Wanaume wa JF mnajishushia CV zenu kwa wadada. Kuweni real, acheni fake life

Wanaume wa JF mnajishushia CV zenu kwa wadada. Kuweni real, acheni fake life

Hahahahah
Ushamjua eeee.
Yaani anapiga picha ofisini afu anakutumia.
Hahahaha, milioni na laki 9 masikhara

Acha tu.
Humu wanaume wote nawaona sawa tu.
I'd fake na hata maisha yao fake tu.
Huyo jamaa yupo humu nimemuona kule mwanzoni

Mwisho nimeweka NUKTA 😂😂😂 Shikamoo Madame. 😂😂😂
 
Ila Watanzania waliowengi ndiyo hao.

Ila mbona hawahawa watoto wa wakulima ndiyo wanawatongoza mitaani na mnawakubali dada zetu....


sisi wakulima wa JF tumewakosea nini?

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hahaaaaa usikute ni tapeli huyo. Mie Kuna wachuga Ana swagga hizo hizo. Eeeh
Duuh naona mnatusema wa chuga aseeh.

Mbona hatuna hizo pan'gan'ga.

Honestly speaking.

JF tunawashamba wengi saana kwa wanawake na wanaume pia (huenda nami nipo).

Na kuna watu humu naamini tukiamua kuwa real kukemea kila ushamba wa humu tutachukiwa saana ilihaki tunajipumzisha huku kijiweni.
 
Sisi wanawake wa humu Jf, tunajua fika kwamba wanaume wa humu....
Wote wana pesa,
Wote wana magari,
Wote wana elimu kuanzia degree,
Wote wamejenga,
Wote wanajua kuvaa,
Wote wazuri....
Ila sasa mie nashindwa kuelewa, kwanini ukikutana na baadhi yao wengi hawako kama wanavyojishaua humu Jf?

1. Anasema ana pesa, ila ukikutana nae ni unga unga mwana mpaka utashangaa ila akiwa jukwani sasa Mengi atasubiri.
Mjue mnajishushia CV

2. Mada za kuchangia zinazohusu magari, naye yumo tena atataja mpaka aina ya gari analomiliki, ila nje ya keyboard ukikutana nae atakutembeza na bodaboda mpaka makalio yaote sugu...alivyo ni tofauti na mmiliki wa hata baiskeli ya guta.
Mjue mnajishushia CV.

3. Kwenye jukwaa la elimu kila mada inayohusu wenye elimu za juu utamkuta akichangia huku akijitapa yeye ni msomi wa degree au masters ila nje ya keyboard sasa, anamiliki certificate of uzushi na uwongo from Kamgambile college.
Mjue mnajishushia CV.

4. Kuna mdau humu nilikuwa napenda sana post zake kuhusu assets anazomiliki yakiwemo makampuni 2 na nyumba 1 pamoja na kijiusafiri.
Siku nakutana nae sikuamini kama ndio yeye, jamaa anaishi chumba ambacho mie kwetu naweza kufugia sungura wawili tu.
Yule jamaa mpaka leo kani-ignore sijui nilimkosea wapi.
Mjue mnajishushia CV.

5. Kuna mmoja nilienda kukutana nae La Chaaz Sinza.
Jamaa nilikutana nae jukwaa la Mitindo na utanashati akijitanaibu kuwa yeye ndie mwanaume smart Jf nzima.
Siku naonana nae sikuamini macho yangu.
Kwanza juu kapiga singlend ya kukata mikono, ana kigimbi sio cha nchi hii.
Nywele za kwapa zimekuwa za brown, jasho sasa kama tuko ndani ya mgodi.
Chini kavaa kipensi cha jeans kimekaa kama kipedo, mguuni ana zile ndala nyeupe zinazouzwa Kariakoo.
Nilivyofika pale nikafungua jukwaa la mitindo nikawa nasoma comment zake huku namuangalia kiupande ili ni-compare nae.
Wanaume acheni kujikweza.
Mjue mnajishushia CV.

6. Kwenye uzuri ndo sisemi.
Aliyekwambia kuvaa miwani ndio uzuri nani?
Sema sura yako ilivyo ili nijue nadili na mtu wa aina gani nilikutana nawe.
Mtu anajisifu handsome wakati anasura ya kumtishia mtoto wakati wa kula na wakati wa kulala.
Mjue mnajishushia CV.

Mbona huku Jf kuna wanaume wako real tu jamani!!!
Humu Jf kuna wanaume ambao akisemacho humu ndicho hikohuko utakutana nacho ukionana nae.
Mie nilijua waongo ni sisi tu, kumbe hata wanaume hamvumi ila mpo.

Utakuta mwanaume anahangaika kujikwenza kwa mwanamke kwa kujisifia jukwaani, ila ukienda nae Pm, utapasuka kwa kicheko.
Sisi wanawake tunafanya hivi kwa ajili ya kuwanasa wanaume, hasa kwa mwanaume unafanya ili iweje?

Wanaume punguzeni mbwembwe.
Msuli haufungwi kwa mkanda.
Kuweni real bhana samtaim bahati mnazipeperusha wenyewe.
Unahangaika nami Pm mwezi mzima, siku ya kuja kuonana nawe najikuta najutia bando langu wakati nachat nawe kipindi chote hiko.

Kuweni serious bhana wanaume wa humu.
Mbona kuna wengine tunapenda wanaume wasio na mvuto?
Tunawapenda wasio na magari wala nyumba wala makampuni wala wenye hizo six pack?

Mtajificha nyuma ya keyboard mpaka lini?
Ndo yaleyale, mnakutana kwenye meetings badala ya kujadili kilichowaleta, mnaanza kumjadili Juma na post zake za kujisifia wakati yuko hapo mbele yenu na hamuamini kama ndo yeye.

Nawaambia wanaume wa JF, MNAJISHUSHIA CV.
Wanaume real wapo...asa nyie endeleeni kufake huku Jukwaani afu tukiyaleta maisha yenu halisi jukwaani muanze kusema wanawake mwalimu wetu kipofu.

Povu ruksa.
Madongo rusha kwa akili maana tutaleta screenshot afu tuanze kutafuta mchawi hapa.
Inaonekana umegongwa na Wana JF wa sampuli tofauti tofauti

Wenye kampuni, magari, nyumba, chumba kimoja n.k

Hongera sana
 
Haha...kwa sisi MMU na chitchat sio wwnaume mzee baba/mama?

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Jamaa umenichekesha sana inawezekana mkawa mna jinsia mbili
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Jamaa umenichekesha sana inawezekana mkawa mna jinsia mbili
Hawa watu matusi yao hayavumiliki.

Amefanya nijichungulie tena.

Au wanaume wa jukwaa la siasa kina britanicca wanazo mbili mbili?
 
Back
Top Bottom