Prakatatumba abaabaabaa
JF-Expert Member
- Aug 2, 2022
- 1,842
- 6,087
Ah wapi huyo ni tapeli, nikijichanganya hakuna rangi nitaacha kuona. Kanizidi kama mwaka mmojaWe jamaa acha uoga,chukua chuma hicho weka ndani ule mema ya nchi😂
Inasikitisha Sana 😥Tuepuke kuoa mwanamke mwenye X....Tena ukute Ex mwenyewe waliachana sababu jamaa hajajipata au kwa kuwa umetokea mwenzangu na Mimi una vihela vyako umeahidi kuhudumia vizuri....Kuna bro wetu ishawahi mtokea hii,yule dada waliachanaga na ex wake kwa kuwa dada ake alikuwa anampa presha adate na mwanaume mwenye pesa waikomboe familia so kweli demu akampata bro baada ya Dem kujipata vizuri akawa anakodi hotel anaenda kukutana na ex wake😭
Kweli ila bado naipinga hiyo hoja eti utii umebase kwenye uchumi tu. Uchumi ni nyenzo tu ila kutomtii mwanaume kumechimbuka ndani zaidi ya uchumi.Mimi sikusoma mada hivyo nilijibu kulingana na comment ambayo huyo jamaa aliniquote, hayo mambo ya kutumiana yapo kwa jinsia zote mbili wala msiwalaumu wanawake tu, tena wanaume ndio mnaona fahari kabisa kuwatumia wanawake kwa madai kwamba wao ndio wanaoumia ninyi jinsia na maumbile yenu vinawabeba
Unaona sasa, kumbe mawazo yako ndo haya! Umejificha wee kumbe unawaza eti mwanaume awe weak kama mwanamke? That'll never happen, men are becoming weak kutokana na mifumo inayo wabeba wanawake, masculinity inazidi kuwa toxifeid ila kamwe mwanaume kuwa kama mwanamke.Basi ifike pahala muiambie jamii kwamba na ninyi ni weak, na mnaweza kuwa victims kama wanawake tu, hamko strong kama mnavyoiaminisha jamii ili ijulikane moja
Hata biashara msiwafungulieIn short msamiati "msomeshe" utoe haupaswi kumuongezea mkeo elimu je ikitokea siku akakwambia anataka atafute kazi inayoendana na elimu yake utasemaje?maana kinachompa mwanamke jeuri ni kule kuwa na kitu nje ya mfumo wako.
Kama umeshamfungulia biashara hizo elimu unahangaika nazo za kazi gani tena?
mimi wangu baada ya kunisumbua sana,nikamsomesha ujasiria mali,ada sh 10,000/,kwa siku tatu,and the case closed..mke wangu alinambia nimsomeshee eti nimpeleke chuo akasome nlicheka mpka nkapaliwa...
najaribu kufikiria kama nawe una elimu kubwa au kama mzee ana watoto wengine wa kike anataka kutufundisha nini?Na hadi leo Baba aliwaasa kaka zangu na wadogo zangu wa kiume akasema oa mwanamke mwenye elimu ya kawaida wanawake wenye elimu kubwa ndoa kudumu mtihani aisee niliamini
Ni sahihi mkuu yani anayepuuza mambo madogo madogo anaanguka kidogo kidogoNdio shida ya kudharau red flags,,,kaka yako toka awali alishaona hapa kuna mushkeli lkn akakaza fuvu kwamba akisha muoa atakuwa amesolve tatizo na hapo ndipo shida ilipoanzia
Always kuwa makini sana na small details
Refer Christina shushoMwanamke akipata tu kipato au umaarufu cha kwanza anakimbilia kuibomoa ndoa yake
Hii comment inatakiwa kuwa pinned 📌 📌Nitoe tahadhari, hata hao wasio na elimu kubwa the same wana matatizo kama huyu binti msomi, wakipata mwenye pesa kukuzidi hakuna rangi utaacha kuona. Oeni wacha Mungu, hawa wanajua thamani ya ndoa hata kama ni wasomi wakubwa na wana pesa hawaharibu ndoa zao. Ndoa kwao ni sehemu ya ibada na ni maadili mema katika jamii. Kuoa kibishibishi kwa tamaa ya kuoa pisi kali au mbaya bila ku predict tabia zake mficho hatari kwa ndoa huja kuleta majuto baadae na ndoa kusambaratika
Hata akipata,usimsomeshe mwanamkeKakamkubwa alijichanganya sana kusomesha na kuoa kabla hakajapata kazi.
Malipo ni hapa hapa duniani unaweza usione ama ukaona lkn majibu lazima upate baadaeKitu ambacho wanaume wengi hamkijui ni Tabia za mwanamke ambae Anajitafuta au ana hali ngumu kimaisha huwa ni kama simba jike mwenye njaa kali so chochote kitakachotokea mbele yake kama kimenona anapita nacho, Maisha ya Binti alietoka Chuoni hana kazi wala Pesa huwa ni kama Wife Material full adabu na utii
Ndio hawa wanawake wa vyuoni au waliomaliza na ajira hawana, simaanishi kuwa hawana haki ya kupata wenza ila uwe makini sana kuwasoma kabla ya kuwaowa, Hao wakishaolewa huwa wanaendelea kuhaso kutafuta ajira sasa usiombee atume maombi alafu ukute upo nae Dar alafu uskie kapangiwa kituo cha kazi Dodoma huko or Mwanza au apate kazi ya maana ukiwa nae hapo ndio utaanza kujua tabia zake halisi
Mwaka 2017 nilimpotezaga kaka yangu, alikipenda kibinti kikiwa mwaka wa pili chuoni akawa anakihudumia,hadi kinamaliza Chuo akakiowa bwana ila kwenye uchumba tu ugomvi ulikuwa hauishi maana kulikuwa na Tetesi yule binti alikuwa na mpenzi wake wa zamani kwa siri ila kilichompeleka pale kwa Bro ni pesa
Kaka akaowa kibishi, Ndoa iko Mwaka wa kwanza tu, Binti akala shavu Kigoma huko shirika linalodeal na wakimbizi pesa nje nje, Ndoa ndio ilipoanza kuwa ndoano hapo maana ilikuwa ni Marufuku kaka kumfuata yule Binti kigoma hadi arudi yeye Dar hao ni wanandoa yani
Za chini chini wambea wakamtonya Kaka kuwa yuke Binti huwa anamsafirisha yule Mwanaume wake wazamani hadi kigoma anafikia kwake mara kwa mara na anamrudisha Dar tena kwa Ndege, Na ndio maana Binti hakutaka kaka Awe anaenda kigoma
Kaka mwaka 2016 mwishoni akanywa sumu ila aliponyea kufa yote ni kama alipata sonona ,akawa hana mtu wa kumwambia, Baada ya lile tukio ndio akaipa Familia ukweli sasa, familia ikaweka kikao yule Binti akaitwa ila akasema yupo Bize Kigoma huko yote jeuri ya pesa na pumzi
Ikabidi sisi kama familia sasa tuongeze ukaribu uliopitiliza, ili ile hali iondoke tukawa tunakaa kwake kwa zamu yote kumpa kampani maana tulishaona Dalili mbaya na ndio tulikuwa tunamtegemea yani wadogo zake ametusomesha na kutupigania sana, Wifi tukawa tukimpigia simu hata kupokea hapokei
Mwaka 2017 mwezi wa Sita akaanza kuugua vitu visivyoeleweka mara Presha mara anadondoka kazini, Alipopelekwa Hospitali kwa uchunguzi ikaonekana Mishipa yake ya moyo imeanza kutanuka tukaambiwa anatakiwa arelax na aache kuwa mtu wa Mawazo , ila kila tukijaribu ikawa mtihani, 2017 mwishoni akafariki alidondoka tu bafuni kumkimbiza Hospitali tayari akawa ameshaondoka hili pigo siwezi kulisahau
Baada ya hili tukio kutokea Baba nae hadi leo hajawahi kuwa sawa kabisa, ila aliwaita watoto wake wote wa kiume kitu nachokumbuka alisema oweni wanawake wenye elimu za kawaida msije kusumbuana huko mbele, na akasema tumewasomesha kwa garama kubwa na sasa mna kazi zenu yeyote atakaeleta tena Mwanamke hapa kama ana Elimu ya juu basi huyo Mwanamke naye ni Sharti awe na pesa na kazi kabla hamjafahamiana yaani kiwaunganishe upendo sio Pesa mlizokuwa nazo
Akasema kuwa ukiniletea hapa Mwanamke Mwenye elimu ya juu na hana kazi wala pesa basi mkatafute baba mwjngine ampokee huyo mwanamke kama mnae la sivyo aishie huko huko, yaani Baba ni kama alivurugwa na ile hali
Ila wansemaga Dam ya mtu ni kama nzito or inaweza kukulilia ila sijui kama ni kweli but yule Binti mwaka 2022 Tabora huko, alipataga ajali mbaya sana Gari aliyokuwa anaendesha ikagongana na lori miguu yote ikabanwa mean ikasagika akakatwa miguu yote kwa sasa ni mlemavu kabisa hana miguu.
Huyu mwanamama anastruggle sana kuangusha kingdom ya kiume.Unaona sasa, kumbe mawazo yako ndo haya! Umejificha wee kumbe unawaza eti mwanaume awe weak kama mwanamke? That'll never happen, men are becoming weak kutokana na mifumo inayo wabeba wanawake, masculinity inazidi kuwa toxifeid ila kamwe mwanaume kuwa kama mwanamke.
Upo sahihi sana, ila usahihi wako utaendelea kuongeza single mothers wengi mitaaniSiyo ubinafsi bali ni kwa sababu jamii ilishaaminishwa kwamba mwanaume ni kiumbe strong hawezi kuzidiwa akili wala nguvu na mwanamke ambaye yeye ni kiumbe dhaifu, jamii ilishaaminishwa kwamba katika mgogoro wowote ule baina ya mwanaume na mwanamke siku zote mwanamke ndiye anayepoteza mwanaume yeye hana cha kupoteza hivyo mwanamke hatakiwi kushindana na mwanaume maana yeye ndiye atakuwa victim, sasa kutokana na hiyo imani iliyojengeka inakuwa ngumu kuamini kwamba eti wanaume nao wanadhuriwa na wanawake ndio maana wanaume wanapolalamika jamii inawapuuza kwa kudhani kwamba hayo malalamiko ni batili na hayana uhalisia
Hawezi, ni kama anaota ndoto za mchana!Huyu mwanamama anastruggle sana kuangusha kingdom ya kiume.
Akifanikiwa atapandisha jinsia ya kike pale juu
Tunazungumzia kutendeana haki, sasa mwanamke akinivizia nimelalala akaniwahi kunidhuru hata kama nina miguvu nitamzuiaje? Utasema mimi ni weak?Basi ifike pahala muiambie jamii kwamba na ninyi ni weak, na mnaweza kuwa victims kama wanawake tu, hamko strong kama mnavyoiaminisha jamii ili ijulikane moja
Hili nafikiri nimeshakujibu kule siwezi kuandika jambo lile lile kila maraKweli ila bado naipinga hiyo hoja eti utii umebase kwenye uchumi tu. Uchumi ni nyenzo tu ila kutomtii mwanaume kumechimbuka ndani zaidi ya uchumi.
Aiseee mnasikitisha sana sasa hiyo mifumo inayowabeba wanawake inaendeshwa na kina nani na kwa faida ya nani, na kwanini wanaume wanaruhusu wanawake wabebwe ilihali wao ndio watawala na wana uwezo na nguvu kuliko wanawake, huwa nashindwa kuelewa inakuwaje mnalalamikia matatizo ambayo mmeyaruhusu wenyewe (maana wanawake ni dhaifu) sasa mnamlalamikia nani ayarekebishe mbona mnafurahishaUnaona sasa, kumbe mawazo yako ndo haya! Umejificha wee kumbe unawaza eti mwanaume awe weak kama mwanamke? That'll never happen, men are becoming weak kutokana na mifumo inayo wabeba wanawake, masculinity inazidi kuwa toxifeid ila kamwe mwanaume kuwa kama mwanamke.
Na unadhani ni kwanini mwanamke akudhuru kwa kukuvizia yani mnachoshindwa kuelewa (au pengine mnaelewa ila hamtaki kukubali) ni kwamba haya wanayofanya wanawake sasa hivi waliyapandikiza wanaume wa zamani waliokuwa na mfumo dume wa kipuuzi, haya ni matokeo ya kuwakandamiza na kuwanyima sauti na uhuru wanawake kwa muda mrefu na matokeo yake walipoanza kutetewa na kupata upenyo wakatake advantage ya hilo, tatizo lenu ninyi hili jambo mnaliangalia juu juu tu hamtaki kujua mzizi wake mnadhani eti linaanzia hapa au liliibuka tu out of nowhere na mkiambiwa ukweli mnakimbilia kuita watu mafeministTunazungumzia kutendeana haki, sasa mwanamke akinivizia nimelalala akaniwahi kunidhuru hata kama nina miguvu nitamzuiaje? Utasema mimi ni weak?