarishi sana kukwamisha ustawi wa watu wetu. Viongozi wanajipatia ukwasi usiomithirika kwa kuwanyonya wananchi mafukara sana kwa kuuza leso, chimvi na maji na kuwabrain wash watu wetu huku hao wanaojiita mitume na manabii wakijilimbikizia mali chafu kutoka kwa jamii fukara hii hali inaumiza sana.

Uhusiano wa moja kwa moja wa viongozi wa dini na wanasiasa. Viongozi wa dini wanatumia ujinga unaosababishwa na wanasiasa na ufukara uliotopea katika jamii kutokana na kukosa pa kwenda ila kuona kuwa dini itamaliza matatizo yao mfano wengi wana wagonjwa wasio na matumaini ya kupona , ufukara na ujinga uliokithiri. Wanasiasa wameshindwa kuweka sheria na mifumo ya kusimamia utapeli huu. Ila pia uoga wa nguvu za hawa matapeli wa dini inawapa kigugumizi kuchukua hatua. Serikali zote duniani zinalinda masilahi ya watu wao ila kwa watanzania na waafrika wengi imekuwa saratani.

Wanasiasa
Hili ni kundi lingine la kutupia macho na jamii yetu. Kwani limekuwa kundi selfish la aina yake. Percent kubwa ya rasilimali zenye mchango mkubwa wa ustawi wa jamii huishia kwa hili kundi mfano , kujipendelea kwa kujipatia magari ya gharama kubwa imekuwa kufuru na new normal . malipo ya wawakilishi wa hawa watu mafukara aka wabunge , mpango wa kuwalipa wake wenza wa viongozi hata kama washachuma wasivyokuwa na kazi navyo. Kujipangia benefiti kama nyumba za bure , kutolipa kodi na hata pamoja na hayo yote kundi hili ndilo linaongoza kuiba rasilimali za Taifa kuanzia ngazi za juu hadi chini kabisa.

Kama kungekuwa na Takwimu kamili za mapato yanayonyonywa na viongozi hawa waliojivisha ngozi ya kondoo na hawa wanasiasa basi jamii ingeamka.

Kuna symbiotic relationship kati ya makundi haya mawili . Moja likitegemea kuchuma uungwaji wa hawa mafukara wasiojitambua na lingine likitumia uhohehae, na ujinga uliozalishwa na hili kundi la pili kuwatapeli na ndo maana kundi moja ambalo lingekuwa mwarobaili liko kimya.

Napendekeza kama jamii tunge review maadui wa maendeleo tuka update na kupachika haya makundi labda mambo yangebadirika maana hali ya mwananchi wa kawaida kabisa ukilinganisha na haya makundi japo yana uhusiano wa moja kwa moja ni mbingu na ardhi.

Shangwe kwa vijana wa Gen Z la nchi jirani kwa kujitambua na kulikalia kooni kwa kutambua janja janja ya hili kundi kuu ambalo limemwaga manyanga na kukata matumizi kila sehemu mfano magari kufuru, bajeti janja janja za kuliibia taifa , pesa za wake wenza nk . Naamini siku moja isiyotabirika mafukara na wajinga wetu nao watagundua janja ya makundi haya.

Nawasilisha.

Nakala kwa bwana Mwanshambwa.
 
Viongozi wa dini. Hili eneo wengi wanaliogopa ila ni eneo hatari sana linaloathiri ustawi wa watu wetu. Lina uhusiano mkubwa sana na politicians. Eneo la dini limekuwa hatarishi sana za kuliibia taifa , pesa za wake wenza nk . Naamini siku moja isiyotabirika mafukara na wajinga wetu nao watagundua janja ya makundi haya.

Nawasilisha .

Nakala kwa bwana Mwanshambwa.
Ni ukweli usiopingika kuwa wanasiasa wanawatumia viongozi wa dini zote kwa maslahi yao, na viongozi wa dini wameshaionja asali ya ubadhirifu, wao sasa wamekuwa mstari wa mbele kuitumia fursa.

Wamekutana wanafik na wanafik wenzao.

Zamani viongozi wa dini walitumika kuhamasisha jamii zao bila malipo wala sadaka za kutokea serikalini, leo kiongozi wa dini analipwa "per diem" tena bahasha nene kila anapoalikwa kwenye mikutano ya kisiasa, kuna dini hapo au unafik tu?
 
Serikali iwache unafik wa kuita "viongozi" wa dini eti "kuomba dua" kwenye shughuli za kiserikali. Dua inaombwa na yeyote yule, si lazima awe Sheikh au kasisi, tena nzuri zaidi ni ya kila mmoja kuomba kimya kimya kivyake.

Inachotakiwa mc aseme tu "dua', kamaliza. hakuna kukaribishwa yeyote kinafik.

Huwa nawashangaa sana viongozi wa Kiislam wanapozusha dua zisizokuwepo katika mafundisho ya Qur'an. Qur'an imetufundisha namna ya kuomba dua na haina mbadala.
 
Kuongoza watu wajinga/makondoo ni rahisi sana...

Dini zinawafanya watu wawe makondoo....

Kwa kufanya hivyo wanawarahisishia wanasiasa kuongoza...

In return, hizo dini nazo zinaachwa zijiendeshe bila kuingiliwa...

NDIYO MAANA HAWATOZWI KODI YA KITU CHOCHOTE KILE..
 
Kwa nchi yetu hili sio jambo geni. Ni dhahiri watu wanafahamu Siasa ndiyo inayoendesha vitu vingi na ina uwezo wa kuathiri vingi.

Tanzania dini bila siasa, sport bila siasa aaah wap
 
Ni ukweli usiopingika kuwa wanasiasa wanawatumia viongozi wa dini zote kwa maslahi yao, na viongozi wa dini wameshaionja asali ya ubadhirifu, wao sasa wamekuwa mstari wa mbele kuitumia fursa.
Kumbe kuna siku unakuwaga na akili timamu?

Hilo andiko la huyo jamaa hapo linachosha kusoma; lakini naona umejitahidi kulisoma na kutoka na mistari hiyo miwili inayo eleweka vyema kuliko andiko zima la huyo mleta mada!
 
Kumbe kuna siku unakuwaga na akili timamu?

Hilo andiko la huyo jamaa hapo linachosha kusoma; lakini naona umejitahidi kulisoma na kutoka na mistari hiyo miwili inayo eleweka vyema kuliko andiko zima la huyo mleta mada!
Matusi ya rejareja hayo. Hakuna binadam asiye na akili, kusema fulani hana akili, ni ujinga wa kibinadam tu. Tatizo ni vipi tunazitumia akili zetu. Wengine ndiyo kama wewe, wanaona wenzao wana akili za muda fulani tu, ni namna tu unavyoitumia akili yako.
 
Matusi ya rejareja hayo. Hakuna binadam asiye na akili, kusema fulani hana akili, ni ujinga wa kibinadam tu. Tatizo ni vipi tunazitumia akili zetu. Wengine ndiyo kama wewe, wanaona wenzao wana akili za muda fulani tu, ni namna tu unavyoitumia akili yako.
Leo umetulia sana. Siwezi kamwe kupinga unacho andika katika hali hii.
 
Shangwe kwa vijana wa Gen Z la nchi jirani kwa kujitambua na kulikalia kooni kwa kutambua janja janja ya hili kundi kuu ambalo limemwaga manyanga na kukata matumizi kila sehemu mfano magari kufuru, bajeti janja janja za kuliibia taifa , pesa za wake wenza nk . Naamini siku moja isiyotabirika mafukara na wajinga wetu nao watagundua janja ya makundi haya.
Nadharia yako inakubalika sana kwa mfano huu uliotoa kuhusu "... kundi kuu..." la huko kwa hao Gen Z waliokataa hadaa.
Huyo mkuu wa "kundi kuu" alilitumia hilo kundi la dini kama nyenzo ya kumweka madarakani. Kila Jumapili anazunguka makanisani huko; kwa sababu anajuwa ndiko alikopatia ukuu wake.
Kwa bahati nzuri kwa nchi hiyo, Gen Z wakaona hadaa za kijinga hizo.

Hapa kwetu, ndio kwanza serikali inajenga makanisa na misikiti!

Lakini matumaini ni haya: mabadiliko yoyote hayatokei kwa sababu kila kondoo na mbuzi waamushwe usingizini.
Mabadiliko huletwa na kundi dogo tu linalojielewa; hayo makondoo na mambuzi hufuata tu nyuma.
 
Kuongoza watu wajinga/makondoo ni rahisi sana...

Dini zinawafanya watu wawe makondoo....

Kwa kufanya hivyo wanawarahisishia wanasiasa kuongoza...

In return, hizo dini nazo zinaachwa zijiendeshe bila kuingiliwa...

NDIYO MAANA HAWATOZWI KODI YA KITU CHOCHOTE KILE..
Uislam umekuja kumweka mtu huru, hizo unazoongelea za ukondoo siyo mafundisho ya Kiislam.

Uislam unatufundisha kuwa kila mmoja wetu anapaswa awe "Khalifa" na kila mmoja wetu anapaswa awe ni mchungaji wa mwenzake. Hakuna kondoo.

Tuamrishane mema na tukatazane maovu na mabaya.
 
Hii ni kawaida yangu, miaka sasa, hunisomi vizuri tu.
Sasa unataka hata nikatafute mifano iliyojaa humu JF inayo kutambulisha kivingine kuliko unavyodai?

Sitaki twende huko leo. Nimekwisha ridhika na hiki nilicho kiona hapa leo, ingawaje najua hii ni hali ya mpito tu!
 
Sasa unataka hata nikatafute mifano iliyojaa humu JF inayo kutambulisha kivingine kuliko unavyodai?

Sitaki twende huko leo. Nimekwisha ridhika na hiki nilicho kiona hapa leo, ingawaje najua hii ni hali ya mpito tu!
Nakupa Rukhsa, tafuta tena haraka sana.
 
Tuamrishane mema na tukatazane maovu na mabaya
Tayari 'controversy' haikai mbali nawe unapoingiza maswala haya ya dini.
Huko "kuamrishana mema na kukatazana maovu na mabaya"..., Nani ana vipimo hivyo vya mema na mabaya?
 
Ni ukweli usiopingika kuwa wanasiasa wanawatumia viongozi wa dini zote kwa maslahi yao, na viongozi wa dini wameshaionja asali ya ubadhirifu, wao sasa wamekuwa mstari wa mbele kuitumia fursa.

Wamekutana wanafik na wanafik wenzao.

Zamani viongozi wa dini walitumika kuhamasisha jamii zao bila malipo wala sadaka za kutokea serikalini, leo kiongozi wa dini analipwa "per diem" tena bahasha nene kila anapoalikwa kwenye mikutano ya kisiasa, kuna dini hapo au unafik tu?
Bi Mkubwa, ukitulia unaandika kwa uchungu.
 
Back
Top Bottom