Dr Matola PhD
JF-Expert Member
- Oct 18, 2010
- 60,050
- 104,466
Kumbe umesharuka? Najuwa mambo mazuri zaidi yanakuja.Wow!!βΊοΈ Kama intention haijabadilika miaka yote hii basi una hoja, unapaswa usikilizwe.π€π€
Ila ngoja kwanza nirudi kwa mabebere ndio tuongee!ππ
Mambo mrembo ,mimi ni mmasai wa rohoni . asante kwa sifalizzy,
usiniambie uko vijijini ndio shughuli yao kuhudumiwa tuu dah!
basi wakija dar wanacope enh kidogo, me love them bana, wana weusi mzuri, wamepanda, those waliokwenda shule wako na brain then wanajituma haooo dah!
Bibi zenu hawakulalamika hayo nyie ndio mlalamikelizzy,
mijanaume ....oopphs sorry
wanaume wa kiafrica wengi ndivyo walivyo...
kazi yao kusugua miguu mwaname ndo atafute...
alime, apike, alee
yaani taabu tupu....
usishangae kwa makabila ya walimaji, mume na mke wakitoka shamba(kama mume siku hiyo kaenda kulima) mke atabeba jembe, mtoto, na atapita kuchuma mboga na kuokota kuni, mume atarudi nyumbani asubiri mke apike ale aende kilabuni.... jioni mke na watoto wende shamba............................
Nilitaka sana kumjibu huyu dada,mama, Binti whatever might that be, embu tuelezee tomaduni na Mila za kabila lako na mpaka sasa zimekusaidia nn ww kama mwafrika na je inaziishi? What I'm seeing here you are dissing and disrespecting people's tribes! Unazungumza as if unajua na kuelewa tomaduni za watu kwa kuzungumza uwongo, usitafute sifa kwa namna hii find other ways na kama huna uwakika na jambo uliza. Wewe si Maasai na hujui lolote licha ya yale ulio yaona,kuambiwa au kusoma mitandaoni na darasani juu ya Makabila mengine.Lizzy, siwezi kukuambia ubaya wa generalisation and judgement, b'cause nimesha kuona mara nyingi ukiwauliza watu kwa nini wanafanya hivo (hasa pale wanapojiuliza kuhusu mila ya kichaga).
Kila kabila na mila yake. Na wamaasai walijenga mila yao kufatana na maisha na mazingira walo kua nayo huko nyuma. Maisha yenyewe yalikua ni ya ufugaji na mazingira yalikua ni mazingira ya savanah.
Katika mazingira hayo hatari zilikua nyingi mno, toka kwa vinyama vya porini au toka kwa clans zingine za kimaasai. kwa hivo walihitaji kugawa kazi za ndani kwa mtindo huu: mwanamke afanye shughuli zote atakazo weza ili mwanaume aweze ku-concentrate katika kuilinda familia yake tokana na dangers hizo. Pia wanaume walikua wanawinda vinyama na kuongeza variety katika chakula cha nyumbani.
Sasa kutokana na 'promotion' ya sekta ya utalii, serikali imegeuza eneo lao asili kua eneo la utalii na wenyewe wamelazimika kubadili mfumo wa maisha from what I have just described hapo juu kugeuka walinzi (that is what they were raised to do). Expropriation hii ilifanyik bila compensation, bila reinsertion na bila msaada wowote wa training, finance au aina yoyote ile kuhakikisha wana-adapt in their new environment. Unaweza kusema kua muda umefika kwa wamaasai ku-revise taratibu zao, na nakubaliana na wewe but it takes time and lots of eeffort toka kwao na toka kwa serikali pia to change it.
I know of one maasai man, na anafanya kazi nzuri tu. But haikutokea by coincidence. Alisaidiwa kwa namna moja au nyingine. Babu yake alisomeshwa na serikali, akawa mwalimu na baba yake alisomeshwa na serikali pia akaingia jeshini na kuendelea hadi ngazi za juu. hiyo 'exposure' ilichangia katika uamuzi wa baba yao kuwapeleka watoto wake wote shule na leo wote wana masomo, wana kazi na wanaendesha maisha kama westerns walivo taka tuendeshe maisha.
Hata hivo turudi kwa hao maasai ambao unazungumzia, yani wale walio porwa eneo zao na kutelekezwa mahala ambapo walishindwa kabisa kuendelea kuhishi kama mila yao ilivo wafunza: are you sure they are useles to their household? labda nikuulize suali moja tu, then tutaendelea from there: Nini kazi ya simba dume?
ChaiDah. . . kumbe waMassai nao wanajua kuFLIRT ehhhh?Hehehe. . nilidhani hayo ni mambo ya watu wa mujini tu.
Nwy siku zote tunasikia na kuambizana kwamba mwanaume ni yule anaeweza kujali,lisha na kulinda familia yake (provide for them). Miongoni mwa watu wanaoonekana wanaume kwenye jamii yetu ni waMassai kwa uhodari wa kuwinda na hata kuua simba kwa mikono, tena wakiwa na mikuki/sime zao ndo kabisa wanaonekana wa ukweliii.
Pamoja na kwamba nimewahi kuishi nao miaka ya nyuma, sikuwahi kujua baadhi ya mila zao juu ya maisha ya kila siku na namna yanavyoendeshwa ila sasa nimejua na ndio nikapata maswali kadhaa juu ya wanaume hao.
Kwanza kabisa hawajengi. Anaejenga ni mwanamke (mke/wake zake), na ole wao mvua inyeshe alafu bwana anyeshewe. . . lazima mama aambulie kibano na aeleze kwanini 'bwana inyeshewe'( in a Massai accent).
Pili chakula anatafuta mama.
Kutwa nikiangalia naona wanawake ndio wanaopita na punda + madumu kwenda kutafuta maji na kuni wanakokujua wao.
Wanaume utawaona wanapita fimbo zao + mbuzi na ng'ombe kupeleka machungani tu BASI. Wakija dukani wanaume wengi ni wanaulizia kiroba na beer. . . wachache sana watataka chumvi, sukari, mafuta, mchele au hata pipi za watoto kuashiria anakumbuka na kujali familia.
Mashine (kusaga na kukoboa) wanaokuja ni wanawake. . .
Kukamua wao. . .
Kupika wao. . .
Malezi wao. . .
Yani wanaume wao ni machungani kwenda kupiga soga huko wakati wamama wanapanda na kushuka na barabara. Kwa ufupi. . .wanalelewa na kutunzwa na wake zao.
Je nao ni wanaume? Au ndo sawa na wale wanaoitwa 'MARIO' mjini? Au yeye sio muAfrika hivyo ule utamaduni wa 'mwanaume wa kiAfrika ni provider' hauwahusu?