Wanaume wa JamiiForums nawajibu kwa nini tunawafungia PM na wengine hatuwajibu

Wanaume wa JamiiForums nawajibu kwa nini tunawafungia PM na wengine hatuwajibu

Ninachoomba tujifunze kama binadamu kufilter nini cha kuongea na wapi. Kwa mfano mmetoka na mtu humu iwe dinner au club au wapi yanayotendeka yaishie humo. Sio jambo baya hata kujuana na member wote humu ila ukionana nao yaishie huko mlichoongea mlichofanya au chochote kile. Kubeba kitu ukakirudisha kwa mtu ambae mlimuongelea sio fresh ni kaunafki fulani.

Kuna watu wanaandika vizuri sana kwenye majukwaa ila hawana siri kwa wanaokutana nao nje ya jukwaa. Hata kama mmekutana kituoni atamtafuta member mwingine huku amwambie jana nilikua na mzigua kituoni morocco ikawa hiki ikawa kile. Hiyo sio poa maana hao wanaoambiwa nao wanarudisha tena. Watu wazima sisi tutendee haki miaka yetu kwa vitendo kwenye majukwaa pm na mtaani ikitokea. Mnatuaminisha na miandiko ya adabu mtu unajua amepata rafiki kumbe mtu mmbea bwana
As long as tunaishi haya mambo hayatoisha, hatuwezi kufanana dunia nzima. Tujifunze tu kuishi kulingana na mazingira. Haya mambo yako tangu enzi na enzi, japo kukumbushana sio mbaya.
 
Back
Top Bottom