cutelove
JF-Expert Member
- Oct 3, 2017
- 3,448
- 7,972
Kuna wanaume anapokuwa anakuaproach utadhani anayoyasema ni ya kweli
Juzi moja nikakutana na mkaka , kama kawaida akaanza swaga nikamwambia nipe muda kidogo nichanganue maneno yako
Leo nikawa nimetoka kwenda mahali mbali kidogo kwa rafiki yangu,akawa amenipigia sim tuonane nikamwambia nipo mbali kidogo ila muda si mrefu nitakuja mjini
Akaniambia nina usafiri vipi nikufuate..nikamwambia utakuwa umenisaidia sana
Basi baada ya dakika kadhaa akaja akanichukua ,wakati anadrive akaanza hili gari langu siku hizi linatumia mafuta vibaya,..nikadakia ooh kumbe gari hili ni lako"akaniambia yes ni gari langu nilinunua hata miezi mitatu haijapita,,nikamwambia hongera!
Mara akapigiwa sim nikahisi akaulizwa uko wapi akajibu maeneo tulipo,sijui hawakuelewana na aliyempigia akakata sim
Baada ya dakika kadhaa si gari likasimamishwa na mzee mwenye kitambi,acha tuvurushwe kutoka kwenye gari huku mzee anagomba kuwa nani kakwambia uchukue gari langu
Basi kijana akakosa la kuniambia akawa ameinamia kichwa chini,..ikabidi nipande daladala nikamuacha mwenyewe amesimama njiani maana alikoswa la kuniambia
Wanaume kupenda sio lazima ujitape vitu ulivyonavyo,utapendwa tu hata kama huna gari au baiskeli
Juzi moja nikakutana na mkaka , kama kawaida akaanza swaga nikamwambia nipe muda kidogo nichanganue maneno yako
Leo nikawa nimetoka kwenda mahali mbali kidogo kwa rafiki yangu,akawa amenipigia sim tuonane nikamwambia nipo mbali kidogo ila muda si mrefu nitakuja mjini
Akaniambia nina usafiri vipi nikufuate..nikamwambia utakuwa umenisaidia sana
Basi baada ya dakika kadhaa akaja akanichukua ,wakati anadrive akaanza hili gari langu siku hizi linatumia mafuta vibaya,..nikadakia ooh kumbe gari hili ni lako"akaniambia yes ni gari langu nilinunua hata miezi mitatu haijapita,,nikamwambia hongera!
Mara akapigiwa sim nikahisi akaulizwa uko wapi akajibu maeneo tulipo,sijui hawakuelewana na aliyempigia akakata sim
Baada ya dakika kadhaa si gari likasimamishwa na mzee mwenye kitambi,acha tuvurushwe kutoka kwenye gari huku mzee anagomba kuwa nani kakwambia uchukue gari langu
Basi kijana akakosa la kuniambia akawa ameinamia kichwa chini,..ikabidi nipande daladala nikamuacha mwenyewe amesimama njiani maana alikoswa la kuniambia
Wanaume kupenda sio lazima ujitape vitu ulivyonavyo,utapendwa tu hata kama huna gari au baiskeli