Wanaume wengi hupenda kuwa kwenye mahusiano na kuoa mwanamke wa aina hii...

Wanaume wengi hupenda kuwa kwenye mahusiano na kuoa mwanamke wa aina hii...

Chinekeee!!😛layball:


Aaaaaaaaaah wapi! Siku hizi kuziada akili tu na timing! Wanawake wenye sifa hizo sio wazuri physically! Na wanaume siku hizi vigezo na masharti kuzingatiwa, hataki mke wa kumuacha nyumbani au kuona aibu kumtambulisha! Binti akiwa mzuri hata kama kiluzi wanabeba tuuuu! Hata shule hamna wanabeba tuuuu! As long as asitake vigezo vikali kama vya Lara Moko!

Ila ukiwa sura ya kazi utapata hadi PHD bilabila! Utakuwa na sifa hizo hadi kuhonga juuu ila bila bila tu! Wanaume akili zao ziko katikati ya miguu! She who controls the thingy btn the legs controls the man!
 
joyness
Kwanza nakupongeza kwa makala nzuri
::
Pili,,wanawake wengi wanayajua vema uliyosema,tena vizuri kabisa ukiwemo wewe! Ni jambo jema
::
Tatu,,nina maswali kwako,,ni kwa nini mnatupa pembeni sifa hizi na kuvaa uhusika tofauti? Je,ni kwa nini wanawake wengi wanawakwepa wanaume wenye pato duni na kuhadaika na pato hewa,wanapokuja kugundua ukweli wanajilaumu kwa kutosikiliza nafsi zao? Na mwisho,,unakubaliana nami kuwa wanaume wengi wanapoteza imani kwa wanawake kila uchao kwa maana ya kuhoji pato kwanza?
=
nashukuru!tatizo ni tamaa unakuta mwingine anaona wenziye wana vitu vizuri na yeye anataka awe navyo kwa haraka.
pia kutokukubaliana na hali duni tulizonazo.
 
nashukuru!tatizo ni tamaa unakuta mwingine anaona wenziye wana vitu vizuri na yeye anataka awe navyo kwa haraka.
pia kutokukubaliana na hali duni tulizonazo.

Excellent!! joyness
 
Last edited by a moderator:
you made my night sweetie joyness

Habari wana jamvi wenzangu. Leo nitazungumazia juu ya aina ya wanawake ambao wanaume wengi hupendelea kuoa.


Wanaume wengi wanapofikia hatua ya kuoa si kwamba wanakurupuka tu na kuoa mwanamke yeyote mwenye sura nzuri, bali huchukua muda wao mwingi kuchunguza mambo mengi juu ya wake ambao wanadhani kwamba wanaweza kuwa pamoja kwa kipindi chote cha maisha.

Wanawake wengi wanajisahau na kudhani kwamba kitu kinachoweza kuwafanya wakapata wachumba ni uzuri hivyo kupoteza muda wao kujichubua na kujiremba ili wawavutie wanaume bila kujua kwamba kuolewa ni zaidi ya uzuri.

Hali sasa hivi imebadilika ni tofauti na kipindi cha nyuma ambapo ukiwa na sura nzuri na umbo la kuvutia basi una asilimia 100 za kuolewa.


Utafiti ambao nimeufanya unaonesha kwamba zaidi ya uzuri wa tabia na umbo, kuna kuna sifa nyingine za msingi ambazo mwanamke anatakiwa kuwa nazo ili aweze kuwa katika mazingira mazuri ya kupata mchumba wa kumuoa kiasi kwamba asipokuwa nazo ataishia kuchezewa tu lakini haitatokea mtu kumtakiwa kwamba anataka kumuoa.
1. MWEYE MAPENZI YA KWELI
Lengo kubwa la mwanaume kuoa ni kutaka kupata mapenzi ya kweli kutoka kwa mwanamke na ikiwezekana waweze kupata watotoa ambapo watoto mara ndio wamekuwa furaha ya ndoa. Wapo wanawake wengine ambao wanonesha wazi kutokuwa na mapenzi ya kweli bali wanakuwa na mapenzi ya kuzuga. Wanachotaka wao aidha kupata umaarufu tu kwamba yuko na mtu fulani ama kuweza kupata pesa alizonazo mwanaume lakini sio kwamba ana mapenzi ya dhati kutoka moyoni mwake.


Mwanamke asiye na mapenzi ya dhati utamgundua tu, muda mwingi utamuona macho yake yako kwenye mfuko wa mwanaume. Akiona kwamba mfuko umetuna utaona anaonesha mapenzi ya hali ya juu lakini pindi hali inapokuwa kubwa mbaya kifedha mapenzi yanaanza kufifia.

Kwanini wanaume wanapenda wana wake wenye mapenzi ya dhati kutoka mioyoni mwao na si kutokana na fedha walizonazo? Hii inatokana na ukweli kwamba maisha siku zote yanabadilika, kama waswahili wanavyosema, kuna kupanda na kushuka.

Sio kwamba kila siku utakuwa na maisha mazuri na kama itatokea hivyo basi ushukuru mungu.Hivyo basi mwanamke wa kuoa lazima afahamu hivyo na awe tayari kuonesha mapenzi yake ya dhati wakati wote wa maisha yao na si kwa kipindi fulani tu cha neema.

Si hivyo tu pia asilimia kubwa ya maisha ya ndoa yanatawaliwa na mapenzi, kwa hiyo nyanja hiyo inakuwa ya msingi sana kwa wanaume wengi kuiangalia ili wasije wakajikuta wanaoa mwanamke ambaye baada ya muda mapenzi yanakwenda likizo hali ambayo inaweza kuwafanya wasiishi maisha ya raha mustarehe.
2. WENYE TABIA NZURI
Tabia njema ndio silaha ya maisha, ukiwa na tabia nzuri kila mtu atakupenda, hiyo ni katika maisha ya kawaida. Lakini linapokuja suala na kuoa tabia inakuwa kitu cha awali sana kungaliwa na hiyo inaweza kuwa na ukweli kwa sababu wapo wasichana wazuri wenye mvuto wa aina yake na maumbile mazuri, lakini wanakosa wanaume wa kuwaoa, ukiuliza kwani utaambiwa anatabia mbaya.


Naweza kusema hilo ndilo limekuwa tatizo kubwa kwa baadhi ya wanawake kukosa wanaume wa kuwaona. Hakuna mwanaume hata mmoja kati ya wale ambao nimejaribu kuongea naye ambaye ameonesha kulidharau suala hilo la tabia.

Si hivyo tu wapo wanaume ambao wameingia kichwa kichwa na kuoa kwa kuangalia sura tu bila kujali tabia, matokeo yake baada ya siku chache yanatokea machafuko ya aina yake hali ambayo imepelekea kuvunjika kwa ndoa kutokana na tabia mbaya alizonazo mwanamke.
3. WENYE UCHU NA MAENDELEO
Hivi karibuni kumekuwepo na mabadiliko ya aina yake kwa wanaume, wengi sasa hivi hawapendi kabisa kuoa mwanamke ambaye hana kazi yaani 'golikipa'. Kama atakuwa hana kazi basi awe na uchu wa maendeleo kwa kujituma kufanya kazi mbalimbali za kimaendeleo kama vile kilimo kwa wale walio vijijini na biashara ndogondogo kwa wale ambao wako mijijini na hata vijijini.


Ile dhana ya kusema mwanamke ni mama wa nyumbani wa kukaa na kujipodoa akimsubiria mwnaume arudi amstarehesha, sasa hivi imepitwa na wakati. Wanaume wengi wanapenda wanawake ambao ni wahangaikaji, wenye ndoto za maendeleo katika maisha yao. Hata kama watakuwa si wafanyakazi lakini wawe wenye kutoa ushauri kwa waume zao juu ya jinsi gani wafanye ili wafanikiwe.
4. WASIOPENDA MAKUU
Kuna wanawake wengine wanakuwa na tabia za ajabu sana kiasi kwamba yaweza kuwa kero kwa wanaume. Wapo wanawake ambao wanapenda makuu bila kujali hali halisi ilivyo. Kuna wanawake naweza kusema wana tamaa, kila wikiendi utamsikia "leo tunakwenda wapi dear?"


Akimuona rafiki yake kanunua simu ya laki tatu na yeye utamsikia akisema, ‘na mimi naomba uninunulie simu kama ya Grace'. Ukienda naye Pub anakuambia, "mimi sinywi pombe za chupa natumia za kopo tena Heineken'. Yeye hajali kiasi cha pesa mwanaume alicho nacho na usipotekelezea anachukia na anaweza hata kupunguza mapenzi.

Wanawake kama hawa wako katika mazingira magumu sana ya kuweza kupata wanaume wa kuwaoa. Mara nyingi katika maisha fedha huzungumza, kama mwanaume atakuwa na pesa ya kutosha itakuwa rahisi sana kwa mwanamke kupata kila atakachopenda lakini si kwa kumwambia mimi nataka kitu fulani.Mwanaune mwenyewe utamsikia akisema, ‘unataka nikununulie simu ya aina gani, au leo unataka twende wapi?' hapo ndipo utakuwa na nafasi ya kusema, ‘mimi nataka uninunulie simu kama ya fulani ama leo nataka twende sehemu fulani.'

Wanaume ni warahisi sana wa kuwapatia wale ambao wanatarajia kuwaoa chochote ambacho watahitaji kama tu pesa haitakuwa tatizo. Kitu ambacho kinawaudhi wanaume wengi ni ile tabia ya mwanamke kupenda mambo makubwa bila kuangalia uwezo uliopo kwa mwanume.


Kuna wanawake wengine wao si wasemaji kabisa, yeye anasubiri leo amemletea hiki, anapokea na kushukuru, kesho akiambiwa twende beach anakubali. Au wengine wanasubiri mpaka waulizwe wanataka nini, ndio wanasema.

Sisemi kwamba uwe mkimya tu hata kama una shida ya kitu fulani na unafahamu kwamba ukimweleza mwenza wako anaweza kukusaidia, hapana! kama unaona kwamba uwezekano wa kupata kile ambacho unakihitaji upo mweleze kwa utaratibu naamini atakuelewa na kukutimizia.Tabia ambayo hawaipendi wanaume wengi ni ile ya kulazimisha ufanyiwe kitu fulani wakati inawezekana uwezekano haupo.
5. WAVUMILIVU
Wapo wanawake ambao sio wavumilivu kabisa katika maisha.Tunajua kwamba maisha siku zote hayatabiriki, yanaweza kutokea matatizo ya kiafya ama kifedha.Huu ndio wakati wa kuona uvumilivu wa mtu.Kama mwanamke anatarajia kwamba siku zote ni za raha tu na pindi matatizo yanapotokea anachukua uamuzi wa kumtoroka mwanume, huyo siyo mwanamke wa kuoa.


Wangapi leo hii huwatoroka waume zao pindi inapotokea kuumwa, kufilisika ama kupatwa na tatizo lolote ambalo kwa namna moja ama nyingine yanaweza kuwafanya maisha yao kutingishika?

Uvumilivu kwa mwanamke utakuwepo kama tu atakuwa na mapenzi ya dhati kama nilivyozungumza hapo awali. Mwanamke mweye mapenzi ya dhati ni lazima atakuwa mvumilivu na atakuwa tayari kuishi katika maisha ya aina yoyote, yawe ya raha ama ya starehe.Hawa ndio wale ambao wanaume wengi wengependa kuwa nao maishani mwao.

Licha ya kupenda kuoa wanawake amabo wana tabia hizo nilizozitaja hapo juu, wanachukizwa sana na wanawake ambao wanavijitabia vidogo vidogo ambavyo kimsingi havikubaliki katka jamii.

Tabia hizo ni kama wambea, wasio wakweli na wawazi, wasioridhika, wagumu kusamehe na wapesi wa kuchukia, wagomvi na wenye roho ya kwanini.

Utafiti huu umefanyikwa kwa baadhi ya wanaume ambao wanatarajia kuoa wanawake ambao wanaoishi katika maeneo mbalimbali
Kwa maana hiyo basi hiyo iwe changamoto kwa wanawake. Wajue kwamba wanaume wanafurahi kuwa na wanawake wa aina gani. Hata kama utakuwa umeshaolewa, kama kuna wakati kunakuwa na kutokuelewana baina yenu, chunguza yawezekana kwamba unakosa mojawapo ya tabia ambazo nimezitaja hapo juu. Waweza kubadilika kwani inawezekana.
 
pole sana,nini ushauri wako kwa mabinti wenye mtazamo kama wako.
Asante!

Mimba ya kukusudia bila ridhaa ya mwanaume ili uolewe naye si kigezo cha/sharti la mwanaume kukuoa.

Kumbebea mimba mwanaume ili akuoe huwa na matokeo mawili either "ukapendwa sana" au "ukachukiwa sana" kuliko watu wote duniani.

Kumbebea mimba mwanaume ili akuoe yadhihirisha uzembe na kushindwa kujimudu kwa mwanamke kwenye mwili wake mwenyewe. Hivyo hawezi kumudu familia.Hawafai kuoa.

Wanaume hatu-oi mimba,tuna-oa tuwapendao kwa dhati bila masharti ya huruma yaani 'mimba'
 
mtaishia kubeba mimba na kila mwanaume ili mwolewe pasipokuolewa

na ndio watoto wa mitaan wanapoongezeka kwa kasi ya ajabu, na kuwatupa choon,mitaroni,mifereni,majalalan viumbe wasio na hatia kwasababu za kubeba mimba kwa ajili ya kuolewa tuweni makini wadada.
 
Asante!

Mimba ya kukusudia bila ridhaa ya mwanaume ili uolewe naye si kigezo cha/sharti la mwanaume kukuoa.

Kumbebea mimba mwanaume ili akuoe huwa na matokeo mawili either "ukapendwa sana" au "ukachukiwa sana" kuliko watu wote duniani.

Kumbebea mimba mwanaume ili akuoe yadhihirisha uzembe na kushindwa kujimudu kwa mwanamke kwenye mwili wake mwenyewe. Hivyo hawezi kumudu familia.Hawafai kuoa.

Wanaume hatu-oi mimba,tuna-oa tuwapendao kwa dhati bila masharti ya huruma yaani 'mimba'

nilihisi ww ni KE kumbe ni ME.
 
hahahahaha umenichekesha sana Asnam, haya ndo mambo ya JF



ila ulipitiliza duh eti nikambebea mimba,hebu fafanua ww ndo ulibeba au binti alikubebea ujue ile sentensi yako ina utata?
 
mimba ili uolewe au ili uzae, au both...... unaweza beba mimba na ukamcha Mungu bana si ulishatubu, labda iwe mimba ya shetani

Sasa hvi kumezuka tabia kwa baadhi ya wanawake wengi kujitegsha wapate mimba ilimradi tu waweze kuolewa na hao wanaume waliopatia hzo mimba na kuasahau kwmba kufnya hvyo ni kinyume na matakwa ya mwenyz mungu so ndgu yngu Hoshea naomba utambue hlo kwnza.
 
Back
Top Bottom