Wanaume acheni kuzaa na wanawake ambao hamtawaoa

Wanaume acheni kuzaa na wanawake ambao hamtawaoa

Ni miaka saba sio nane. Kama yupo timamu na anajiweza kimalezi nje ya hapo, huwezi acha mtoto akae miaka 7 na mama ambaye ni mlevi, mdangaji anafanya matukio ya kukosa adabu mbele ya watoto.
Ndiyo mkuu, upo sahihi.
pia sheria inasema kama mama tashindwa kulea mtoto/watoto basi baba atakabidhiwa hao watoto/mtoto baada ya uchunguzi kufanyika juu ya malezi mabaya kutoka kwa mama.
 
Wanawake wa siku hizi macho yao yapo juu Kwenye pesa yaani akishaona pesa anachanganyikiwa mazima anajikuta ameukwaa uja uzito wa mtu ambaye hata hamfahamu vizuri.

Kuna member hapo juu kasema suala la kubeba mimba Ni maamuzi ya mwanamke.
 
Sisi huku bado sana mambo hayo, tunajipigia tu. Akizaa atajijua, na hata akienda mahakamani unakuta gharama za matunzo siyo kubwa.

Diamond alipelekwa mahakamani alivyomkataa mtoto wa Mobeto. Diamond akaamuliwa aanze kutoa matunzo ya mtoto. Huwezi amini, Diamond na mihela yake yote aliiambia mahakama kuwa uwezo.wake ni kutoa sh 200k kwa mwezi. Ndiyo maana Mobeto akaamua kujikataa kwa Diamond mazima akasema yule siyo mtoto wa Diamond
Gold digger alitaka kuleta usanii kwenye jumba la sanaa
 
Wanawake kama wanaweza zaa na wazee Rika za babu zao, wanaume za watu, vichaa, na kadhalika usishangae wao kuzaa na mtu asiye na sifa za kuwa baba wa familia anayoianzisha bila utaratibu.
Kama unajua hivyo basi pia huna sababu ya kutulaumu wanaume
 
My point exactly. Majuto ya kuzaa na mwendawazimu au mwanamke asiyejitambua ni ya maisha yote. Utakuwa kila ukiwaona watoto unatamani ungewapa mama wa kueleweka ili waweze kuwa katika mazingira ya upendo na amani. Ila ndio umeshabugi na hauwezi rudisha muda nyuma.

Unaona mfano yule kijana aliyezaa na Giggy money kwan hakuwa akiona matukio na fujo za Giggy money?

Ila kwa upuuzi tu akajiona yeye ana akili kushinda nature akaacha kufuga kuku wa nyama atakata kufuga kunguru sijui ili iwe nini mwisho wa siku maana kunguru mbali na kwamba hafugiki lakini pia hana faida yoyote kusema utamla nyama kama kuku.

Leo mwanamke yule yule ambaye alipuuza kumuepuka anampelekesha mitandaoni na kumchafulia jina lake na familia yake hata pasipo kumchokoza au kumfanya lolote anashangaa anapigiwa simu "Wewe baba fulani umeona alichopost giggy leo huko Instagram, amekutukana balaa, kwan umefanyaje hadi kakasirika vile" kumbe Giggy money amekunywa tu savannah nyingi amevuta na bange zimeamsha wazimu akatafuta sababu ya kutoa kichaa chake na akaamua kumuwashia moto mwanaume aliyezaa nae mtoto.

Wewe unadhani yule kijana anajiskiaje kwasasa kuona mtoto wake analelewa na mama kama Giggy money ambaye anatumia pesa za udangaji kumtunza mtoto huku yeye akikosa access ya kukaa na mtoto lakini pia akitazama mtoto wake anakuwa katika mazingira ya fujo hivyo anajiskiaje? [emoji848][emoji848][emoji848][emoji848]
Mo jay lazma anajuta kuzaa na gigy mara aone connection ya mzazi mwenzie,pia yule mtoto wake wa kike atakuwa kwenye malez mabaya..

Mkuu nimejifunza kitu kikubwa tuweke mbegu zetu sehemu sahihi.
 
Sasa kabla haujatomba lazima ujue kuwa pale nikizama sitoboi why unazama?

Ni sawa na kuvuka na pikipiki kwenye mto wenye maji mengi wakati wa mvua. Usiseme nitajua nikifika katikati. Unatazama kwa macho tu unajua kuwa huu mto mimi sitavuka salama haya maji yana nguvu sana yatanizoa na pikipiki yangu.
Sawa mkuu. Ila sasa utamu wa mapenzi ni kama tuseme ni ka Drug. Ulishawahi kuwaona drug addicts?. Ukiwapa mfano wako huu ambao kiukweli ni very logical na inamake sense ila sasa kampe drug addict huo mfano tuone kama utamtoa humo kwenye drug addiction japo akiwa na mind status ambayo inaweza kupita na hiyo chance atapita, ila majority huwez mtoa mtu kwenye drug addctn kisa umetoa mfano ambao ni logial una make sense. Utaingia kichwani kwake sawa ila unaweza ukatoweka humo kichwani mwake after a short time or after sometime.

Sasa mapenzi yanaweza kufeel kama Drug pia. Utapiga utaua ila wenzako wanaendelea hivyo hivyo. Binadamu ndo wako hivyo sasa..

mambo ni mengi muda ndo mchache.
 
Wewe ndio unatakiwa usikojolee ndani Vaa kondom
Sasa mbona KE unawapiga kavu bila ndom na wapo kimya. Na hata ukimjulisha kuwa naelekea kukojoa sasa hachukui hatua yoyote zaidi ya kuongeza miguna ya utamu na unamkojolea ndan kabisa na anajua tena anafurahia. Sasa unataka kuwarekebisha wanaume? utakojolewa ndan na wadau wanakula kona na namba ya simu wanabadilisha.

Utajua hujui.
 
Mlishasema Mimba ya Bahati mbaya ni ya kwanza TU nyingine zote ni MAAMUZI
Hakuna mimba ya bahati mbaya isipokuwa ya kubakwa, au kwa minor, minor anaweza asielewe mzunguko vizuri au asielewe njia za uzazi wa mpango.

Binafsi ningemuomba metal mada aandike uzi wenye heading vise versa na hiyo ya sasa.
 
Ila mkuu mwanaume anaushawishi katika ilo swala naweza sema asilimiaa 70
Dogo punguza utahira basi kidogo, unavyowatetea wanawake mwisho wa siku unaonekana tahira hata kwa hao wanawake wenyewe....

Kwamba mwanaume ndio anachangia kwa 70% kwenye suala zima la mwanamke kubeba mimba? Dogo hivi ina umri gani kwanza?

Mwanamke kama hakuelewi au hajaipenda mbegu yako hawezi akakubebea mimba ng'ooo yaani hata umtombee vipi, kama hajapanga kuzaa na wewe huwezi kumpa mimba hata iweje kwenye zama hizi ambazo kuna njia chungu nzima za kuzuia mimba pamoja na cheap abortions.

Yaani kabisa umekaa hapa unakaza fuvu kwamba wanaume tuko responsible kwenye suala la ubebaji wa mimba, na wakati wao ndio waamuzi wa mwisho na akiamua asikuzalie hata kama mimba ina miezi sita anaweza akaipoteza na huna la kumfanya...

Wewe dogo unaonekana ni mgeni wa wanawake na tayari umeshamezwa na mfumo jike ambao umewafanya wanaume wengi wawe watetezi wa wanawake hata pale ambapo hakuna nmna sahihi ya kuwatetea.
 
Inakwaza na kufedhesha sana kwasasa kuona kuna ongezeko kubwa la watoto ambao hawajulikani baba zao ni akina nani na hata kama baba wanajulikana basi hawapo katika maisha ya mtoto.

Big up kwa akina baba ambao wanapambania kuwatunza na kuwalea watoto wao wa damu na kuwajibika kama baba na kutowatenga hawa watoto.

Kimsingi baba ni mtu muhimu sana katika maisha ya mtoto na baba anapokosekana katika maisha ya mtoto ni rahisi sana kwa mtoto kupoteza direction ya Maisha utu uzimani.

Mtoto wa kiume unakutana na mdada haujui history yake haumfahamu anaishi kwa mwenendo gani kisa tu kakuruhusu kumpelekea moto unaachia mbegu zako kwenye mji wake wa uzazi ukijua wazi matokeo yake ni yapi.

Hivi huwazii mtoto wako anapozaliwa huyo ndie atakuwa mama yake na wewe ndie baba yake na ndio mwanzo wa familia? Why sasa unaanzisha kitu kikubwa namna hiyo katika hali ya kizembe sana.

Hauoni kuwa unakuja kumpa maisha ya mateso na maumivu huyo mtoto ambaye alitakiwa kukuzwa kwenye maisha ya upendo wa baba na mama na yeye aje kuwa raia mwema?

Je, umemuwazia huyo mwanamke namna atateseka na mtoto huyo usiku pekee yake mchana pekee yake, hapo inakupa fahari gani kama mwanaume kuona damu yako ipo huko na wewe upo huku usijali inaishi maisha ya namna gani?

Kama kwako ni muhimu kuchuja nafaka, si upige hata nyeto au uzingatie ngono salama ambayo haitaleta mtoto ambaye hautakuwa hiyari kumlea kwa upendo?

Hivi unatakiwa uwe na akili ya namna gani hadi kukimbia mtoto wako mwenyewe ambaye hata ukimtazama unajiona kabisa wewe yule pale katika mwili na damu?

Hebu ifike muda tuanze kuambiana ukweli, hawa watoto tunaweza wapata katika mazingira salama na tukawalea. Kama mwanamke ni mkorofi hushindwi kuchukua mtoto wako ukapeleka kwa bibi yake yaani mama yako au ukatafuta mwanamke akusaidie kulea hata beki tatu wapo kibao ambao utamuacha pale room kwako akae na mtoto na wewe umpatie mshahara na akusaidie kuishi na mtoto wako vizuri tu hadi atakapofika umri wa kuanza kujisimamia.

Trust me, mtoto yupo salama zaidi akikua mazingira ya shida pembeni ya baba yake kulikoni akiishi maisha ya shida pembeni ya mama yake ambapo ni rahisi kuharibika tabia na kuwa tatizo ukubwani.

Siku zote linapokuja swala la kulea mtoto huwa wanaume kuna ile tabia ya kujitisha kuwa mtoto atateseka akilelewa na watu baki, huu ni upotoshaji mkubwa sana. Ipo mifano hai ya wanaume waliolea watoto wao wenyewe bila mama wa mtoto kwa msaada wa mfanyakazi na familia yake hadi mtoto kawa mtu mzima, si watoto wa kiume tu hata wa kike.

Inawezekana na nirahisi sana zaidi ya unavyofikiria. Mimi nimeshalea wajomba wawili kwa msaada wa bibi yao na dada wa kazi baada ya kuona upumbavu wa mama zao unavyowagharimu watoto. Ndio maana nauchukia sana usingle mother sababu naelewa madhara na mateso yake kwa watoto wasio na hatia.

Inaanza na wewe kuwajibika na sio kuwategemea hawa mabinti wa sasa ambao hawawajibiki na maamuzi yao. Kama wewe hautatoa mbegu zako kwa mtu ambaye hautaanza nae familia masingle mother watatokea wapi na watoto watapatikana vipi?

Hebu wanaume tuchague kuwajibika na sio kuwa vilaza ambao kwa makusudi tunachagua kushirikiana na wanawake irresponsible kuleta watoto duniani na kuwatesa bila hatia. Hebu tuanze kuwa na maono ya wapi tunapeleka uzao wetu ili tusipoteze mbegu zetu zikaotea mibani.

Utafurahi siku unakutana na binti yako amekuwa mdangaji, kahaba, ana ma'tattoo amekuwa mtu wa hovyo kama akina Giggy money, au Amber Rutty?

Au unakutana na mtoto wako wa kiume amekuwa kituko, kasuka marasta au kaweka dreads, matattoo mwili mzima, kavaa mlegezo, anakimbiza bodaboda halafu wewe ni mtu na heshima zako unapita, unaweza kumrekebisha tena samaki aliyekauka? Ni kazi rahisi sana kujenga kizazi bora kupitia malezi bora ya watoto kuliko kurekebisha taifa na jamii iliyoharibika kwa gharama na program za kuwarekebisha watu wazima ambao wamekomaa kiakili na wameshapinda.

Acheni kuzaa watoto ambao hamna mpango wa kuwalea na kuwatunza kwa upendo kifamilia mnatutesea watoto wasio na hatia na kuleta laana ambazo hazikuwa na nafasi kwenye jamii yetu. Watoto waliopo kwa sasa iwe ni funzo tubadilike
Mada nzuri changamoto za ujana ndio chanzo hadi unakuja kuzinduka unakuta ushampa mtoto wa watu mimba

Binafsi naona ni vyema kupambana na chanzo na si matokeo kwakuwa nyege siku zote hazina muongozo.

MAADILI ndio nguzo ya yote hayo, watoto wakike walelewe kama dhahabu wafichwe na wafunzwe kuona aibu na kukataa wanapotongozwa barabarani, wavikwe mavazi yenye stara toka wakiwa wadogo hadi wanakua, waamlishwe utiifu kwa wakubwa n.k

Vijana wakiume walelewe katika kujua nini maana ya uwanaume na si kushinda kutongoza visichana na tabia zingine za kihuni wakizani kuwa ndio uwanaume(uwanaume una miiko), wafunzwe heshima na kuwaheshimu wanawake sio kutukana mitusi ya nguoni barabarani kuwatukana wazazi wao wa kike ni upuuzi.

Na yote hayo yanaweza kufanyika kuanzia ngazi ya familia, ukoo, kijiji, mji mpaka taifa kwa ujumla mfano mzuri ni kijiji cha huko Arusha(nimeona fb) wameweka by-law na kukataza wadada kuvaa nusu uchi,mfano mwingine ni nchi za kiarabu zimefanikiwa kutunza maadili kwa kiasi fulani.
 
Nakumbuka miaka ya nyuma binti akiwekwa mimba anafukuzwa nyumbani. Anaambiwa nenda kaishi kwa huyo aliyekupa mimba. Tena wababa ndiyo walikuwa wakali hivyo binti lazima aende kwa mwanaume aliyempatia mimba wataishi pamoja then mwanaume atafanya utaratibu wa kujitambulisha. Kwa sasa mabinti wengi wanalelewa na single mom hivyo hata akipata mimba hakuna wa kumlazimisha aende kwa mwanaume. Mwishoni naye anakuwa single mom. Pia nyumba aliyokuwa na baba ilikuwa inaogopeka hivyo hata vijana wa kiume walikuwa wanaogopa kwamba hapa nikiweka mimba Msala kwangu. Leo hii nyumba hazina mwanaume heshima uoga umepotea. Kizazi kinazidi kuharibika, vijana waliolelewa na single mom wengi wao hawana adabu, mabangi, matusi hovyo hovyo ni shida kwa kweli.
 
Mimi mfano nikigundua huyu demu hajatulia, tabia mbovu,mkorofi,anakauli mbovu, na kadhalika,then siwezi weka mbegu zangu kwenye mji wake wa uzazi maana najua hatafaa kuwa mke so hafai kuwa mama.
Wanawake huwa wanatabia ya kuigiza.
U-single mother hutokea kwa namna nyingi unaweza kumuoa, ukapata mtoto halafu ukagundua mkeo anagongwa na jamaa huko nje.
 
Back
Top Bottom