Wanasiasa (Zitto na Kitila) acheni kuingilia mambo ya mipira, Mnategemewa kuwa mfano katika kuheshimu mamlaka

Wanasiasa (Zitto na Kitila) acheni kuingilia mambo ya mipira, Mnategemewa kuwa mfano katika kuheshimu mamlaka

Hawazuiwi kuwa mashabiki ila wanatakiwa kuwa mashabiki katika level ambayo ni ya kawaida tu na si katika hiyo waliyoiparamia. Hawa watu tumewakabdihi majukumu makubwa ya nchi. ACT Wazalendo ni ya Watanzania, siyo ya Zitto. Tunaomba sana hawa watu watusaidie kwenye maswala yenye maslahi mapana ya Taifa; wamsaidie Mama, angalau hata kwa kumkosoa tu inatosha,
Kabisa
 
Maoni ya wengi, yanashangaza. Hata, baadhi ya wachambuzi Redioni, mfano RFA, nao wameniacha hoi. Wametusikilizisha sauti ya msoma hukumu, inaonyesha kosa la wazi la Manara. Yaani, kile kitendo cha kutoka alikokaa, na kwenda kupiga kelele mbele ya VIP, walikokaa wenye hadhi hiyo. Tunaambiwa, aliambiwa aondoke hapo mbele. Aliondoka, na kurudi tena. Pia akambiwa aondoke, mpaka Karia naye akaingilia kati, kumtaka aondoke hapo mbele.
Sasa, wao wameng'ang'ania kuwa, Karia naye alistahili adhabu! Sijui kwa kosa gani?
Kanuni ziko wazi
 
Wana kimbelembele Cha kujifanya wanajua kila kitu, Manara ingawa wengi wanamhisi ni mzaramo kwao ni kigoma Kwa kifupi adhabu aliyopewa na makosa yake ya kujirudia ni ndogo mno alitakiwa afungiwe miaka kumi na kuendelea tapeli wa magari Leo ndio.tunamwona mstaarabu
Manara aliwahi kufungia mpira miaka 7, uongozi wa KARIA ndiyo uliukuja kumtoa kwa kusikiliza rufaa!
Hivyo manara ni sikio la kufa
 
Sakata la Manara tuwaachie TFF!
Walichokiamua wao sisi kama watazamaji tunatakiwa kuheshimu!
Kama kuna rufaa mwacheni mhusika mwenyewe!

Kuilaumu TFF ni ishara ya kupungukiwa hekima; Watu kama ZITTO sikutegemea kabisa waoneshe ujinga hadharani!
Kuna yule pia anajiita Prof. MKUMBO, huyu naye sikutegemea aanike ujinga wake namna hii ni mkumbo tu.

Mambo ya mipira yanaongozwa na kanuni na sheria!

Kanuni zikikiukwa ni lazima kanuni zitumike kuamua!
Mbona watu wasiyo na majina wakihukumiwa huwa hamsemi?
Au kanuni zimewekwa kwa baadhi ya watu hawatakiwi kuguswa?

Wanasiasa pelekeni ujinga wenu huko; Mnajitia mnajua kila kitu hapa duniani, Siasa nyinyi, Mambo ya dini nyinyi, mambo ya vita nyinyi, mapenzi nyinyi na sasa na mambo ya mipira mnajitia wasemaji?

Mlitaka ahukumiwe nani?
Kama Haji manara hakukosea Je aliomba radhi kitu gani?
Kama aliomba radhi maana yake alitenda kosa basi TFF wamemuwajisha kama kanuni inavyotaka!
Wanaosema kwanini KARIA Hakuitwa wanatakiwa wajue, nani kamfuata mwenzake kwenye tukio!..
Kibaka akikuvamia nyumbani kwako hata kama ulimjeruhi kwa kujihami bado mkosaji ni yule KIBAKA aliyekuja kuvamia!

Manara alivamia ndiyo maana kawajibishwa!

Mnaomshauri Manara akate Rufaa mnamjaza ujinga KULE NDIYO WATAMPIGA NYUNDO YA MIAKA 5 na faini juu!

Tena asipokaa sawa watashauriana na AZAM wampokonye kabisa hata king'amuzi ili asiangalie mpira wenyewe!

HAKUNA ALIYE JUU YA SHERIA! wanasiasa uchwara achaneni na mpira!

Ambao hamkumbuki ni kwamba TFF Ilishawahi kumfungia manara kwa miaka 7 , uongozi mpya wa kalia ulipoingia ukasikiliza rufaa yake wakamwachia!
MJINGA ni yule anayetoa maoni yake lakini anakashifu maoni ya wengine kwa vile tu yanakinzana na utashi na matamanio yake!

Katika hilo hata ngumbaro anadiriki kumkebehi mtu kama Prof Mkumbo na Msomi Zitto kabwe kuwa ni wajinga! huku akishindwa kukosoa ama kujadili haja walizotoa kimantiki!

Katika misingi ya asili ya haki mlalamikiwa na mlalamikaji wote huitwa na kutoa maelezo yao mbele ya kamati au mamlaka ya kutoa haki, kabla ya kuchambua maelezo ya pande zote mbili pamoja na ushahidi wao, hatua ambayo itaiwezesha kamati kutoa uamuzi wa haki kutokana na nguvu za hoja!
Huo utaratibu wa mshitaki kuwa ni huyo huyo, muendesha mashtaka awe ni yuleyule na mtoa hukumu ni yuleyule tunabananga natural justice!

Ni mwelekeo tenge na usio na afya, unaopaswa kusitishwa kwa kwa nguvu zote.
JADILI!
 
MJINGA ni yule anayetoa maoni yake lakini anakashifu maoni ya wengine kwa vile tu yanakinzana na utashi na matamanio yake!

Katika hilo hata ngumbaro anadiriki kumkebehi mtu kama Prof Mkumbo na Msomi Zitto kabwe kuwa ni wajinga! huku akishindwa kukosoa ama kujadili haja walizotoa kimantiki!

Katika misingi ya asili ya haki mlalamikiwa na mlalamikaji wote huitwa na kutoa maelezo yao mbele ya kamati au mamlaka ya kutoa haki, kabla ya kuchambua maelezo ya pande zote mbili pamoja na ushahidi wao, hatua ambayo itaiwezesha kamati kutoa uamuzi wa haki kutokana na nguvu za hoja!
Huo utaratibu wa mshitaki kuwa ni huyo huyo, muendesha mashtaka awe ni yuleyule na mtoa hukumu ni yuleyule tunabananga natural justice!

Ni mwelekeo tenge na usio na afya, unaopaswa kusitishwa kwa kwa nguvu zote.
JADILI!
 
Back
Top Bottom