Wanaume wa JF mnajishushia CV zenu kwa wadada. Kuweni real, acheni fake life

Wanaume wa JF mnajishushia CV zenu kwa wadada. Kuweni real, acheni fake life

am real as my name......machalii wa chuga hatuna mboyoyo mob
 
Sisi wanawake wa humu Jf, tunajua fika kwamba wanaume wa humu....
Wote wana pesa,
Wote wana magari,
Wote wana elimu kuanzia degree,
Wote wamejenga,
Wote wanajua kuvaa,
Wote wazuri....
Ila sasa mie nashindwa kuelewa, kwanini ukikutana na baadhi yao wengi hawako kama wanavyojishaua humu Jf?

1. Anasema ana pesa, ila ukikutana nae ni unga unga mwana mpaka utashangaa ila akiwa jukwani sasa Mengi atasubiri.
Mjue mnajishushia CV

2. Mada za kuchangia zinazohusu magari, naye yumo tena atataja mpaka aina ya gari analomiliki, ila nje ya keyboard ukikutana nae atakutembeza na bodaboda mpaka makalio yaote sugu...alivyo ni tofauti na mmiliki wa hata baiskeli ya guta.
Mjue mnajishushia CV.

3. Kwenye jukwaa la elimu kila mada inayohusu wenye elimu za juu utamkuta akichangia huku akijitapa yeye ni msomi wa degree au masters ila nje ya keyboard sasa, anamiliki certificate of uzushi na uwongo from Kamgambile college.
Mjue mnajishushia CV.

4. Kuna mdau humu nilikuwa napenda sana post zake kuhusu assets anazomiliki yakiwemo makampuni 2 na nyumba 1 pamoja na kijiusafiri.
Siku nakutana nae sikuamini kama ndio yeye, jamaa anaishi chumba ambacho mie kwetu naweza kufugia sungura wawili tu.
Yule jamaa mpaka leo kani-ignore sijui nilimkosea wapi.
Mjue mnajishushia CV.

5. Kuna mmoja nilienda kukutana nae La Chaaz Sinza.
Jamaa nilikutana nae jukwaa la Mitindo na utanashati akijitanaibu kuwa yeye ndie mwanaume smart Jf nzima.
Siku naonana nae sikuamini macho yangu.
Kwanza juu kapiga singlend ya kukata mikono, ana kigimbi sio cha nchi hii.
Nywele za kwapa zimekuwa za brown, jasho sasa kama tuko ndani ya mgodi.
Chini kavaa kipensi cha jeans kimekaa kama kipedo, mguuni ana zile ndala nyeupe zinazouzwa Kariakoo.
Nilivyofika pale nikafungua jukwaa la mitindo nikawa nasoma comment zake huku namuangalia kiupande ili ni-compare nae.
Wanaume acheni kujikweza.
Mjue mnajishushia CV.

6. Kwenye uzuri ndo sisemi.
Aliyekwambia kuvaa miwani ndio uzuri nani?
Sema sura yako ilivyo ili nijue nadili na mtu wa aina gani nilikutana nawe.
Mtu anajisifu handsome wakati anasura ya kumtishia mtoto wakati wa kula na wakati wa kulala.
Mjue mnajishushia CV.

Mbona huku Jf kuna wanaume wako real tu jamani!!!
Humu Jf kuna wanaume ambao akisemacho humu ndicho hikohuko utakutana nacho ukionana nae.
Mie nilijua waongo ni sisi tu, kumbe hata wanaume hamvumi ila mpo.

Utakuta mwanaume anahangaika kujikwenza kwa mwanamke kwa kujisifia jukwaani, ila ukienda nae Pm, utapasuka kwa kicheko.
Sisi wanawake tunafanya hivi kwa ajili ya kuwanasa wanaume, hasa kwa mwanaume unafanya ili iweje?

Wanaume punguzeni mbwembwe.
Msuli haufungwi kwa mkanda.
Kuweni real bhana samtaim bahati mnazipeperusha wenyewe.
Unahangaika nami Pm mwezi mzima, siku ya kuja kuonana nawe najikuta najutia bando langu wakati nachat nawe kipindi chote hiko.

Kuweni serious bhana wanaume wa humu.
Mbona kuna wengine tunapenda wanaume wasio na mvuto?
Tunawapenda wasio na magari wala nyumba wala makampuni wala wenye hizo six pack?

Mtajificha nyuma ya keyboard mpaka lini?
Ndo yaleyale, mnakutana kwenye meetings badala ya kujadili kilichowaleta, mnaanza kumjadili Juma na post zake za kujisifia wakati yuko hapo mbele yenu na hamuamini kama ndo yeye.

Nawaambia wanaume wa JF, MNAJISHUSHIA CV.
Wanaume real wapo...asa nyie endeleeni kufake huku Jukwaani afu tukiyaleta maisha yenu halisi jukwaani muanze kusema wanawake mwalimu wetu kipofu.

Povu ruksa.
Madongo rusha kwa akili maana tutaleta screenshot afu tuanze kutafuta mchawi hapa.
Story yako haija balance tunasubiri upande wa pili wa story

Ila na wew umetisha First date unaenda La chazz....
 
Mie sina hata hamu na wanaume wa humu.
Nimekutana na mkaka akasema anamiliki kampuni...hahahhah
Chinekeeee.

Bora hata mie ninayemiliki makalio.
Yule kaka sijui kaniblock, simuoni kabisa jukwaani.
Hahaa mxiiieeww daahh
 
Hahaa
Utajua mwenyewe bwana.. Sisi ambao tuna comment hatunaga lolote mnazipitaga comment zetu kwa kuchechemea msiziguse..
Oya masela wadananda endeleeni ivo ivo
 
4. Kuna mdau humu nilikuwa napenda sana post zake kuhusu assets anazomiliki yakiwemo makampuni 2 na nyumba 1 pamoja na kijiusafiri.
Siku nakutana nae sikuamini kama ndio yeye, jamaa anaishi chumba ambacho mie kwetu naweza kufugia sungura wawili tu.
Yule jamaa mpaka leo kani-ignore sijui nilimkosea wapi.
Mjue mnajishushia CV.
.
Namba 4 imekuanika. kwa waelewa wameshajua wewe ni mtu wa aina gani.
 
Nilikuwa sijawahi kuona huu uzi. Aisee!!! Mie na mpenzi wangu Tee wife material tumependana ivyo ivyo, masuala ya kudanga hana. Na jinsi alivyo avatar yake ni same

Lakini nyie wadangaji mnataka mambo makubwa wakati hatuna kitu, Mtaishia patupu! Mimi sina kitu lakini nimekuelewa, nikija kama nilivyo nitaambulia matusi na kejeri au short reply(kama unalazimishwa) nani anaetaka hayo mambo?

Lazima nijipambanue' ni mwendo wa copy na pest wa maisha ya mshikaj wangu pembeni na wewe utaona umefika. Suala la kukutana Ni jingine maana naweza jipanga nika fake vile vile. Mwisho wasiku nimeweka bajeti laki moja mpaka nakudinya kisha nakupga chini na maisha yanaendelea.

Fake lazima. Bila hivyo hupati mtu hapa jf.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom