Wanasiasa wanaposhindana kuijua Biblia na Koran badala ya Katiba na Sera za Nchi

Wanasiasa wanaposhindana kuijua Biblia na Koran badala ya Katiba na Sera za Nchi

Zygot

JF-Expert Member
Joined
Apr 14, 2016
Posts
2,265
Reaction score
2,919
Tangu awamu ya 4, 5 na sasa awamu ya 6 hali imekuwa kutoa mifano ya Biblia na Koran, Bungeni na majukwaani. Wanasiasa wanaotoa hotuba zinazostahili kuwa msikitini na kanisani.

Leo hii mkuu wa mkoa wa Mwanza anamwita rais Samia ni mtumishi aliyeletwa na Mungu. Sijui anatutisha au anajisemea kumfurahisha rais. Awamu ya 4 Kikwete tuliambiwa ni mteule wa Mungu na akapewa support hata na viongozi wa dini. Ni kweli aliyotenda alitumwa na Mungu? Awamu ya 5 uzi ule ule! Leo hii maumivi hadi kooni.

Huku ni kufilisika kisiasa. Hatukuwachagua wala hamkuteuliwa ili kutufundisha misahafu. Wanasiasa ni wasimamizi wa vyombo vya utawala. Tunahitaji uelewa wenu wa katiba ya nchi, sera pamoja na sheria zake. Hatuhitaji busara za kujua misahafu ambayo usimamizi wake uko chini ya watu wengine.
 
Sioni tatizo. Vitabu vya dini vinatoa reference nzuri zinazojenga jamii.
 
Sioni tatizo. Vitabu vya dini vinatoa reference nzuri zinazojenga jamii.
Siamini hilo! Jamii zilizostaarabika na kufuata utu Duniani, hazina hata sara kwenye mikutano ya kitaifa. Tembelea Japan, China, UK, ........Sisi ni unafiki mwingi na kuigiza halafu wizi mwingiii!.
 
Back
Top Bottom