Wanasimba naomba mpite hapa niwaambie kitu (vitu)

Wanasimba naomba mpite hapa niwaambie kitu (vitu)

Mario Kejob

JF-Expert Member
Joined
Apr 14, 2020
Posts
441
Reaction score
536
Tatizo lililopo hapa ni mfumo. Wachezaji walioondoka waliacha mfumo wa uchezaji ambao waliobaki wameshindwa kuufuata. Na hao walikuwa wanatengeneza rhythm ya timu na jinsi itakavyo flow na kushambulia.
Kinachotakuwa kufanyika ni kurudi kwenye flow iliyozoeleka ya pira biriani la pasi nyingi mpaka goli linapatikana kuliko kinachofanyika sasa hivi kutumia mipira ambayo haijazalisha goli lolote katika mechi tatu sasa.
Wale mabwana walioondoka walikuwa wanachangia 60% ya magoli na assists zote. Walikuwa ni miamba kweli kweli.
Kuanzisha mfumo mpya au rhythm mpya ni kazi kweli. Wapenzi wa Msimbazi watakuwa na kipindi kigumu sana kuukabili ukweli wakati suluhisho likiendelea kutafutwa. Mpaka sasa hivi kocha hana first eleven ya wachezaji waliopo na ndio ujue kazi ngumu kiasi gani.
Ma-striker wetu wote ambao si wanyumbulifu hawatokuwa na mchango mkubwa msimu huu kwani mpishi wao hayupo tena na upangaji wa timu bado inamshinda kocha wetu. Ningependa kuona anawapa game time ya kutosha hao wanaodhania kuziba mapengo ya walioondoka lakini simuoni kufanya hivyo. Ni kama tu amechanganyikiwa.
 
Hizi habari za kuondoka kwa chama na miq....tushazichoka sasa, Mnaongea jambo ambalo kila mtu analifahamu. Lakini kwa kukumbusha tu hata chama na miq walivyokuwepo Simba Ugenini alikuwa anacheza mpira huu huu, kwahiyo huu mpira wala sio mgeni Simba, labda wewe ndio umeubaini saivi.
 
Tatizo lililopo hapa ni mfumo. Wachezaji walioondoka waliacha mfumo wa uchezaji ambao waliobaki wameshindwa kuufuata. Na hao walikuwa wanatengeneza rhythm ya timu na jinsi itakavyo flow na kushambulia.
Kinachotakuwa kufanyika ni kurudi kwenye flow iliyozoeleka ya pira biriani la pasi nyingi mpaka goli linapatikana kuliko kinachofanyika sasa hivi kutumia mipira ambayo haijazalisha goli lolote katika mechi tatu sasa.
Wale mabwana walioondoka walikuwa wanachangia 60% ya magoli na assists zote. Walikuwa ni miamba kweli kweli.
Kuanzisha mfumo mpya au rhythm mpya ni kazi kweli. Wapenzi wa Msimbazi watakuwa na kipindi kigumu sana kuukabili ukweli wakati suluhisho likiendelea kutafutwa. Mpaka sasa hivi kocha hana first eleven ya wachezaji waliopo na ndio ujue kazi ngumu kiasi gani.
Ma-striker wetu wote ambao si wanyumbulifu hawatokuwa na mchango mkubwa msimu huu kwani mpishi wao hayupo tena na upangaji wa timu bado inamshinda kocha wetu. Ningependa kuona anawapa game time ya kutosha hao wanaodhania kuziba mapengo ya walioondoka lakini simuoni kufanya hivyo. Ni kama tu amechanganyikiwa.
CAF wamesema kocha wetu sio Msomi, tumcahngieni jamani akasome hata QT
 
Alipofariki Mafisango Kuna watu walisema Simba haitapata mbadala wake. Leo wengine mmemsahau kwasababu ya Chama na Louis. Siku zijazo mtalalamikia kuondoka kwa wachezaji wengine na sio Chama na Louis tena!
Siku zote vipaji vikubwa vikubwa huwa vinaibuliwa Simba, kina Chama na Micquissone walipoingia Simba ukali haukuonekana mwanzoni, baaaadae ndo tumeona balaa lao, hao wengine ndani ya Simba wataibuka tu ni suala la muda!
 
Siku zote vipaji vikubwa vikubwa huwa vinaibuliwa Simba, kina Chama na Micquissone walipoingia Simba ukali haukuonekana mwanzoni, baaaadae ndo tumeona balaa lao, hao wengine ndani ya Simba wataibuka tu ni suala la muda!
Umeonae!
 
Ukweli ni kwamba Simba imesajili wavulana wengi mpango wao wataichezea timu kwa muda mrefu kwaiyo itahitaji kuwa vumilia, Yanga wamesajili wachezaji wenye umri mkubwa na uzoefu kwakua wanaitaji kurejesha ufalme wao wa kutwaa Mataji.
Ki uhalisia dalili za nani atafanya vizuri msimu huu ziko wazi Ila muda ni mwalimu mzuri.
 
Kagere
Mugalu
Bokoboko

Muwape muda watakuwa kwenye rythim blo so kuwa na subira
 
Siku zote vipaji vikubwa vikubwa huwa vinaibuliwa Simba, kina Chama na Micquissone walipoingia Simba ukali haukuonekana mwanzoni, baaaadae ndo tumeona balaa lao, hao wengine ndani ya Simba wataibuka tu ni suala la muda!
Kwahiyo chama na micquissone wamevumbuliwa vipaji vyao simba?
 
wewe umeanza kuwafaamu wakiwa timu gani ?
Swala sio kuwafahamu swala ni wewe ulipodai wamevumbuliwa vipaji simba?

Hivi unajua kama chama kabla ya kuja bongo alishacheza ligi ya misri? Nchi ambayo nafasi za wachezaji wa kigeni ni 4 tu?

Konde boy si alikua mamelod?

Ko huko kote walikua hawajulikani wakaja julikana Simba?
Sometimes tuwe tunaongea ukweli na kufwatilia vitu.
 
Hizi habari za kuondoka kwa chama na miq....tushazichoka sasa, Mnaongea jambo ambalo kila mtu analifahamu. Lakini kwa kukumbusha tu hata chama na miq walivyokuwepo Simba Ugenini alikuwa anacheza mpira huu huu, kwahiyo huu mpira wala sio mgeni Simba, labda wewe ndio umeubaini saivi.
Hao wameanza fuatilia mpira leo mdau mambo ya misimu iliyopita hawayajui......eti pira biriani pasi nyingi uwanja wenyewe ule ukipiga mpiea rula unadunda dunda mpaka unamfikia mchezaji ushapoteza muelekeo....


Pambaneni viwanja viwekwe nyasi bandia
 
Hao wameanza fuatilia mpira leo mdau mambo ya misimu iliyopita hawayajui......eti pira biriani pasi nyingi uwanja wenyewe ule ukipiga mpiea rula unadunda dunda mpaka unamfikia mchezaji ushapoteza muelekeo....


Pambaneni viwanja viwekwe nyasi bandia
Misimu yote viwanja vya mikoani Simba anacheza mipira mirefu....
Nashangaa saiv imekuwa kesi.
 
Back
Top Bottom