Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Uje Kigoma nikupeleke kwa mtaalamu mmoja; yaani pesa zote za box Nyani Ngabu anakubembeleza upokee!
Yaani kadada kamemset mzee (uncle wake wife) mpaka amekuwa kama zezeta. Picha kamili ipo hivi. Huyu ni mzee wa heshima kabisa, ni bosi wa taasisi moja nyeti hapa Dar. Siku moja hivi kama mwaka umepita huyo mzee alisepa home, akawa hajulikani alipo. Baadae tukasikia amepanga nyumba sehemu hapahapa Dar anaishi na mwanamke, (yaani kaacha nyumba yake ya kama 600 million, mke waliyeishi wote kama 20 yrs hivi, mtoto mmoja aged 20 na gari 2 ndogo). Huyo mke mpya akawa karibu na ndugu wa mwanaume mpaka alipopata uhakika kwamba mzee harudi tena nyumbani kwake. Akaanza kutimua ndugu mmoja mmoja mpaka akabaki yeye na mdingi tu. Kapewa mtaji anapiga dili za kwenda China kufuata bidhaa. Akisafiri anamwita mamake ndo aje akae na mumewe, ati hataki kumwacha na mtu mwingine. Sijui wanamlisha nini. Mdingi wa watu, yaani ukimwona kama msukule. Yupoyupo tu. Juzijuzi kulikuwa na shughuli ya kiukoo ndugu wakaamua kufanyia kwake, u know what? Eti huyo mother house kafunga vyumba vyote kaacha kimoja tu wazi kwamba wageni wote wa mumewe (wa kike na kiume) watumie hicho, ambacho mdogo wa mumewe amefikia humo! Halafu ndugu zake yeye wote wawili wa kike watumie vyumba 2 vilivyo empty. Walipolalamika, mama (huyo mdada sasa, ambae ni mdogo kwa my wife) kaja juu kishenzi, kwamba amefunga vyumba vingine kwa sababu last week aliibiwa pea ya viatu. Mdingi yupo kimya kama kamwagiwa mtaji, mkewe anadhalilisha ndugu zake wapatao 15, wawili kati yao ni wakubwa zake kisa pea ya viatu sijui vya 50,000. Mshahara wa huyu mzee ni kama 6 million per month. Utu wa mtu kwa pea ya viatu!!!!! Ndugu wakabeba mizigo yao hao wakasepa lakini wakaahidi hawatarudi tena. Mzee kampigia wife wangu simu kujaribu kureconcile (yeye ndio alianzisha kulalamika kuwa hawawezi kudhalilishwa na akataka kumchapa makofi mke wa uncle yake). Sasa mzee wa watu alichoongea hata hakieleweki, inaonekana ndugu anawapenda na dawa zimekolea. Wife hajui amsaidieje uncle wake wakati ndugu wengine wamemsusa mdingi, including mama yake mzazi!!! Tumsaidieje huyu mzee?? Wakati huohuo wadada acheni zenu bana!! Mnakuwaje na roho mbaya kuliko shetani? Ah!
hapo sasa, yani ujinga wa huyo mzee utuhumu wanawake wote!!! mjini shule shamba kilimo!! mwambie arudi kijijini akalime....
Yaani kadada
kamemset mzee (uncle wake wife) mpaka amekuwa kama zezeta. Picha kamili
ipo hivi. Huyu ni mzee wa heshima kabisa, ni bosi wa taasisi moja nyeti
hapa Dar. Siku moja hivi kama mwaka umepita huyo mzee alisepa home,
akawa hajulikani alipo. Baadae tukasikia amepanga nyumba sehemu hapahapa
Dar anaishi na mwanamke, (yaani kaacha nyumba yake ya kama 600 million,
mke waliyeishi wote kama 20 yrs hivi, mtoto mmoja aged 20 na gari 2
ndogo). Huyo mke mpya akawa karibu na ndugu wa mwanaume mpaka alipopata
uhakika kwamba mzee harudi tena nyumbani kwake. Akaanza kutimua ndugu
mmoja mmoja mpaka akabaki yeye na mdingi tu. Kapewa mtaji anapiga dili
za kwenda China kufuata bidhaa. Akisafiri anamwita mamake ndo aje akae
na mumewe, ati hataki kumwacha na mtu mwingine. Sijui wanamlisha nini.
Mdingi wa watu, yaani ukimwona kama msukule. Yupoyupo tu. Juzijuzi
kulikuwa na shughuli ya kiukoo ndugu wakaamua kufanyia kwake, u know
what? Eti huyo mother house kafunga vyumba vyote kaacha kimoja tu wazi
kwamba wageni wote wa mumewe (wa kike na kiume) watumie hicho, ambacho
mdogo wa mumewe amefikia humo! Halafu ndugu zake yeye wote wawili wa
kike watumie vyumba 2 vilivyo empty. Walipolalamika, mama (huyo mdada
sasa, ambae ni mdogo kwa my wife) kaja juu kishenzi, kwamba amefunga
vyumba vingine kwa sababu last week aliibiwa pea ya viatu. Mdingi yupo
kimya kama kamwagiwa mtaji, mkewe anadhalilisha ndugu zake wapatao 15,
wawili kati yao ni wakubwa zake kisa pea ya viatu sijui vya 50,000.
Mshahara wa huyu mzee ni kama 6 million per month. Utu wa mtu kwa pea ya
viatu!!!!! Ndugu wakabeba mizigo yao hao wakasepa lakini wakaahidi
hawatarudi tena. Mzee kampigia wife wangu simu kujaribu kureconcile
(yeye ndio alianzisha kulalamika kuwa hawawezi kudhalilishwa na akataka
kumchapa makofi mke wa uncle yake). Sasa mzee wa watu alichoongea hata
hakieleweki, inaonekana ndugu anawapenda na dawa zimekolea. Wife hajui
amsaidieje uncle wake wakati ndugu wengine wamemsusa mdingi, including
mama yake mzazi!!! Tumsaidieje huyu mzee?? Wakati huohuo wadada acheni
zenu bana!! Mnakuwaje na roho mbaya kuliko shetani? Ah!
Wale watu walipomleta yule mwanamke mzinifu ili ahukumiwe Yesu akasema asiye na dhambi awe wa kwanza kumrushia jiwe kisha aliinama chini na kuandika neno alipoinuka hakuona mtu. sasa mwaulizwa mfanyenje kumnusuru mzee wa watu nyie mwaanza kuponda na kushutumu. Tena wanaume nyie mnathubutu kha!!! Mimi nina kioo changu hapa naona kama mutu tano hivi wana nyumba za pembeni. tatizo la mzee kuhamia na kuitekeleza familia. ushauri; watafutwe wazee wachache wamwone, wamsikie, waseme naye kisha wamshauri cha kufanya huenda naye ana neno litakalosadia kupata ufumbuzi
huyo mume atarudi tu kwa mkewe.ila asije akapuputishwa.maana huyo mwanamke inaonyesha amemiliki kila kitu.wangeucheza mchezo.wakatafuta hirizi,na majani majani wakayaweka chini ya godoro la huyo mama,baadae wakavitoa wakasema kaviweka huyo mama,ili huyo bwana kidogo azinduke,kabla hajapuputishwa wote